Rushwa ni sehemu ya maisha yangu

Rushwa ni sehemu ya maisha yangu

chakufia nini

JF-Expert Member
Joined
Apr 14, 2015
Posts
692
Reaction score
456
Wadau,

Kwa kweli huwa siku zote nimejiandaa kisaikolojia kununua haki zangu kwani kwa mwendo wa Bongo hii unaweza ukafa huku unajiona.

Nikienda hospitali zetu hizi za serikali ili nipate huduma haraka inavyostahili lazima nikate kitu kidogo, nikienda TRA ili mambo yaende super lazima nikate, TANESCO ili waje mapema kuniwekea umeme home lazima nikate, yaani kila kona napokwenda huwa najiandaa na kafungu kidogo ka kukata ili mambo yaende maana nchi hii bila kumshika mtu mkono mambo hayaendi.

Pia na wale wote wanaoingia 18 zangu maeneo ya kazini kwangu,aisee, mwendo ni ule ule manake hata usipopiga wewe wakubwa zako watapiga tu na maisha yataendelea, ni bora nipige tu.

Siyo siri, Rushwa ni sehemu ya maisha yangu. Inanisaidia sana kuendesha maisha haya.

Ebo!

Chakufia nini..
 
Mtihani wa Darasa la saba uliupata kwa Rushwa, Ukafeli mtihani ukahonga ili kuingia shule ya "kulipia" umemaliza Form four ukafeli mtihani tena, Ukahonga ili usahihishiwe mtihani tena na tena ikaonekana umefeli hivyo UKAHONGA ili upate Cheti cha Form Ili UHONGE uingie Chuoni ukaomee Upolisi.

Umemaliza Upolisi kazi Ukapangiwa kituo ambacho mazingira yake hukuyapenda UKAHONGA ili upate Uhamisho. Ulivyopata uhamisho ukapangiwa mjini Ukaja UKAHONGA na kumbambikizia kesi Mtu ambae ulimnyang'anya Mke wake na hivyo UKAHONGA ili wamfunge.

RUSHWA IMEKUWA SEHEMU YA MAISHA YETU
 
Mtihani wa Darasa la saba uliupata kwa Rushwa, Ukafeli mtihani ukahonga ili kuingia shule ya "kulipia" umemaliza Form four ukafeli mtihani tena, Ukahonga ili usahihishiwe mtihani tena na tena ikaonekana umefeli hivyo UKAHONGA ili upate Cheti cha Form Ili UHONGE uingie Chuoni ukaomee Upolisi. Umemaliza Upolisi kazi Ukapangiwa kituo ambacho mazingira yake hukuyapenda UKAHONGA ili upate Uhamisho. Ulivyopata uhamisho ukapangiwa mjini Ukaja UKAHONGA na kumbambikizia kesi Mtu ambae ulimnyang'anya Mke wake na hivyo UKAHONGA ili wamfunge.

RUSHWA IMEKUWA SEHEMU YA MAISHA YETU

bila hivyo maisha hayaendi mkuu
 
Sadly ndio ukweli huo.. Usipotoa rushwa huduma hupati.. Wakati mwingine unalazamisha kutoa rushwa kuuruka urasimu..
 
Back
Top Bottom