William J. Malecela
R I P
- Apr 27, 2006
- 26,584
- 10,464
Nakuhakikishia siyo King Maker, he is not learned, but bright and smart, anza kuamka wewe, mwamshe baba na mama ili waamshe chama uone moto utakao waka humo ndani. Jamaa ni habari nyingine, kama Mkulu anabow down kwa huyu jamaa, naamini unakokwenda one day, you will too.
Nakuhakikishia siyo King Maker, he is not learned, but bright and smart, anza kuamka wewe, mwamshe baba na mama ili waamshe chama uone moto utakao waka humo ndani. Jamaa ni habari nyingine, kama Mkulu anabow down kwa huyu jamaa, naamini unakokwenda one day, you will too.
Hili Riburushi kwa nini mnalionea aibu jamani?
Mnataka atutawale hadi kwenye familia zetu?Jamani inauma sana mi ngoja niende kwa bibi Swanga nampiga na kombora kali afie mbali atatunyanyasa mpaka lini?Kama mmeshindwa mi namloga.
Maneno mazito sana haya Mkuu nami nayaafiki kabisa.
Shisye nakuheshimu, naomba tuheshimiane, kwa vile hunijui, sikujui, our common denominator ni jamii forums, hizo interest zangu binafsi hapa ni zipi? Anipigie mimi simu kama nani?.
Pasco:
Nakuhakikishia siyo King Maker, he is not learned, but bright and smart, anza kuamka wewe, mwamshe baba na mama ili waamshe chama uone moto utakao waka humo ndani. Jamaa ni habari nyingine, kama Mkulu anabow down kwa huyu jamaa, naamini unakokwenda one day, you will too.
- Hapana, humsaidii wala kumkomoi anybody, soon utakuja kugundua the truth kwamba kuna somebody aliyewekeza kwenye kampuni ya Mwakyembe, halafu huyo huyo akakimbilia kwa Nchimbi, kumpa info sasa guess what Nchimbi akazifikisha kwa Rostam, matokeo yake zikatoka gazeti la Mtanzania, na sasa shujaa wetu Mwakyembe amepunguzwa nguvu, na ndio maana ya maneno unayoyaita mazito, Bwa! ha! ha! ha! in the end ni sisi wananchi ndio tutalipia Maneno mazito sana.
Respect!
FMES
Sichangii huu mjadala kwa nia ya kumtetea yeyote yule bali kutetea maslahi ya Tanzania na Watanzania. Hakuna ushahidi wowote wa Mwakyembe kuhusika na ufisadi dhidi ya Watanzania. Kuwa na share za thamani ya shilingi millioni 1 kwenye kampuni ambayo haijulikani lini itaanza usambazaji umeme kamwe siwezi kuuita huo kama ni ufisadi. Lakini kwa upande wa fisadi Rostam kishatufisadi Watanzania shilingi bilioni 240 (Kagoda 40 billioni na Richmond/Dowans bilioni 200) na juzi karibu ifikie bilioni 300 kama siyo Watanzania kusimama kidete kupinga ununuzi wa mitambo iliyochoka. Hilo la Mwakyembe kupunguzwa nguvu utalijua wewe na sijui huyo aliyempunguza nguvu ni nani na kafanya hivyo kwa faida ya Watanzania au ya mafisadi!!!mimi natetea maslahi ya Tanzania na Watanzania
Maneno mazito sana haya Mkuu nami nayaafiki kabisa.
Sasa kidogo na mimi ndio naanza kupata picha ya ugomvi wa King Maker na Dr. Harry. issue siyo conflict of interest ni conflict ya kimaslahi. wote wanamiliki kampuni za kufua umeme majina karbu yafanane. mmoja ana eneo hana mkataba. mmoja ana mkataba hana eneo.
kwa maoni yangu, wote ni mafisadi.
Da hii kali.
Kwa hiyo mtu akiwa na mkataba hana eneo, au ana eneo hana mkataba, then, ..kwa mujibu wa JF pundit, ana qualify kuwa fisadi!!
Hapa inabidi tuanze kufanya juhudi ya kujuzana kiswahili sasa..duh!
Kaazi kwelikweli
Heshima mbele,
Nimewaita wote mafisadi only in this particular case. Mwenye mkataba, ameweza kupata mkataba baada ya kuwahakikishia Tanesco kuwa analo eneo, kumbe hana!.
Mwenye eneo, amefanya 'inside trading' kwa kujua ukipata eneo, unapata mkataba, hivyo akakimbia kimbilia kuanzisha kampuni ya wazalendo na kukimbilia kutafuta eneo, na akapata, katika safari ya kufuatilia mkataba, ndipo aliposhangaa mkataba kapewa mwenye eneo.
Cha muhimu kwa mwananchi ni umeme wa uhakika, cha muhimu kwa mfanya biashara ni mkataba, kupata eneo,
Fweza itaongea. Na mwenye eneo asiye na mkataba afanyenye?. Dawa ni kupiga kelele for public sympathy.
Hicho kilio cha public sympathy sio ili wananchi wapate umeme, bali uwezekano wa kukosa ulaji. Ndio maana conclusion yangu, wote mafisadi.
Nakubaliana na wewe, 'between the two devils, choose the lesser' kwa vile ya dowans sasa ni wimbo, naomba nisiendeleze kuuimba utapanda chart mpaka utahit.Ukweli mbele,
Bado hoja yangu ipo palepale. Haijalishi nani ana mkataba au ana eneo au vyote viwili ( as I don't have a good background kuhusu contracts za huu mradi wa umeme wa nguvu za upepo), kinachonisumbua mimi ni kuhusu mitambo ya DOWANS na ni yupi baina ya hawa mabwana mwenye ka-historia ka ku-screw fedha za wavujajasho. Mradi huo wa Singida, wala haujaanza, na hata kama ni uwizi au ufisadi unawezaje kumkamata mtu kabla hajaiba?
Vilevile Dr. Harry, kama ulivyopenda kumwita, ameamua kumbana 'fisadi mwenzake' asitutie ktk hasara nyengine kwenye DOWANS, hili kwangu ni jambo la kheri, na sidhani kama hiyo nayo inaingizwa kwenye kapu la ufisadi.
- Anyways, ni maoni yako, ila ya kwangu ni kwamba Mwakyembe will never be the same, ile moral authority aliyokuwa akiongea nayo before haya hayajafichuliwa hatakuja kuwa nayo tena, hiyo ni political fact na hata yeye mwenyewe anajua hilo, sasa kilichoguswa hapo ni masilahi hasa ya taifa kwani waliomchokonoa unafikiri ni wajinga?
- - I respect the man na ninaamini kwamba sio fisadi na hakufanya kwa nia mbaya, lakini mbele ya jamii jina limepungua nguvu na hasa katika vita vya mafisadi, huwezi kupigana navyo huku ukiwa na hata harufu tu ya mis-appropriate, tulioumia ni taifa sio anybody na ndio maana hasa ya masilahi ya taifa, ingawa na wewe una the way ya kuyaona masilahi ya taifa, ila kwangu mimi masilahi ya taifa yameguswa kutokana na kumpunguza nguvu Mwakyembe, maneno ya kwamba yeye na Rostam originally walitaka kuanzisha kampuni moja, lakini Rostam akakataa kuwekeza hela zake, ndio kila mmoja akaamua kuanzisha kampuni yake na sasa wanagombea uwanja wa umeme Singida, huwezi kusema kwamba politically sio damaging kwa jina la DK, tena yanapotokea Chadema.
- - The damage is done, na sasa watakaolipia ni sisi taifa, yaani wananchi na hilo ndio hasa lilokuwa the goal ya mafisadi, that is how I see it lakini na wewe unaweza kuona tofauti ndio demokrasia at work.
Respect.
FMES
Sawa mkuu. Tupo pamoja.
Brother BAK long time upo salama ??Na Alfred Lucas
Mwanahalisi~Maslahi ya taifa Mbele
MFANYABIASHARA na mbunge wa Igunga, Rostam Aziz amesitisha uchapishaji magazetini wa taarifa yake ya kukana tuhuma za ufisadi.
Taarifa iliyokuwa inakwenda kwa njia ya tangazo, ilikuwa inakana kuhusika kwake na kampuni ya kufua umeme kwa njia ya upepo ya Wind East Africa Limited.
Kampuni hii inatuhumiwa kupora ardhi ya wananchi katika kijiji cha Kisasida, mkoani Singida na taarifa zinasema tayari watu wameanza kuhamishwa kwa nguvu kama inavyofanywa kwenye maeneo yenye migodi ya madini mbalimbali.
Taarifa zinasema uhamishaji watu kwa nguvu unafanywa kwa msaada wa Mkuu wa Mkoa wa Singida, Parseko Kone.
Hata hivyo, madai hayo yamekanushwa vikali na Kone akisema, "Mimi sijaenda huko na wala si kazi yangu kuhamisha watu. Kuna watu hapa wanafanya siasa na wanadhani kwamba mimi ni kikwazo katika kufanikisha malengo yao."
Alisema, kampuni zinazodaiwa kugombea eneo awali zilikuwa kampuni moja. "Hizi kampuni awali zilikuwa moja. Zimegawanyika kutokan na sababu zao binfasi," alisema Kone katika mahojiano na gazeti hili kwa njia ya simu.
Wananchi waliohojiwa katika eneo anapotaka kujenga mradi, wamesema kampuni ya Wind East Africa Limited haijawahi kuwalipa hata senti tano kama fidia.
Tayari kampuni ya Rostam imepewa mkataba na Shirika la Umeme nchini (Tanesco) kwa njia ya upendeleo. Wameingia mkataba bila kuwa na miliki ya ardhi.
Hata hivyo, katika taarifa yake aliyositisha uchapishaji wake, Rostam anamtuhumu mbunge wa Karatu, Dk. Willibrod Slaa kuwa anampakazia kwa kudai kuwa anamiliki kampuni ya Wind East Africa Limited.
Taarifa hiyo (MwanaHALISI inayo nakala), inasema anazushiwa na kwamba hahusiki na kampuni hiyo, bali imekuwa kawaida ya Dk. Slaa na washirika wake kumchafua yeye kwa kumpachika tuhuma zinazomhusisha na kampuni zilizokumbwa na kashfa za ufisadi.
Dk. Slaa anamtuhumu Rostam kuwa ni fisadi mkubwa, na kwamba ni mmiliki wa kampuni ya Kagoda Agriculture Limited iliyochota zaidi ya Sh. 40 bilioni kutoka Benki Kuu ya Tanzania (BoT). Hata hivyo, Rostam hajakana kumiliki Kagoda.
Rostam pia hajakana taarifa zilizohusu andishi la wakili wa Mahakama Kuu, Bhydinka Michael Sanze kuwa aliitwa na Rostam ofisini kwake 50 Mirambo, jijini Dar es Salaam , kusaini nyaraka zilizowezesha Kagoda mabilioni kutoka BoT.
Katika andishi hilo la wakili Sanze, Rostam anatajwa kuwa ndiye kinara wa mpango wa kuchota mabilioni ya shilingi kutoka Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ndani ya BoT akitumia Kagoda.
Ni katika andishi hilo ambamo Rostam anadaiwa kuwahusisha rais mstaafu Benjamin Mkapa, katibu mkuu wa zamani wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Philip Mangula na aliyekuwa Gavana wa BoT, Dk. Daud Ballali.
Wakili Sanze anaeleza kuwa Rostam, Peter Noni na Bered Malegesi walimthibitishia (yeye Sanze) kuwa Rostam alikuwa kwenye kikao ambapo Mkapa alitoa maelekezo kwa gavana Ballali kutoa fedha hizo kwa Rostam, kupitia Kagoda, kwa ajili ya shughuli za uchaguzi ndani ya CCM.
"Rostam mwenyewe alisema, ‘system yote inajua,'" anaeleza Sanze. Hata katika taarifa aliyotaka ichapishwe katika vyombo vya habari, Rostam hakukana Kagoda.
Akizungumza kwa njia ya simu kutoka Karatu juzi, Dk. Slaa alisema ana uhakika kampuni ya Wind East Africa Limited ni mali ya Rostam akishirikiana na aliyekuwa waziri mkuu, Edward Lowassa.
"Sikiliza bwana. Hii ni kama Kagoda. Kwenye nyaraka za usajili hakuna wanapoonekana. Lakini katika baadhi ya nyaraka nilizonazo, wanaonekana wamesaini vitu mbalimbali na kutumia anuani ya kampuni ya Rostam wakati wa kusajili.
"Nawasubiri wakane. Nitawaumbua maana nimejiandaa kikamilifu. Mimi si mtu wa kukurupuka na Rostam anajua hivyo," anasema Dk. Slaa.
Anasema bado anaamini kuwa hakuna mgongano wa maslahi, isipokuwa ufisadi unaofanywa na Rostam Aziz na rafiki zake, wakisaidiwa na mkuu wa mkoa wa Singida.
Dk. Slaa anasema akina Rostam wanataka kuzalisha umeme wakati hawana eneo. "Hicho ndicho chanzo cha ugomvi wao na Dk. Mwakyembe (Harrison Mwakyembe, Mbunge wa Kyela)."
Alisema, "Nimekwenda Singida. Naufahamu vema mradi unaodaiwa. Nimeongea na wanakijiji Singida na viongozi wao. Kina Mwakyembe wanataka kuwakomboa wananchi, lakini kina Rostam wanataka kuwakandamiza.