KOMBORA KIOTANI-13
BONIFACE BIRAGE
“Kivipi?”
“Mazungumzo yote hatuwezi kutrace hiyo namba.Anatumia secured line!”
“Ina maana hakuna IT anayeweza kuidhibiti hiyo namba?Simu itaingiaje ikulu bila kutrace huo ni upuuzi!”Kilua akawa mkali sana.
“Mheshimiwa hawa watu wanajificha sana.Yaani hata rekodi ya mazungumzo hatuwezi kuipata!”
“What?”Kilua akashtuka zaidi.Kabla hajafanya mengi akaingia mtumishi mwingine akaleta bahasha kwa mheshimiwa rais.Ile bahasha Kilua aliipokea nakuifungua akakutana na picha iliyomtisha sana!Mumewe alikuwa kafungwa kamba pamoja na mwanaye!Kilua alihis kupotea akili!
Walinzi wake waliona jambo lile wote waka taharuki familia ya rais ilikuwa imetekwa!Walinzi walikuwa na wakati mgumu kwani punde tu Kilua alipoapishwa kuna kikosi kilitumwa mahususi kuwalinda familia yake lakini mpaka sasa hawajapata mrejesho ni vile hawakuwa wameuliza.Huo ulikuwa uzembe kwa sheria zao!Kila mmoja alijiandaa kukabiliana na lawama.
“Mheshimiwa tutawatafuta popote walipo watapatikana.”alijaribu moja ya walinzi wale.
“Kwanza sitaki mtu yeyote ajue kwamba familia yangu imetekwa hicho sitaki kijulikane kabisa.Kufanya hivyo ni kuwahatarisha.”alisema akijikaza asiangushe machozi.
“Mheshimiwa lak…”
“Hakuna wakujua kama mume wangu na mwanangu katekwa.Hiyo ni oda!”alisema mheshimiwa rais.
“Lakini.”alitaka kusema kitu Yule wakala wa mawasiliano.
“Hii ni binafsi nisingependa litumike kama ajenda kwa taifa.Tayari tuna matatizo mengi hili litagusa pabaya.”
“Ok mheshimiwa tuambie unachojua kuhusu utekaji huu.Maana wewe pekee ndo umeongea na mtekaji.”aliuliza kiongozi wa ulinzi.
“Siwezi kusema lolote lakini maelezo yote nitatoa mwenyewe.Yoyote anayechezea familia yangu anajua anachokifanya ni kama ameniweka kiganjani.Siamini yeyote.Jana tu ananitajia hadi majina ya watu niliokaa nao mkutanoni!Hadi nguo nilizovaa!”Kilua ni kama alitaka kulia lakini akajikaza tu!Walinzi wakagundua mwanamke huyu anapitia kipindi kigumu sana.Umepewa nchi ghafla unakutana na hali ngumu bado familia yako imetekwa.Hakika ilihitaji ujasiri wa hali ya juu.
“Mheshimiwa tutampata huyu asidi.Wameigusa familia ya kwanza.”walijaribu kumhakikishia uimara wao katika kushughulika na hali kama zile.
“No.Msifanye chochote familia yangu ipo hatarini hata siamini kama ikulu ni sehemu salama kwa upande wangu.”
Walinzi walibaki kimya.Lilikuwa tukio la kufedhehesha na lazima hatua zichukuliwe haraka iwezekanavyo.
“Narudia tena nawapa amri hakuna wakujua habari hii zaid yenu.Nahitaji kujua adui aliyepo ikulu ni nani?”Kilua alisema akijikaza kulia.Ina maana nyendo zake zilikuwa zinakaguliwa kw asana.Walinzi walimwelewa.
“Nahitaji mpelelezi makini aweze kujua ni nani aliyefanikisha mume wangu na mtoto wa tekwe.”alisema Kilua akiwa anamaanisha kwa umakini.Walinzi walisikitika kila mmoja akipandisha hasira nakuapa wakimkamata huyo aliyeiteka familia ya rais basi hatakuwa na msalia mtume nikumfutilia mbali.Lazima baadae watajadiliana maana wao ndo watakaoulizwa kuhusu tukio ilo la kutekwa kwa familia ya rais.
“Mheshimiwa tumepokea agizo lake tutalifanyia kazi tutakagua kila eneo hadi tujue.Lakini kama huamini vikosi vya taifa basi tutaomba sisi wenyewe tufuatilie jambo hili tutawatuma watu wafanye ukaguzi na kweli tutampata mumeo.We are the best on this issue.”alisema chifu Ditu kiongozi wa ulinzi wa rais.
“Naomba usiri katika hili.”
“Hapana mheshimiwa hutakiwi kutuomba umeshatoa oda na sisi tunafuata oda tu.”Ditu alisisitiza.Kabla hajatoka akasema.
“Kuna file nalitaka.”
“Kama ni mambo ya siri kuna mtu wa kushughulika nalo.”alisema Dittu.
“Nani?”
“Katibu mkuu.”
“Namtaka ofisini kwangu haraka iwezekanavyo.”
“Alikufa kwenye tukio la jana.”sekretari alisema.Kilua akasugua kichwa.Palepale akamgeukia sekretari.Uzuri Serambovu hakuwepo hapo alikuwa ametangulia chumba cha mkutano.
“Nani anaweza kunipa hilo file?”
“Mimi nina uwezo huo.”alisema sekretari Sada.
Kilua aliwapa ishara walinzi wake wampishe.Walitii nakutoka nje,Kilua akabaki na Sada mule ndani,”Nataka file namba 13:14”
Sada alishtuka sana!Alibadilika ndani yamuda mfupi nakuonesha hofu ambayo hata Kilua aliweza kuiona,”Kuna nini Sada?”
Sada alizunguka pale ofisini huku akiwa kwenye mawazo mazito sana.Kitu hicho hakutaka aulizwe kabisa au kiangukie kwenye uamuzi wake kwamba kipo wapi.Alitamani katibu mkuu angekuwepo pale ajibu hayo mambo lakini sio yeye.
“Sada kuna kitu gani ambacho unaogopa kunitajia hilo file nimeomba nipewe kwani kuna ugumu gani?”
“Mheshimiwa naomba niache kazi tafadhali sana.”alisema Sada akiwa na wasiwasi sana.
Kilua akazidi kupatwa na hofu,”Uache kazi wakati nafikiria kukuteua kuwa katibu mkuu?”
“Hapana hilo file limeteketeza watu.Kila aliyetaka kuingilia amekuwa akiishia pabaya.Makatibu takribani watatu walipoteza nafasi zao kisa hilo file!”
“Hebu niambie vizuri?”habari ilimteka Kilua kusikia kwamba file nambari 13:14 lina kiza kinene.
“Ilianza awamu zilizopita kila aliyetaka kugusa hilo file alidhibitiwa sana.Hata rais Kisusi jambo hilo lilimpa wakati mgumu sana.Wakati alipotaka kuingilia ndo ikaja taarifa kauawa kwenye maonesho ya uhuru.”
Kilua akawa anameza yale maelezo,”Kwani hilo file lina nini hadi rais asiweze kuliingilia?”aliuliza Kilua.Huku akijaribu kukumbuka vitisho vya Yule bwana aliyemwambia anajua hadi watu aliokaa nao mezani.
“Hilo file sijabahatika kuliona.Kulipata linahitaji password ya katibu mkuu au sekretari halafu ifuate ya rais.Lakini Theory inayolizunguka siielewi yasemekana uongozi uliopita ndo wenye hiyo password na mpaka uombe hiyo password ndo uweze kulifungua.Theory pekee ninayoiamini ni ya kwamba viongozi wa awamu Fulani ndo walianzisha hilo file na ajenda halisi ya file hilo tatizo ni kwamba wao wenyewe hakutaka kabisa file hilo liguswe na uongozi ujao.Hivyo likawekewa password na jina pekee linalotambulika kuhusu file hilo ni hiyo namba 13:14.”aliendelea kuchuja nakupembua mwana Sada.
“Linaweza kuwa nini?”
“Ni kama mkataba wa kitu Fulani cha siri sana.Mara kadhaa nilimsikia rais Kisusi akizungumza hilo jambo.Lilimsumbua sana na kila alipotaka kutupia jicho alipata vizuizi vingi!”
“Mhh.”aliguna Kilua tafakari ikiwa ngumu kuelewa.
“Kwani mheshimiwa imekuwaje?Nilifarijika sana nilipojua unachukua madaraka nikajua hakuna atakayekuja na ajenda ya hili file na mambo yataenda kawaida.Lakini siku ya kwanza tu ofisini umeanza kuulizia hili file.Au ndo maana familia yako imetekwa?”aliuliza Mwana Sada.Kilua alitikisa kichwa haikujulikana kama alisema ndio au hapana.Lakini tayari kapokea maelezo mazito kuhusu file nambari 13:14.Sasa ameanza kuunganisha doti zote hadi ajue hilo file lina umuhimu gani kiasi cha kusababisha familia yake iingie kwenye majaribu makubwa sana.Wakati anawaza hilo simu tena ya ofisini kwake.Akaipokea.
“Ni rais wa Savanna Lands natumai una majibu ya wapi balozi wangu yupo?”
“Mheshimiwa sina jibu la kuridhisha kuhusu balozi wako.Kupotea kwake sijui kitu chochote kile.Wewe ndo mwenye majibu sahihi.”Kilua alizungumza kwa ukali kidogo.Habari ya file lile ilimnyima hadi amani yake akiwaza mwanae na mumewe na tayari kuna tishio kubwa la ndani.
“Mheshimiwa kwa heshma zote nataka balozi apatikane la sivyo nitachukua hatua ikiwezekana majeshi yangu yaje kwako yamtafute balozi wangu!”alisema kwa ukali rais wa Savanna Lands.Kilua alikosa jibu ilibidi akate simu palepale!
Kabla hajafikiria simu yake ya mkononi ikaita tena bila kujishauri sana akaipokea,”Halo?”
“Tuma majeshi yako katika jimbo la Kibatari.Halafu ambia kikosi cha anga kuna ndege ya jeshi la Savanna LANDS imeruka hadi kwenye anga letu hiyo ndege itungue sasa hivi!”ilikuwa sauti ile ya mtu asiyemjua.Ina maana huyu mtu anaintelijensia gani kujua haya mambo?Alijua anaongea na rais wa Savanna Lands.
“Kwanini nifanye hivyo?”
“Wewe ni rahisi na sasa hivi huna mkuu wa majeshi wewe ndo amiri unauwezo wa kuongozi amri hiyo.”
Kilua akavuta pumzi ndefu nakuzishusha,”Lakini nina uhakika gani?”
“Unataka mumeo na mwanao wapate mlo wa leo?”sauti ikauliza.
Ina maana familia yake inanyimwa hata chakula?Roho ikamuuma sana!Bila hata kuwaza.Akamgeukia sekretari,”Nataka simu ya kambi ya jeshi ya Kibatari?”bila hata kujishauri kwa mara nyingine akajikuta akicheza ngoma hiyo.
“Kuna simu maalum inayotumiwa na amiri jeshi pekee.Ngoja nikuunganishe.”alisema Sada akasogea kwenye meza a rais akaingia kwenye droo kuna simu flani hivi kubwa akaitoa halafu akampa na Kilua.