Safari ya Marekani

Utadhani usa ni mbinguni,pumbavu zao
 
Nimesoma mahali november wanaweza anza toa visitors visa...ila sio source ya kueleweka
 
Utadhani usa ni mbinguni,pumbavu zao
Sio mbinguni lakini watu wengi all over the world wanataka kuhamia huko kutafuta maishi ukilinganisha mfano na watu wanaotaka kwenda Tanzania kutafuta maisha. Therefore inabidi wabane. Nchi yao ina demand kubwa.
 
2 tu...Marekani,ujerumani na uholanzi (nadhani ni hiyo hiyo ujerumani).nategemea kwenda ufaransa na London pia.Hii Covid imefanya kilakitu kiwe kigumu.
Mkuu Germany na uholanz taratibu zao za visa zikoje? Hazina ugumu sana kama U.K canada na Australia???
 
Mkuu Germany na uholanz taratibu zao za visa zikoje? Hazina ugumu sana kama U.K canada na Australia???
Nadhani Ya ujerumani wanikua very strict,kwasababu walinipa schengen visa ambayo ningeweza kuingia kwenye nchi 26 za Europe.All in all ukiwa mkweli na sababu ya kueleweka lazima upewe visa yeyote.Wale watu wamefanya kazi hiyo muda mrefu so wanajua ukidanganya.Interview ya marekani took less than 5 minutes was the easiest.
 
Huo sio ushauri aliouomba
 
Oh ..aisee kama Ps yako tayari ina stamps za nchi kama hizo za Europe atlist inaongeza nguvu katika kupewa visa nyingine

Ina gharimu kiasi gani kufuatilia visa hiyo na docs gani zilihitajika?
 
Oh ..aisee kama Ps yako tayari ina stamps za nchi kama hizo za Europe atlist inaongeza nguvu katika kupewa visa nyingine

Ina gharimu kiasi gani kufuatilia visa hiyo na docs gani zilihitajika?
Gharama ya visa inategemea na nchi unayokwenda.Documents zinategemea na dhumuni la safari.kama unategemea kusafiri nenda kwenye website ya embassy ya nchi utakayotaka kwenda kuna maelezo yote.siwezi nikasema documents zipi au gharama gani kwasababu dhumuni la safari ni tofauti.ilakilakitu kiko wazi na majibu yote ya maswali yako utapata huko.Ni rahisi tu ukifuata maelezo yao. Kuhusu maswali Kama wadau wengine walivyosema huko juu na pia inategemea na sababu ya safari
 
Mkuu kwa nini ni ngumu kwa mtu kupata kazi USA kwa visit Visa?.
 
Mkuu kwa nini ni ngumu kwa mtu kupata kazi USA kwa visit Visa?.
Kupata kazi au kuomba kazi USA unahitaji vitu viwili, 1: Kitambulisho cha state (sawa na kitambulisho cha taifa Tanzania) na 2: Social security number (sawa na Tax ID number ya mtu binafsi kwa tanzania).

Ukiwa na student visa, unaweza kwenda kwa mamlaka husika ukapata hivyo vitu viwili. Ukioa raia wa USA pia unapata residency card hivyo unapata hivyo vitu viwili kiurahisi. Ila kwa visitor visa, HAKUNA JINSI YA KUPATA HIZO cards 2 ya SSN na ID card. Kwa hio ndio maana kuliko mtu uje USA na visitor visa kama unakuja kutafta maisha, BORA UBAKIE AFRICA TU hadi uweze pata visa nyingine. Wengi huwa wanateseka sana sana.
 
Shukrani sana mkuu,maelezo mazuri sana nimeelewa vizuri inaonekana una experiance na exposure kubwa juu ya jambo hili,kwa ushauri ni njia ipi rahisi kwa mtu anayetaka kwenda Us kwa madhumuni ya kutafuta maisha anaweza tumia?.
 
Shukrani sana mkuu,maelezo mazuri sana nimeelewa vizuri inaonekana una experiance na exposure kubwa juu ya jambo hili,kwa ushauri ni njia ipi rahisi kwa mtu anayetaka kwenda Us kwa madhumuni ya kutafuta maisha anaweza tumia?.
Student visa ni njia rahisi zaidi. Inapatikana kiurahisi provided kwamba ulifanya vizuri shuleni au teari una degree moja na unataka kuongeza nyingine nje ya nchi. Pia unaweza fanya kazi flani flani zikakusaidia kujisomesha wakati unaendeleza michongo mingine ya maisha ukiwa na hio student visa.

Njia nyingine nzuri zaidi ila sio rahisi sana, ni kupata manzi Mmarekani. Unaweza mtafuta kupitia online dating sites au wale wanaokuja bongo kwa utalii.. ila tatizo hao kuna competition kubwa sana na waTz wenzako. Manzi huyo mnapendana kisha anakusaidia kila kitu uje USA kimaisha. Lakini umweke sawa tokea mwanzo kwamba una nia ya ku-invest bongo usije tekwa ukapotea kimoja ughaibuni
 
Barikiwa sana kiongozi,nimekuelewa mno,watu kama ninyi ndio mnahitajika katika jamii za wapambani.
 
Hongera mkuu, wengi wanakayanga Ulaya na Marekani wa trip za kiofisi tu, ila kama ume-save hadi kupanga trip lako la binafsi aisee we si wa kawaida - its life time adventure kwa kweli, mimi naiita hii ni life time achievement yaani kutoka bara A kwenda bara B kwa mpunga wako si jambo dogo.

Unajua mtu anaweza ukamaliza maisha yako ya hapa duniani bila kupanda flight ya walau masaa 6 -8 angani - yaani we ni wa Mwanza - dar - kigoma - arusha umemaliza.

Big up, ukifika huko basi piga mapicha picha ututumia hapa kwenye huu uzi wako.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…