Synthesizer
JF-Expert Member
- Feb 15, 2010
- 11,143
- 18,774
Wengi hawajaliona hilo, kwamba Kenyatta mara kadhaa amejaribu kumfundisha uungwana na ujirani mwema Magufuli.
Tunaanza na suala la kampeni za uraisi Kenya. Tofauti na protokali za nchi, Magufuli alionyesha waziwazi kumuunga mkono Raila dhidi ya Uhuru. Raila alshindwa lakini hilo halikuwa neno kwa Uhuru Kenyatta, hakuweka kinyongo.
Baada ya hapo likaja suala la vifaranga kutoka Kenya. Vikachomwa moto bila huruma, unyama unyama tu, japo hakukuwa na haja ya kufanya hivyo. Kutumia uungwana hata wangesema vifaranga virudishwe Kenya, lakini sio serikali ya Magufuli. Ikawa kama pigo jingine toka Tanzania kwenda Kenya.
Magufuli alipoamuru ng'ombe wa Wamasai wa Kenya walioingia uapnde wa Tanzania wapigwe mnada, kitendo hicho kilimuuma sana Uhuru. Wakenya nao walikamata ng'ombe wa Tanzania walioingia upande wa Kenya, lakini Uhuru aliwaambia wasilipe kisasi wawarudishie wafugaji wa Tanzaia ng'ombe wao. Akaenda mbali, akatoa fedha za serikali kuwafidia wafugaji walioporwa mifugo yao na Tanzania.
Mara tu ya ng'ombe wa Kenya kupigwa mnada, Tanzania tukapata janga la tetemeko kule Kagera. Uhuru Kenyatta akatoa msaada wa mamilioni ya fedha kusaidia wahanga wa lile tetemeko - japo nasikia fedha hizo hazikuwafikia wahanga kama Uhuru alivyotaka. Ikawa si neno kwa Uhuru, hakujali.
Hatukuishia hapo. Magufuli akaamua wafanyakazi wa Kenya waliokuwa Tanzania kwa vibali wafukuzwe nchini. Wakafukuzwa kama wahalifu japo walikuwa na machango mkubwa kwenye international schools zetu na mahotelini nk. Uhuru Kenyatta hakuona nongwa, akautangazia ulimwengu kwamba Watanzania wanaruhusiwa si tu kufanya kazi Kenya, bali pia hata kuoa na kuolewa. Akaenda mbali zaidi na kumwambia Magufuli ampelekee madaktari zaidi ya 300 wa kutoka Tanzania wakafanye kazi Kenya - japo hili lilikuja kupingwa na kuzuiwa na chama cha madaktari Kenya. Lakini Uhuru alisharidhia kwamba hana tatizo kuchukua madaktari toka Tanzania.
Sasa Kenya wakakamata dhahabu ya Tanzania. Kimsingi hawakuwa na lazima ya kuirudisha Tanzania. Lakini bado Uhuru akafunga safari kuja Chato kumwambia Magufuli kuna dhahabu tumekamata, na kwa kuwa tunaona ilitoka Tanzania basi nitafanya mpango irudishwe Tanzania. Uhuru hakuona kwamba hiyo ilikuwa nafasi nzuri ya kulipiza kisasi cha ng'ombe wa Kenya ambao Tanzania iliwakamata na kuwauza.
Nimemkubali sana Uhuru Kenyatta kwa suala la ujirani mwema na uungwana,, zaidi ya Raisi wangu mwenyewe Pombe Magufuli. Huo ndio ukweli.
Sasa basi, kama Magufuli ameshindwa kuelewa nini maana ya kuwa muungwana na jirani mwema kwa yale yote Uhuru Kenyatta alivyofanya licha ya kufanyiwa mtima nyongo na Tanzania, basi Magufuli hatakaa ajifunze maana ya kuwa muungwana na jirani mwema kamwe!
Tunaanza na suala la kampeni za uraisi Kenya. Tofauti na protokali za nchi, Magufuli alionyesha waziwazi kumuunga mkono Raila dhidi ya Uhuru. Raila alshindwa lakini hilo halikuwa neno kwa Uhuru Kenyatta, hakuweka kinyongo.
Baada ya hapo likaja suala la vifaranga kutoka Kenya. Vikachomwa moto bila huruma, unyama unyama tu, japo hakukuwa na haja ya kufanya hivyo. Kutumia uungwana hata wangesema vifaranga virudishwe Kenya, lakini sio serikali ya Magufuli. Ikawa kama pigo jingine toka Tanzania kwenda Kenya.
Magufuli alipoamuru ng'ombe wa Wamasai wa Kenya walioingia uapnde wa Tanzania wapigwe mnada, kitendo hicho kilimuuma sana Uhuru. Wakenya nao walikamata ng'ombe wa Tanzania walioingia upande wa Kenya, lakini Uhuru aliwaambia wasilipe kisasi wawarudishie wafugaji wa Tanzaia ng'ombe wao. Akaenda mbali, akatoa fedha za serikali kuwafidia wafugaji walioporwa mifugo yao na Tanzania.
Mara tu ya ng'ombe wa Kenya kupigwa mnada, Tanzania tukapata janga la tetemeko kule Kagera. Uhuru Kenyatta akatoa msaada wa mamilioni ya fedha kusaidia wahanga wa lile tetemeko - japo nasikia fedha hizo hazikuwafikia wahanga kama Uhuru alivyotaka. Ikawa si neno kwa Uhuru, hakujali.
Hatukuishia hapo. Magufuli akaamua wafanyakazi wa Kenya waliokuwa Tanzania kwa vibali wafukuzwe nchini. Wakafukuzwa kama wahalifu japo walikuwa na machango mkubwa kwenye international schools zetu na mahotelini nk. Uhuru Kenyatta hakuona nongwa, akautangazia ulimwengu kwamba Watanzania wanaruhusiwa si tu kufanya kazi Kenya, bali pia hata kuoa na kuolewa. Akaenda mbali zaidi na kumwambia Magufuli ampelekee madaktari zaidi ya 300 wa kutoka Tanzania wakafanye kazi Kenya - japo hili lilikuja kupingwa na kuzuiwa na chama cha madaktari Kenya. Lakini Uhuru alisharidhia kwamba hana tatizo kuchukua madaktari toka Tanzania.
Sasa Kenya wakakamata dhahabu ya Tanzania. Kimsingi hawakuwa na lazima ya kuirudisha Tanzania. Lakini bado Uhuru akafunga safari kuja Chato kumwambia Magufuli kuna dhahabu tumekamata, na kwa kuwa tunaona ilitoka Tanzania basi nitafanya mpango irudishwe Tanzania. Uhuru hakuona kwamba hiyo ilikuwa nafasi nzuri ya kulipiza kisasi cha ng'ombe wa Kenya ambao Tanzania iliwakamata na kuwauza.
Nimemkubali sana Uhuru Kenyatta kwa suala la ujirani mwema na uungwana,, zaidi ya Raisi wangu mwenyewe Pombe Magufuli. Huo ndio ukweli.
Sasa basi, kama Magufuli ameshindwa kuelewa nini maana ya kuwa muungwana na jirani mwema kwa yale yote Uhuru Kenyatta alivyofanya licha ya kufanyiwa mtima nyongo na Tanzania, basi Magufuli hatakaa ajifunze maana ya kuwa muungwana na jirani mwema kamwe!