MINOCYCLINE
JF-Expert Member
- Apr 2, 2015
- 8,011
- 16,748
Tunafanana kila kitu na Rwanda kwa sababu hiyo wa Rwanda ndio ana rimoti ya wa hapa.Uko sahihi kabisa kwamba mawazo ya Kagame ndiyo yanayoongoza hata nchi yetu.
Jarida la Financial Times (FT) linaripoti kuwa baada ya uchunguzi wa muda mrefu limegundua kuwa nchi ya Rwanda imekuwa ikichakachua takwimu zake za umasikini nchini humo, ikumbukwe kuwa France24 ilisharipoti mwaka 2015 kuwa serikali ya Kagame inachakachua takwimu zake za uchumi.
Uchakachuaji mkubwa zaidi ulifanyika mwaka 2015 punde kabla ya kura ya maoni iliyomwongezea Kagame (ambaye alishakuwa madarakani kwa miaka 15) muda wa kukaa madarakani kwa miaka mingine karibu ishirini! katika mazingiza hayo Kagame alikataa katakata kukubali takwimu zilizo onesha kuwa umasikini unaongezeka nchini Rwanda.
FT pia lilichapisha kwa mara ya kwanza barua ya ndani ambayo wafanyakazi watano wa benki ya dunia waliwaandikia viongozi wa taasisi hiyo mwaka 2015, katika barua hiyo wafanyakazi hao walilalamikia kile walicho kiita "uchakachuaji wa takwimu na kushindwa kwa Rwanda kutoa data za uhakika kwa uwazi", pia waliendelea kuandika kuwa "kile kilichokua kinaendelea kilikua na hatari ya kuichafua heshima ya benki ya dunia ikiwa nchi ya Rwanda itaendelea na mchezo wake".
View attachment 1180958
My take: naona kila siku mambo yanazidi kujijidhihirisha kuwa ni wapi mheshimiwa wetu anachota 'idea' zake za ajabuajabu na zisizo za kitanzania.
Utaambiwa wewe ni mchocheziUnaficha umaskini kwa manufaa ya nani?Unasema uchumi unakua wakati hata Lori la mafuta likianguka watu wanakimbilia kuiba na wanakufa kwa mamia,kama sio umaskini ni nini?
Uko sahihi kabisa kwamba mawazo ya Kagame ndiyo yanayoongoza hata nchi yetu.
Wale ccm mpya watakuja kumtetea kagame swahiba wa jiwe
Naona ndugu yetu michombero wabongo wamekugusaWakati ukikimbilia kuwashwawashwa na mambo ya ndani ya Rwanda tunaomba pia utuhakikishie kama hata nchi yako ya Tanzania nayo haipiki data zake katika mambo yake mbalimbali ya Kimaendeleo. Ukiachia mbali hao Wazungu ambao hawajaanza Chuki zao na Rais Kagame leo ila kwa wenye Akili tunatambua kuwa Rwanda ya sasa chini ya Kagame imepiga hatua nyingi ukilinganisha na ilivyokuwa japo nakiri kuwa bado kuna Changamoto kadhaa za Kidemokrasia na Kisiasa ila Rais Kagame amejitahidi na yapo Maendeleo kadhaa utayakuta nchini Rwanda ambayo ilichafuka Kimapigano ( Mauaji ya Halaiki ) zaidi ya mara mbili katika Historia ambayo huwezi kuyakuta nchini Tanzania ambako wanajinasibu kuwa ni Baba wa Amani Afrika kama siyo duniani. Halafu ni Upumbavu uliopitiliza kila mara Kuhusisha Mapungufu ya Rais JPM Kiuongozi na Kisiasa na Urafiki wake na Rais Paul Kagame wa Rwanda. Kuna Watu mnajiita Wasomi lakini arguments zenu haziakisi hivyo na si ajabu ndiyo maana hata Elimu ya nchini mwenu ina Changamoto Kubwa kama siyo nyingi.
Nafikiri ushaanza kunisahau sasa,usikimbilie kwa Moderator tuu.Unazomwagiwa Kila Siku au?
tuuwie radhi ndugu yetu kutoka Rwanda, huku Tanzania tumeshazoea uhuru wa kutoa maoni na kusema ukweli hata kama utamuumiza kiongozi mkuu, wewe kama mnyarwanda nadhani huwezi kulitambua hilo kwa namna Kagame anavyowajaza propaganda.
Argument kuu hapa ni serikali ya kagame kupika takwimu ili kujinufaisha kisiasa na pia ili kuwapotosha nchi wahisani, kumbuka kuwa Rwanda ni moja ya wapokea misaada wakubwa zaidi barani Africa, kutokea 1994 benki ya dunia pekee imetoa zaidi ya dola bilioni nne kwa Rwanda.
anaiga vitu vingi sana kutoka kwa huyo jamaa, sijui hata usalama wetu ukoje kwa sababu kipindi cha JK ambapo tulikua tunawabana kiasi lakini bado kuna majasusi wa kinyarwanda walikua wanapenya hadi sehemu nyeti kabisa za nchi tena kwa muda mrefu, sasa hivi leo inawezekana hata hawajifichi wanarandaranda tu kwenye korido za jumba jeupe.
Wauwaji ya kimbari yaliyo tokea Rwanda hayaja wahi kutokea Tanzania na kamwe hayatakuja kutokea pamoja na changamoto nyingi tulio nazo.Bado hujajibu Hoja yangu na huenda haya Majibu yako yanathibitisha kuwa Wewe ni ' Kichwa Maji ' na ndiyo maana umenijibu Kitoto mno. Nakuuliza tena je hayo unayodai kuwa yanafanyika nchini Rwanda hapa Kwenu Tanzania hayafanyiki au hayajazoeleka? Hivi kuna kinachoweza Kufanyika nchini Rwanda halafu kiwe ama hakifanyiki au hakijawahi Kufanyika nchini Tanzania au katika nchi nyinginezo za Afrika? Na ni kwanini Urafiki wa Rais JPM na PK Kwenu nyie ni tatizo? Hata kama mnawasema kutokana na Changamoto zao je unataka kusema hakuna Mambo mengine mazuri na ya Kimaendeleo ambayo Tanzania inaweza Kuiga kutoka Rwanda na Rwanda inaweza Kuiga kutoka Tanzania? Nasubiri Jibu lako ili nizidi Kukudharau.
Naona ndugu yetu michombero wabongo wamekugusa
Utaambiwa wewe ni mchochezi
Kuficha taarifa za umaskini ndo uchochezi wenyewe
Nafikiri ushaanza kunisahau sasa,usikimbilie kwa Moderator tuu.
Wauwaji ya kimbari yaliyo tokea Rwanda hayaja wahi kutokea Tanzania na kamwe hayatakuja kutokea pamoja na changamoto nyingi tulio nazo.
Hivyo wala usipende kuilinganisha nchi yetu pendwa na Rwanda
Kurukaruka kwa maharage ndio kuiva kwake hukoHizo Mbili zako ulizozitaja hapo ndiyo zinamilikiwa na hao Mapolisi / Mapilato wako wa Jamvi uliowataja hapa au?
Kurukaruka kwa maharage ndio kuiva kwake huko
Ndugu yangu nakushauri uwe unasoma kwa makini. Nani kasema ujamaa? Tafadhari usiwe unaadika kama hujasoma tutakupuuza humu jukwaani.Mnalazimisha siasa za kijamaa hapa Tanzania kwenye kizazi hiki, lakini ukweli ni kuwa ujamaa sio formation inayoendana na mahitaji ya kizazi hiki. Hiyo kulazimisha ndio maana unaona nguvu kubwa zinatumika kulazimisha hali hiyo ikiwemo kuchezea box la kura ili kujaza wanaccm kwenye uongozi, watakaoungana mkono chochote atakacho Magufuli ambaye bado anaamini kwenye siasa za ujamaa. Ukweli ni kuwa siasa za ujamaa zilifail toka enzi za Nyerere, na siku Magufuli anatoka madarakani kesho yake asubuhi mambo yake mengi yatafutiliwa mbali.