huyu jamaa post zake zote ni mavi tu moja ya post yake nii hiii mjue kwamba nilichoandika kwamba hawa watafuta ajira wanakausumbufu flani ni kweli.HII NDO MOJA YA POST ZAKE
Mwezi Novemba mwaka 2013 hadi February 2014, nilikuwa jijini Dar Es Salaam ktk mihangaiko yangu ya maisha.
Lakini nikaona si vyema nikae bure, wakati ule suala la watanzania wenzetu kukamatwa ktk viwanja mbalimbali vya ndege duniani wakiwa wanavusha madawa ya kulevya likiwa "hot". Nikaamua kulifuatilia.
Nilifanya uchunguzi binafsi jijini Dar Es Salaam na kujiridhisha kuwa wauzaji na watumiaji wa madawa ya kulevya walikuwa wanajulikana bayana mitaani, nikajiuliza; je ni kweli jeshi la polisi halioni watu hawa? Kama vigogo wanaohusika na usafirishaji wa madawa ya kulevya hawapatikani kwa nini isideal na hawa retailer wanaouza madawa ya kulevya mitaani huku wakijulikana?
Nikachunguza na kupita kufanyia utafiti maeneo kadhaa jijini Dar ambako wanauza madawa ya kulevya tena ilipobidi hadi kukutana na wauzaji ili tu kujiridhisha. Kisha nikafanya maamuzi mazito.
Wakati nimesharudi niko Tanga nikamwandikia barua pepe IGP nikimpatia majina na maeneo ya kijiografia hadi nyumba ambazo madawa ya kulevya yanauzwa. Nikaona ni busara pia nika CC; barua ile kwa maRPC wote mikoa yote, na maofisa wote wa jeshi la polisi makao makuu. Baada ya mwezi kupita bila majibu ya mrejesho nikatuma barua kwa njia ya posta(hard copy) kwenda kwa IGP nikimweleza kwa urefu maeneo na majina ya wauzaji wa madawa ya kulevya ktk maeneo kadhaa jijini Dar Es Salaam. Pia nikampigia simu kwenye namba yake 0754 785 557(IGP Mangu) nikimweleza nimemtumia barua pepe na barua ya nakala ngumu kuja mezani kwake.
Bahati mbaya naamini taarifa ile haikufanyiwa kazi, kwani kulikuwa maeneo ambayo nilitakiwa nitoe ushirikiano na nilikuwa tayari kufanya hivyo muda wowote ikibidi hata kwa gharama zangu, nilimweleza hivyo.
Najua ni hatari kwangu ktk suala hili lakini nilikuwa tayari kufa kwa ajili ya taifa langu, kumwaga damu kwa ajili ya kuleta ustawi wa vijana wenzangu wanaoharibika kwa madawa ya kulevya. Nilidhamiria kumwaga damu yangu ili iwe wino wa kielelezo cha upigaji vita wa madawa ya kulevya.
Kitendo kile cha jeshi la polisi kupuuza taarifa nyeti kama hizi ziliniacha mdomo wazi hadi leo na sijajua nini kusudi lake.
Je linawaogopa drug dealers? Lina maslahi binafsi(personal interest)? Jeshi lote hawakuziona barua zangu zaidi ya 48?
Bado natafakari!!
Shukrani A. Ngonyani,
February 10, 2015
Tanga,
ngonyani@naij.com/Sirngonyani@gmail.com
+255784 37 97 99.
UPDATES.......
Kuna wachangiaji wamedai niweke ushahidi wa vielelezo/barua nilizotuma ili waweze amini.
Nadhani na nafikiri tena upya kuweka hapa. Huenda huu ukawa mtego tu wa wahusika wajue kama majina yao yamo kwenye orodha au la.
Pia ifahamike kuwa mimi ni verified member hapa, natumia jina langu halisi sio kama wao na fake ID zao, pia nimeweka physical adress yangu na mawasiliano yangu hata namba ya simu, nimeweka original passport size yangu kama avatar, mwenye mashaka nami mimi nitamwekea mara tatu kwake.