Kanungila Karim
JF-Expert Member
- Apr 29, 2016
- 20,746
- 25,638
Wanawake wengi warembo/wazuri husalia peke yao na kufa katika hali hiyo kutokana na sababu tofauti.
Wengi huwa na tabia za kuudhi hali ambayo huwafukuza wanaume walio na uwezo wa kuwaoa.
Umewahi kushangaa sababu za wanawake warembo zaidi kutoolewa?
Umewahi kujiuliza Nani anataka kupanda miwa kwenye shamba karibu na shule?(sijui kama hiyo miwa itabaki salama na jopo lote la wanafunzi lililopo hapo shuleni)
Wanaume sio wajinga na katika asilimia kubwa ya wanawake wanaoolewa huwa ni waajabu sana ukiwaangalia kwa machoni kwa jinsi walivyo, mpaka unakuta wengine wanajiuliza, ‘huyu mwanaume mzuri hivyo anamuoa mwanamke ambaye hawaendani’.
Ukiwa mzuri utapndwa na wanaume wengi ila watakupenda kwa lengo moja tu, ‘Mapenzi’ baada ya hapo utakuwa wa kuchezewa na kuachwa.
Kuna sababu tano ambazo huwafanya wanawake warembo/wazuri kusalia wapweke.
- Tabia
- Baadhi ya wanawake hao huwa na maringo sana
- Ghali kuwatunza
- Wabinafsi na wenye chuki
Wasichojua ni kuwa wanaume huwatumia tu na kuwaacha kutokana na tabia zao ili kutafuta mwanamke mzuri wa kuoa.
- Hawataki kuwa wazazi
Kama una sifa za aina hiyo, huenda ni wakati wako kubadilika ikiwa unataka kupata mume.
