S 300 air defense batteries

S 300 air defense batteries

Labda kwa sasa baada ya vurugu za kutaka kupinduliwa. kwenye sakata la hizo S-300 nchini Cyprus, Turkey, alienda kununua silaha za makombora ya surface to surface kutoka Israel pia alipeleka kwa siri marubani kadhaa wa ndenge za kivita wakafundishwe namna ya kuzibomoa hizo s-300. Isriaeli iliwafundisha namna ya kuzikwepa. Sasa sijajua kama Isreal alishindwa namna ya kuziingia ama la. Kwa hiyo inaonekana Turkey naye ni ndumila kuwili na mnafiki kama m-UK. Nadhani, Russia inatakiwa imchukulie kwa tahadhari sana Turkey.
Yeah nazungumzia kwa sasa,maana Kuna kipindi (nahisi mwaka juzi Kama sikosei) Turkey alitishia kuondoa Rada za Marekani Turkish PM Erdogan, in Iran, says NATO radar could be dismantled if needed (hizi zinaichunguza Iran 24/7)ambazo Israel pia hutumia taarifa zake kuichunguza Iran. Sijui mwishowe walimalizanaje

Urusi mwenyewe hamwaamini Uturuki 100% Kama ilivyo kwa US ndo maana walitaka kumpindua Erdogan wamweke kibaraka wao
 
Ila kumbuka huwa kuna kwa ajili ya Export na Kwa ajili ya matumizi ya Ndani. ZAa ku export haziwezi kuwa sana na za kutumia nyumbani. Hiyo iko hata kwenye Ndege. Usidhani ndege ambazo USA namuuzia Muisraeli ziko sawa na anazo tumia yeye hata kama ni Aina moja
Uko sawa mkuu, Ndo maana Israel akipokea ndege toka US huwa wazifumua wanaongeza vitu vyao wenyewe ili kuziongezea ufanisi ndo maana Kuna baadhi ya wachambuzi wanasema kwamba F-16 za Israel Ni Kali kushinda za Marekani mwenyewe.
Hata hii F-35 Israel ndo nchi pekee ambayo imepewa ruhusa na Marekani kuziongezea vitu vyao bila ya kuomba ruhusa toka kwa Lockheed Martin.
 
Mkuu uwe basi mara moja moja unajishughurisha kutafuta taarifa. Kule syria kuna S-200 ya enzi za USSR, hizo S-300.zimetoka wapi? Irani mwenyewe anazitafuta sana.
Acha kukurupuka mkuu kama unajisaidia kwenye kiza... Soma vizuri nilichoandika kuna sehemu nimetaja s300?... Au nxmsgdkandvdgskavsjs!?
 
Mkuu ni hivi,Cyprus alinunua hiyo mitambo ya S-300 toka Russia ili kuongeza ulinzi wake wa Anga dhidi ya Air power ya Turkey(Kipindi hicho Turkey na Cyprus walikua hawaelewani sijajua kwa Sasa kama bado Ni maadui).

Sasa baada ya Makubaliano ya Russia na Cyprus kukamilika kuInstall hiyo mitambo ndani ya Cyprus,Uturuki ikatishia kuivamia Cyprus na kuwaambia kwamba wakitaka hilo lisitokee bhas hiyo mitambo irudishwe ilikotoka (Russia).

Bhas Cyprus alichoamua ni kufanya Makubaliano na Ugiriki kwamba Cyprus iwape mitambo ya S-300 huku Ugiriki iwape Cyprus silaha nyingine tofauti na S-300.

Hivyo ndo Jinsi Ugiriki ilivyolamba Dili la kuipata S-300.

Huo mgogoro unaitwa Cypriot S-300 Crisis unaweza kuutafuta ukausoma mwenyewe zaidi.
Na nikwanini mfumo wa ulinzi wa makombora ya masafa marefu yaani S-300,S-400,S500 kutoka Russia wamagharibi wanauogopa Sana kwani una nn kikubwa mpaka uwatishe hivyo....kumbuka juzi Us katangaza yoyote atakayenunua mfumo huo wa ulinzi kutoka Russia atawekewa vikwazo Tena vikali inaonekana una nguvu za ziada hebu tudadavulie mkuu...
 
Haha!! Mkuu Marekani sidhani kama wameshindwa kutengeneza hizo engine za Urusi maana wangeweza kuingia mkataba na Russia wakatengeneza under license tatizo Ni gharama ya utengenezaji ndani ya USA ni kubwa Sana ukilinganisha na Bei anayonunua toka Russia. Congress nakumbuka wakati wa Obama walitaka kupitisha azimio la kusitisha ununuzi wa engine za Urusi ili Marekani waanze kutengeneza zao ikaonekana gharama zmya kununua Ni nafuu kuliko kutengeneza,sikujua tena ule mjadala uliishia wapi.

Mkuu hizo simulation hazikua labda za kutumia computer Bali ilikua ni mazoezi kamili ya kijeshi ambapo S-300 ziliwashwa kabisa (Kumbuka Ugiriki ana S-300 alizonunua toka Cyprus baada ya kua na mgogoro na Uturuki)

Pia wayahudi kwenye SEAD operation Ni wazuri Sana(fatilia Operation Mole Cricket 19)
Kama wewe unajinadi una uchumi mkuwa, ni nini ushindwe kutengeneza hizo Engen mwenyewe ikiwa unaweza...?

Tuachane na mambo ya Propaganda mkuu, kuna vitu vingine sio rahisi ku copy.
 
Kama wewe unajinadi una uchumi mkuwa, ni nini ushindwe kutengeneza hizo Engen mwenyewe ikiwa unaweza...?

Tuachane na mambo ya Propaganda mkuu, kuna vitu vingine sio rahisi ku copy.
Mbona Urusi alienda kununua warships toka kwa Wafaransa (deal likasitishwa baada ya ishu ya Ukraine),Ina maana yeye alishindwa kutengeneza zake?! France looking for warship buyers after cancelling Mistral deal with Russia
Egypt Buys Two French Warships Originally Built for Russia
 
Nimeipitia, kumbe Turkey mkorofi. Yaani anataka awe mbabe peke yake pale Middle East ndiyo maana alikuwa anashirikiana na Daesh kuidhoofisha Syria.

Turkey sio kama ni Mkorofi, bali Turkey ndio kama mpaka wa Asia na Europe na actually ni kama anaiunganisha Asia, East na West Europe
Historia pia inawabeba, ubabe wao ni wa muda tangu kile kipindi cha Ottoman Empire
 
Simulation siyo actual exercise; in most cases simulation inakuwa na 25-60% error. Kwenye issue za usalama hata 1% ni grave error ! Wafanye simulation zao wakimaliza waende Iran kujaribu kama wanaudhubutu.
Hii umetoa wapi mkuu?
 
Wakuu hivi kati ya s-300 s-400 s-500 na ile THAAD ipi ina nguvu sana?
Na ukiacha hiyo THAAD marekani wanao mfumo mwingine?
 
Back
Top Bottom