Russia yatishia kujibu mapigo ya Marekani

Russia yatishia kujibu mapigo ya Marekani

wrong turn

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2013
Posts
438
Reaction score
170
Russia imeitahadharisha Marekani kuhusu mpango wake wa kupeleka mabomu 20 ya kisasa ya nyuklia kwenye kituo chake cha kijeshi nchini Ujerumani.
Msemaji wa Ikulu ya ya Rais wa Russia Kremlin.

Dmitry Peskov amesema hatua hiyo itavuruga mlingano wa kistratijia barani Ulaya na utajibiwa kwa hatua za kurejesha mlingano huo. Msemaji wa Kremlin ameongeza kwamba hiyo ni hatua nyingine hatari ya kuzidisha mivutano barani Ulaya. Amesema hatua hiyo haiwezi kuimarisha utulivu, kujenga imani na kuimarisha usalama barani Ulaya.

Msemaji wa ikulu ya Rais wa Russia hakusema ni hatua gani zitakazochukuliwa na Moscow iwapo Marekani itatekeleza azma yake ya kupeleka mabomu ya kisasa ya nyuklia kwenye kambi yake huko Ujerumani lakini shirika la habari la Interfax la Russia limenukuu maafisa wa jeshi la nchi hiyo wakisema kuwa yumkini Russia ikajibu hatua hiyo kwa kupeleka makombora yake mapya ya nyuklia ya Iskander-M katika eneo la Kaliningrad huko Ulaya mashariki kwenye mipaka ya nchi za Poland na Lithuania.



Chanzo: Irib
 
hyo Iskander ht sio tishio kwa america may b to europe coz ht David sling ya israel inaweza kuishoot down
 
hyo Iskander ht sio tishio kwa america may b to europe coz ht David sling ya israel inaweza kuishoot down

yeye analenga nchi za ulaya, Urusi ana makombola ya kupiga New york moja kwa moja, haihitaji kwenda kuyaweka sijui wapi, kombora ya kilomita 11,000 unazani zinapiga wapi?
 
yeye analenga nchi za ulaya, Urusi ana makombola ya kupiga New york moja kwa moja, haihitaji kwenda kuyaweka sijui wapi, kombora ya kilomita 11,000 unazani zinapiga wapi?

But kumbuka US ana missiles defenses ambayo inaweza kushoot down hayo makombora na ss hv anafanyia utafiti system ambayo itaweza kushoot down makombora yenye warheads nying km tsar bomb
 
Wataalamu wa Mabomu na Vita wa Kibongo wamekutana... Makamu wetu wa Raisi ni mwana fizikia nadhani mambo ya Uranium yupo njema so kuhusiana na Nuclear yupo njema aulizwe
 
Mpaka sasa ivi russia hajaweza ku balance nguvu za kijesh za marekani duniani.....marekani ana ma base karibia dunia nzima...sasa kama hadi nchi kama poland iko NATO we unategemea kun balance apo?....Izi mamboa us kaanza zaman sana toka kuanguka kwa soviet union miaka ya 90s....so russia kachelewa sana kuuau swala la ku balance geographical military power
 
Back
Top Bottom