Ndugu wanaJF,
Kulingana na maneno ya misemo ya kiswahili kila mwosha naye huoshwa, ni dhahiri Saed Kubenea mbunge wa jimbo la Ubungo CHADEMA ameosha wengi na imefika wakati kaongeza CV ya ubunge mbali na uandishi wa habari za kikachero. Ninapopita kwenye vyombo vya habari anavyomiliki ninakuta muda mwingi ZITTO, ZITTO sijui huyu Ztto ni nani anayetrend kwenye vyombo vyake vya habari vya Mawio na mwanahalisi tu, kwa stori ambazo vyombo vingine havizioni kama ni habari na haviziandiki kwa kuwa ni uzushi na uongo wa kutungwa.
Ukiona Zitto ametajwa BBC, DW, Mwananchi,etc ni habari njema kwa Taifa akimwagiwa sifa kama mwanasiasa kijana wa mfano wa kuingwa, lakini ukisoma habari za Zitto mwanahalisi au mawio utashangaa hawa jamaa wao wanatoa wapi hizi habari au ndio ugonjwa wa chuki unaosemekana anaugua Kubenea? Kubenea inasemekana hauna vyeti vya shule kulingana na ulivyokuwa unajinadi wakati wa kampeni october 2015, nenda kwenye magazeti yako ya Mawio na Mwanahalisi uchapishe CV na utuoneshe vyeti vyako au tuma mtu hapa JF tujiridhishe tuhame mada.
Mwisho kabisha, nakushauri japo najua hauwezi acha tabia yako inayosemekana ni ya undumilakuwili leo Lowassa ni Fisadi mchafu asiyesafishika hata kwa dodoki na unasema una ushahidi lundo, kesho Lowasa sio fisadi ni msafi hahitaji hata kunawa kwa sabuni. Dr Slaa Rais mtarajiwa aliyeko mioyoni mwa watanzania kwa ubora wake kesho Dr Slaa ni hovyo msaliti wa mabadiliko. Ikiwa unashindwa kutumia akili ya vyuo vyako vya hapa na pale ulivyoongeza elimu ya juu India na kwingineko huko na kule, basi tumia hata ya Elimu ya chekechea tulikojifunza " Is it possible to hold three things in one hand?"
Inaaminika na kusemwa sana mwanamke hawezi tumikia mabwana watatu asiitwe kahaba. Uandishi wewe, Upelelezi wewe, uwakilishi wa wananchi wewe, uongozi wa propaganda za chadema wewe. Acha, acha kabisa kutaka kuongeza umaarufu kwa kukashfu watu weka CV zako Mawio na Mwanahalisi. Acha kabisa kuwadanganya watanzania kwa kivuli cha mwandishi wa habari uliobobea. Umetoka kwenye mstari umekiuka misingi ya uandishi katubu haraka iwezekanavyo.