KENZY
JF-Expert Member
- Dec 27, 2015
- 35,797
- 86,566
Sio kwa sifa alizonazo.Nadhani point ni kuamini hivyo ni suala la sababu za kuamini, kama ingekuwa ni issue ya uthibitisho basi nadhani Mungu mwenyewe angefanya kila mtu amjue pasina shaka na hivyo kusingekuwa na wanaomkana na kutafuta uthibitisho.
Kwahiyo ni sahihi kusema hauamini Mungu kwa kuwa hauoni sababu za kuamini uwepo wake au hauoni nafasi ya Mungu kiasi cha kukufanya uamini kuwepo huyo Mungu, lakini haileti maana kusema et hakuna Mungu kwa sababu hakuna uthibitisho hasa ukizingatia pia kuwa uthibitisho haufanyi jambo liwepo au lisiwepo ndio maana unaweza ukashuhudia jambo kabisa ila ukakosa ushahidi wa kuthibitisha ulichokishuhudia.