Rushwa kwa watumishi ipo lakini kula kwa uangalifu usikamatwe

kavulata

JF-Expert Member
Aug 2, 2012
12,310
12,606
Kinachohalalisha kosa kufanyika ni kosa lenyewe na dhamira wakati wa kulitenda kosa. Kuna wakati rushwa inaombwa kwa nia njema ili mtumishi apate nguvu na moyo wa kutoa huduma.

Rushwa inapofusha macho na masikio ya wanaoidai, na wakati mwingine rushwa inafunga midomo ya wanaoipokea. Lakini kuna wakati rushwa inasababisha matokeo chanya kwenye utoaji huduma hasa pale inapoombwa ili mtu apate chunywa chai, apate nauli na kujia kazini , kulipa ada ya mtoto na kulipa pango la chumba.

Wakati mwingine mtumishi atalazimika kuomba na kupokea rushwa sio kwa kupenda wala hiari yake ila kama njia halali ya kupata chakula, ada ya mtoto, kodi ya pango, nauli ya kutokoa na kurudi kazini, kuhudumia gari, kurejesha deni la benk lenye riba kubwa, adhabu za road traffic, kufua uniform, nk.

Waziri husika sio mjinga hata kidogo, anahafamu viwango vya mishahara vya watumishi wake wote. Waziri hajui watumishi wake wanaishi wapi, umbali gani kutoka kazini na kwenye nyumba za kodi kiasi gani maana hakuna nyumba za watumishi, lakini anataka watumishi wanaowahi kazini, nadhifu na wanaochangamkia wateja wao.

Waziri hataki kufahamu mtumishi amekula nini (maana hata canteen hakuna), anakujaje na kuondokaje kazini maana hana usafiri kwa watumishi, hataki kujua kama mtumishi ana watoto wangapi na wanasoma wapi anachohubiri ni huduma safi iliyotukuka, ubaya wa kula rushwa na wizi wa vitendea kazi.

Mhudumu kwa hali hiyo lazima atafanya mambo yafuatayo wakati akisubiri siku ya kustaafu ya kustaafu kwake.

1. Atatoa huduma mbovu kwa wateja wake kutokana na njaa au msongo wa mawazo
2. Atadai au kupokea rushwa hata kama hataki
3. Ataiba vitendea kazi vya mwajiri wake
4. Ataiba muda wa mwajiri akifanyakazi binafsi za kujalizia upungufu.
5. Atajaa madeni mwili mzima kutoka kwa watu binafsi, taasisi za kukopesha, gengeni, shuleni, vyuoni, kwenye bucha, nk
6. Atajiuza mwili wake au kuingia kwenye biashara haramu
7. Ataacha kazi

Je, mtumishi afanye nini kama kipato cha ajira hakimtoshi kugharamia mahitaji yake ya msingi kabisa?

Ukiona mtumishi anapata mshahara mdogo lakini bado anafanyakazi hapohapo kazima mtumishi huyo ama anakula rushwa, mwizi wa mali za mwajili, mwizi wa muda wa mwajiri au anafanya vitu haramu.
 
Rushwa ni adui mkubwa wa haki,
usikubali kutoa Rushwa.
toa taarifa bure takukuru unapo ombwa rushwa ili hatua kali zichukuliwe.
tusikubali kuilea rushwa.
nashauri takukuru pambaneni na rushwa hadi ibaki historia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Rushwa ni adui mkubwa wa haki,
usikubali kutoa Rushwa.
toa taarifa bure takukuru unapo ombwa rushwa ili hatua kali zichukuliwe.
tusikubali kuilea rushwa.
nashauri takukuru pambaneni na rushwa hadi ibaki historia.

Sent using Jamii Forums mobile app
Thubutuu, hao takukuru hawana mahitaji yaliyokosa majibu? Takukuru hawataki watoto wao wasome shule nzuri, kulala pazuri, kuwa na usafiri, na kupata mlo kamili?
 
0987654.jpg
 
Thubutuu, hao takukuru hawana mahitaji yaliyokosa majibu? Takukuru hawataki watoto wao wasome shule nzuri, kulala pazuri, kuwa na usafiri, na kupata mlo kamili?
ndio maaana sio kila mtu tu anaweza kufanya kazi ya kuzuia na kupambana na rushwa, tunapaswa kuwa na watu waadilifu na wazalendo, Rushwa lazima itokomezwe bila kuoneana aibu. ina wezekana endapo wananchi wataamua kuwafichua wala rushwa ktk ofisi mbali mbali za serikali

Sent using Jamii Forums mobile app
 
ndio maaana sio kila mtu tu anaweza kufanya kazi ya kuzuia na kupambana na rushwa, tunapaswa kuwa na watu waadilifu na wazalendo, Rushwa lazima itokomezwe bila kuoneana aibu. ina wezekana endapo wananchi wataamua kuwafichua wala rushwa ktk ofisi mbali mbali za serikali

Sent using Jamii Forums mobile app
Hahaah, ndiyo maana hata ma professor wanakimbilia kwenye siasa ambako wanaweza kupata angalau nyumba ya kulala. Juzi nilipita kule Chanika nikakuta Prof aliyekimbilia kwenye siasa anamiliki nyumba na eneo ambalo anyebaki kwenye kufundisha isingekuwa rahisi kuvimiliki.
 
Hahaah, ndiyo maana hata ma professor wanakimbilia kwenye siasa ambako wanaweza kupata angalau nyumba ya kulala. Juzi nilipita kule Chanika nikakuta Prof aliyekimbilia kwenye siasa anamiliki nyumba na eneo ambalo anyebaki kwenye kufundisha isingekuwa rahisi kuvimiliki.
Rushwa haikubaliki kamwe kwa namna yoyote ile na ukibahatika kukamatwa hapo ndipo utajua rushwa ni tamu au chungu.
TAKUKURU iko macho kila kona ya nchi, mwananchi fichua vitendo vya rushwa popote ulipo ili hatua zichukuliwe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Rushwa haikubaliki kamwe kwa namna yoyote ile na ukibahatika kukamatwa hapo ndipo utajua rushwa ni tamu au chungu.
TAKUKURU iko macho kila kona ya nchi, mwananchi fichua vitendo vya rushwa popote ulipo ili hatua zichukuliwe

Sent using Jamii Forums mobile app
Rushwa haikubaliki lakini njaa inakubalika,
 
Kinachohalalisha kosa kufanyika ni kosa lenyewe na dhamira wakati wa kulitenda kosa. Kuna wakati rushwa inaombwa kwa nia njema ili mtumishi apate nguvu na moyo wa kutoa huduma.

Rushwa inapofusha macho na masikio ya wanaoidai, na wakati mwingine rushwa inafunga midomo ya wanaoipokea. Lakini kuna wakati rushwa inasababisha matokeo chanya kwenye utoaji huduma hasa pale inapoombwa ili mtu apate chunywa chai, apate nauli na kujia kazini , kulipa ada ya mtoto na kulipa pango la chumba.

Wakati mwingine mtumishi atalazimika kuomba na kupokea rushwa sio kwa kupenda wala hiari yake ila kama njia halali ya kupata chakula, ada ya mtoto, kodi ya pango, nauli ya kutokoa na kurudi kazini, kuhudumia gari, kurejesha deni la benk lenye riba kubwa, adhabu za road traffic, kufua uniform, nk.

Waziri husika sio mjinga hata kidogo, anahafamu viwango vya mishahara vya watumishi wake wote. Waziri hajui watumishi wake wanaishi wapi, umbali gani kutoka kazini na kwenye nyumba za kodi kiasi gani maana hakuna nyumba za watumishi, lakini anataka watumishi wanaowahi kazini, nadhifu na wanaochangamkia wateja wao.

Waziri hataki kufahamu mtumishi amekula nini (maana hata canteen hakuna), anakujaje na kuondokaje kazini maana hana usafiri kwa watumishi, hataki kujua kama mtumishi ana watoto wangapi na wanasoma wapi anachohubiri ni huduma safi iliyotukuka, ubaya wa kula rushwa na wizi wa vitendea kazi.

Mhudumu kwa hali hiyo lazima atafanya mambo yafuatayo wakati akisubiri siku ya kustaafu ya kustaafu kwake.

1. Atatoa huduma mbovu kwa wateja wake kutokana na njaa au msongo wa mawazo
2. Atadai au kupokea rushwa hata kama hataki
3. Ataiba vitendea kazi vya mwajiri wake
4. Ataiba muda wa mwajiri akifanyakazi binafsi za kujalizia upungufu.
5. Atajaa madeni mwili mzima kutoka kwa watu binafsi, taasisi za kukopesha, gengeni, shuleni, vyuoni, kwenye bucha, nk
6. Atajiuza mwili wake au kuingia kwenye biashara haramu
7. Ataacha kazi

Je, mtumishi afanye nini kama kipato cha ajira hakimtoshi kugharamia mahitaji yake ya msingi kabisa?

Ukiona mtumishi anapata mshahara mdogo lakini bado anafanyakazi hapohapo kazima mtumishi huyo ama anakula rushwa, mwizi wa mali za mwajili, mwizi wa muda wa mwajiri au anafanya vitu haramu.
Unayo nije nichukue?
 
Back
Top Bottom