GE2025 RPC Marko Chilya: Hakuna anayeweza kuzuia uchaguzi

GE2025 RPC Marko Chilya: Hakuna anayeweza kuzuia uchaguzi

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

DuaZaMama

JF-Expert Member
Joined
Jun 2, 2025
Posts
1,882
Reaction score
4,129
Jeshi la Polisi Mkoani Ruvuma limewataka wananchi kujiepusha na vitendo vya vurugu au uhalifu kuelekea siku ya kupiga kura ya uchaguzi mkuu itakayofanyika Oktoba 29, mwaka huu.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma, SACP Marko Chilya, ametoa kauli hiyo katika mahojiano maalumu na mwandishi wa habari wa Bongo FM, kuhusu mikakati ya Jeshi la Polisi katika kuimarisha amani kabla na wakati wa uchaguzi.

RPC Marko amesema Jeshi la Polisi mkoani humo limejiandaa kuimarisha ulinzi na usalama huku akionya wale wanaofikiri kuwa wanaweza ‘kuzuia’ uchaguzi usifanyike.

Soma Pia: GE2025 - Kamanda Chilya: FFU si ‘Fanya Fujo Uone’, huo si utendaji wetu wa kazi

Chanzo: Bongo Fm
 
Policcm akisema hivyo maana yake ameshaandaa virungu na bunduki za kutosha za kupigia na pia kuulia watu. Kwa hiyo sisi wengine tumejiandaa kubakia zetu nyumbani huku tukifurahia wakati wetu vizuri.
 
So watatulazimisha kutoka majumbani na wanajua hata taarifa zenu hatuja updates tumeshapoteza uhalali wa kupiga kura
 
Anatetea ugali, na uzuri ametukuta watanzania sisi ni wanyonge, vizazi vijacho kauli kama hizi anajikuta kazungurukwa na wahuni
 
Policcm akisema hivyo maana yake ameshaandaa virungu na bunduki za kutosha za kupigia na pia kuulia watu. Kwa hiyo sisi wengine tumejiandaa kubakia zetu nyumbani huku tukifurahia wakati wetu vizuri.
Unaambiwa police wametengewa bajeti ya zaidi ya 400b kwa ajili tu ya kukabiliana na vurugu zinazoweza kutokea kipindi cha uchaguzi.

Just imagine, kodi ya mtanzania inatumika kukabiliana na mtanzania pale atakapojaribu ku exercise haki yake ya kikatiba...
 
Anatetea ugali, na uzuri ametukuta watanzania sisi ni wanyonge, vizazi vijacho kauli kama hizi anajikuta kazungurukwa na wahuni
Huu uchaguzi kuna maaskari watautumia kupandishiwa vyeo kwa kuua wanainchi... hili taifa lina laana
 
Kuna tofauti kati ya kuzuia uchaguzi na kuandamana kwa amani kama katiba inavyomtaka mtanganyika.
 
Unaambiwa police wametengewa bajeti ya zaidi ya 400b kwa ajili tu ya kukabiliana na vurugu zinazoweza kutokea kipindi cha uchaguzi.

Just imagine, kodi ya mtanzania inatumika kukabiliana na mtanzania pale atakapojaribu ku exercise haki yake ya kikatiba...
Nimeziona Toyota double cabin mpya (zero kilometer) za kutosha eti kwa ajili ya uchaguzi! Aisee haya mambo yanaogopesha mpaka basi. Kama kuna watu walikuwa wanambip, sasa ameamua kupiga.

NB:- Mwanamke siyo kiumbe wa kushindana naye!
 
Policcm akisema hivyo maana yake ameshaandaa virungu na bunduki za kutosha za kupigia na pia kuulia watu. Kwa hiyo sisi wengine tumejiandaa kubakia zetu nyumbani huku tukifurahia wakati wetu vizuri.

..virungu na bunduki vitatumika kupiga hewa.

..uchaguzi utakosa uhalali kutokana na idadi ndogo ya watu watakaojitokeza siku ya kupiga kura.
 
Na hakuna mtu anayeweza kulazimisha watu kupiga kura yaani vice versa is true
 
Policcm akisema hivyo maana yake ameshaandaa virungu na bunduki za kutosha za kupigia na pia kuulia watu. Kwa hiyo sisi wengine tumejiandaa kubakia zetu nyumbani huku tukifurahia wakati wetu vizuri.
halafu nyinyi ndio mange anawasubiria muingie rodini.....
 
..virungu na bunduki vitatumika kupiga hewa.

..uchaguzi utakosa uhalali kutokana na idadi ndogo ya watu watakaojitokeza siku ya kupiga kura.
mange anasema muwe barabarani saa 8 kamili mchana......
 
Back
Top Bottom