Romney asema Donald Trumph ni tapeli

faure

Member
Jan 25, 2016
12
2
Aliyekuwa mgombea urais wa marekani kwa tiketi ya Chama cha Republican katika uchaguzi mkuu wa Mwaka 2012 Mitt Romney amesema Donald Triumph ni tapeli anayetaka kuingia ikulu ya white house.

Romney ameonya ikiwa Republican itampitisha Mfanyabiashara huyo kuwania urais itakuwa ni sawa na kumpa tiketi Hillary Clinton kushinda urais wa Marekani.

Romney amesema atatoa hutuba ametoa hotuba kali alhamisi ya leo na kusema sera za Triumph ni kitisho kikubwa kwa Republican na Marekani kwa ujumla.

akijibu shutuma za Romney, Trump amesema Mitt Romney ni mtu aliyefeli na hafai kutoa ushauri wowote kuhusu uchaguzi.

Uchaguzi mkuu wa Marekani unatarajiwa kufanyika mwezi Novemba.


Chanzo: BBC
 
Tatizo hao ndio wale watu walio athilika na siasa
Na trump alisha sema huu wakati wa dunia kuongozwa kwa ukweli kwasababu siku zote siasa ndio zinaleta matatizo.
 
Tatizo hao ndio wale watu walio athilika na siasa
Na trump alisha sema huu wakati wa dunia kuongozwa kwa ukweli kwasababu siku zote siasa ndio zinaleta matatizo.
Hivi umemfuatilia kweli Trump, au unapata tu habari za vijiweni. Mara nyingi simkubali Romney. Lakini alivyomweleza Trump kwenye hotuba hii ni kweli kabisa.
 
Hivi umemfuatilia kweli Trump, au unapata tu habari za vijiweni. Mara nyingi simkubali Romney. Lakini alivyomweleza Trump kwenye hotuba hii ni kweli kabisa.
Kama huo ni ukweli alikuwa wapi kuuongea siku zote hadi ametegea ameshindwa ndio aanze kuongea hivyo. Mara nyingi watu walio shindwa wanakuwa na maneno mengi sana.
 
Kama huo ni ukweli alikuwa wapi kuuongea siku zote hadi ametegea ameshindwa ndio aanze kuongea hivyo. Mara nyingi watu walio shindwa wanakuwa na maneno mengi sana.
Kwamba amechelewa kuongea haiondoi ukweli wa anachosema. Msikilize tena utaona kwamba shutuma za utapeli ni za kweli, kwamba hana mpango wowote anaouweka hadharani kudhihirisha atafanya nini ni kweli, kwamba ana matusi ya nguoni na lugha isiyomstahiki kiongozi wa juu ni kweli, kwamba anapalilia ubaguzi ni kweli fuatilia madai yake juu ya Wamexico na Waislamu, kwamba hana mpango wa diplomasia na kwamba atalipua nchi na kubeba maliasili zao ni kitu ambacho ameahidi. Na kwa hakika sidhani kama Romney ataivuruga momentum ya Trump. Trump atakibomoa chama chao.
 
Kwamba amechelewa kuongea haiondoi ukweli wa anachosema. Msikilize tena utaona kwamba shutuma za utapeli ni za kweli, kwamba hana mpango wowote anaouweka hadharani kudhihirisha atafanya nini ni kweli, kwamba ana matusi ya nguoni na lugha isiyomstahiki kiongozi wa juu ni kweli, kwamba anapalilia ubaguzi ni kweli fuatilia madai yake juu ya Wamexico na Waislamu, kwamba hana mpango wa diplomasia na kwamba atalipua nchi na kubeba maliasili zao ni kitu ambacho ameahidi. Na kwa hakika sidhani kama Romney ataivuruga momentum ya Trump. Trump atakibomoa chama chao.
Hadi trump ameshinda kwenye hayo majimbo 7 inamaana wamarekani wengi wameulewa anamaanisha nini. Na wamemuona anafaa kuwa rais lakini hizo zingine ni propaganda tu
na hazita wafikisha popote.
 
Hadi trump ameshinda kwenye hayo majimbo 7 inamaana wamarekani wengi wameulewa anamaanisha nini. Na wamemuona anafaa kuwa rais lakini hizo zingine ni propaganda tu na hata na hazita wafikisha popote.
Nikueleweshe kidogo. Sasa hivi wanatafuta mgombea wa chama chao. Na si kwamba Wamarekani wanapiga kura sasa hivi. Yapo makundi makuu matatu ya watu: Democrats, Republicans na Independent. Hicho unachokiona ni ktk Republican anaonekana kwenda kwenye ushindi wa kuwakilisha chama chake. Sasa je, makundi hayo mengine mawili yatamkubali? Isitoshe, inaeleweka kwamba chama cha Republicans wamekuwa wakijikita kwenye sera za kibaguzi. Jambo hilo ndilo lililowanyima ushindi wa uraisi 2012. Democrats nao wanaendelea kutafuta mgombea wao, naamini utakuwa umesikia. Sanders na Clinton wanachuana. Ktk kura za maoni, inaoneka wote wawili wanamshinda Trump.
Nasikitika kuona Wabongo wengi wanadhani huu ni ushabiki tu wa kimpira badala ya kutafuta habari kamili zenye kuaminika.
 
Nikueleweshe kidogo. Sasa hivi wanatafuta mgombea wa chama chao. Na si kwamba Wamarekani wanapiga kura sasa hivi. Yapo makundi makuu matatu ya watu: Democrats, Republicans na Independent. Hicho unachokiona ni ktk Republican anaonekana kwenda kwenye ushindi wa kuwakilisha chama chake. Sasa je, makundi hayo mengine mawili yatamkubali? Isitoshe, inaeleweka kwamba chama cha Republicans wamekuwa wakijikita kwenye sera za kibaguzi. Jambo hilo ndilo lililowanyima ushindi wa uraisi 2012. Democrats nao wanaendelea kutafuta mgombea wao, naamini utakuwa umesikia. Sanders na Clinton wanachuana. Ktk kura za maoni, inaoneka wote wawili wanamshinda Trump.
Nasikitika kuona Wabongo wengi wanadhani huu ni ushabiki tu wa kimpira badala ya kutafuta habari kamili zenye kuaminika.
Hata kwenye hizo kura za maoni bado trump amepiga hatua kwasababu kunawatu wameshindwa vibaya na ndio hao hao wanao mpiga majungu.
 
Hata kwenye hizo kura za maoni bado trump amepiga hatua kwasababu kunawatu wameshindwa vibaya na ndio hao hao wanao mpiga majungu.
Ni kweli anapeta ukilinganisha na republicans wengine. Na hao unaowaita wapiga majungu wamechelewa kutambua jinsi gani yeye ana mvuto mkubwa kwa watu fulani. Wachunguzi wengi wanasema kwamba Trump ni Frankestein ambaye republicans walimuumba na sasa ameamka anawaumbua. Wanavuna walichopanda. Republicans wamekuwa bize kuwakashifu na kuwashambulia wahamiaji, wamekuwa bize kuwashutumu Waislamu, wamekuwa bize wakishambulia watu wanaodai haki, wamekuwa bize kupinga jitihada zote za kukabiliana na majanga ya mazingira na mabadiliko ya tabianchi, wamekuwa bize wakiwabeza wanasayansi na wataalamu wa fani mbalimbali, wamekuwa bize kuzuia serikali isiweze kufanya kazi hasa wakati huu wa Obama, wananchi wengi wamepata picha kwamba serikali (ambayo republicans wameapa kuikwamisha kila kona) haifanyi kazi. Haya mambo yamekaa vichwani mwao, na sasa wanataka mtu ambaye anasema yote hayo kwa nguvu zaidi. Kwa hivyo wanawataka watu ambao wako nje. Trump anafit hiyo profile kwa sababu hajafanya kazi serikalini. Alichokifanya Romney sidhani kama kitasaidia kumzuia Trump. Ni ukweli tu. Wanaompenda Trump hawajali kabisa sababu zilizotolewa na Romney. Nilichosema hapo mwanzo ni kwamba Romney kasema ukweli kabisa (kama kachelewa kusema au la haipunguzi ukweli). Unapochunguza habari hizo, usifanye ushabiki kama vile Trump ni mtu wa timu yangu ya Yanga au Manchester. Angalia hoja. Na wala usiingie kwenye mtego wa kumshabikia mtu kwa sababu ya tamko moja. Mwangalie kwa ujumla wake. Kwa ujumla wake, Trump hafai kabisa. Ni mtu hatari sana. Kama dunia iliingia kwenye misukosuko wakati wa Bush Jr, itakuwa mara mbili yake endapo Trump atakuwa raisi.
 
Back
Top Bottom