Keynez
JF-Expert Member
- Feb 12, 2007
- 3,661
- 6,637
Salamu kwenu wote.
Nianze kwa kusema kuwa sijawahi kuwa mwanachama wa chama chochote cha siasa hadi sasa na kwa kweli sijawahi kuwaza kuwa nitakuja kuwa mwanachama wa CCM. Mimi ni mfuatiliaji wa siasa kiujumla, kwa maana ya general political discussions', za ndani na za kimataifa.
Mara ya kwanza na ya mwisho kupiga kura katika chaguzi za Tanzania ilikuwa 1995 pale nilipompa kura yangu Augustine Mrema, wakati huo akiwa NCCR-Mageuzi. Katika nyuzi zangu nyingi tu za nyuma nimekuwa 'critical' siyo tu kwa CCM na utendaji wa majukumu ya serikali pamoja na jinsi wanavyoendesha siasa lakini pia siku zote nimekuwa mkosoaji wa udhaifu na makosa wanayofanya wapinzani. Vyama vya upinzani vina udhaifu mkubwa ambao ukiwa na uelewa ni ngumu sana kuvipigania.
Baada ya huo utangulizi, ngoja niende sasa kwenye mada kuu.
Ki ukweli huu mfumo wa demokrasia kiujumla unaojaribu kuupractice (kuanzia uhuru wa kutoa maoni yako na hadi mfumo wa vyama vingi) unapata changamoto kubwa na mimi kwa maoni yangu ni kwa sababu elimu ya HAKI na WAJIBU wa kila mtanzania haikufundishwa na kufanywa kuwa sehemu ya DNA yetu. Hili ni jambo muhimu sana. Hii ndiyo inaleta matatizo katika ofisi za umma na hata binafsi, utekelezaji wa majukumu mbalimbali ya kijamii, upambanaji wa rushwa, utendaji katika vyombo vya usalama kama polisi, siasa zetu, nk.
Nakwenda CCM kwa sababu ni ngumu sana kufanya siasa za upinzani Tanzania ukiwa tu defensive, utaumia tu, au kwa lugha ya kigogo, utapata tabuuu sana. Niliwahi kulisema sana huko nyuma.
Naenda CCM kujaribu kumuelimisha Mtanzania ajue Haki na Wajibu wake kama Mtanzania. Hilo litakuwa lengo langu kuu. Najua Mtanzania akielimika kwenye hili, atakuwa kiongozi bora pale atakapopewa majukumu ya kiuongozi, atakuwa mpiga kura bora mwenye uwezo wa kupambanua mambo mbalimbali ya kijamii na kitaifa lakini pia akipigania mawazo yake kwa nguvu zake zote huku vyombo vya kumlinda vikifanya kazi zake kwa uhuru, atakuwa baba na mama bora, atakuwa mtoto na kijana bora mwenye maono na malengo chanya, atakuwa jirani bora, atakuwa polisi bora mwenye kuheshimu haki za raia na kutambua wajibu wa wake na wa raia, atakuwa mfanyabiashara mzalendo anayeheshimu sheria za nchi na kanuni za kazi yake lakini pia anayejua haki zake na kuna vyombo vya kumlinda na kumpigania, nk.
Siendi CCM kuunga mkono juhudi! Naenda huko kumbadilisha Mtanzania, one at a time. Nina mawazo mengi ila nahitaji platform sahihi itakayonisaidia nisikike na mawazo yangu yafanyiwe kazi.
Napeleka siasa mpya ndani ya CCM. Ni matumaini yangu nitapokelewa vizuri!
Nianze kwa kusema kuwa sijawahi kuwa mwanachama wa chama chochote cha siasa hadi sasa na kwa kweli sijawahi kuwaza kuwa nitakuja kuwa mwanachama wa CCM. Mimi ni mfuatiliaji wa siasa kiujumla, kwa maana ya general political discussions', za ndani na za kimataifa.
Mara ya kwanza na ya mwisho kupiga kura katika chaguzi za Tanzania ilikuwa 1995 pale nilipompa kura yangu Augustine Mrema, wakati huo akiwa NCCR-Mageuzi. Katika nyuzi zangu nyingi tu za nyuma nimekuwa 'critical' siyo tu kwa CCM na utendaji wa majukumu ya serikali pamoja na jinsi wanavyoendesha siasa lakini pia siku zote nimekuwa mkosoaji wa udhaifu na makosa wanayofanya wapinzani. Vyama vya upinzani vina udhaifu mkubwa ambao ukiwa na uelewa ni ngumu sana kuvipigania.
Baada ya huo utangulizi, ngoja niende sasa kwenye mada kuu.
Ki ukweli huu mfumo wa demokrasia kiujumla unaojaribu kuupractice (kuanzia uhuru wa kutoa maoni yako na hadi mfumo wa vyama vingi) unapata changamoto kubwa na mimi kwa maoni yangu ni kwa sababu elimu ya HAKI na WAJIBU wa kila mtanzania haikufundishwa na kufanywa kuwa sehemu ya DNA yetu. Hili ni jambo muhimu sana. Hii ndiyo inaleta matatizo katika ofisi za umma na hata binafsi, utekelezaji wa majukumu mbalimbali ya kijamii, upambanaji wa rushwa, utendaji katika vyombo vya usalama kama polisi, siasa zetu, nk.
Nakwenda CCM kwa sababu ni ngumu sana kufanya siasa za upinzani Tanzania ukiwa tu defensive, utaumia tu, au kwa lugha ya kigogo, utapata tabuuu sana. Niliwahi kulisema sana huko nyuma.
Naenda CCM kujaribu kumuelimisha Mtanzania ajue Haki na Wajibu wake kama Mtanzania. Hilo litakuwa lengo langu kuu. Najua Mtanzania akielimika kwenye hili, atakuwa kiongozi bora pale atakapopewa majukumu ya kiuongozi, atakuwa mpiga kura bora mwenye uwezo wa kupambanua mambo mbalimbali ya kijamii na kitaifa lakini pia akipigania mawazo yake kwa nguvu zake zote huku vyombo vya kumlinda vikifanya kazi zake kwa uhuru, atakuwa baba na mama bora, atakuwa mtoto na kijana bora mwenye maono na malengo chanya, atakuwa jirani bora, atakuwa polisi bora mwenye kuheshimu haki za raia na kutambua wajibu wa wake na wa raia, atakuwa mfanyabiashara mzalendo anayeheshimu sheria za nchi na kanuni za kazi yake lakini pia anayejua haki zake na kuna vyombo vya kumlinda na kumpigania, nk.
Siendi CCM kuunga mkono juhudi! Naenda huko kumbadilisha Mtanzania, one at a time. Nina mawazo mengi ila nahitaji platform sahihi itakayonisaidia nisikike na mawazo yangu yafanyiwe kazi.
Napeleka siasa mpya ndani ya CCM. Ni matumaini yangu nitapokelewa vizuri!