Sijui kama mnakumbuka vizuri historia ya Tanzania. Kulikuwa na amani kiasi chake kabla ya Idd Amin Dadaa Nduli wa Uganda hajaanza fyokofyoko kwa Ng'walimu JKN. Kama kawaida Ng'walimu alimsikiliza tu kama hayupo hivi, akirusha kaneno kamoja kamoja. Amin akatafsiri hiyo kuwa ni udhaifu wa Tanzania. Alipoingiza kichwa kwenye ardhi ya Tanzania ndipo muziki mzito uliposikika na ndo ukawa mwisho wa Amin kuwa kibopa wa Uganda.
Somo wake Kagame naye anafuata nyayo pasipo kukumbuka ingawa alihusika na mambo ya Uganda kwa sana. Kile JK anachokisema mara moja moja kingemkumbusha Kagame. Lakini kafungua domo kama vile Kiboko majini anayedhani maji yota anaweza kuyakausha kwa kuyanywa. Tanzania wanazima adui kwa kumaliza chanzo cha adui na sio dalili za adui. Kaburu na Mreno wanaelewa sana hilo, japo damu za kitanzania zinapotea nyingi wakati wa zoezi hilo, na ingawa hatima yake ni kumaskinika zaidi kwa nchi. Kagame kuanza mzozo na Tanzania maana yake amechoka kuendelea kuwa mkubwa wa nchi yake na kuishi humo, anaisaka njia ya kuondokea kama Kaburu, Mreno na Amin walivyojipatia njia hiyo kwa mgongo wa Tanzania. Vita Kongo kweli haitaisha kama Rwanda na Uganda wapenda vita hawatasafishwa na kutakaswa kabisa. Hatima yake Tanzania itaendelea kujaziwa wakimbizi wa nchi hizo kuja kutuulia wafanyabiashara wetu na kupora mali asili zetu kwa mitutu nasi tubaki kulialia kila siku kwa kuuwawa kwetu.