Ruge Mutahaba haya ni maoni kwako

Ruge Mutahaba haya ni maoni kwako

bomouwa

JF-Expert Member
Joined
Jun 19, 2014
Posts
1,149
Reaction score
800
Nimekua nikisikia jinsi baadhi ya wasanii wa muziki wa bongo fleva ambao wengi hatukatai kama kampuni ya clouds media group na ile ya zamani ya prime time promotion imefanya mengi hususani katika muziki huu wa kizazi kipya na kufanya wasanii wa kitanzania kutambulika saaana ndani na hata nje ya mioaka ya nchi, kwakweli kwa hapo nawapa hongera zao saana.

Lady jaydee ni mkongwe katika mziki wa bongo na mara kwa mara alikua akisikika akisema kua ananyonywa na watu wachache lakini pia katika kipindi cha mkasi Gadna alikiri kwakusema swala la Mke wake na clouds media group lingeweza kuzungumzwa lakini kimsingi hapa ni kwamba Ladyjaydee alichoka na manyanyaso ya uongozi hapa alimzungumzia Ruge na ilifika mahali Jide aliapa kabisa kua hata akifa basi clouds wasije piga nyimbo wala kuomboleza kwa namna yoyote ile na akaongeza hata msibani Ruge asije kuzika, ukitafakari ni maneno magumu na mazito.

Nimejaribu kutafakari juu ya maneno yaliokua yanasemwa juu ya diamond katika shoo yake ya fiesta pale leaders club ambapo alizomewa saaana na mashabiki waliosemekana wametumwa na watu fulani ambao hata hivo hawakutajwa, lakini wakati huohuo Ali kiba alishangiliwa mnoo na dhahiri ilionyesha wazi kuna jambo nyuma ya pazia linaendelea ambalo watu baki hatuelewi... Watanzania tunapenda kufata mkumbo na ndo maana hata hatujui mustakabali ya yale tuyafanyayo.

Diamond amekua balozi kwa nguvu na jasho lake mwenyewe na ubunifu hata kufanya tanzania ijulikane zaidi na ndo maana hata tuzo anapata kwa wingi maana kiukweli kabisa ANAJITUMA na kwa hilo anastahili pongezi nyingi na watanzania tumpe haki yake.

CLOUDS FM wameibuka kwa kumpa promo Ally kiba ya ajabu saana yaani kila dakika 5 lazima usikie tangazo lake kimsingi si jambo baya lakini hii yote inasemekana ni juhudi za kuuzima ufalme wa kijana Diamond maana wanasema amekataa kua chini ya menejiment ya Ruge na badala yake akamkubali babu tale swala ambalo sasa clouds wameamua kumkomoa na Dj fetty kwa kipindi fulani alisema hajui kelel za kumzomea diamond zilitoka wapi lakini wenyewe kwa wenyewe wanasema "bosi hamtaki hata kumsikia".

MY TAKE
Ruge kama hela unazo na ikumbukwe tu kwa imani zetu za dini Mungu hapendi chuki wala hapendi kabisa dhuluma na kama unataka maisha ya pepo basi watendee mema kama kweli unania ya dhati ya lkuendeleza vijana hawa katika tasnia ya mziki na Mungu atakubariki.

Ieleweke mimi simtetei mtu ila mtu mwenye juhudi na asaidiwe.
Nawasilisha
 
Nawapenda sn clouds lkn swala la jide na maneno.maneno ndio dah
 
acha tuunganishe DOT.
diamond.png
 
Kwl tumia akili kufikilia boss sasa ww unadhani watu waliokiwa wakimzomea diamond walitumwa na clouds ambao ndio waandaaji wa shoo za fiesta ilikuvuga shoo zao wenyewe hii pumba?

Pia unasema wamempa promo ali kiba ilikumkomoa diamond? Sasa ww unataka kiba asipewe promo kisa wana beef name diamond mbona pinna hujaiongelewa? Kwann watanzania hatutaki kusupport kitu kizuri yaan ni kudiss tu jipange mtoa maada
 
Kwani ukipanda ngazi ndio hushuki jamani??? eeh!!! hebu muacheni dimondi wa watu ajishukie zake ngazi kuwafuata kina mr. nice

Wapi nechaaaaaa, hapo ndo homu mpango mzima.

Tanzania ilitangazagwa na kina mchonga bwanaaaa!!! Hata matwiga nayo yanatupaisha daimondi wa nini, kama hujui richmond imetupaisha, dowans imetupaisha, na hiki kibao kinachopigwa kila siku na European Union Escrow usiseme, tuko juu ile mbaya hatuhitaji domo la daimondi.

OVER.
 
Mtu muongo utamjua tu.

Eti kampuni ya zamani Prime Time Promotion! Kwani hiyo kampuni imekufa? Kwa taarifa yako hao Prime Time Promotion ndo waandaaji wa Fiesta mpaka kesho.

Suala la kuwatoa na kutambulisha wasanii hata diamond na Davido waliunganishwa na Ruge Kwenye fiesta ya 2013 ndo akaenda kufanya kibao cha Number One Remix. Kusema ni juhudi zake tu ndo zimemfikisha pale bila kutambua mchango wa hawa watu ni unafiki mkubwa na kutokuwatendea haki.

Wewe utakua TeamDiamond hivyo roho inakuuma kila usikiapo sauti ya Kiba radioni. Ile ni Biashara hata Diamond akitaka promo analipia na kila dk2 utamsikia hewani. Hiyo ni Tour ya kiba na imelipiwa kwa hiyo usitake watu na kampuni zao wasifanye biashara kisa wewe na matim-Ushuzi yako.

Kama ulihudhulia pale Escape 1 wakati Diamond katoka kulamba tuzo 3 sauzi wala ungeleta huu upuuzi eti wanataka kuzika Ufalme wa Diamond. Diamond alisema hivi,' na mbali ya kupokea tuzo 3 bado nilisikitika sana kwani nilikua mpweke kila nikigeuka najikuta niko mtanzania peke yangu. Natamani wasanii wa tanzania wawe wengi kwenye jukwaa la kimataifa. Ili nikiwa nageuka hivi nawaona akina Linah, ally(kiba), n.k tafta youtube kwa maelezo zaidi. Sasa watu wanafanyia kazi ushauri wake nyie mbulukenge mnakuja hapa kuatama? Au mlitaka asikike peke yake ilhali yeye mwenyewe ashasema hapendezwi na ile hali?

Suala la kuzomewa umeliona kwenye Fiesta tu? Mbona juzi kati kwenye Tigo Kiboko yao concert iliyoandaliwa na tigo kwa kushirikiana na Ipp pale leaders alizomewa huwalaumu ipp? We utakua na chuki binafsi na clouds wala hamna kingine?

Ruge hasimamii wasanii ndugu. Labda unipe orodha ni wasanii gani wanaosimamiwa na Ruge. THT ina menejiment yake na yeye anabaki kama mlezi.. na huko wanadeal na wasanii wachanga pamoja na wale waliokulia pale. Sasa unaposema kuwa alitaka kusimamia kazi za mond huoni kuwa unaongopa mchana kweupe? Lini Tht ikaingia mkataba na wasanii wakubwa? Nipe hata mmoja ndo niamin hizi pumba zako. We una chuki binafsi.

Hao watangazaji wenyewe si ajabu hata hujawahi kuonana nao zaidi ya kuwaona kwenye magazeti ya shigongo. Eti hata wao wenyewe kwa wenyewe wanasema boss hamtaki? Wewe una uhusiano gani na mfanyakazi yoyowe pale alokwambia hayo au ni story za kwenye vijiwe vya kahawa? Huyohuyo Diamond anashinda THT anatumia vyombo vyao vya mziki sasa hayo kama sio majungu ni nini?

Hivi unaposema Diamond ni mbunifu, unaweza kunambia mziki wa Diamond na wasanii wa Tanzania kwa ujumla una ubunifu gani kuwafanya watu wa kimataifa waukubali? my namba wani ina ubunifu gani zaidi ya kukopi na kupest niondoko ya kinaijeria?

Mimi naamin Diamond ni msanii wa kimataifa(afrika) hivyo haitaji tena promo ya clouds kwani sio kampuni ya kimataifa. Na ndio maana hata yeye diamond haangaiki kulipia promo ya ndani.

Hizi promo za ndani waachie akina alli kiba na wenzie wajitangaze ndani watengeneze pesa ya madafu hapahapa ili wapate msingi mzuri wa kuja kupiga midolari ya kimataifa.

Tatizo la watanzania hatupendi ushindani. Mtu akipata changamoto ya ushindani ndo anaanza kutafta mchawi badala ya kukaza buti. Kama mnasema msanii ni wa kimataifa iweje mnalilia promo ya ndani? Au clouds inasikika Nigeria?
 
Back
Top Bottom