ChoiceVariable
JF-Expert Member
- May 23, 2017
- 43,076
- 49,780
Akina mama na nyie msipende kulea Watoto kimayai hasa wa kiume maana walikuwa na maisha yakawagomea wanakata tamaa na kuingia kwenye vitu vya ajabu ajabu mwisho wanakuwa hatari sana Kwa usalama wa wazazi.
Kwa Watoto wa kike sana sana watakuwa Malaya ila hawawezi kufikia hatua ya kuwa makatili kama wanaume.
----
Kikulacho ki nguoni mwako, hivyo ndivyo unavyoweza kusema baada kijana mwenye umri wa miaka 26, mkazi wa Kijiji cha Lessoroma, Wilaya ya Rombo mkoani Kilimanjaro, Deogratius Shirima kwa kudaiwa kumuua mama yake mzazi kwa kumkata shingo wakati akimzuia asibomoe nyumba.
Tukio la kuuawa kwa mwanamke huyo, Doris Shirima (51) lilitokea Septemba Mosi mwaka huu na kuzua taharuki kwa wakazi wa kijiji hicho cha Lessoroma na maeneo ya jirani.
Kijana huyo ambaye anadaiwa kuwa ni mvutaji bangi, kwa mara kadhaa amekuwa akimsumbua mama yake ambaye ni mjane kwa kubomoa nyumba yake anayoishi na kumfanya mama yake huyo kurekebisha nyumba mara kwa mara.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Yahaya Mdogo amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo amesema limetokea Septemba Mosi mwaka huu na kwamba kijana huyo alimuua mama yake kwa kumpiga na kitu chenye ncha kali sehemu za shingoni na kichwani na kusababisha kifo chake.
"Ni kweli tukio hili limetokea huko Kijiji cha Lessoroma wilayani Rombo Septemba Mosi saa tatu usiku, mwaka huu huko Kijiji cha Lessoroma ambapo mtoto mwenye umri wa miaka 26 alimuua mama yake mzazi kwa kumkatakata na kitu chenye ncha kali maeneo ya shingoni na kichwani na kusababisha kifo chake," amesema.
Aidha Kamanda Mdogo amesema tayari Jeshi la Polisi linamshikilia mtuhumiwa huyo kwa kuhusika na mauaji ya mama yake.
Chanzo: Mwananchi
My Take
Vijana bangi na pombe sio chani hasa kama una maisha magumu ,hupelekea maamuzi ya ajabu ajabu.
Kwa Watoto wa kike sana sana watakuwa Malaya ila hawawezi kufikia hatua ya kuwa makatili kama wanaume.
----
Kikulacho ki nguoni mwako, hivyo ndivyo unavyoweza kusema baada kijana mwenye umri wa miaka 26, mkazi wa Kijiji cha Lessoroma, Wilaya ya Rombo mkoani Kilimanjaro, Deogratius Shirima kwa kudaiwa kumuua mama yake mzazi kwa kumkata shingo wakati akimzuia asibomoe nyumba.
Tukio la kuuawa kwa mwanamke huyo, Doris Shirima (51) lilitokea Septemba Mosi mwaka huu na kuzua taharuki kwa wakazi wa kijiji hicho cha Lessoroma na maeneo ya jirani.
Kijana huyo ambaye anadaiwa kuwa ni mvutaji bangi, kwa mara kadhaa amekuwa akimsumbua mama yake ambaye ni mjane kwa kubomoa nyumba yake anayoishi na kumfanya mama yake huyo kurekebisha nyumba mara kwa mara.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Yahaya Mdogo amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo amesema limetokea Septemba Mosi mwaka huu na kwamba kijana huyo alimuua mama yake kwa kumpiga na kitu chenye ncha kali sehemu za shingoni na kichwani na kusababisha kifo chake.
"Ni kweli tukio hili limetokea huko Kijiji cha Lessoroma wilayani Rombo Septemba Mosi saa tatu usiku, mwaka huu huko Kijiji cha Lessoroma ambapo mtoto mwenye umri wa miaka 26 alimuua mama yake mzazi kwa kumkatakata na kitu chenye ncha kali maeneo ya shingoni na kichwani na kusababisha kifo chake," amesema.
Aidha Kamanda Mdogo amesema tayari Jeshi la Polisi linamshikilia mtuhumiwa huyo kwa kuhusika na mauaji ya mama yake.
Chanzo: Mwananchi
My Take
Vijana bangi na pombe sio chani hasa kama una maisha magumu ,hupelekea maamuzi ya ajabu ajabu.