Rugemalira aibua mapya, anataka kumtaja mwizi wa fedha za Escrow

Rugemalira aibua mapya, anataka kumtaja mwizi wa fedha za Escrow

Rwega; umeshashikwa na ngozi brother; kuchomoka kwako ni kugumu. Ule mzigo mkubwa mmmhhh ngoja tuone....
 
Ruge ameingiza mambo ya siasa katika upelelezi, tutatupa ushahidi wake
 
Mfanyabiashara James Rugemalira anayekabiliwa na kesi ya utakatishaji fedha ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa anahitaji kuonana na Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP) ili ampe ushahidi wa nani anayepaswa kukamatwa katika kesi hiyo.

View attachment 656763
December 8, 2017 Rugemalira aliieleza mahakama hiyo kuwa unahitajika ushirikiano baina yake na upande wa mashtaka ili kumbaini mwizi wa Sh.Bil 309 za Serikali.

Mbali ya Rugemalira, Mshtakiwa mwingine ni mmiliki wa IPTL Harbinder Singh Sethi ambapo kwa pamoja wanakabiliwa na mashtaka 12 ya uhujumu uchumi, utakatisha fedha na kuisababishia Serikali hasara ya USD 22, 198,544.60 na Sh.Bil 309.

Rugemalira ameyaeleza hayo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi baada ya Mwendesha Mashtaka wa Takukuru, Leornad Swai kudai upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika, hivyo anaomba ahirisho.

Baada ya kueleza hayo, Rugemalira alinyoosha mkono ambapo amesema kuwa anaushukuru upande wa mashtaka ulimchukua gerezani na kumpeleka Upanga kwa mahojiano na kumrudisha salama gerezani.

“Leo nimekuja na ushahidi, hivyo naomba nikutane na DPP ili niweze kumsaidia kumjua mwizi anayepaswa kukamatwa, kwani lengo letu ni kuonyesha kuwa tupo Innocent,” alieleza Rugemalira.

Kutokana na maelezo hayo, Hakimu Shaidi alimtaka Rugemalira kuwasiliana na mawakili wake ili waandike barua ya kuwasilisha kwa DPP kuhusu suala hilo la ushahidi wake, ambapo ameahirisha kesi hiyo hadi January 5, 2018.


Chanzo: Millard Ayo
Hapa JK na genge lake lazima waumbuke.
 
Seemaaa usiogopee semaaa
Huyo mzee Ruge asitupoteze na asijaribu kuvuruga kesi. Kwani alishindwa nini kuutoa huo ushahidi takukuru au mahakamani? Na kwani ni lazima aombe kibali cha mahakama kumwandikia dpp?
 
Back
Top Bottom