S2dak_Jr
Senior Member
- Jul 15, 2012
- 198
- 45
Asubuhi naamka na kwenda kazini na kukuta Hiace inayomilikiwa na mtu anayeitwa California ikiwa imepaki.
Mara naona vijana wanaofanya kazi katika shimo la dhahabu la mtu aitwaye Omary wakielekea kwenye Hiace hiyo na kupanda.
Niliposogea, niliona vijana hao wakiwa wanavuta Bangi huku wakiwa wamewasha udi.
Mara gari liliondoka na lilipofika Misigiri likapaki kwenye Bar/Grocery moja iitwayo Manka. Hapa vijana walianza kunywa pombe aina ya Konyagi. Na baada ya muda gari liliondoka na kuelekea Ndago.
MAHUSIANO YA WACHIMBAJI HAO NA MH. MWIGULU.
Itakumbukwa kuwa eneo la Mgodi wa Mgongo/Sekenke lilikuwa na mgogoro kati ya wachimbaji hao na mtu mmoja anayeitwa John Binna. Huu mgogoro ulirushwa kwenye Media mbalimbali ikiwemo TBC kama mtakumbuka.
Mgogoro huu uliingiliwa Mh. Mwigulu na kuamuru Mgodi hao wa dhahabu uchimbwe na WAPIGA KURA WAKE.
Hivyo hata leo Mh. Mwigulu akija na kuwaambia twendeni Ndago mkafanye fujo, sidhani kama wachimbaji watakataa.
Punde nitawaletea picha za gari, eneo lao la kazi, vijana na Bar waliyokuwa wanakunywa Konyagi.
Source: nilikuwepo eneo la mgodini.
UPDATES NEWS FROM Mkuu T.2015.CDM
Mara naona vijana wanaofanya kazi katika shimo la dhahabu la mtu aitwaye Omary wakielekea kwenye Hiace hiyo na kupanda.
Niliposogea, niliona vijana hao wakiwa wanavuta Bangi huku wakiwa wamewasha udi.
Mara gari liliondoka na lilipofika Misigiri likapaki kwenye Bar/Grocery moja iitwayo Manka. Hapa vijana walianza kunywa pombe aina ya Konyagi. Na baada ya muda gari liliondoka na kuelekea Ndago.
MAHUSIANO YA WACHIMBAJI HAO NA MH. MWIGULU.
Itakumbukwa kuwa eneo la Mgodi wa Mgongo/Sekenke lilikuwa na mgogoro kati ya wachimbaji hao na mtu mmoja anayeitwa John Binna. Huu mgogoro ulirushwa kwenye Media mbalimbali ikiwemo TBC kama mtakumbuka.
Mgogoro huu uliingiliwa Mh. Mwigulu na kuamuru Mgodi hao wa dhahabu uchimbwe na WAPIGA KURA WAKE.
Hivyo hata leo Mh. Mwigulu akija na kuwaambia twendeni Ndago mkafanye fujo, sidhani kama wachimbaji watakataa.
Punde nitawaletea picha za gari, eneo lao la kazi, vijana na Bar waliyokuwa wanakunywa Konyagi.
Source: nilikuwepo eneo la mgodini.
UPDATES NEWS FROM Mkuu T.2015.CDM
*NI KATIKA MKUTANO WA MNYIKA,MWENYEKITI WA KATA UVCCM AUAWA,18 WAJERUHIWA
Raymond Kaminyoge, Dar na Gasper Andrew, Singida VURUGU kubwa zilizotokea kwenye mkutano wa hadhara zikiwahusisha wafuasi wa Chadema na CCM zimesababisha kifo cha Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana (UVCCM) wa Kata ya Ndago, wilayani Iramba, Yohana Mpinga (30) na majeruhi mmoja.Wafuasi hao wa Chadema na CCM walishambuliana kwa kutumia silaha za jadi ikiwamo mawe, wakati wa mkutano wa hadhara uliokuwa unahutubiwa na Mbunge wa Ubungo, John Mnyika.Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Singida, Linus Sinzumwa alithibitisha kutokea kwa vurugu hizo na kifo cha mwenyekiti huyo baada ya kupigwa kwa silaha za jadi.Kamanda Sinzumwa alifafanua kwamba, kutokana na tukio hilo, jeshi hilo linawashikilia watu 18 wa kata hiyo kwa mahojiano zaidi na watakapobainika kuhusika na ghasia hizo watafikishwa mahakamani.Alisema majeruhi huyo wa vurugu hizo anayejulikana kwa jina la Ramadhani Hussein (27), amelazwa katika Kituo cha Afya cha Ndago baada ya kujeruhiwa vibaya.
"Tukio hilo la kusikitisha lilitokea Julai 14 mwaka huu saa 10 alasiri katika Kijiji cha Ndago," alisema Kamanda.Alisema siku ya tukio, Chadema kilikuwa na kibali cha kufanya mkutano wa hadhara katika kijiji hicho na mgeni rasmi alikuwa Mbunge Mnyika.Kamanda Sinzumwa alisema kuwa, baada ya Chadema kuanza mkutano huo, viongozi wake walianza kutoa kashfa mbalimbali dhidi ya Mbunge wa Jimbo la Iramba Magharibi (CCM), Mwingulu Nchemba.
Alisema kitendo hicho kiliwaudhi baadhi ya watu waliokuwa wamehudhuria mkutano huo."Wananchi hao walichukizwa na kitendo cha kukashifiwa mbunge wao na walianza kupiga kelele kuwa hawataki mbunge wao akashifiwe na badala yake, wakawataka Chadema wawe wanaeleza sera zao na si vinginevyo," alisema.Kamanda huyo alisema licha ya tahadhari hiyo, viongozi hao waliendelea kueleza kashfa za Mbunge Nchemba na ndipo vurugu zilipoanza.
Alifafanua kwamba, vurugu hizo zilianza baada ya wafuasi wa CCM waliokasirishwa na kashfa zilizokuwa zikitolewa na viongozi wa Chadema kuanza kuwarushia mawe wafuasi wa Chadema. Kamanda Sinzumwa alisema askari polisi wachache waliokuwapo, walizidiwa nguvu na makundi hayo."Huyu Mwenyekiti wa Vijana wa CCM, Yohana alikimbilia kwenye nyumba ya Mwalimu Shume Manase ili kuokoa maisha yake, lakini kundi la wafuasi wa Chadema wakiwa wamebeba fimbo na mawe, walimpiga sehemu mbalimbali mwilini na kusababisha kifo chake papo hapo," alisema.
Kamanda huyo alisema licha ya watuhumiwa 18 kukamatwa, polisi bado inaendelea na msako wa kuwatafuta watu wengine waliohusika katika tukio hilo ili wafikishwe mahakamani.Kauli ya MnyikaAkizungumzia vurugu hizo, Mbunge wa Ubungo, John Mnyika alisema mbinu chafu zinazotumiwa na CCM za kupiga mawe mikutano yao ya hadhara kamwe haitakidhoofisha chama chao katika harakati zake za kuwakomboa wananchi kutoka katika maisha magumu.
Mnyika alisema amefurahi kufika katika jimbo hilo la Mbunge Nchemba kwa sababu ya propaganda zake, ambazo amekuwa akizitoa bungeni na alivyofanya ziara kwenye jimbo lake la Ubungo na kuwahutubia watu wa Manzese.Mnyika alisema wakati wowote kuanzia sasa viongozi wa juu wa chama hicho watafanya ziara kwenye kata zote za Mkoa wa Singida ili, kuwafahamisha wananchi hatua za kuchukua katika uchaguzi ujazo
Mbunge wa jimbo la Ubungo jijini Dar-es-salaam,John Mnyika,kizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofayika juzi katika kijiji cha Ndago jimbo la Iramba magharibi mkoani Singida
Last edited by a moderator: