S2dak_Jr
Senior Member
- Jul 15, 2012
- 198
- 45
- Thread starter
- #61
Baada ya lile jengo kulia kwa Mh. Mnyika linafuatia jengo la Kituo cha Polisi Ndago. Yaani ni kama hatua 30 kutoka aliposimama Mh. Mnyika.
Ikumbukwe pia CDM walitoa taarifa Polisi kuwa kuna wahuni wanarusha mawe na wakafungua jalada. Lakini cha kushangaza Polisi hawakuwachukulia hao vijana waliotumwa hapo ili wafanye fujo.
Kuna maswali haya ya kujiuliza:
i) Je, Polisi walikuwa wanajua nini kitatokea ndio maana walipuuzia taarifa ya CDM?
ii) Je, vijana waliokuwa wanarusha mawe ni wa CDM au CCM? Na kama ni wa CDM, kwa nini wawarushie mawe viongozi wao? Na kama ni wa CCM, walipata wapi kiburi cha kurusha mawe kama si kulindwa na Polisi kwa maelekezo ya mwigulu?
Hapa Mnyika akihutubia kabla ya kuanza kuvurumushiwa mawe na CCM