chamlungu
JF-Expert Member
- Oct 22, 2012
- 326
- 339
Wakuu jana tarehe 1.11.2014 nilisafiri kutoka Dar kuja hapa Igunga. Nilipanda basi la Mohamed Trans la Kahama.Tuliondoka Dar saa 12.30, tukafika Dodoma saa 8 hivi. Wakatuambia basi letu lina tatizo, tukafaulishwa kwenye basi jingine. Kabla hatujafika Manyoni likaanza kuchemsha. Tukalazimika kusimama mara 2 kuongeza maji. Tulipofika Singida tukafaulishwa tena kwenye basi jingine. Nilifika hapa Igunga saa 4 hivi. Kuweni makini na hayo mabasi ya MOHAMED TRANS mengi yamechoka kabisa