Riwaya: SIN

SIN 219


Muandishi…………………………………………….EDDAZARIA G.MSULWA(G.Authour)


Age ……………………………………………………18+


Simu………………………………………………… 0657072588(whatsapp) au 0768516188


Website……………………………………………… www.storyzaeddytz.com





ILIPOISHIA


β€œWe…e.ww…eee ni nani hadi una nivua madaraka?”
β€œMkuu sio mimi ila katiba ina nielekeza kama raisi ata shindwa kutoa amri katika kipindi ambacho jeshi lina hitaji kuingia vitani basi huna sifa ya kuongoza kwa kipindi hicho. Tafadhali kuna watu na wageni wengi waliopo hapa ikulu hivyo nina kuomba ujiheshimu katika hilo la sivyo vijana wangu wata tumia nguvu.”
Raisi Mtenzi akamtazama jenerali wa jeshi kwa macho makali na yaliyo jaa hasira. Akanyanyuka taratibu na akatoa simu yake mfukoni na kumkabidhi jenerali wa jeshi na taratibu akatoka ofisini hapo huku wanajeshi hao wawili wakihakikisha hazungumzi na mtu yoyote wala kuingia sehemu yoyote hadi katika chumba maalumu ambacho ata kaa humo hadi pale oparesheni ya kuwaondoa wanajeshi wasio julikana itakapo kishwa ndani ya nchi.





ENDELEA


Jenerali wa jeshi akamtazama mr the Brain kwa sekunde kadhaa kisha akatoka ofisini hapo na kurudi katika ukumbi huo.
β€œTusikilizane”
Jenerali wa jeshi alizungumza na watu wote wakaa kimya kumsikiliza. Kijana wake mmoja akachukua bibilia pamoja na bibilia kwa ajili ya kumuapisha kuchukua nafasi ya muda kuongoza nchi. Watu wote waka simama huku wafanyakazi wengine wakiwa wana jiuliza kimoyo moyo ni wapi alipo raisi Mtenzi. Jenerali wa jeshi akala kiapo hicho na akawa raisi wa muda. Baada ya zoezi hili kuisha jenerali akakakwenye kiti ambacho ana kaa raisi peke yake wakiwa ndani ya chumba hicho.
β€œNchi kwa sasa ime weza kuvamiwa na maadui. Hatuwezi kufumbia macho hawa maadui wanao endelea kuivamia hii nchi na jeshi likiwepo. Niwahakikishie jambo moja tu. Tuta wapiga tena tuna wapiga kipigo cha mbwa Koko.”
Jenerali alizungumza huku wakuu wa majeshi wa kambi zote nchini Tanzania wakiwa wana fwalilia kikao hicho kwa kupitia mfumo wa video call.
β€œMuna jua ni nini cha kufanya. Wanajeshi wote ambao wame ingia nchini Tanzania waanze ushambuliwa sasa hivi”
β€œSawa mkuu”
Wakuu wa kambi zote za jeshi wakajibu kwa pamoja na shuhuli ya kuwasaka wanajeshi ambao hadi sasa hawajajuliakana kama ni wa nabii Sanga ikaanza.


***


β€œRaisi Mtenzi amepigwa chini”
Samson alizungumza huku uso wake ukiwa ume tawaliwa na tabasamu pana sana.


β€œUna maanisha nini?”
Josephine aliuliza huku macho yame mtoka.


β€œNiliweza kumtumia rafiki yangu ninaye fanya naye kazi pale ikulu video zile za wale wanajeshi wa nabii Sanga na aliweza kuziweka hadharani na ameniambia kwamba jenerali wa jeshi alihitaji kuanza kufanya mashabulizi kwa wanajeshi hao ila raisi Mtenzi akwa hatoa amri. Hivyo jenerali wa jensi ame weza kuongoza nchi kwa muda hadi pale watakapp waua wanajeshi wote walio vamia nchi”
β€œIme wezekana vipi kwa raisi kutolewa madarakani?”
Magreth alihoji.
β€œIna wezekana na katiba ina mruhusu jenerali wa jeshi kuchukua madaraka kwa muda pale tu raisi anapo onyesha ana lege lega kutoa maamuzi hususani pale nchi inapo kuwa katika wakati wa kuvamiwa. Hivyo adui yetu sasa tuna weza kumpiga mbele na nyuma”
Samson alizungumza kwa kujiamini.
β€œAisee Mungu ni mwema. Ata sikiliakilio chetu”
β€œNdio hivyo sister Josephine”
β€œJenerali wa jeshi ni rafiki wa baba mzuri tu. Je nina weza kuonana naye?”
Cleopatra alizungumza huku akiwatazama wezake.


β€œUna taka kuonana naye umuambie nini?”
β€œNimpe picha halisi kwamba wanajeshi hao ni wa nabii Sanga na pia nina hitaji kuwafutia nyinyi makosa na muweze kutoka nje tena na kufanya kazi kama kawaida”
β€œHilo ni wazo zuri. Cleopatra ana weza kusafisha majina yetu na adui yetu akakamatwa na kusekwa ndani”
Evans naye alishauri.
Josephine akatafakari kwa muda kisha akamtazama Cleopatra usoni mwake.


β€œUna weza kwenda ila ina bidi kuzungumza na RPC Karata kwanza. Mage mpigie RPC”
β€œSawa”
Magreth akampigia RPC Karata na kumueleza mpango wake na RPC Karata akamtuma mlinzi wake kwa ajili ya kumchukua Cleopatra.
β€œCleopatra nina kuomba ukawe very smart utakapo kutana na jenerali wa jeshi. Tuna hitaji kuwa hurukwa maana hatuna makosa ambayo yana weza kutufanya kuwa katika hali kama hii”
β€œMusijali nina elewa kila kitu”
β€œJamani nime weza kupata location ya meli ya nabii Sanga ilipo”
Samson alizungumza huku akiendelea kuminya minya laptop yake na watu waote wakatazama laptop hiyo.
β€œVizuri niingizie hiyo location kwenye simu yangu na nikifika ikulu nita muonyesha jenerali.”
Samson akafanya hivyo na kumuingizia Cleopatra ramani inayo onyesha ni wapi ilipo location ya meli ya nabii Sanga. Hazikupita dakika tano dereva wa RPC Karata akafika nyumbani hapo na wakaondoka na Cleopatra.
β€œIna bidi twende kuvamia meli hiyo”
Evans alizungumza wa kujiamini na kuwafanya watu wote kumtazama.
β€œShemeji hatuwezi kupambana na watu wengi kama hao tuta kufa. Tumuombee Cleopatra aweze kuaminika huko anapo kwenda”
Josephine alizungumza kwa upole huku kila mmoja akiwa ameyaweka matumaini yake kwa Cleopatra


***


Wanajeshi wa nchi ya Tanzania wakasambaa katika jiji la Dar es Salaama huku shuhuli za usafiri na shuhuli nyingine zikisimama kwa muda. Hapakuwa na mwananchi aliye ruhusikwa kutembea wala magari yanayo toka mkoani kuingia katika jiji la Dar es Salaam. Kwa ufupi jiji zima lime zibitiwa na wanajeshi. Wanajeshi wa nabii Sanga ambao wameingia jiji Dar es Salaama kwa lengo la kumsaka mrs Sanga wakaanza kupatwa na machale ya kuona hali ya utulivu inayo endelea ndani ya jiji hilo.


β€œMkuu tuna ona jiji limetulia hakuna raisi wana otembea wala magari?”
Kiongozi wa kikosi hicho alizungumza na nabii Sanga kwa kutumia simu.
β€œUna maanisha nini?”
β€œYaani jiji lipo kimya hatuoni magari wala watu. Au ndio hiyo shuhuli ya kumtafuta mke wako?”
β€œNdio si muna jua kwamba amesha kuwa makamu wa raisi hivyo musiogopo. Hakikisheni na nyinyi muna ifanya kazi niliyo waagiza”
β€œSawa mkuu”
Nabii Sanga akakata simu na mkuu huyo wa jeshi la nabii Sanga akaamrisha vijana wake kuingiza magari yao yapatayo thelathini huku yakiwa yamejaa wanejeshi katika jiji la Dar es Saalam.
β€œWame ingia kwenye mtego wetu”
Mwanajeshi mmoja wa Tanzania aliye kaa gorofa ya tano alizungumza kwa kutumia simu ya upepo huku akitazama gari hizo kwa kutumia darubini. Wanajeshi wa Tanzania walio samba maeneo mbalimbali katika jiji la Dar es Salaam waliweza kusikia sauti hiyo ya mwenzao.
β€œT Zero wapo wangapi?”
β€œZipo gari thelathini na tano mkuu na tume ziweka katikati”
β€œT Tena una nisikia?”


Jenerali alizungumza na vijana wake wote wakamsikia.
β€œNdio mkuu nina kusikia”
β€œTroops yako ina watu wangapi?”
β€œWatu ishini mkuu”
β€œHakikisheni kwamba hatoki mtu”
β€œSawa jenerali”
Wanajeshi wa Tanzania walio jificha katika magorofa eneo la Morroco. Wakaziweka silaga zao tayari kw amashambulizi. Mkuu wa kikosi cha wanajeshi wa nabii Sanga akatoa ishara ya gari hizo zikasimama.
β€œMoyo wangu una poteza amani kabisa?”
β€œKwa nini mkuu”
Kijana wake alimuuliza.
β€œHuu ukimya sio wa kawaida katika jiji la Dar es Salaam. Yaani hadi sasa hivi hatuoni hata daladala moja?”
β€œHata mimi nina shangaa mkuu”
β€œNa kama mrs Sanga angekuwa ana tafutwa, basi tungeona polisi wakiwa wame zagaa kila mahala. Ila ni kimya na sio kawaida”
β€œSo mkuu turudi au?”
β€œNgoja kwanza”
Mkuu huyo akafungua mlango wa gari lake aina ya JEEP, akachukua darubini yake na kuanza kutazama kwenye magorofa yaliyopo eneo hilo la Morocco mataa.
β€œFuckk ambushhhhhh!!”
Alizungumza mara baada ya kumuona mwanajeshi mmoja akiwa amemuelekezea bundiki. Kitendo cha kujaribu kuingia ndani ya gari, akatandikwa risasi ya bega na akaanguka chini. Mvua ya risasi ikaanza kuwanyeshea. Hakika hapakuwa na aliye tarajia kukutana na kipigo kama hicho. Wanajeshi wa Tanzania wakazidi kuwashambulia wanajeshi wa nabii Sanga ambao walijikuta wakitawanyika kwa kukimbia huku kila mmoja akijitahidi kuhakiki ana okoa maisha yake kwani ambushi hiyo hawakuitegemea.


***


β€œMbona mitaa ipo kimya sana?”
Cleopatra alimuuliza mlinzi wa RPC Karata huku wakiwa katika gari hilo la RPC.


β€œKun oparesheni inayo endelea ya wanajeshi hivyo hakuna gari wala mtu anaye ruhusia kukota nje kwa msaa zaidi ya sita.”
β€œDuuu”
β€œNdio”
β€œMbona wewe una endesha?”
β€œHii gairi ni ya RPC hivyo ina julika”
β€œRPC mwenyewe yupo wapi?”
β€œIkulu”
β€œSawa sawa”
Wakafika ikulu na kijana huyo akaeleza kwamba Cleopatra ni mgeni wa RPC hivyo akaruhusiwa kuingia.


β€œUta pumzika hapo hadi RPC atakapo toa commanding room”
β€œSawa je jenerali yupo?”
β€œNdio naye yupo kwenye chumba hicho. Wakitoka ndio uta kutana nao”
β€œSawa”
Cleopatra akaa kwenye chumba maalumu cha wageni kupumzika. Mlinzi wa raisi Mtenzi akaingia sebleni na kumuita Jery pembeni ili wazungumze. Wakatoka nje ya seble hiyo kwa ajili ya mazungumzo.
β€œVipi?”
β€œSio shwari”
β€œUna maanisha nini?”
β€œMzee kwa sasa yupo kizuizini na nchi ina ongozwa na jeshi na jenerali sasa hivi ndio raisi wa muda”
Jery akastuka sana huku akimtazama mlinzi huyo.
β€œAcha kunitania?”
β€œHuo ndio ukweli. Raisi kwa sasa yupo kizuizini na haruhusiwi kuonana na mtu yoyote na hadi hapa ninavyo zungumza ni kwamba wana jeshhi wame funga mitaa yote na watu wote wapo ndani, huko barabarani hakuna gari linalo ruhusiwa kutembea”
β€œHembu hayo melezo njoo uyazungumzie huku ndani kwa maana nina hisi una nichanganya”
Wakarudi sebleni na kuka kwenye sofa zilizop hapo sebleni.
β€œBaba kuna tatizo lime tokea”
Jery alianza kuzungumza na kumfanya nabii Sanga kukaa vizuri.
β€œKuna nini mwanangu”
β€œAhaa baba ame wekwa kizuizini na sasa hivi jeshi ndio lina ongoza nchi”
β€œNINI?”
Nabii Sanga alihamaki huku akihisi kama tumbo likimkata kwa maumivu makali.
β€œNdio mzee. Sasa hivi jenerali wa jeshi ndio raisi wamuda. Amemtoa madarakani raisi Mtenzi na kumuweka kizuizini mara baada ya kugundua kwamba kuna wanajeshi ambao wame vamia jiji hili na hawajulikani ni wapi walipo tokea. Raisi alipaswa kutoa amri kwa jeshi ila akashindwa. Hivyo ilimlazimu jenerali kuchukua mamlaka na inavyo sadikika kwamba wanajeshi hao ndio walio mteka makamu wa raisi’
Nabii Sanga akahisi kama nguvu za mwili zikimuishia. Taratibu akakaa chini huku mapigo yake ya moyo yakimuenda kasi sana.
β€œBaba upo salama?”
Jery aliuliza huku akimsogelea baba yake mkwe.
β€œYaa nipo salama. Vipi ime kuwaje?”
β€œHapa ninavyo zungumza wanajeshi hao wame pewa ambushi ya maana na sidhani kama wata weza kutika ndani ya hili jiji wakiwa hai”
Maneno ya mlinzi huyo yakazidi kumfanya nabii Sanga kuhisi mapigo yake ya moyo yanayo kwenda kwa kasi kubwa yata toboa kifua chake.
β€œBaba hii presha”
Jery alizungumza huku akikimbilia chumbani kwake. Akamkuta Julieth akiwa ame lala fofofo kitandani.Jery kwa haraka akachukua kisanduku chake cha kuhifadhia vifaa vya huduma ya kwanza. Akatoka chumbani hapo na kurudi sebleni na kumkuta nabii Sanga akiwa ameiweka simu yake sikioni mwake. Simu ya kijana wake aliye toka kuongea naye muda mchache ulii pita, ina endelea kuita pasipo kupokelewa. Jasho jingi lina mwagika nabii Sanga usoni mwake, hakika katika siku aliyo pata mapigo ya kutisha ni leo.
β€œBaba kaa vizuri nikupime presha?”
β€œHapana Jery. Nina hitaji kuondoka hapa ikulu, muamshe Julieth tuna ondoka sasa hivi”
β€œSamahani mze hilo halito wezekana kwa maana sisi walinzi wote wa raisi tume pokonywa silaha zetu. Ime tolewa hakuna mtu hata mmoja kutoka nje ya ikulu hii.”
β€œNahiaji kuonana na huyo jenerali wa jeshi?”
β€œHaiwezekani mzee wangu. Yaani hapa ninavyo kuambia ni kwamba kuanzia getini hadi ndani ya ikulu, wanao linda ni wanajeshi na sio sisi walinzi wa raisi”
β€œSawa ila nina hitaji kuondoka now. Jery muamshe Julieth tuna ondoka sasa hivi nina kwenda kuonana na huyo jenerali wa Jeshi”
Nabii Sanga alizungumza na kutoka sebleni hapo na kuwaacha Jery na mlinzi huyo kushangaa. Nabii Sanga akamuomba mwanajeshi mmoja kuitiwa jenerali wa jeshi.
β€œMkuu kwa sasa yupo bize”
β€œMuambie ni dharura nina hitaji kuondoka”
Nabii Sanga alisisitizia, kutokana nabii Sanga ana sifa nzuri na watu wengi wana mfahamu kwamba ni mtu wa Mungu basi mwanajeshi huyo akamuelewa na akalekea katika commanding room na akamnong’oneza jenerali wa jeshi.
β€œAna taka nini?”
β€œSijajua mkuu ila na sehema ni muhimu sana”
Jenerali wa jeshi akatazama jinsi wanajeshi wake wanavyo endelea kupambana na wanajeshi wa nabii Sanga. Akanyanyuka na kutoka nje kwa maana hata yeye ana muheshimu sana nabii Sanga na isitoshe ni mara kadhaa ame kuwa akihudhuria katika kanisa la nabii Sanga kwa ajili ya kusali.
β€œHabari yako Jenerali”
β€œSalama heshimiwa yako mtumishi”
β€œNashukuru ndugu yangu. Nina omba nafasi ya kuweza kuondoka hapa ikulu na kuelekea nyumbani kusali”
β€œAhaa samahani mtumishi wa Mungu hivi sasa nchi ipo katika hali ya hatari hususani hapa Dar es Salaama hivyo huto weza kutembea kwa gari huko barabarani ni hatari sana”
β€œNime kuja na helicopter yangu na nina imani nita ondoka nayo. Nina kuomba niondoke na mkwe wangu pamoja na binti yangu. Kukaa hapa ikulu na mke wangu alitekwa mbele ya macho ya watu wengi hivyo nina kosa amani sana ndugu yangu nina kuomba sana uweze kuniruhusu’”
Jenerali wa jeshi akamtazama nabii Sanga anaye omba kwa unyenyekevu. Kutokana ni mtu anaye muamini na kumuheshimimu sana, akamruhusu aweze kuondoka na helicopter yake.
β€œMungu akubariki katika kila ulifanyalo”
β€œNina shukuru sana mtumishi”
Nabii Sanga akarudi sebleni na kumkuta Jery na Julieth wakiwa salama. Wakaondoka na kuelekea kiwanja cha helicopter. Wakaingia kwenye helicopter hio na taratibu ikaanza kupaa kuelekea hewani.


β€œTuelekee nchini Kenya”
Nabii Sanga alimueleza rubani wake na akatii.
β€œBaba vipi mama?”
β€œAta patikana na kila jambo lita kwenda vizuri. Jery nina kuamini na nina imani kwamba uta mlinda mwanangu”
β€œNdio baba nipo tayari kufa kwa ajili ya mke wangu”
Jery alizungumza kwa msisitizo huku akimshika mkono wa kulia Julieth ambaye naye amejawa na wasiwasi kwa maana Jery alimueleza kinacho endelea huko mtaani na Jery pekee ndio hajui baba yake mkwe na mke wake ni watu wa aina gani.


***


β€œJenerali pia kuna binti ana hitaji kukuona”
Mlinzi wa jenerali wa jeshi alizungumza kabla ya jenerali hajarudi kwenye chumba cha kuongozea oparesheni hizo.


β€œNi nani?”
β€œMtoto wa mzee Mbogo”
β€œYupo hapa nchini?”
β€œNdio na yupo hapa ikulu. Yupo katika chumba cha mapumziko”
β€œTwende nikamuone”
Jenerali akaanza kuongoza kwa mwendo wa haraka hadi katika chumba hicho. Alipo ingia tu, Cleopatra akanyanyuka kwa haraka na kamkimbilia na kumkumbatia kwa nguvu huku akiangua kilio cha uchungu sana. Jenerali akamkumbatia kwa dakika kadhaa Cleopatra kisha akamuachia.
β€œCleopatra mbona una lia mwaangu?”
β€œBa mdogo, baba ame uwawa?”
Jenerali akastuka sana huku akimtazama Cleopatra usoni mwake kwa maana anacho jua yeye ni kutekwa kwa mzee Mbogo ila swala la kuuwawa kwake halitambui kabisa.
β€œNa nani aliye muua?”
β€œNABII SANGA NA WANAJESHI WAKE”


Jenerali macho ya mshangao yakamtoka kiasi cha kuhisi kupagawa. Akamtazama Cleopatra machoni mwake na kugundua kwamba anacho kizungumza ni kitu cha ukweli kwani ana mfahamu Cleopatra toka utotoni mwake na ana muelewa vizuri sana.


****************************************************************************************************************


****


ITAENDELEA


Haya sasa. Cleopatra ame mueleza jenerali ukweli na ameaminika. Nabii Sanga, mkwe wake pamoja na mwanaye wana kimbilia nchini Kenya wakia katika helicopter je nabii Sanga ta kamatwa ikiwa jenerali kwa sasa ndio ana ongoza nchi? Usikose sehemu ya 220.
 
SIN 220


Muandishi…………………………………………….EDDAZARIA G.MSULWA(G.Authour)


Age ……………………………………………………18+


Simu………………………………………………… 0657072588(whatsapp) au 0768516188


Website





ILIPOISHIA


Jenerali akaanza kuongoza kwa mwendo wa haraka hadi katika chumba hicho. Alipo ingia tu, Cleopatra akanyanyuka kwa haraka na kamkimbilia na kumkumbatia kwa nguvu huku akiangua kilio cha uchungu sana. Jenerali akamkumbatia kwa dakika kadhaa Cleopatra kisha akamuachia.
β€œCleopatra mbona una lia mwaangu?”
β€œBa mdogo, baba ame uwawa?”
Jenerali akastuka sana huku akimtazama Cleopatra usoni mwake kwa maana anacho jua yeye ni kutekwa kwa mzee Mbogo ila swala la kuuwawa kwake halitambui kabisa.
β€œNa nani aliye muua?”
β€œNABII SANGA NA WANAJESHI WAKE”


Jenerali macho ya mshangao yakamtoka kiasi cha kuhisi kupagawa. Akamtazama Cleopatra machoni mwake na kugundua kwamba anacho kizungumza ni kitu cha ukweli kwani ana mfahamu Cleopatra toka utotoni mwake na ana muelewa vizuri sana.





ENDELEA


β€œWewe ume juawaje kama nabii Sanga ame muua baba yako”
Cleopatra akaanza kusimulia kuanzia walivyo toka uwanja wa ndege hadi ajali ilivyo tokea. Akasimulia jinsi namba Josephine na Magreth walivyo mueleza siri ambazo zina fanywa na nabii Sanga na familia yake na kitu cha pekee alicho kificha ni jinsi na namna ambavyo RPC Karata anavyo wapatia ushirikiano wa moja kwa moja.
β€œShenzi wan a toroka hawa”
Jenerali wa jeshi alizungumza huku akitoka kwa mwendo wa kasi chumbani hapa na kukimbilia commanding room. Akapiga simu katika kitengo cha jeshi kinacho husiana na anga.
β€œNina hitaji F-16 mbili ziweze kuifwatilia helicopter aina ya Sikorsky SH-3 sea king inayo milikiwa na nabii Sanga. Tuna elewana”
β€œUme eleweka jenerali”
Sauti nzito ilisikika upande wa pili wa simu hiyo na marubani wanao endesha ndege hizo za kijeshi aina ya jeti F-16 wakaingia ndani ya ndege hizo za kivita na kuondoka katika kambi ya jeshi la anga na kuelekea upande ilipo elekea helicopter hiyo ya nabii Sanga yenye uwezo wa kutua katika bahari.


***


β€œBaba naogopa?”


Julieth alizungumza huku mwili mzima ukimtetemeka kwa woga. Taratibu Jery akamkumbatia huku akimtazama usoni mwake.


β€œUsiogope mwanangu kila jambo litakwenda kuwa sawa”
Mlio wa alama nyekundu ukaanza kulia kwenye kioo kidogo kilichopo pembeni ya rubani wa helicopter hiyo.


β€œMuheshimi kuna jeti mbili za jeshi zina tufwatilia kwa kasi ya ajabu sana nini tuna fanya?”
Rubani alizungumza huku akimtazama nabii Sanga aliye kaa pembeni yake.


β€œHili jambo sio zuri”
β€œNdio muheshimiwa. Ina bidi wewe na familia yako muweze kuingia baharini kabla hawajatufikia”
Nabii Sanga akageuka nyuma na kumtazama Jery pamoja na Julieth.
β€œJery una weza kuogelea?”
β€œNdio baba”
β€œKwenye siti ya nyuma kuna mitungi ya hesi ya kuogelea. Vaeni kwa haraka turukie ndani ya bahari”
β€œNgoja kwanza baba kwani kuna nini kinacho endelea au ndio baba yangu amesha pinduliwa madarakani?”
β€œMimi na wewe hatujui”
β€œOhooo wamesha tufikia”
Rubani alizungumza na kumfanya nabii Sanga macho kumtoka. Ndege hizo mbilli za jeshi zika iweka katikati helicopter ya nabii Sanga.


β€œRubani wa Sikorsky SH-3 sea king rudi katika ardhi ya Tanzania sasa hivi hili sio ombi ni amri”


Rubabi mmoja wa ndege hizo za kijeshi alizungumza huku wakiitazama helicopter hiyo inayo kwenda kwa kasi ya ajabu sana.


β€œMkuu kuna oder ya kurudi kwenye ardhi ya Tanzania tuna fanyaje?”
Nabii Sanga akatazama upande wa kushoto alipo kaa yeye. Rubani wa ndege ya upande aliopo yeye akampa ishara ya kugeuza helicopter hiyo.


β€œKwa nini tugeuze?”
Nabii Sanga aliuliza mara baada ya kuvaa headphone kubwa zilizopo eneo hilo la rubani.


β€œTuna kuheshimu sana nabii Sanga ila una paswa kumuamuru rubani wako kuigeuza hiyo helicopter”
β€œMusipo nieleza sababu siwezi igeuza helicopter yangu na isitoshe simuamini mtu yoyote kama mke wangu aliweza kutekwa akiwa ikulu nina imani kwama muna weza kunifanyia figisu figisu kama hizo”
β€œMuheshimiwa tuna kuambia kwa mara ya mwisho. Geuza helicopter yako la sivyo tuta ishambulia”
β€œKwa hiyo muna taka kumuua mume wa makamu wa raisi, mshauri wa raisi pamoja na mtoto wa raisi si ndio?”
Nabii Sanga aliuliza kwa ukali sana kiasi cha kuwafanya marubani hao kushindwa kujibu swali hilo. Rubani mmoja ika bidi awasiliane na jenerali.
β€œMkuu wame kataa kugeuza helicopter na ndani ya helicopter yupo Jery mtoto wa raisi Mtenzi.”
Jenerali wa jeshi akashusha pumzi huku akiwa ana tafakari nini cha kufanya.
β€œWapeni vitisho vitatu vikubwa”
β€œSawa mkuu”
Ndege hizo za jeshi sika tawanyika kama zina rudi nyuma.


β€œWame kwenda wapi?”
Nabii Sanga aliuliza huku akichungulia dirishani.
β€œSijui mkuu kwa maana hata hapa kwenye rada yangu sizioni.”
Rubani alizungumza huku mapigo ya moyo yakimuenda kasi sana kwani toka aanze kuendesha helicopter hiyo hajawahi kukumbana na mtafaruku wa ndege za kijeshi.
β€œOn target”
Rubani mmoja wa ndege hizo za jeshi alizungumza, kisha akaminya batani yake nyekundu iliyo andikwa fire. Rubani wa ndege ya pili naye akaminya bomu jengine kulilenga bomu alilo livyatua mwenzake na yakakutana eneo la mbele inapo elekea helicopter ya nabii Sanga mita mia moja kutoka ilipo na yakalipuka na kumfanya rubani wa helicopter ya nabii Sanga kuukwepa mlipuko huo ulio wastua kila mmoja ndani ya helicopter hiyo.


β€œOhoo Mungu wangu”
Nabii Sanga alihamaki huku mapigo ya moyo yakimuenda kasi. Akamtazama Julieth na kumuona akimwagikwa na machozi huku akiona kifo kina mjia mbele yake. Jery naye yupo kimya huku akiwa ameshikwa na bumbuwazi. Gafla wakaziona ndege hizo zikwa zime wazunguka tena na kwa muda huu rubani hazioni tena ndege hizo kwenye rada yake.


β€œTuna rudi tena nabii Sanga na familia yako. Rudini katika ardhi ya Tanzania na tupo hapa kwa ajili ya kuwa sindikiza kurudi Tanzania”
Sauti ya rubani mmoja ilisikia vizuri kwenye headphone walizo vaa nabii Sanga na rubani wake. Nabii Sanga akavuaa headphone hiyo na kumtazama rubani wake.
β€œKuna umbali gani kutoka hapa hadi kwenye meli?”
Rubani akazima headphone hiyo ili watakacho kizungumza yeye na bosi wake kisisikike na marubani hao wa ndege za kijeshi.
β€œKuna umbali wa milies kama elfu moja mkuu”
β€œTuna weza kufika?”
β€œNdio ila ni hatari sana kuzionyesha ndege hizi za kijeshi eneo ambalo kambi yetu ilipo”
β€œHatuwezi kuingia nchini Kenya hivi wana weza kuomba ruhusa ya kuingia Kenya na kujikuta tyna kwenda kuzuiwa”
β€œSasatuna fanyaje mkuu”
β€œGeuza helicopter tuna elekea kwenye meli. Kama ni kufa basi tukafie kwenye ile meli”
β€œSawa mkuu”
Rubani akavaa headphone yake na nabii Sanga naye akavaa headphone hiyo na helicopter ika geuzwa kutoka upande wa Magharibi Kaskazini kuelekea upande wa Kaskazini mashariki”
β€œWana elekea wapi hao?”
Rubani wa ndege alimuuliza mwenzake.


β€œHata sijui”
β€œMkuu wame geuza ila hawaelekei Kenya tena kwa sasa wana elekea upande wa Kaskazini Mashariki”
β€œEndeleeni kuwafwatilia”
β€œJe tuwapatie vitisho tena”
β€œHapana nina imani hiyo helicopter ina weza kuisha mafuta na tuta ona wapi wata ishia”
β€œSawa mkuu”
Nabii Sanga akaminya batani moja iliyo andikwa call 2. Simu hiyo aliyo ipiga moja kwa moja ikapokewa katika meli yake.


β€œTupo katikati ya mazoezi. Kuna jeti F-16 zina tufwatili tuna hitaji msaada wa haraka”
β€œTume kusoma mkuu tuna kuja’
Nabii Sanga akatabasamu huku akimtazama rubani wake.


β€œBaba si turudi tu”
β€œHadi sasa hivi hatujui mama yako yupo wapi. Ametekwa mbele ya watu tena ikulu. Una hisi nita rudi nchini. Isitoshe baba yako mkwe ametolewa madarakani kwa kulazimishwa una kuna usalama huko”
Nabii Sanga alizungumza kw amsisitizo huku akimtazama Julieth usoni mwake. Ndege nne za kijeshi aina ya Sukhoi Su-27ambazo nabii Sanga alizinunua miaka miliwi katika nchi ya Russia zikaanza safari kutokea katika meli hiyo kubwa ya nabii Sanga. Ndege hizo zenye uwezowa kukimbia kwa kasi ya 2500km/h zikambaa katika anga zikiwa zime jipanga mstari mmoja huku zikienda kwa kasi ya spidi moja.


β€œWhat’s fuc**”
Rubani wa ndege ya F-16 alizungumza huku wakiziona ndege hizo zikija kwa kasi sana.


β€œHizi ndege ni za nchi gani?”


Rubani wa ndege ya pili auliuliza.


β€œSijui. Jenerali kuna ndege nne je wewe ndio ume zituma?”
β€œHapana sio mimi zipo vipi?”
β€œNi ndege za Russio…..Fuc**”
Rubani hakumalizia maelezo yake, akakwepa bomu moja lililo lengwa kwenye ndege yake kwa ustadi wa hali ya juu. Jambo hilo likawaashiria marubani hao wa ndege za jeshi la anga za Tannzania F-16 kwamba sasa wapo kwenye hatari kubwa. Mashambulizi yakaanza ya kurushiana makombora yanayo kwenda kwa kasi sana. Huku ndege mbili zikiisindikiza helicopter ya nabii Sanga kuelekea kwenye meli yake huku ndege mbili zikihakikisha kwamba wana zizuia ndege hizo za F-16.


β€œBaba mkwe hizo ndege zime tokea wapi?”
β€œJery aliuliza.”
β€œNita kuambia tukifanikiwa kufika salama”
Nabii Sanga alizungumza kw akujiamini huku helicopter yake pamoja an ndege hizo anazo zimiliki zikizidi kunjanja mawingo na kupotea katika macho ya marubani wa ndege za F-16.


β€œMuna hitaji msaada wowote?”
Sauti ya jenerali ilisikika vizuri kwa marubani wa F-16.


β€œHapana mkuu tuna wahimili. J triangle”
Rubani mmoja alimueleza mwenzake lugha wanayo ielewa wao wenyewe.


β€œPoa J1”
Wakaanza kuziendesha ndege hizo huku wakichora umbo la pembe tatu kitu kiliocho wachanganya marubani wa ndege za nabii Sanga ambao kazi yao ni kushambulia hadi wakajikuta risasi na mabomu yakiwaishia.


β€œNi muda wetu mother fuc**”
J alizungumza huku wakianza kufanya mashambulizi ya ustadi wa hali ya juu kusababisha ndege hizo mbili za nabii Sanga kulipuka na marubani wake na mabaki yakaangukia baharini. Wakajaribu kuelekea uelekeo ilipo kwenda helicopter ya nabii Sanga pamoja na ndege zake mbili ila wakashindwa kuzipata.
β€œJenerali, hatuoni dalili yoyote ya helicopter ya nabii Sanga”
β€œRudini kambini”
β€œSawa mkuu”
Maribani wakageuza ndege hizo na kurudi nchini Tanzania.


***


β€œCleopatra ana piga simu”
Josephine alizungumza huku akitazama simu yake.
β€œMpokelee na muweke loudspeaker β€œ
Josephine akapokea simu hiyo huku akiwatazama wezake.
β€œNdio”
β€œNime weza kuzungumza na jenerali na nime mueleza kila kitu kuhusiana na nabii Sanga.”
β€œAme semaje kuhusiana na sisi?”
β€œHajazungumza chochote ila ameweza kutoka hapa nilipo”
β€œKwani upo wapi?”
β€œNipo kwenye chumba cha kupumzikia”
β€œJe ulimuambie tukio la sisi kumteka mke wa nabii Sanga.”
β€œHapana vipi nimueleze”
β€œNgoja kwanza usikate simu. Jamani vipi aseme”
β€œIna weza kuwa hatari kwetu kwa mana hadi sasa hivi hatujahakikishiwa usalama wetu na bado tuna onekana kama wasaliti wa nchi”
Evans alishauri.
β€œSawa nime waelewa nita itahidi kumueleweha hali halisi jenerali”
β€œSawa kuwa makini”
β€œPoa”
Cleopatra akakata simu.
β€œSamson kuna kipi kipya?”
β€œKuna haya mapambano yaliyo tokea pale Morocco mataa. Naona wanajeshi wa nabii Sanga wame uwawa sana”
Samson alizungumza huku akiwaonyesha video hiyo.
β€œJamani hii nchi ina mambo ya ajabu. Ina kuwaje mtu mmoja na apata nguvu ya kumiliki jeshi lake yeye mwenyewe. Una jua hii ita tisha?”
Magreth alilalama.
β€œNi kweli ila ingekuwa ni ngumu sana kwa watu kumjua nabii Sanga kama ni mtu mbaya kwa maana ukiangalia huduma yake ya kuombea watu na wakapata miujiza ya kupona. Ni muumini wake yupi ambaye uta kwenda kumuambia kwamba nabii Sanga ni mtu mbaya na akakuelewa.”
β€œHilo unalo lizungumza Jsospehinei ni kweli aisee”


Samson naye aliunga mkono.
β€œNime pata wazo”
Josephine alizungumza huku akisisimama.


β€œWazo gani?”
β€œHuyu ni mke wake na ana weza kufahamu kila kitu kuhusian ana mume wake. Nita mpatia mateso hadi aweze kuaja ni wapi ilipo kambi ya mume wake ikiwezekana huu mchezo tukaumalize mapema. Hatuwezi kutoboa siri nita kata kidole chake kimoja baada ya kingine”
Magreth akaingia ndani ya chumba hicho huku akiongozana na Evans. Tatibu mrs Sanga akanyanyua uso wake na kuwatazama watu walio ingia ndani hapo.


β€œUme amkamama”
Magreth alizungumza huku akimtazama mrs Sanga kwa macho ya jejeli.
β€œKu..u…mbe ni wewe?”
β€œYaa ni mimi mke mwenza. Za masiki mengi mengi”
Maneo ya kejeli ya Magreth yakamkera mrs Sanga ila kwa bahati mbaya hana ujanja wa kunyanyuka katika kiti hicho alicho fungwa. Akatazama jeraha lake katika paja na kukuta akiwa amefungwa bandeji.
β€œHivi una jua mume wako ame niharibia sana maisha yangu”
β€œMpumbavu wewe, laiti kama ninge jua ninge kuua toka kipindi kile mshenzi wewe”
β€œIla ndio hivyo hukuniua. Una jisikiaje kama mimi na wewe tukawa marafiki”
β€œSiwezi kuwa na rafiki na mtoto wa malaya kama wewe”
Magreth akafumba macho yake kwa sekunde kadhaa huku akisikilizia maumivu ya tusi hilo aliko tukanywa na mrs Sanga. Akafumbua macho yake huku akiwa ana tabasamu.


β€œOkay hakuna shaka juu ya hilo ila ngoja nikuonyeshe kitu kimoja”
Akamnyooshea mkono Evans.
β€œNini?”
β€œKisu”
Evans akamkabidhi Magreth kisu hicho.
β€œUsipo zungumza ukweli nina kwenda kukata kidole cha kuanzia mkono wa kushoto hadi wa kulia kimoja baada ya kingine. Naamini hapo ndipo utakapo niongezea cheo kingine na kuniita mtoto wa gaidi”
Magreth akashika kidole cha mwisho cha mkono wa kushoto wa mrs Sanga.


β€œNiambie ni wapi ilipo mbeli yenu”
Magreth alizungumza kwa sauti ya upole huku akimtazama mrs Sanga usoni mwake. Galfa milio ya risasi zikaanza kuingia ndani ya dirisha la chumba hicho na kumfanya Evans kumsukuma mrs Sanga na Magreth na wakaanguka chini huku naye akirukia katika kona ya chumba hicho huku sebleni nako hali ikiwa sio shwari kabisa huku Josephine na Samson nao wakiajibaza kwenye kuta kwani mvua hiyo ya risasi inayo ingia ndani ya nyumba hiyo hawajui kama ina toka kwa wanajeshi wa nchi ya Tanzania ua jeshi la nabii Sanga.


****************************************************************************************************************


**


ITAENDELEA


Haya sasa. ni wanajeshi gani ambao wana shambuli nyumba hiyo. Je Magreth, Josephine, Evans na mrs Sanga wata fanikiwa kuwa salama ndani ya nyumba hiyo kwa maana ambushi hiyo ime kuja muda na wakati ambao waha hawajautegemea? Usikose sehemu ya 221.
 
SIN 221


Muandishi…………………………………………….EDDAZARIA G.MSULWA(G.Authour)


Age ……………………………………………………18+


Simu………………………………………………… 0657072588(whatsapp) au 0768516188


Website





ILIPOISHIA


β€œNini?”
β€œKisu”
Evans akamkabidhi Magreth kisu hicho.
β€œUsipo zungumza ukweli nina kwenda kukata kidole cha kuanzia mkono wa kushoto hadi wa kulia kimoja baada ya kingine. Naamini hapo ndipo utakapo niongezea cheo kingine na kuniita mtoto wa gaidi”
Magreth akashika kidole cha mwisho cha mkono wa kushoto wa mrs Sanga.


β€œNiambie ni wapi ilipo mbeli yenu”
Magreth alizungumza kwa sauti ya upole huku akimtazama mrs Sanga usoni mwake. Galfa milio ya risasi zikaanza kuingia ndani ya dirisha la chumba hicho na kumfanya Evans kumsukuma mrs Sanga na Magreth na wakaanguka chini huku naye akirukia katika kona ya chumba hicho huku sebleni nako hali ikiwa sio shwari kabisa huku Josephine na Samson nao wakiajibaza kwenye kuta kwani mvua hiyo ya risasi inayo ingia ndani ya nyumba hiyo hawajui kama ina toka kwa wanajeshi wa nchi ya Tanzania ua jeshi la nabii Sanga.





ENDELEA


β€œMageeee”
Josephine aliita huku akiwa amejawa na wasiwasi mkubwa sana.


β€œBeee ngojeni nina kuja”
Magreth alizungumza huku akitambaa mithili ya mtoto mchanga. Akafungua moja ya sanduku lililomo ndani ya chumba hicho. Akatoa silaha zake za kininja kisha kwa haraka akava anguo zake za kuzuia risasi tayari kwa kujiandaa kwa mashambulizi. Mabomu ya machozi yakaanza kuingia kwa kupitia dirishani kitendo kilicho wafanya Josephine na Samson kukimbilia katika chumba walichopo Magreth, mrs Sanga na Evans.
β€œIngieni chini”
Magreth alizungumza huku akisimama Evans akafungua mfuniko wa chumba kilichopo chini ya ardhi. Akamvuta mrs Sanga na kumdumbukiza ndani ya chumba hicho akiwa na kiti chake kisha wakafwatia, Josephine na Samson.


β€œKuwa makini baby”


Evans alizungumza huku akimtazama Magreth aliye jiandaa tayari kwa kazi ya kuwalinda wengine.


β€œIngia”
Magreth alizungumza kwa msisitizo kisha Evans akaingia katika chumba hicho na Magreth akaufunga mfuniko huo na kuvuta zulia na kufunika mfuniko huo na hata mtu akiingia ndani ya chumba hicho sio jambo rahisi kwa mtu kuweza kugundua kama kuna chumba cha chini ya ardhi. Magreth akatazama dirishani na kuona wanajeshi wa nabii Sanga wakianza kusogelea nyumba hiyo. Kwa haraka sana akatoka nje na kuanza kurusha silaha zake zilizo kaa katika muundo wa nyota, ambazo kila iliyo mpata mwanajeshi mmoja ilimjeruhi vibaya sana. Wanajeshi wa nabii Sanga wakajawa na mshangao kuona jinsi risasi wanazo mpiga Magreth zikidunda mwilini mwake huku yeye akeindelea kuwashambulia kwa kutumia silaha hizo. Magreth mara baada ya kuishia na silaha hizo za nyoa. Akachomoa mnyororo wake wenye kisi kikali mbele kilicho jipinda kidogo mithili ya nyego. Magreth akaendelea kuwashambulia wanajeshi hao na myororo huo ambao kisu hicho endapo kina pita kwenye mguu basi kina utenganisha mguu huo. Wanajeshi ishirini na sita walio tumwa kumfwata mrs Sanga ambaye ana kifaa kidogo ndani ya mwili wake kinacho muonyesha ni wapi anapo elekea(GPRS Device track), mambo yakaanza kuwawia ugumu. Magreth kwao ikawa ni kikwazo kikubwa sana, kwani kadri muda unavyo zidi kwenda ndivyo jinsi wanavyo kufa. Milio hiyo ya risasi iliwafikia wanajeshi ambao nao wapo kwenye oparesheni ya kuwasaka wanajesi hao wavamizi. Gari za jeshi zipatazo sita zikafika eneo hilo na wanajeshi hao wakaanza kufanya mashambulizi kwa wanajeshiwa nabii Sanga huku wanajeshi wengi wakiwa wana mtambua Magreth akiwa katika mavazi yake hayo.


Wanajeshi ishirini na nne wa nabii Sanga wakauwawa vibaya sana na wakasalia wanajeshi wawili ambao Magreth aliwajeruhi vibaya sana.
β€œPole sana”
Kiongozi wa kikosi hicho cha wanajeshi alizungumza huku akimtazama Magreth amabye nguo zake hizi zime jaa damu nyingi sana.
β€œAsanteni. Vipi vijana wako wapo salama?”
β€œNdio vijana wangu wote wapo salama”
β€œMume kuja kutukamata au?”
β€œUna maanisha nini?”
Magreth akaka kidogo huku akimtazama mkuu wa kikosi hicho na akagundua kwamba hatambui juu ya agizi lililo kuwa lime tolewa na raisi Mtenzi.
β€œUsijali.”
Magreth alizungumza na kuingia ndani, akatoa zulia hilo na kufungua mfuniko huo na kukutana na Evans aliye shika bastola huku akimuelekezea.
β€œVipi?”
β€œHali ipo shari ila kuna wanajeshi wa Tanzania?”
β€œWao ndio walikuwa wana shambulia?”
β€œHapana ni wanajeshi wa nabii Sanga. Ila musitoke kwa sasa hivi nita waambia muda wa kutoka”
Magreth mara baada ya kuzungumza hivyo, akafunga mfuniko huo kisha akaweka zulia hilo na akarudi nje na kuwakuta wanajeshi wakukusanya maiti za wanajeshi hao wa nabii Sanga.


β€œWale wawili wapo wapi?”
β€œWamewahishwa hospitalini kwa maana tuna hitaji kuweza kupata maelezo kutoka kwao na jenerali wa jeshi ana hitaji kuzungumza nawe”
β€œSawa”
Magreth akakabidhiwa simu na captain wa kikosi hicho na akaiwake sikioni mwake.
β€œHabari”
β€œSalama Magreth nina shukuru kwa ulicho kifanya juu ya hao wanajeshi”
β€œNina shukuru sana mkuu”


β€œKuna mambo mengi ambayo Cleopatra ameweza kunieleza hapa. Nahitaji tuonane na kama muna mshikilia mrs Sanga nina omba muweze kumkabidhi kwa haowanajeshi”
β€œAahhaa muheshimiwa. Ita kuwa ni jambo la busara sana kama nikikukabidhi wewe mwenyewe huyu mwana mama. Nina imani ana weza kutueleza siri nyingi sana anazo zifanya yeye na mume wake”
β€œSawa wewe na wezako muta elekea hadi kwenye kambi ya jeshi kisha mimi nita kuja hapo na helicopter kukutana nanyi”
β€œSawa ila nina omba unihakikishie kwamba hamuto nikamata?”
β€œSiwezi kufanya hivyo kwa maana nimesha pata picha halisi ya nani ambaye ni adui hapa na ni nani ambaye ame sababisha haya mambo yote.”
β€œNina shukuru jenerali”
β€œAsanteni sana”
Magreth akamkabidhi simu campteni huyo kisha akarudi ndani na kufungua mfuniko huo ambapo Evans na wezake wakatoka. Wakaingia kwenye moja ya gari la jeshi huku wakiambatana na mrs Sanga na kuondoka katika nyumba hiyo huku matairi ya gari la Magreth pamoja na pikipiki yake yakiwa yameme pigwa risasi za kutosha katika mashambulizi hayo yaliyo dumu kwa dakika 40 pasipo mapumziko.


***


β€œKuna habari yoyote kuhusiana na mke wangu?”
Nabii alimuuliza msaidizi wake mara baada ya kushuka ndani ya helicopter hiyo.
β€œHapana mkuu na hadi sasa hivi kikiso cha pili kime shambuliwa na wanajeshi wote wameuwawa”
β€œWalikuwa wangapi?”
β€œIshirini na sita”
β€œDuuu”
Nabii Sanga alizungumza kwa masikitiko. Jery muda wote amejawa na mshangao kwa maana ukubwa wa meli hiyo na wanajeshi waliopo eneo hilo hakika ni jambo la kumshangaza kwa upande wake.
β€œJulieth hapa ni wapi?”
β€œTupo kwenye meli mume wangu”
β€œNdio nina tambua kwamba tupo kwenye meli. Ila ni mali ya nani?”
β€œKila unacho kiona ndani hapa ni mali ya baba pamoja na mama”
β€œNini?”
β€œYaa usishangae”
Jery akamtazama nabii Sanga na kujaribu kumtathimini ni mtu wa aina gani kwa maana sio jambo raisi kwa mtu wa kawaida kumiliki jeshi kubwa kiais hicho. Wakaingia ndani na nabii Sanga akaonyeshwa video ya mashambulizi yaliyo kuwa yana fanywa na vijana wake katika nyumba ambayo alishikiliwa mrs Sanga.
β€œHuyu binti ni mshenzi sana”
Nabii Sanga alilalama huku akiwa amejawa na hasira sana.


β€œTufanye nini mkuu kwa maana tumepoteza ndege mbili, pia tume poteza wanajeshi zaidi ya stini”
Nabii Sanga akaka kimya kwa dakika kadhaa.
β€œRaisi wa Marekani amefikia wapi?”
β€œNilipokea simu masaa mawili yaliyo pita wakidai kwamba raisi ametua na ndege yake katika nchi ya Madagascar. Hivyo waliniomba ukifika niweze kumpigia ili uzungumze naye kwani wana details zote za kila kitu kinacho endelea kati yako na nchi ya Tanzania”
β€œWashenzi sana hawa nao, sijui mpelelezi wao ni nani mpigie video call”
β€œSawa”
Mazungumzo yote yakiendelea kati ya nabii Sanga na msaidizi wake, Jery alibaki akiwa ameduwaa kwa maana alikuwa ana mchukulia baba yake mkwe wake huyo ni mtu mnyenyekevu na mwenye hekima nyingi sana mbele za watu ila hii hasira anayo iona kwenye uso wa baba yake mkwe ni ishara kwamba baba yake mkwe huyo ana ushetani ndani yake.


β€œYupo hewani muheshimiwa”
Nabii Sanga akakabidhiwa simu hiyo.
β€œSanga habari yako”
β€œSio salama kabisa.”
β€œNatambua kwamba sio salama. Sasa sinto weza kufika nchini kwako kwa hali unayo pitia”
β€œNatambua hilo huwezi kufika. Niambie ni wapi tuna kutana ili tuweze kujadili juu ya hichi kinacho endelea?”
β€œNjoo Madagascar nita kusubiria”
Nabii Sanga akajifikiria kwa sekunde kadhaa, kisha akakubaliana kukutana na raisi wa Marekeni katika nchi ya Madagascar.


β€œBaba ni hatari kwenda kuonana naye huko”
Julieth alishauri mara baada ya nabii Sanga kukata simu.


β€œUsijali mwanangu. Pia nina hitaji kwenda kuwaombea hifadhi ya kudumu wewe na mume wako muweze kuishi nchini Marekani kwa usalama na muondoke kwenye hili jambo. Nina hisi mbaya sana za siku zijazo juu ya usalama wetu”
β€œNina omba kuuliza swali”
Jery aliuliza kwa sauti ya upole kidogo.
β€œUliza tu mwanangu”
β€œBaba wewe ni nani kiuhalisia?”
Swali la Jery likawafanya nabii Sanga na Julieth kutazamana kwenye nyuso zao.


β€œNi story ndefu Jery ila acha kwanza mambo yakae sawa”
β€œHapana nina taka kujua wewe ni nani haswa na kwa nini una tawala jeshi kubwa kama hili ikiwa wewe sio kiongozi wa serikali na kazi yako ya utumishi wa Mungu ina kufaa uwatawale kondoo wa bwana na sio wanajeshi walio jazia miili kama hawa ninao waona.”
Jery alizungumza kwa msisitizo ulio mfanya nabii Sanga kukaa kimya kwa sekunde kadhaa.


β€œIla baby”
β€œNo haya ni mazungumzo yangu mimi na baba mkwe wangu. Usiyaingilie Julieth”
Jery alizungumza kwa kufoka na kumfanya Julieth kukaa kimya nabii Sanga akamtazama Jery usoni mwake kwa sekunde kadhaa.
β€œJery fanya ufanyavyo ila usije ukasahau mimi ni nani kwako. Kama una hitaji kujua mimi ni nani ngoja”
Nabii Sanga akachukua rimoti ya tv na kuwasha. Jery na Julieth wakajawa na mshangao mkubwa sana mara baada ya kuina video ya raisi Mtenzi akimuua mzee Mbogo kwa kumpiga risasi.
β€œFamilia yangu ina ingia kwenye matatizo haya yote kwa ajili ya baba yako. Nina jitahidi kumlinda baba yako ili ake salama kwa maana endapo hiyo video ika patwa na serikali ya Tanzania haijalishi baba yako ni raisi au laa, ataozea jela”
Nabii Sanga alizungumza huku akizima tv hiyo. Jery mwili mzima alihisi ukimuishia nguvu.
β€œNa isitoshe ata hesabika ni msaliti wa nchi. Una jua adhabu ya msaliti ni nini, yeye na familia yake wote wana kwenda na maji. So ukiangalia muunganiko huo una husika na mwanangu, sipo tayari kama baba kuona mwanangu ana uwawa ndani ya familia ya msaliti ndio maana nime amua kwa nguvu zote kuhakikisha nina kulinda wewe, baba yako na familia yangu”
Nabii Sanga alizungumza kwa msisitizo huku akimkazia macho Jery aliye jikuta akiishiwa pozi.
β€œWewe ni mwanaume, mwanangu ni mwanamke, nina hitaji umlinde kwenye maisha yako yote kama ulivyo kula kiapo pale kanisani. Tumeelewana?”
β€œNdio tume elewana”
Nabii Sanga akanyanyuka na akatoka ofisini hapo na kumuacha Jery akiwa kwenye alama ya kujiuliza maswali yaliyo kosa majibu.
***


Jenerali wa jeshi akafika katika kambi ya jeshi kwa usafiri wa helicopter moja kwa moja akapelekwa hadi katika wodi anayo pewa matibabu mrs Sanga.
β€œVipi amepata majeraha makubwa sana?”
Jenerali alimuuliza daktari anaye muhudumia mrs Sanga.
β€œHapana hajapata majeraha makubwa zaidi ya pajani mwake”
β€œSawa hakikisha kwamba ana kuwa salama”
β€œUsijali mkuu”
Mrs Sanga aliye jifanya kama mtu aliye lala aliweza kusikia kila kitu kinacho zungumziwa ndani ya chumba hicho. Jenerali akaingia kwenye chumba walipo Magreth, Josephine, Samson pamoja na Evans akasalimiana nao kwa kupeana mikono na akaanza kuwahoji ni kwa nini walikuwa na mpango wa kumtoa raisi Mtenzi madarakani. Josephine akaanza kusimulia kila jambo kuanzia maono aliyo kuwa akionyeshwa na Mungu juu ya uovu wa raisi Mtenzi akaadithia jinsi walivyo pata ushahidi wa nabii Sanga na familia yake na ukubwa na ubora wajeshi analo litawala.
β€œMuna taka kuniambia kwamba siri hizo mulimuambia mzee Mbogo?”
β€œNdio kwa maana yeye ndio mtu tuliye kuwa tuna muamini na kwa bahati mbaya aliweza kutekwa na katika maono niliweza kuona akiuwawa”
β€œNa nani?”
β€œSijajua ila niliona akiwawa kwa kupigwa risasi. Ina tubidi kutafuta ushahidi wa kudhibitisha ni nani ambaye ni muuaji”
β€œIla nabii Sanga nilikuwa nina mchukulia ni mtu mmoja mwema sana. Ila kumbe ni shetani kupitiliza”
β€œNdio hivyo mkuu. Kuna mengi sana wameyafanya. Tukipata lile faili tuta weza kuwaingiza wote mikononi mwa sheria”
β€œIla tumemshikilia mke wake ita kuwa ni rahisi kwa yeye kutaja siri za familia yake”
Jenerali alizungumza huku akiwatazama Magreth na Josephine.


β€œHiyo ni ngumu kwa yeye kutoboa siri hizo. Yule mwanamke ana kifua cha kuhifadhi siri nyingi. Nime pata wazo moja”


Magreth alizungumza.
β€œWazo gani Mage”
β€œIna bidi tumuachie huru mrs Sanga. Ila Samson nina hisi una weza kumtrack kila anapo kwenda na ni lazima ata elekea kwenye jeshi lao na hapo ndo ita kuwa ni mpango mzuri wa sisi kwenda kusambaratisha kabisa meli ya nabii Sanga.”
β€œMuna picha ya hiyo meli?”
β€œNdio”
Samson akafunua laptop yake na kumuonyesha jenerali wa jeshi meli hiyo kubwa.
β€œAisee hii meli kubwa ya kivita, ili kuuivamia meli hii ina bidi tuwe na meli kubwa kama hii au kupita meli hiii”
β€œKwani Tanzania hatuna hiyo meli?”
β€œHapana hatuna na isitoshe nabii Sanga ana hadi jet za kivita. Yaani dakika hizi za mwisho ndio nime weza kumfahamu vizuri yule mzee. Ila laiti kama ninge mfahamu mapema kabla ya mambo kuwa mabaya kama hivi haki ya Mungu ninge mshuhulikia mapema sana”
β€œJenerali. Una faa kuwa raisi, una uchungu wa kuwa raisi una onaje uka endelea kuwa raisi moja kwa moja”
β€œKikatiba nina weza kuongoza nchi kwa masaa ishirini na nne hadi 48. Baada ya hapo siwezi kuwa raisi na nina paswa kuachia madaraka. Labda itokee tu kwamba raisi ameamua kuachia madaraka basi nita kuwa raisi kwa miezi mitatu kabla ya watu kuingia kwenye uchaguzi. Kwani hadi sasa nchi haina makamu wa raisi wala waziri mkuu”
Josephine akafumba macho yake kwa dakika mbili kisha akafumbua.
β€œUta kuwa raisi wa hii nchi ila kwa sharti moja tu”
β€œSharti gani?”
β€œNi lazima tutafute ushahidi unao tudhibitishia kwamba raisi Mtenzi ana makosa na tukiupata ushahidi huo basi yeye mwenyewe ata achia madaraka na uta msweka jela. Mtu atakaye tusaidia kufanya hivyo ni kumuachia mrs Sanga kuondoka nasi tuta mfwatilia kwa umakini hadi anapo elekea.”
Josephine alizungumza na watu wote wakakubaliana naye na mikakati ya kumuachia mrs Sanga ikaanza ka mwaana yeye ndio ana weza kuwafanikisha kupata kila wanacho kihitaji kwa wakati huu.


****************************************************************************************************************


***


ITAENDELEA


Haya sasa, je mpango wa kumuachia mrs Sanga una weza kuzaa matunda? Je wata fanikiwa kupata ushahidi wa kumfanya raisi Mtenzi kuachia madaraka ndani ya masaa 48 kabla ya jenerali kurudisha madaraka kwa raisi Mtenzi ambaye kwa sasa yupo kizuizini? Usikose sehemu ya 222.
 
SIN 222


Muandishi…………………………………………….EDDAZARIA G.MSULWA(G.Authour)


Age ……………………………………………………18+


Simu………………………………………………… 0657072588(whatsapp) au 0768516188


Website………………………………………………





ILIPOISHIA


β€œKikatiba nina weza kuongoza nchi kwa masaa ishirini na nne hadi 48. Baada ya hapo siwezi kuwa raisi na nina paswa kuachia madaraka. Labda itokee tu kwamba raisi ameamua kuachia madaraka basi nita kuwa raisi kwa miezi mitatu kabla ya watu kuingia kwenye uchaguzi. Kwani hadi sasa nchi haina makamu wa raisi wala waziri mkuu”
Josephine akafumba macho yake kwa dakika mbili kisha akafumbua.
β€œUta kuwa raisi wa hii nchi ila kwa sharti moja tu”
β€œSharti gani?”
β€œNi lazima tutafute ushahidi unao tudhibitishia kwamba raisi Mtenzi ana makosa na tukiupata ushahidi huo basi yeye mwenyewe ata achia madaraka na uta msweka jela. Mtu atakaye tusaidia kufanya hivyo ni kumuachia mrs Sanga kuondoka nasi tuta mfwatilia kwa umakini hadi anapo elekea.”
Josephine alizungumza na watu wote wakakubaliana naye na mikakati ya kumuachia mrs Sanga ikaanza ka mwaana yeye ndio ana weza kuwafanikisha kupata kila wanacho kihitaji kwa wakati huu.





ENDELEA


β€œJe tuna weza kum tracke kila anapo kwenda kwa kutumia njiani gani?”
Josephine aliuliza huku akiwatazama wengine.
β€œSura yake. Ninayo picha yake uso wake hapa basi hata aende popote basi ita kuwa ni rahisi kwetu kum tacke”
Samson alijibu.


β€œKwa hiyo nina weza kumuachia?”
β€œNdio”
β€œSawa ila ina bidi tucheze mchezo hapa. Ina bidi muonnekane kama nyinyi nime waweka chini ya ulinzi. Hiyo ita mpumbaza akili yake na kuhisi kwamba tume wapata nyinyi n ahata kama akiondoka basi ata ondoka akiwa na amani”
β€œSawa mkuu”
Josephine na wezake wakaingizwa katika mahabusu za hapo kambini. Kisha jenerali wa jeshi akaelekea katika wodi aliyo lazwa mrs Sanga na kumkuta akiwa amekaa kitandani. Akampigia saluti ikiwa ni ishara ya kumuheshimimu.
β€œHabari yako makamu wa raisi?”
Mrs Sanga akakaa kimta kwa sekunde kadhaa huku akitafakari heshima hiyo aliyo pewa.
β€œSalama”
Mrs Sanga alijibu kwa upole.


β€œNina imanani kwa sasa una endelea vizuri. Tuna mshukuru Mungu kwa sasa upo salama”
β€œNdio, nahitaji kwenda kupumzika nyumbani, kukaa hapa kuna nikosehesha amani kabisa.”
β€œSawa mkuu ngoja niandae usafiri wa kukutoa hapa”
β€œSihitaji magari mengi. Nahitaji gari moja na dereva mmoja basi ina nitosha”
β€œIla wewe ni makamu wa raisi?”
β€œNdio fanya kama nilivyo kuagiza. Wale washenzi walio niteka wamekamatwa?”
β€œNdio mkuu wapo chini ya uangalizi”
β€œNahitaji kuwaona kabla sijaondoka hapa”
β€œSawa, je una weza kutembea?”
β€œNdio”
Mrs Sanga akasimama huku akiyasikilizia maumivu ya paja lake.
β€œNisaidie kunishika mkono”
Jenerali akamshika mrs Sanga na akachomoa sindano ya dripu la maji iliiyo chomwa katika mkono wake wa kushoto na wakaanza kutembea kuelekea kwenye mahabusu za kambi hiyo ya jeshi.
β€œHawa hapa mkuu”
Mrs Sanga akawatazama Magreth na wezake.


β€œNaomba nizungumze nao”
β€œNi hatari muheshimiwa nikikurusuhusu kuingia ndani”
β€œHapa hapa ila nahitaji kuzungumza na huyo aliye vaa mavzir yake kama spider man”
Mrs Sanga alizungumza kwa dharau kidogo. Taratibu Magreth akasikama na kumsogelea mrs Sanga katika mlango huo wa nondo. Mrs Sanga akamtazama jenerali wa jeshi kwa ishara ya kumuomba aweze kusogea na jenerali akasogea pembeni mita kadhaa kutoka mlangoni hapo.
β€œWewe panya wakati huu ume ingia katika mdogo wa mamba nina kuapia haki ya Mungu ndani ya haya masaa ishirini na nne uta kuwa umesha kuwa mwenyeji kuzimu”
Mrs Sanga alizungumza kwa dharua.
β€œYaani nita hakikisha nina kuua wewe na hao panya wako. Na wewe nita kuua kwa mateso kama uliyo nipatia mimi kenge wewe. Hamkujua kwamba mimi ni makamu wa raisi ehee?”
Mrs Sanga alizungumza kwa kujiamini huku akiwa ameshika moja ya nondo. Magreth akautazama mkono wa mrs Sanga ulio shika nondo hiyo na kumfanya mrs Sanga kuachia nondo hiyo kwa haraka huku akiogopa kushambuliwa.
β€œNaondoka sasa hivi ila nita rudi kwa ajili ya nyinyi panya”
Mrs Sanga alizungumza kisha taratibu akanza kuchechemea na kumfanya jenerali wa jeshi kumsogelea na kumshika mkono na wakaanza kutemebea kuelekea nje. Akamkabidhi kwa dereva mmoja wa jeshi na akaingia ndani ya gari aina ya Jeep.


β€œNaelekea nyumbani kwangu”
Mrs Sanga alimuambia dereva huyo na taratibu wakaondoka kambini hapo.
β€œYaani huyu mwanamke mjinga kweli”
Magreth alizungumza huku wakitoka katika mahabusu hiyo. Wakarudi katika chumba walicho kuwa na Samsona akaanza kazi ya kumtafuta mrs Sanga kwa kutumia satelaite na haikumchukua hata dakika tano akafanikiwa kumuona.
β€œAmeniambia ana kwenda nyumbani kwake”
Jenerali wa jeshi alizungumza huku akitazama tv kubwa iliyopo ndani hapo ikimuonyesha kila anapo elekea mrs Sanga na dereva wa gari hilo la jeshi.


β€œNyumbani kwake kuna kamera nyingi sana, Samson si una weza kuzi hack?”
Evans alizungumza.
β€œYeah hakuna linalo shindikana katika tecnolojia ya sasa hivi”
Samson alizungumza huku vidole vyake vikiminya batani za laptop yake kwa kasi ya ajabu sana.


β€œKila kitu kipo hewani”
Samson alizungumza huku vipande sita vya kamera tofauti tofauti nyumbani kwa nabii Sanga vikionekana kwenye tv hiyo.


β€œDogo upo vizuri sana”


Jenerali wa jeshi alizungumza huku akimtazama Samson usoni mwake.


β€œNashukuru sana mkuu”
Wakashuhudia gari hilo likisimama nje ya gati la nyumba ya nabii Sanga na mrs Sanga akashuka na kuingia ndani na dereva akaondoka.
***


Mrs Sanga akatazama mandhari ya nyumba yake hiyo jinsi yalivyo tulia na akamini kwamba hakuna mtu yoyote ndani hapo. Akatembea kwa kuchechemea hadi ndani. Jinsi walivyo kuwa wameiacha nyumba hiyo siku walipo ondoka ndivyo jinsi alivyo ikuta.


β€˜Ina maana mume wangu haja rudi?’


Mrs Sanga alizungumza kimoyo moyo huku akianza kupandisha gorofani kwa mwendo wa taratibu. Akaingia chumbani kwake na kujilaza kitandani kwa sekunde kadhaa kisha akafungua shelfu iliyopo chumbani hapo na akatoa simu ambayo hairekodiwi mazungumzo yake. Akatafakari kwa sekunde kadhaa kisha akapiga simu katika ofisi ya mume wake iliyopo katika meli. Simu ikaanza kuita na baada ya muda kidogo ikapokelewa.
β€œNi mimi”
Mrs Sang alizungumza.


β€œOhoo boss acha nikuunganishe na mkuu”
Mrs Sanga akasubiria kwa sekunde kadhaa na akaisikia sauti ya mume wake.
β€œMke wangu upo salama?”
β€œYes baby”
β€œOhoo asante Mungu ni nani aliye kuteka?”
β€œNi Magreth na wezake na hivi sasa wame weza kushikiliwa na wanajeshi”
β€œWanajeshi gani?”
β€œWa nchi ya Tanzania”
β€œNa wewe upo wapi?”
β€œMimi nipo nyumbani na jenerali wa jeshi ndio aliye tuma wanajeshi wake wakanisaidia”
β€œMke wangu nina kuomba unisikilize vizuri tena kwa umakini wa hali ya juu. Hivi sasa ninavyo ongea na wewe raisi Mtenzi yupo kizuizini. Nchi ina ongozwa na jeshi na hakuna utawala wa raisi Mtenzi. Mimi, Julieth na Jery tupo kwenye meli mke wangu. Huyo Jenerali ndio adui kwa sasa na hao kina Magreth ata kuwa ana shirikiana nao kwa asilimia mia moja”
β€œOhoo Mungu wangu”
Mrs Sang akasimama kwa haraka na kusimama pembeni ya dirisha la hapo chumbani kwake na kuchungulia nje na kuona ukimya.
β€œSa…saasa nina fanya nini mume wangu?”
β€œNisikilize kwa umakini mke wangu”
β€œNdio mume wangu”
β€œSi una ifahamu njia iliyopo chini ya ardhi hapo nyumbani kwetu?”
β€œNdio”
β€œSasa kusanya kila kilicho muhimu hapo nyumbani kwetu usiache ushahidi wowote uatakao tuweka matatani. Kisha pita katika njia hiyo na utokea baharini na si una weza kuendesha hiyo Triton submarine?”
β€œNdio nina kumbuka mume wangu”
β€œSawa fanya hivyo na kama wata kuwa wamekuachia huru basi tambua wata kuwa wana kufwatilia hata kuku track. Wana weza ku hack hizo kamera za hapo nyumbani, nenda kwenye kile chumba cha mitambu, zima kamera zote”
β€œSawa mume wangu. Ila nina maumivu ya pajani kwa maana nilichomwa kisu cha mguuni”
β€œPole sana mke wangu. Ila fanya hivyo kwa maana hadi sasa hivi mambo sio salama”
β€œSawa”
Mrs Sanga akakata simu, akaingia bafuni na kuoga haraka haraka huku akiwa na wasiwasi. Akavaa suruali, tisheti pamoja na raba za mazoezi. Akazikunja vizuri nywele zake kisha akavaa kofia pamoja na miwani kisha akaingia katika chumba kinacho hifadhia mfumo mzima wa kamer pamoja na umeme wa nyumba hiyo. Akazima kamere zate pamoja na umeme. Kisha akarudi chumbani kwake na kuchukua nyaraka muhimu za mali zao pamoja na kiasi chote cha pesa wanacho kihifadhi ndani hapo. Akaifunga nyumba yao kwa ndani kisha akabeba behi hilo alilo hifadhia pesa pamoja na nyaraka muhimu kisha akaingia kwenye chumba kilichopo chini ya ardhi ambapo ndipo nabii Sanga anapo fanyia sala zake za kihestani. Akaingia kwenye mlago ulio jificha ambao ukitazama kwa kawaida una weza kuhisi ni ukuta tu. Mlango huo unao fanan na ukuta, una batani za siri za kufungulia ambazo nazo pia kwa mtu wa kawaida sio rahisi kuweza kuziona. Baada ya kuufungua mlango huo, akaingia ndani na njia hiyo ya siri sana. Akawasha tochi ya simu yake huku mfuko mwengine akiwa na simu hiyo ambayo mazungumzo yake sio rahisi kunaswa na mtandao wowote. Akaufunga mlango huo kisha akaanza kutembea huku akichechema, hakika halikuwa ni jambo rahisi sana kwake kutembea na maumivu hayo. Kwa mara kadhaa alijikuta akisimama kupumzika huku damu za kidonda chake ziki mtiririka taratibu. Akatembea kwa lisaa moja na eneo la baharini ambapo kuna submarine hiyo inayo ingia watu watatu tu. Akaingia ndani ya submarine hiyo iitwayo, Triton. Akaiwasha huku akishusha pumzi nyingi.


β€œMagreth nita kuua malaya wewe”
Mrs Sanga alizungumza huku taratibu akianza kuindesha submarine hiyo yenye uwezo wa kuingia hadi futi 36000 chini ya bahari hivyo sio rahisi kwa satelaite kuiona.


β€œBaby”
Mrs Sanga alizungumza huku akitazama tv ndogo iliyo pembeni yake inayo muwezesha kuwasiliana moja kwa moja na nabii Sanga aliyopo kwenye meli yake.
β€œNaam”
β€œNimeanza safari sawa vijana wata kusubiria ufike. Mimi nina kwenda Madagascar kuonana na raisi wa Marekani”
β€œSawa mume wangu, ila watoto wapo salama?”
β€œNdio wapo salama”
β€œSawa nina kuja”
Mrs Sanga akaendelea na safari hiyo ya kuelekea ilipo meli yao huku akimuomba Mungu aweze kufika salama na kuonana na familia yake tena.
***


β€œMtafute ujue yupo wapi?”
Jenerali wa jeshi alizungumza huku akizunguka zunguka ndani ya chumba hicho. Hakika hapakuwa na mtu aliye weza kuamini kwamba mrs Sanga ana weza kupotea katika mtego wao walio weza kuupanga.
β€œIna bidi twende kwenye hiyo nyumba yake”
Magreth alizungumza huku akihahaha.
β€œNita kwenda nawe”
Evans alizungumza na jenerali wa jeshi akawakubalia ombi lake hilo. Wakakabidhiwa pikipiki moja ya jeshi na Evans akawa dereva na wakaondoka kambini hapo kwa kasi ya ajabu kuelekea nyumbani kwa nabii Sanga. Ndani ya dakika arobaini wakafika nyumbani hapo. Wakajaribu kufungua geti ila wakashindwa.


β€œTuzunguke huku”
Evans alizungumza na wakaelekea eneo alilo ruka siku aliyo fika nyumbani hapo kwa nabii Sanga. Wakaingia kwa umakini ndani huku kila mmoja akiwa na silaha yake mkononi. Wakajaribu kufungua mlango wa kuingilia ndani ila wakakuta ukiwa ume fungwa. Evans akavunja kioo cha moja ya dirisha kwa kutumia kitako chake cha bunduki kisha akafungua kitasa cha dirisha moja wapo la sebleni na wakaingia ndani. Wakaanza kukagua sehemu moja baada ya nyingine katika nyumba hiyo ila hawakuweza kuona kitu chochote.
β€œShitii hayupo”
Magreth alizungumza huku akimwagikwa na jasho.
β€œIna kuwaje sasa”
β€œHata sielewi. Ngoja”
Magreth akaona ngazi zinazo elekea chini, tarati wakaanza kushuka katika ngazi hizo na kuingia katika chumba kilicho tulia na kina michoro kadhaa ambayo ina ashiria ushetani.


β€œWhat’s fuc**”
Evans alizungumza huku akishangaa sana.
β€œIna maana huyu jamaa nguvu zake za unabii ana tumia nguvu za kishetani?”
Magreth aliuliza.


β€œNdio maana yake. Hembu piga picha”
Magreth akatoa simu yake mfukoni na kuanza kupiga picha michoro yote iliyomo ndani ya chumba hicho na akamtumia Samson kwenye simu yake.
β€œSasa ata kuwa amekimbilia wapi?”
β€œHata sifahamu ila nina hisi kuta kuwa na njia ya siri katika hili jumba”
Evans alizungumza huku akiendelea kuangaza angaza ndani ya chumba hicho. Hawakuweza kugundua chochote kama kuna mlango wa siri kwa maana mlango huo una fanania na ukuta. Wakatoka katika chumba hicho na kuendelea kutafata kwenye vyumba vingine ila kwa bahati mbaya hawakuweza kuona kitu chochote na wakaamini kabisa ndio tayari wamesha mpoteza mrs Sanga.
***


Kwa mara kadhaa macho ya mlinzi yana Mtazama Leila aliye lala katika moja ya chumba kilichopo chini kabisa ya meli hiyo. Uzuri wa umbo la Leila hakika uka mfanya mlinzi huyo kumpangia mipango ya kupata penzi lake. Akatazama saa yake ya mkononi ina muonyesha ni saa mbili usiku. Akafungua chumba hicho na kuingia ndani, Leila akaka kitako huku akimtazama mwanaume huyo mrefu aliye jazia misuli yake huku kifuani mwake akiwa amevalia jaketi la kuzuia risasi ambazo kuna magazine kadhaa za bunduki ame zichomeka pamoja bastola moja. Mwanajeshi huyo akaiweka bunduki yake chini huku akiwa amejawa na tabasamu pana sana.
β€œShiiii usipige kelele kwa maana nita kuua”
Mwanajeshi huyo alizungumza huku akianza kumsogelea Leila kwa mwendo wa taratibu. Leila akahisi woga uki mtawala sana kwa maana kwenye maisha yake haja wahi kuingiliwa na mwanaume pasipo ridhaa yake. Taratibu mwanajeshi huyo akamvaa Leila na kumlaza chali, Leila akaanza kufurukuta huku akibana mapaja yake. Mwanajeshi huyo ika mlazimu kutumia nguvu zake kuyapanua mapaja ya Leila ambayo ameyabana kwa nguvu sana. Katika kurupushani hizo Leila akachomoa bastola iliyo chomekwa kwenye jaketi hilo, japo ni mara yake ya kwanza kutumia bastola ila akakumbuka baadhi ya filamu za mapigano alizo wahi kuzitazama kwenye luninga. Akavata trigal ya bastola hiyo iliyo fungwa kiwambo cha kuzia risasi na kusababisha risasi moja kutoa na kumpata mwanajeshi huyo barabara kichwani mwake na kuangukia pembeni yake. Leila akanyanyuka huku mwili ukimtetemeka kwa woga, hakuwahi kufiirika kama ata kuja kuua siku. Baada ya dakika kama tano akapata wazo, akaanza kupapasa mwanajeshi huyo mifukoni mwake na kile anacho kitafuta kwa bahati nzuri akafanikiwa kupata simu aina ya iphone.


β€˜Finger print’


Leila alizungumza huku akishika kidole gumba cha mwanajeshi huyo na kukigusisha katika sehemu ya kufungulia lock hiyo ya kutumia kidole kwa bahati nzuri simu ikafunguka. Leila akaiingiza namba ya Evans kwa haraka kwenye simu yake na kuipiga na kwa bahati nzuri akakuta simu hiyo ina patikana hewani.
β€œHaloo”
β€œGeorge ni mimi”
β€œLeila!!?”


Evans aliuliza kwa mshanagao mkubwa sana kwa maana hakutarajia kupigiwa simu na Leila kwa muda na wakati kama huo.


****************************************************************************************************************


****


ITAENDELEA


Haya sasa, Leila amefanikiwa kumpigia simu Evans, je ata fanikiwa kutoka salama kwenye meli hiyo ikiwa ni meli iliyo jaa wana jeshi wengi sana? Usikose sehemu ya 223.
 
SIN 223


Muandishi…………………………………………….EDDAZARIA G.MSULWA(G.Authour)


Age ……………………………………………………18+


Simu………………………………………………… 0657072588(whatsapp) au 0768516188


Website………………………………………………





ILIPOISHIA


Katika kurupushani hizo Leila akachomoa bastola iliyo chomekwa kwenye jaketi hilo, japo ni mara yake ya kwanza kutumia bastola ila akakumbuka baadhi ya filamu za mapigano alizo wahi kuzitazama kwenye luninga. Akavata trigal ya bastola hiyo iliyo fungwa kiwambo cha kuzia risasi na kusababisha risasi moja kutoa na kumpata mwanajeshi huyo barabara kichwani mwake na kuangukia pembeni yake. Leila akanyanyuka huku mwili ukimtetemeka kwa woga, hakuwahi kufiirika kama ata kuja kuua siku. Baada ya dakika kama tano akapata wazo, akaanza kupapasa mwanajeshi huyo mifukoni mwake na kile anacho kitafuta kwa bahati nzuri akafanikiwa kupata simu aina ya iphone.


β€˜Finger print’


Leila alizungumza huku akishika kidole gumba cha mwanajeshi huyo na kukigusisha katika sehemu ya kufungulia lock hiyo ya kutumia kidole kwa bahati nzuri simu ikafunguka. Leila akaiingiza namba ya Evans kwa haraka kwenye simu yake na kuipiga na kwa bahati nzuri akakuta simu hiyo ina patikana hewani.
β€œHaloo”
β€œGeorge ni mimi”
β€œLeila!!?”


Evans aliuliza kwa mshanagao mkubwa sana kwa maana hakutarajia kupigiwa simu na Leila kwa muda na wakati kama huo.





ENDELEA


β€œNdio ni mimi?”
Leila alizungumza kwa kubabaika.”
β€œUpo wapi?”
β€œSijui nipo wapi ila nime tekwa na wanajeshi”
Leila alizungumza huku akitetemeka sana.
β€œTulia niambie vizuri. Umetekwa na wanajeshi wanao fananijae?”
β€œNgoja nikutumie picha zao”
Leila akampiga picha mwanajeshi huyo kisha akamtumia Evans kwa njia ya whatsapp”
β€œUme ziona baby?”
β€œYaa nime ziapta sasa fanya hivi. Katika hiyo simu washa kitu kilicho andikwa location na hakikisha kwamba simu una iacha on”
β€œSawa baby, mwenzio nina ogopa”
β€œUsiogope mpenzi wangu nina kuja kukuokoa”
Leila akafanya kama alivyo elekezwa na Evans.
β€œUsichelewe fanya haraka”
β€œOkay, katika hicho chumba kuna choo?”
β€œNdio baby”
β€œBasi ingiza huo mwili wa huyo mwanajeshi ndani ya chuoo. Kaa na hiyo bastola ulinzi binafsi”
β€œSawa”
Leila akakata simu na kuanza kuuvuta mwili wa mwanajeshi huyo kwa nguvu zake zote hadi ndani ya choo anacho kitumia. Akaanza kufuta damu zote zilizo mwagika kisha akaiweka bastola hiyo chini ya mto wake pamoja na simu hiyo kisha akajilaza kama alivyo kuwa amelala mwanzoni huku moyoni mwake akimuomba Mungu George aweze kufika eneo hilo haraka sana.


***


β€œSamson ume pata hiyo location ya namba ilipo tokea”


Evans alizungumza mara baada ya simu kukatika.
β€œDakika moja”
Samson alijibu huku akiwa bize sana na laptop yake.
β€œBINGOOOO”
Samson alizungumza huku akijawa na tabasamu.


β€œKazi nzuri sana Samson”
Josephine alizungumza huku akiwa amejawa na tabasamu pana. Kila mtu akaona jinsi eneo la meli hiyo ilipo.


β€œDuu ipo mbali sana hiyo meli”
Jenerali wa jeshi alizungumza huku wakitazama meli hiyo.
β€œMkuu naomba ramani”
Evans alizungumza na akaagizwa mwanajeshi mmoja ambaye baada ya dakika tano akarudi akiwa na ramani kubwa. Evans akaitandaza ramani hiyo juu ya meza kubwa.


β€œSisi tupo hapa?”
Evans slizungumza huku akigusa ramani ya nchi ya Tanzania. Kutoka hapa tutapita kaskazini kwa kisiwa cha Madagascar kisha ndio tuna ingia kwenye zone ya hii meli.”
Evans alizungumza huku akionyesha eneo wanalo paswa kupita katika ramani hiyo.
β€œHii tunayo iendea sasa ni vita. Ina bidi majeshi yaweze kujipanga kuhakikisha kwamba kuanzia angani, ardhini na majini tuna pambana kuhakikisha kwamba adui haingizi shambulizi kwetu na pia tuna mpiga adui. Kazi nzuri mume fanya ila kwa sasa ni wakati wa jeshi kuchukua nafasi”
Jenerali wa jeshi alizungumza huku akiwatazama Josephine na wezake.
β€œIna maana una tutoa kwenye hii oparesheni?”
Magreth aliuliza kwa sauti ya unyonge.


β€œHapanana siwezi kuwatoa. Ila nime waonyesha jinsi na namna ambavyo nchi ina elekea.”
Josephune akasimaam huku akiwa na tabasamu.
β€œMungu amenionyesha wamba hii vita tuna kwenda kushinda na huu ndio mwisho wa nabii Sanga. Nchi ya Tanzania ita kwenda kuwa na nguvu pamoja na uwezo kuanzia uchumi, kijeshi na mambo mengine. Yote hayo yatakamilika chini yako jenerali Saidi Mollel”
Josephine alizungumza huku akimtazama jenerali Saidi Mollel, Mmasai wa kwanza katika nchi ya Tanzania kuwa katika cheo kikubwa cha ujenerali wa jeshi.
β€œNina shukuru. Nina waomba niweze kukutana na wakuu wa vitengo vyote. Josephine nina imani uta wawakilisha wezake kwenye kikao hicho”
β€œSawa”
β€œAu nime kosea kumchagua yeye pekee?”
β€œHapana ni jambo jema na zuri pia”
Josephine na jenerali Mollel wakatoka ofisini hapo na kuingia katika ukumbi wa mikutano na baada ya dakika tano wakuu majeshi ya anga, ardhini na majini wakawa tayari wamefika kambini hapo kwa ajili ya kikao hicho cha dharura.. Wakaanza kupanga mikakati ya namna gani wanavyo weza kufikika meli ya nabii Sanga na mashambulizi yakafanyika pasipo ya yeye kufanya mashambulizi katika nchi ya Tanzania na kuwadhuru wananchi. Kikao hicho kikachukua masaa matatu mfululizo na baada ya hapo vikosi vya anga, majini na nchi kavu vikaandaliwa.


β€œVipi kikao kime kwenda vizuri?”
Magreth alimuuliza Josephine.
β€œYaa na mikakata iliyo pangwa tuna imani kwamba nabii Sanga ana kwenda kufa kifo kibaya sana.
β€œJe sisi tuta kuwa kwenye kikosi gani?”
Evans aliuliza.
β€œNime weza kuwaombe nafasi wewe na Magreth katika kikosi cha majini. Kwa kume andliwa mpango huo ambao kuna meli kumi na mbili. Sita katika hizo ni meli za silaha na mabomu makubwa makubwa ambazo zina shambulia kwa masafa marefu. Meli nne ni Aircraft Carrier ambazo kila moja ime bebe jeti za kivita pamoja na helicopter za kivita. Mbili zilizo salia ni submarine ambazo zita kuwa katika mashabulizi yanayo tokea chini ya bahari”
β€œ***** walai, yule mzee ana kwenda kufa vibaya sana”
Evans alifurahia kwa maana watu wote ndani ya chumba hicho wana mchukia nabii Sanga na familia yake. Jenerali wa jeshi akarudi ikulu majira ya saa nane usiku na kukuta hali ni shari kabisa kwani ulinzi alio uacha ikulu hapo wa vijana wake hakika walinzi watiifu wa raisi Mtenzi hawakuweza kufanya chochote. Majira ya saa kumi kamili usiku vikosi vyote kama ilivyo pangwa vikaingia majini na kuanza safari ya kuisaka meli ya nabii Sanga. Magreth na Evans nao ni miongoni mwa wanajeshi waliopo katika moja ya meli ya kivita iliyo sheheni wanajeshi wa majini walio jiandaa tayari kwa vita hiyo. Josephine na Samson nao wakaingia ikulu na moja kwa moja wakaelekea commanding room kwa ajili ya kujishuhudia jinsi oparesheni hiyo inavyo kwenda kwa maana katika kila meli kume fungwa kamera inayo lete mawasiliano ya moyo kwa moja ikulu.
β€œMuheshimiwa raisi ni muda wa kuwa hutubia wana jeshi wako”
Mwanajeshi mmoja alizungumza huku akimkabidhi jenerali Mollel kipaza sauti ambacho akizungumza watu wote walipo kwenye meli hizo za kivita pamoja na submarine wana sikia anacho kizungumza. Jenerali Mollel ambaye bado ni raisi wa muda akashusha pumzi nyingi sana huku akikitazama kipaza sauti chake.
β€œHii ni vita. Ni vita ambayo sote tuna kwenda kushinda, ni kosa kubwa sana kwa adui kuingia kwenye nchi yetu na kukanyaga ardhi ya nchi yetu alafu sisi kama walinda usalama tuka shindwa kurudisha mashambulizi kwa adui yetu. Tuta mpiga Sanga na wanajeshi wake, hana nguvu juu ya nchi yetu. Hii ni oparesheni ya kuua na sio ya kukamata. Nina hitaji kuona mwili wa wanabii Sanga ukiwa mikononi mwenu na nyinyi nyote nina hitaji muweze kurudi salama na kuendelea maisha yenu na familia zetu. Mungu ibariki Tanzania, Mungu wabariki wapiganaji wetu. AMEN”
Baada ya jenerali Mollel kuzungumza watu wote wakasimama ndani ya ukumbi huo na wimbo na wimbo wa taifa ukaanza kuimbwa kuhakiksiha wana wapa moyo na munkari wanajeshi wote wanao kwenda kupambana katika vita hiyo.


Magreth akajikuta machozi yakimbubujika usoni mwake. Uchungu ulio changanyikana na hasira na jinsi anavyo usikia wimbo wa taifa hakika akatamani hata kuweza kuifikia meli hiyo ya nabii Sanga kwa wakati huo huo. Wanajeshi wote walimo ndani ya meli hiyo wame simama wima huku kila mmoja akiimba wimbo wa taifa. Wimbo wa taifa ulipo isha wakaanza kushangulia kwani katika vita kuna mambo mawili tu ambayo hutokea kurudi ukiwa hai au ume kufa.


***


β€œMama nina hisia mbaya na hii siku”
Julieth alizungumza huku akimtazama mama yake aliye lala kitandani huku katika paja lake akiwa amezungushiwa bandeji, kwani ni masaa manne yame pita toka alipo fika katika meli hiyo.
β€œKwa nini?”
β€œYaani sielewi tu mama ila nina hisia mbaya sana hata sielewi”
β€œMwanangu acha woga na wasiwasi. Hili ndio eneo salama kabisa ambalo hakuna mtu yoyote atakaye weza kutufikia”
β€œNo mama nina hisia mbaya na wewe una jua nikiwa nina hisia mbaya ni lazima kuwe na jambo lina tokea.”


Julieth alizungumza kwa msisitizo hadi machozi yakaanza kumlenga lenga. Mrs Sanga akamtazama mwanaye na akaanza kuamini juu ya jambo analo lizungumza binti yake.


β€œUna waza nini?”
β€œSijui ni nini kinacho nijia kichwani mwangu ila nina jisikia vibaya tu”
β€œMume wako kwanza yupo wapi?”
β€œOfisini”
β€œAmetambua kwamba sisi ni kina nani?”
β€œAmetambua kidogo sana ila hajajua mengi kuhusiana na sisi”
β€œMume wako ni kijana mzuri sana. Kijana ambaye una paswa kuwa naye kwenye maisha yenu yote. Julieth”
β€œBee mama”
β€œNina kuomba umpende sana Jery. Pale alipo wewe ndio mdugu yake wa pekee uliye salia. Ume nielewa mwanangu?”
β€œNdio mama ila mbona hujali juu ya jambo niliko kueleza”
β€œHuo ni wasiwasi wako tu. Ila usiwe na shaka Hii meli ni kubwa mwanangu, mimi na baba yako ilitugarimu mabilioni ya dola kuinunua hivyo ina ulinzi wa kutosha na wala usijali”
Mrs Sanga alimshawishi Julieth hadi wasiwasi ukapungua. Jery kwa maraca kadhaa ana irudia rudia kuitazama video ya baba yake jinsi anavyo muua mzee Mbogo. Mzee ambaye alikuwa karibu sana na familia yake kabla hata yeye hajazaliwa. Kifo cha mzee Mbogo hakika kina uumiza moyo wake hadi akajutia kuwa na baba kama mzee Mtenzi. Jery akaiingiza video hiyo kwenye simu yake huku akihisi mapigo yake ya moyo yakimuenda kasi sana.


β€œIna bidi niwalinde hawa nilio nao”
Jery alizungumza huku akimuwazia Shani ambaye ana ujauzito wake pamoja na Julieth. Katika mawazo yake akamkumbuka Josephine, aliye kuwa mshauri namba moja wa baba yake na pia ni binti mwenye uwezo wa kuona maono. Akaitafuta namba ya Josephine katika rekodi za simu yake na akafanikiwa kuipata. Akaitazama kwa sekunde kadhaa kisha akampigia. Jambo la kumshukuru Mungu simu ya Josephine ikapatikana.
β€œHaloo”


Sauti ya Josephine ilisikika vizuri masikioni mwake.
β€œNi mimi”
β€œJery”
β€œYes ni mimi. Nina kutumia video moja ambayo ita kusaidia na pia nina kuomba sana uweze kumsaidia Shani katika kipindi hichi ambacho sinto kuwepo”
β€œUpo wapi kwani Jery?”
β€œSiwezi kukuambia kwa sasa ila nakuomba sana uweze kumsaidia Shani”
β€œSawa nina kuhaidi nita msaidia”
Jery akaka simu kisha akamtumia Josephine video ya ukatili alio ufanya baba yake, kisha akazima simu yake. Julieth akaingia ofisini hapo.
β€œMume wangu nina wasiwasi”
β€œWasiwasi wa nini?”
β€œSijui nina hisi kuna jambo baya lina weza kutokea ila nina muambia mama yeye ila nina muona kama hajali”
β€œSo wewe una hitaji tufanye nini?”
β€œNahitaji tundoke”
β€œTuelekee wapi?”
β€œPopote ila nina hitaji tuondoke”
Jery akajishauri kwa sekunde kadhaa.
β€œTwende Madagascar kisha tuta fanya process za kuelekea nchini Marekeni tukaishi huko kwa maana nina uraia pia wa Marekenia”
β€œWazo zuri mume wangu, twende tuka muambie mama”
Jery na Julieth waka elekea chumbani kwa mrs Sanga na kumueleza juu ya ombi lao hilo.
β€œMimi nime wakubalia ila je baba yenu atawakubalia”
β€œNina uhakia ata kubali na nita kwenda kuoanan naye huko huko Madagascar”
Julieth alizungumza kwa msisitizo
β€œSawa ila si una fahamu akaunti zetu zote?”
β€œNdio mama”
β€œNiwatakie safari njema mimi nita msubiria baba yako hapa hapa kwenye meli”
β€œSawa mama”
Jery na Julieth wakajindaa kishaa wakaondoka na helicopter kuelekea nchini Madagascar.


***
β€œMkwe wangu na mwanangu wa kike ndio watu wa muhimu sana kwangu kwa kipindi hichi. Wapatie hifadhi ya kudumu katika nchi yako na serikali yako isiweze kufwatilia pesa zao ni wapi zilipo tokea. Endapo uta kubaliana na hilo wala huto weza kusikia nikitoa siri zako kwa mtu yoyote”
Nabii Sanga alizungumza huku akimtazama raisi wa Marekeni katika kikao hicho cha siri sana ambacho hata raisi wa nachi hiyo ya Magascar hafahamu kama raisi wa Marekeni yupo nchini kwake.
β€œHilo halina shaka, endapo uta kiuka makubaliano yetu basi binti yako na mkweo nita waua?”
β€œHilo halito weza kutokea”
β€œSawa”


Nabii Sanga na raisi wa Marekani wakatia saini katika mikataba waliyo kubaliana kisha nabii Sanga akaondoa katika hoteli hiyo akiwa na walinzi wake wawili anao waamini. Akawasha simu yake na kukuta ujumbe wa meseji kutoka kwa mke wake ukimueleza kwamba mwanaye na mkwe wake wapo njiani kuelekea Madagascar .


β€œHuu ni ujinga gani sasa?”
Nabii Sanga alizungumza huku akikaa siti ya nyuma ya gari hilo aina ya Ranger rover sport.


β€œNina omba hilo faili”
Mlinzi wake akamkabidhi fiali lililo mkataba huo. Akapiga picha kadhaa kwa simu yake kisha akamtumia Julieth na akampigia simu.
β€œMupo wapi?”
β€œNdio tuna karibia kuingia Antananarivo?”
β€œSawa njooni hotelini, nina kuandikia jina la hoteli”
β€œHaya”
Nabii Sanga akaelekea hadi kwenye hoteli aliyo kodisha chumba. Baada ya lisa amoja Jery na Julieth wakafika hotelini hapo.
β€œNi kwa nini mume amua kuondoka?”
Nabii Sanga aliwauliza huku akiwakazia macho.
β€œBaba nime kosa amani kabisa ya kuishi mule kwenye meli. Mimi na mume wangu tume kubaliana kuelekea nchini Marekani”
β€œMarekeni muna hisi ndio eneo mutakalo kaa kwa amani?”
β€œNdio”
Nabii Sanga akawakabidhi mkataba huo alio ingia na raisi wa Marekani.
β€œNina watakia maisha mema na tuta wasiliana pale mitakapo kuwa muna hitaji msaada wetu. Kwa sasa ngoja nirudi kwenye meli nika onane na mama yenu. Nina wapenda sana”
Nabii Sanga alizungumza kwa hisia kali kisha akawakumbatia kwa pamoja Jery na Julieth kisha akaondoka hotelini hapo na kurudi eneo ilipo meli yake.


***


Machozi yakazidi kumwagika Josephine kila anavyo itazama video raisi Mtenzi akimuua mzee Mbogo. Toka atumie video hiyo ni lisa ana nusu ila hajamuonyesha mtu yoyote. Akarudi katika commanding room na akamuita jenerali Mollel kwa ishara.
β€œVipi mbona macho mekundu sana”
β€œCleopatra yupo wapi?”
β€œAme pumzika kwa sasa”
Taratibu Josephine akamkabidhi jenerali Mollel simu yake yenye video aliyo tumiwa na Jery. Jenerali Mollel macho yakamtoka mikono ikaaanza kumtetemeka kwa hasira huku mapigo ya moyo yakimuenda kasi sana, kwani alisikia tu jujuu kwamba mzee Mbogo ame uwawa na nabii Sanga ila kumbe muuaji halisi ni raisi Mtenzi ambaye kwa sasa yupo chini ya ulinzi kwa muda na itakapo timu asubuhi basi raisi Mtenzi ata rudi kwenye nafasi yake ya uraisi kama kawaida.


****************************************************************************************************************


****


ITAENDELEA


Haya sasa, wanajeshi wa Tanzania wapo safarini kuelekea ilipo meli ya nabii Sanga kwa ajili ya mapambano na jeshi la nabii Sanga. Jenerali Mollel naye ame shuhudia video ya rafiki yake kipenzi mzee Mbogo akiuliwa na raisi Mtenzi na yame baki masa machache kabla ya raisi Mtenzi kurudi madarakani je ata rudi? ZIME BAKI SEHEMU MBILI ZA MWISHO HIVYO Usikose sehemu ya 224.
 
SIN 224


Muandishi…………………………………………….EDDAZARIA G.MSULWA(G.Authour)


Age ……………………………………………………18+


Simu………………………………………………… 0657072588(whatsapp) au 0768516188


Website………………………………………………





ILIPOISHIA


β€œVipi mbona macho mekundu sana”
β€œCleopatra yupo wapi?”
β€œAme pumzika kwa sasa”
Taratibu Josephine akamkabidhi jenerali Mollel simu yake yenye video aliyo tumiwa na Jery. Jenerali Mollel macho yakamtoka mikono ikaaanza kumtetemeka kwa hasira huku mapigo ya moyo yakimuenda kasi sana, kwani alisikia tu jujuu kwamba mzee Mbogo ame uwawa na nabii Sanga ila kumbe muuaji halisi ni raisi Mtenzi ambaye kwa sasa yupo chini ya ulinzi kwa muda na itakapo timu asubuhi basi raisi Mtenzi ata rudi kwenye nafasi yake ya uraisi kama kawaida.





ENDELEA


β€œNifwate”
Jenerali Mollel alizungumza huku wakitoka ndani ya chumba hicho na Josephine akaanza kumfwata kwa nyuma. Moja kwa moja wakaingia katika chumba alicho fungiwa raisi Mtenzi. Taratibu Raisi Mtenzi akanyanyuka kitandani alipo jilaza na kukaa kitako huku akimshangaa Josephine aliye wesza kufika eneo hilo.


β€œHuyu msaliti ume mtoa wapi?”
Raisi Mtenzi aliuliza kwa sauti ya ukali huku akimtazama Josephine usoni mwake. Jenerali Mollel akamkazia macho raisi Mtenzi hasdi raisi Mtenzi akahisi kwamba kuna tatizo.


β€œNini mbona una nitazama hivyo?”
Raisi Mtenzi aliuliza kwa kujistukia.


β€œMuheshimiwa raisi kwenye kipndi chako chote ulicho fanya kazi na mimi nilisha wahi kukukosea?”
Jenerali Mollel aliuliza.


β€œHapana”
β€œHuyu binti hapa alisha wahi kukukosea?”
β€œNdio, wewe si una ona ni msaliti kabisa. Ita kuwa ni jambo zuri ukamuingiza magereza na asubuhi nikirudi kwenye kiti changu ata kuwa mtu wa kwanza kumuhukumu”
β€œBaada ya kufunikwa na kifusi ni wengi walhitaji kukutoa madarakani ikiwemo makamu wako bwana Madenge Jr. Nilishangaa na kuhisi kwamba ana fanya makosa. Mimi na Magreth tuliweza kukutoa kwenye mikono ya kifo, tukahatarisha maisha yetu. Nilifunga bila kula kwa ajili ya kukuombea mtu kama wewe na Mungu aliweza kuyasikia maombi yangu na kweli ukarudi kwenye kiti chako. Ila kwa nini Mungu hakunionyesha kwamba wewe ni mtu mmbaya na nisinge jaribu kujihusisha kabisa na wewe na ninge endelea na maisha yangu huko mtaani?”
Josephine alizungumza huku akimwagikwa na machozi mwake.


β€œBinti usiniletee uchuro. Hata ulie machozi ya damu ni lazima nikuhukumu na kukupeleka jela”
β€œJela, una hisi nina stahili kukaa jela. Unavyo ona una stahili kuendelea kuwa raisi wa hii nchi, unavyo jihisi una akili iliyo timia kuongoza hili taifa. Mungu alivyo kupa nafasi ya kuwa raisi, nawe una itumia vibaya usidhani ata endelea kuwaona watu wake wakiendelea kuteseka kwa watu kama wewe. Ni lazima ata kushusha tu na ata mpandisha mwengine ambaye ana weza kufikisha hii nchi kwenye ahadi ya hadhina aliyo tukusudia Watanzania tuifikie.”
Josepehine alizungumza kwa uchungu sana.


β€œUli muua mwanao, ukaona haitoshi. Ukataka kumuua mkwe aliye beba mimba ya mwanao, ukaona haitisho ukamuua hadi mzee Mbogo. Mtu aliye yatoa maisha yake, muda wake kwa ajili ya hii nchi. Mtu aliye weza kukuonya juu ya kuwashambulia Al-Shabab na ukakataa na mwishowe waka ua mamia ya watu hapa Dar es Salama na kutia hasara ya majengo mengi. Bado una hisi wewe ni rahisi ehee?”
β€œBinti funga kinywa chako kabla sija kuvuruga huo uso. Na sija muua Mbogo kama huyo Mungu wako wa kipimbavu ndio aliye kuonyesha basi muambie arudie kukuonyesha tena. Mpumbavu wewe”
Raisi Mtenzi alizungumza kwa kujiamini huku akitaka kumsogelea ila Jenerali wa jeshi akachomoa bastola yake kiunoni na kumnyooshea raisi Mtenzi.
β€œWewe mpumbavu ume toa wapi ujasiri wa kunionyeshea mimi bastola. Kumbuka hata kama nipo kizuizini usisahau nguvu yangu na tambua kwamba mimi ndio niliye kufanya uwe hapo”
Raisi Mtenzi alizungumza kwa kufoka sana.
β€œNina tambua hilo ila kuanzia hivi sasa ina bidi uandike barua ya kujiudhuru”
β€œMseng** kweli wewe. Una hisi nilivyo kua nina hangaika huko kuomba kura ulinisaidiaa?”
Jenerali Mollel akatoa simuya Josephine mfukoni mwake na kuiweka video ya raisi Mtenzi akimuua mzee Mbogo. Raisi Mtenzi akastuka huku akihisi kama moyo wake una kwenda kupasuka kwa mshangao huo.


β€œHii video ya kumuua mkuu wa kitengo cha NSS ndio kidhibitisho kwa jamii kwamba wewe ni mtu wa aina gani. Mbili uta hukumia kwa hii video kwa maana si rahisi wala mtu yoyote ambaye yupo juu ya sheria hapa nchini. So hadi ina timu saa moja kamili asubuhi nina hitaji kuiona barua yako ya kujiudhuru nafasi ya uraisi na nita kusemehe kwa heshima yako ila la sivyo ninge kufungulia mastaka na sheria ya nchi nina imani kwamba una ifahamu, uta nyongwa hadi kufa.”
Jenerali Mollel maraa baada ya kuzungumza hivyo akashusha bastola yake chini na kuirudisha kiunoni mwake. Hakika raisi Mtenzi alihisi maumivu makali sana kwenye moyo wake. Hakuelewa ilikuwaje hadi nabii Sanga akaamua kumrekodi. Taratibu akalala kitandani huku Josephine akimtazama kwa macho ya hasira.
β€œMuuaji mkubwa, Mungu amenionyesha hufai kuwa raisi wa hii nchi. Ubinafsi ume kutawala huku ukijidai ni mzalendo wa nchi kumbe ubinafsi tu”
Josephine mara baada ya kuzungumza maneno hayo akatoka ndani hapo.


β€œEndapo uta kuwa umesha fanya maamuzi kwenye kichwa chako. Uta gonga mlango na kijana wangu ata kusikilza na ata kuja kuniita. Angalizo, usifanye jambo lolote la kiupuuzi kwa maana mwanao yupo kwenye mikono ya nabii Sanga ambaye kwa sasa tume fahamu kila aina ya uchafu alio ufanya katika hii nchi na hivi ninavyo zungumza. Wanajeshi wangu wapo njiani kuifwata meli ya nabii Sanga na kumpiga”
β€œNgo….o…ja kwanza Mollel”
Raisi Mtenzi alizungumza kwa upole na suati iliyo jaa kigugumizi.


β€œNakusikiliza”
β€œUmesema ume fahamu uchafu wa nabii Sanga”
β€œNdio, hapa ndio nime pata picha ni kwa nini ulishindwa kutoa amri ya wanajeshi kuwakabili wanajeshi wa nabii Sanga. Ina maana una mjua vizuri”
β€œHapa mimi nina mjua kama mkwe mwenzangu”
β€œOhoo mkwe mwenzako?”
β€œNdio”
β€œJe wanajeshi wake?”
β€œNi…ni…liwaona na….na…..nilifika kwenye meli yake”
β€œOhoo kwa maana ulifahamu kwamba ni mtu hatari kwa ajili ya hii nchi. Alijifanya kwamba yupo juu ya sheria na wewe raisi kama msimamizi wa sheria za nchi ukawa una kenua kenua meno. Kwa nini ume kuwa hivyo, wewe sio yule Mtenzi ninaye mfahamu. Jasiri mwenye maamuzi ya uhakika hata yakiwa ni magumu ila una amua. Kwa nini uliamua kumuua mtu ambaye ndio mkono wako wa kulia, uliohifia kukupindua au?”
Jenerali alizungumza kwa msisitizo na jinsi sauti yake ilivyo nzito hadi raisi Mtenzi akahisi ina mtetemesha masikioni mwake.
β€œMtoto wa Mbogo yupo hapa, ila sinto muambia chochote wala kumueleza chochote juu ya hii video kwa maan ani unyama mkali sana ulio ufanya kwa baba yake na una jua jinsi alivyo kuwa ana kuchukulia yule binti. Akijua juu ya hili ni lazima ata kustaki na kitakacho fwata una kijua”
Jenerali mara baada ya kuyazungumza maneno hayo akaanza kutembea kuelekea mlangoni.
β€œMollel”
β€œNaam”
β€œNina shukuru β€œ
β€œKwa lipi?”
β€œKwa kila kitu”
Jenerali Mollel akamtazama raisi Mtenzi jinsi alivyo jikausha.
β€œNaelewa kipindi unacho pitia. Nabii Sanga alijaribu kukutumia yeye ili kupata nguvu kwenye hii nchi. Ndio maana wanajeshi wasio rasmi walikuwa wana randa randa kwenye hili jiji. Ila nchi ipo salama na hakuna panya hata mmoja ambaye ana weza kukatiza kwenye mipaka ya hii nchi”
β€œNina ombia moja”
β€œNakusukiliza”
β€œNina kuomba katika mapambano hayo mwanangu na mkwe wake waweze kuwa hai. Nina kuomba hata mutakapo wapata nina kuomba sana muweze kuwaachia huru. Hilo ndio ombi langu la mwisho nikiwa kama raisi na baba anaye mpenda mwanaye”
Jenerali Mollel akashusha pumzi huku akimtazama raisi Mtenzi usoni mwake.
β€œNime kuelewa muheshimiwa”
Jenerali Mollel akasimama wima na akapiga saluti kisha akaanza kutembea kuelekea mlangoni.
β€œKama itawezekana nina omba nishuhudie hiyo oparesheni jinsi inavyo kwenda kwenye hii tv ya hapa chumbani kwangu”
Jenerali Molele akasimama kwa sekunde kadhaa kisha akageuka. Akatoa simu yake na kumpigia kijana wa I.T katika commanding room na kumuagiza aunganishe kile kinacho onekena kwenye oparesheni kionekane kwenye tv hiyo ya chumbani na agizi hilo likatimia ndani ya dakika moja.


β€œJe kuna jambo jengine mkuu?”
β€œHapana ila nina omba umuombe msamaha sana Josephine kwa niaba yangu”
β€œSawa mkuu”
Jenerali Mollel akatoka ndani hapo na vijana wake wawili walio simama mlangoni wakampigia saluti na mmoja akaufungua mlango.
β€œHakikisheni kwamba muna kuwa makini na muheshimiwa kila baada ya nusu saa kuanzia hivi sasa mume muna mtazama”
β€œSawa mkuu”
Jenerali Mollel akaondoka na kurudi kwenye commanding room. Raisi Mtenzi taratibu akaanza kuangalia luninga hiyo iliyopo chumbani kwake. Nyimbo za uhamasishaji wanazo ziimba wanajeshi wanao kwenda kupambana na jeshi la nabii Sanga, zika zidi kumuumiza moyo wake. Machozi yakaanza kumbubujika huku akiendelea kujilaumu ni kwa nini alimkaribisha nabii Sanga kwenye maisha yake hususani maish ya familia yake. Gafla akastuka mara baada ya hisia zake kumtuma kama amemuona mke wake akiwa amesimama katika moja ya pembe ya chumba hicho. Macho yakamtoka huku mapigo ya moyo yakianza kumuenda kasi. Hisia zake zika zidi kumtuma na kumuona mke wake akimnyooshea mkono wa kulia huku akimuita amfwate.


β€œSitakiiiiiiiiiiii”
Raisi Mtenzi alizungumza huku akiwewesuka. Akachukua mtu mmoja na kujifunika usoni mwake ili asiweze kuona chochote


β€˜Mume wanguuu’


Raisi Mtenzi alihisi kama ana itwa akafumbua uso wake ila hakuweza kuona kitu chochote. Akili yake ikazidi kuvurugika mara baada ya kuanza kukumbuka matukio mabaya aliyo yafanya hususani ya mauaji kipindi alipo kuwa askari polisi. Akakumbuka jinsi alivyo waua majambazi sita peke yake huku askari wezake wanne alio kuwa ame ongozana katika oparesheni hiyo mpakani mwa Tanzania na Randwa, wakiuwawa kwa kupigwa risasi. Raisi Mtenzi akaanza kutetemeka huku jasho likimwagika, japo chumba kina A/C(Air condition) ila jasho likazidi kumwagika. Akakumbuka jinsi alivyo muua mzee Mbogo aliye muomba wazungumze ila ila hakuhitaji kumsikiliza zaidi ya kumtandika risaisi.


β€˜Mikono yangu ni michafu sana, mikono yangu ina damu’


Raisi Mtenzi alizungumza kimoyo moyo huku akitetemeka kiswa sawa. Katika maisha yake yote hakuwahi kukumbana na hali kama hiyo. Akashuka kitandani huku akiitazama mikono yake, akapiga hatua hadi katika choo kilichopo katika chumba hicho. Akasimama mbele ya kioo kilichopo bafuni hapo. Gafla akaona askari ambao ni marafiki zake walio kufa kipindi cha nyuma katika baadhi ya mapambano mbali mbali ya majambazi.
β€œOndokeniiii”
Raisi Mtenzi alizungumza huku akipiga piga kioo hicho kwa ngumi na kikapasuka vipande vipande. Taratibu raisi Mtenzi akakaa chini huku machozi yakimbubujika. Akatazama moja ya kipande cha kioo. Akakivuta taratibu, hisia zake kika mfanya amuone mke wake akiwa amesimama mbele yake huku akiwa ametabasamu.


β€˜Njoo mume wangu, nina kusubiria nime kumiss’


Raisi Mtenzi alihisi kuisikia sauti ya mke wake masikioni mwake. Akatazama kiganja cha mkono wake wa kushoto na taratibu kwa kutumia kioo hicho akajikata mishipa inayo ingiza damu kwenye kiganja cha mkono huo wa kushoto na kusababisha damu nyingi sana kuanza kuruka mithili ya bomba la maji lililo pasuka. Kadri muda unavyo zidi kwenda ndivyo kiwango kikubwa cha damu kinavyo zidi kumwagika hadi ikafika wakati kizunguzungu kilicho ambatana na mwili kuishiwa nguvu. Macho yake yakaanza kukosa mwanga taratibu na giza likaanza kuchukua nafasi yake kwenye mfumo wa macho yake.


β€œNi nusu saa ingia mcheki muheshimiwa”
Mwanajeshi mmoja alimuambia mwezake, akafungua mlango wa chumba hicho na kuingia ndani. Hakumuona raisi Mtenzi ndani hapo, ila taa ya bafuni akaona ikiwa ina waka. Akatembea kwa tahadhari hadi katika mlango wa kioo wa bafu hilo. Akasikilizia kinacho endelea ndani ya bafu kwa sekunde kumi, ila hakusikia mlio hata wa maji yakimwagika. Akatoa bastola yake na kuufungua mlango huo taratibu na jambo la kumshukuru Mungu, mlango upo wapi. Akaingia kwa tahadhri, macho yakamtoka mara baada ya kumuona raisi Mtenzi akiwa amekaa chini huku damu zikiwa zime tapaka ndani ya chumba hicho. Kwa kutumia kifaa cha mawasiliano akamjulisha mwenzake aingia ndani hapo huku yeye akianza kumpa huduma ya kwanza raisi Mtenzi. Mwenzake akaingia ndani hapo naye akajikuta akishangaa.


β€œIta madakatri haraka”
Madaktari wa ikulu wakaitwa na kuingia ndani hapo. Jenerali Mollel naye akaingia ndani hapo na kukuta raisi Mtenzi akipalazwa kwenye kitanda cha magurumu.
β€œImekuwaje?”


Jenerali Mollel alizungumza
β€œAmejaribu kujiua mkuu”
β€œShitii….Dokta vipi?”
β€œTuna omba tuweze kumshuhulikia”
Madaktari wa ikuku walizungumza huku wakikivuta kitanda hicho na kumtoa raisi Mtenzi ndani hapo. Wakakimbiza hadi katika chumba maalumu cha matibabu kwa ajili ya raisi na wakaanza kutundikia dripu za damu na kumuwekea mashine ya kumsaidia kupumua. Madaktari wakajitahidi kardi ya uwezo wao kuokoa maisha ya raisi Mtenzi ila bahati haikuwa upande wao kwani hali aliyo kuwa amefika raisi Mtenzi ni kufa tu. Madaktari hao wawili wanao muhudumia raisi Mtenzi wakatazamana huku wakiwa wametawaliwa na hofu kubwa sana.
β€œRekodi muda ame fariki saa kumi na dakika thelathini na sita usiku”
Daktari alizungumza mara baada ya kutazama saa yake ya mkononi. Akatoka chumbani hapo na mtu wa kwanza kukutana naye ni jenerali Mollel.
β€œDokta vipi?”
β€œTume jaribu kadri ya uwezo wetu ila tume shindwa na muheshimiwa raisi amefariki saa saa kumi usiku na dakika thelathini na sita”
Jenerali Mollel akakaa kimya kwa dakika mbili kisha akamtazama daktari.
β€œNahitaji kuuona mwili wake”
β€œSawa una weza kuingia”


β€œIla hili jambo sihitaji lijulikane kwa mtu yoyote hadi nitakapo kuambia”
β€œHakuna shaka mkuu”
Jenerali Mollel akaingia ndani ya chumba hicho na kukuta daktari akiuweka vizuri mwili wa raisi Mtenzi. Taratibu jenerali Mollel akavua kofia yake na kusogelea kitanda hicho.
β€œTume shindwa kuokoa maisha yake kwa maana alijikata mishipa mikubwa hivyo damu nyingi ziliweza kutoka na akachelewa kuwahiwa hivyo akafariki.”
β€œNime kuelewa daktari nahitaji hili jambo libaki siri kwenu na kwangu. Nita waambia ni muda gani wa kulitangaza kwa wananchi”
β€œSawa mkuu”
Jenerali Mollel akamtazama raisi Mtenzi usoni mwake. Hakika hakutarajia kama raisi Mtenzi ata jiua kirahisi namna hiyo.


β€˜Mungu akusamege kwa yale yote uliyo yafanya. Amen’


Jenerali Mollel alizungumza kimoyo moyo na kutoka chumbani hapo na kumuacha daktari akiendelea kuusafisha mwili wa raisi Mtenzi tayari kwa kuhifadhiwa Mochwari.


***


β€œUna jisikiaje mke wangu?”
Nabii Sanga alizungumza huku akipanda kitandani kwa maana ni muda mchache ndio ame fika katika meli yake akitoka Madagascar.
β€œSafi ni maumivu tu ya mguu ndio yana nisumbua sumbua”
β€œPole sana mke wangu”
β€œNashukuru watoto ume onana nao?”
β€œYaa na nilisha waombea nafasi ya kuishi nchini Marekani nina imani kwamba wata kwenda kuisha kwa amani”
β€œMungu awasaidie. Ila daa mambo yame tokea haraka sana mume wangu. Yaani sasa hivi ninge kuwa ni makamu wa raisi”
β€œNdio ila sija kata tamaa mke wangu. Ni lazima tuichukue nchi”
β€œKivipi ikiwa kwa asilimia sabini ya siri zetu zipo hadharani”
β€œUsijali mke wangu bado nina nguvu kwa waumini wangu. Nita hakikisha kwamba nina ipa pigo moja la fundisho nchi ya Tanzania hadi wajute kuwa na mtu kama mimi”
β€œIla mume wangu haya mambo nina ona kama yame kwisha. Tuachane nayo, tuna umri mkubwa sasa una onaje tuka ishi maisha yetu ya starehe kwa miaka hii iliyo baki”
Nabii Sanga akakaa kimya kwa sekunde kadha huku akimtazama mke wake.
β€œHicho ndicho unacho kihitaji?”
β€œNdio mume wangu nina hitaji tutulie sasa. Tume tafuta pesa kwa kipindi kingi cha maisha yetu. Una onaje sasa ukawa ndio muda na wakati wa kula matunda yetu”
β€œMmmm sawa mke wangu kama ume amua hivyo acha tufurahie”


Nabii Sanga alizungumza huku akianza uchokozi wa kumpapasa mke wake maungo yake.


β€œMume wangu nime umia bwana”
β€œKidogo mke wangu”
Nabii Sanga akaipanua miguu ya mke wake taratibu na kuanza kumyonyoa kitumbua na kumfanya mrs Sanga kuanza kutoa miguno taratibu. Gafla wakaanza kusikia king’ora cha hatari na kuwafanya waduwaae.


β€œKuna nini mume wangu?”
Mrs Sanga aliuliza huku akiwa amejawa na wasiwasi mwingi sana.


β€œNgoja nika angalie”
Nabii Sang alizungumza huku akishuka kitandani akavaa suruali yake pasipo hata kuvaa nguo ya ndani. Akavaa tisheti na kutoka ndani hapo.
β€œKuna nini kinacho endelea?”
Nabii Sanga alimuuliza mwanajeshi wake mmoja.
β€œNahisi kuna hatari”
Nabii Sanga akakimbilia hadi katika chumba cha manahodha wa meli yake kubwa.
β€œVipi mbona kuna king’ora cha hatari kuna nini na wana jeshi wana kimbia kimbia?”
β€œMuheshimiwa, milles ishirini kutoka hapa tulipo kuna meli za kujeshi zina tusogelea na zote zina onyesha zina kuja huku tulipo tuambie nini tufanye?”
Nahodha mkuu wa meli hiyo alizungumza msisitizo huku akimtazama nabii Sanga usoni mwake.
β€œZime tokea wapi?”
β€œTume gundua kwamba zina tokea nchini Tanzania”
Nabii Sanga akahisi kuchanganyikiwa huku akiona alama sita za meli za jeshi zikisogelea meli yake.
β€œMkuu tupe amri tukilegea wana tufika na wata tushambulia”
β€œMeli ina silaha za kutosha?”
β€œNdio mkuu”
β€œNdege za kivita zime baki ngapi?”
β€œJeti nane zime baki”
β€œJiandaeni kwa vita na tuna anza kuwashambulia wao tume elewana?”
β€œSawa mkuu, na tuna uchungu nao kwa maana wame weza kuwaua vijana wetu. Sasa ni wakati wa kulipa”
Kampteni wa meli alizungumza kwa msisitizo na akaanza kutoa maagizo kwa kutumia kipaza sauti na kuwataarifu wanajeshi wote ndani ya meli hiyo kuhakikisha wana jiandaa kwa vita hiyo inayo kuja mbele yao.


****************************************************************************************************************


***


ITAENDELEA


Haya sasa, nabii Sanga na wanajeshi wake wana jiandaa kuzikabili meli za kivita za nchi ya Tanzania. Nabii Sanga amepanga kufanya mashambulizi kabla hawajafikiwa je ni nini kita tokea katika vita hiyo? Ungana nami katika fina episode ya kisa hichi cha kusisimu kilicho andaliwa na mimi muandishi wako Eddazaria G.Msulwa. Sehemu ya 225.
 
SIN 225(final episode)


Muandishi…………………………………………….EDDAZARIA G.MSULWA(G.Authour)


Age ……………………………………………………18+


Simu………………………………………………… 0657072588(whatsapp) au 0768516188


Website








ILIPOISHIA


β€œZime tokea wapi?”
β€œTume gundua kwamba zina tokea nchini Tanzania”
Nabii Sanga akahisi kuchanganyikiwa huku akiona alama sita za meli za jeshi zikisogelea meli yake.
β€œMkuu tupe amri tukilegea wana tufika na wata tushambulia”
β€œMeli ina silaha za kutosha?”
β€œNdio mkuu”
β€œNdege za kivita zime baki ngapi?”
β€œJeti nane zime baki”
β€œJiandaeni kwa vita na tuna anza kuwashambulia wao tume elewana?”
β€œSawa mkuu, na tuna uchungu nao kwa maana wame weza kuwaua vijana wetu. Sasa ni wakati wa kulipa”
Kampteni wa meli alizungumza kwa msisitizo na akaanza kutoa maagizo kwa kutumia kipaza sauti na kuwataarifu wanajeshi wote ndani ya meli hiyo kuhakikisha wana jiandaa kwa vita hiyo inayo kuja mbele yao.





ENDELEA


β€œWhat……the fuc**”
Kapten wa meli ya nabii Sanga alizungumza huku macho yakimtoka kwa maana rada yake ina muonyesha tayari ndege zipatazo kumi za kivita zipo juu ya anga lao.


β€œMkuu ni wakati wa wewe kuondoka?”
Capteni alizungumza huku akimtazama nabii Snaga.
β€œKuna nini?”
β€œTulihisi adui zetu wapo mbali, ila wapo juu yetu kwa sasa. Tafadhali nina kuomba uweze kuondoka, mchukueni mkuu na mumpeleke sehemu salama”
Capteni wa meli aliwaambia wanajeshi wawili na wakatoka na nabii Sanga ndani ya chumba hicho huku wakikimbia kwa kasi kuelekea eneo la chini kilipo chumba cha nabii Sanga na ofisi zake.
β€œMke wangu kwanza, andaeni manohari yangu ndogo”
β€œSawa mkuu”
Nabii Sanga akaanza kukimbia kwenye kordo hiyo huku akipishana na wanajeshi wake ambao kila mmoja ana jipanga kwa ajili ya mashambulizi hayo, kwani king’ora bado kina lia kwa sauti ya juu sana. Nabii Sanga akaingia kwenye chumba kwake na kumkuta mke wake akiwa amesimama huku wasiwasi mwigi sana ukiwa ume mtawala.
β€œBaby tuondoke. Tumevamiwa”
Nabii Sanga alizungumza huku jasho likimwagika usoni mwake.
β€œNa….na nani?”
Mrs Sanga alizungumza huku kigugumizi kikiwa kime mtawala.
β€œNa jeshi la Tanzania. Sio salama kuwepo eneo hili mke wangu”
Mrs Sanga akahisi kama kuishiwa nguvu. Nabii Snaga akampa mngo mke wake na kuinama kidogo.
β€œPanda mgongoni baby”
Mrs Sanga akamtazama mume wake anaye mwagikwa na jasho huku wasiwasi mwingi ukiwa ume mtawala. Akapanda mgononi na wakatoka chumbani hapo na wakaanz akukimbia kuelekea chini ya meli hiyo ambapo kuna manohari ya dharura. Ndege za kivita za jeshi la Tanzania aina ya Gr F 16C, zikaanza kushambulia wanajeshi wanao jaribu kujibu mashambulizi kwa kutumia risasi pamoja na mizinga ya mabomu. Hakika haikuwa siku nzuri sana kwa wanajeshi wa nabii Sanga. Ndege hizo za kivita zinazo endeshwa na marubani wenye ujuzi wa hali ya juu zikaendelea kufyatua risasi nyingi huku wanajeshi wengine walipo katika helicopter aina ya UH-60 Black Hawk wakianza kushuka kwa kutumia kamba ndege na kuingia kwenye meli ya nabii Sanga. Magreth akamtazama Evans huku nao wakiwa katika moja ya helicopter za aina hiyo, waliyo panda wakitokea kwenye meli waliyo kuwa wana safiria.


β€œGo go go”
Mmoja wa wanajeshi aliyopo katika helicopter hiyo alizungumza huku Evans akawa wa kwanza kusihika kamba ya kushukia futi mia hamsini kutoka angani. Magreth naye akiwa katika mavazi yake ya kazi akashika kamba moja na kuanza kuburuzika kwa utaalamu kuelekea chini huku akifwatia wanajeshi wengine na jukumu lao kubwa ni kuhakikisha kwamba wana muokoa Jery pamoja na Leila.
β€œLocation ina onyesha huku”
Evans alizungumza huku akitazama alama ya simu ambayo Leila aliwapigia. Kwa haraka wakaanza kushuka kuelekea katoka eneo hilo huku njiani wakikutana na vikwazo wanajeshi. Evans na bunduki yake aina ya M4 carbine akaendelea kuwapiga risasi wanajeshi wa nabii Sanga huku kwa mara kadhaa akibadilisha magazine. Magreth na silaha zake za kininja naye hakuwa mbali na Evans kwani lengo lao ni moja kuhakikisha wana mtoa Leila akiwa hai ndani ya meli hiyo. Wakafanikiwa kufika katika chumba alicho fungiwa Leila. Wakaingia ndani humu na kumkuta Leila akiwa amejikunyata kwenye moja kona ya kitanda kwa maana hiyo mikiki mikiki ya silaha anayo isiki nje ina mtisha sana.
β€œLeila ni mimi”
Evans alizungumza huku akiweka silaha yake pembeni ya kitanda hicho. Leila akafumbua macho yake, akamtazama Evans kwa sekunde kadhaa kisha akamkumbatia huku machozi yakimwagika.
β€œNimekumiss baby”
Leila alizungumza huku akimbusu Evans mdomoni mwake kitendo hicho kika uumiza moyo wa Magreth japo wapo katika ulingo wa vita ila wivu wake upo pale.
β€œMuda wa kuondoka ume fika”
Magreth alizungumza kwa msisitizo ili kukatisha katika hisia za Leila.
β€œUna weza kutembea?”
β€œNdio”
β€œNifwate kwa nyuma”
Wakaanza kutoka ndani hapo huku Magreth akiwa ametangulia mbele, Leila akiwa katikati na Evas akiwa nyuma kuhakikisha wana toka salama.
β€˜Nabii Sanga’


Magreth alikumbuka.
β€œSikia Evans mtoe huyu demu huko nje nina msaka nabii Sanga”
β€œHuwezi kwenda peke yako tuna kwenda wote”
β€œFanya kama nilivyo kuagiza, usijali kuhusiana na mimi, jali kuhusiana na huyu demu wako”
Magreth alizungumza kwa uchungu na ukali kiasi na kuwafanya Evans na Leila kutazamana.
β€œNendeni”
Evans akashusha pumzi kidogo, kisha akakubali kuondoka eneo hilo na Leila. Magreth akachomeka upanda wake mgongoni kishaa akachomoa bastola yake na kuanza kukimbia kukimbia kuelekea kwenye vyumba akijaribu kuingia chumab kimo baada ya kingine. Kwa bahati mbaya akiwa katika moja ya kordo akakutana na mwanaume mwenye mwili mkubwa huku akiwa amejazia misuli, na mwanajeshi huyo amesimama katika njia hiyo kuhakikisha kwamba hakuna mtu anaye pita kuelekea chini alipo kwenda nabii Sanga na mke wake.
β€˜Nini tena hichi?’


Magreth alizungumza huku akimtazama mwanajeshi huyo anavyo kuja. Hakika ukubwa wa mwana jeshi huyo una weza kumfanianisha na mpiganaji myereka aitwaye Big show.


β€˜Hili ndio litaniongoza na kunieleza ni wapi alipo nabii Sang’


Magreth alizungumza huku akirudisha bastola yake eneo alipo ichomoa. Mwanajeshi huyo akarusha teke lililo mfanya Magreth kupiga magoti chini na likapita kwa juu. Magreth akampiga ngumi mbili za haraka mwanajeshi huyo kwenye sehemu zake za siri na kumfanya agumie kwa maumivu huku akijishika sehemu hiyo. Magreth akachomoa kisu kidogo kwenye mfuko wake na kuanza kumchana chana mwajeshi huyo kwenye mwili wake. Japo mwanajeshi huyo ni pande kubwa la jitu ila kwa Magreth lilijikuta likizidiwa ujanja, japo kwa mara kadhaa anajaribu kurusha ngumi nzito nzito ambazo Magreth anapo zikwepa na kupiga wa mbao, basi una vunjika. Magreth akamdandia mabegani mwanajeshi huo na akamchoma kisu hicho pembeni ya shingo yake na kukichomoa na damu nyingi zikaanza kuvuja mithili ya ng’ombe anaye chinjwa. Wakaaanguka na mwanajeshi huyo chini.


β€œYupo wapi nabii Sanga”
β€œFuc** you bi***”
Mwanajeshi alizungumza maneno hayo ya matusi na yakawa ndio ya mwisho kutoka kinywani mwake na akafariki. Magreth akatazama ngazi zinazo shuka chini ya meli hiyo kwa haraka akasimama na kuanza kushuka kwenye ngazi hizo. Akakuta kordo ndege na kwa mbali akamuona nabii Sanga akiata kona ya kulia huku mgononi mwake akiwa amembeba mke wake.
β€œShitii”
Magreth alizungumza huku akianza kukimbia kwa kasi ya ajabu sana. Akakunja kona hiyo na kukutana na kordo nyingine fupi ambayo ina kona ya kuelekea kushoto. Akaanza kukimbia na kwa bahati nzuri na mbaya kwa nabii Sanga na mke wake, akawakuta wakiwa wamesimama kwenye mlango huku nabii Sanga akujitahidi kuingiza namba za siri.
β€œSimameni hapo hapo”
Magreth alizungumza huku akiwa ameshika bastola yake mkononi na kumuelekezea nabii Sanga na mke wake. Nabii Sanga taratibu akageuka huku yeye na mke wake wakimshangaa Magreth.
β€œNi wewe”
Nabii Sanga alizungumza huku akimshusha mke wake chini taratibu.
β€œYes ni mimi”
β€œMagreth ume fika mbali sasa.”
β€œOhoo kweli nime fika mbali. Leo ndio story yenu ina kwisha hapa wewe na huyu malaya wako mzee”
Magreth alizungumza kwa kujiamini.
β€œMalaya mzee ni wewe. Kama ni mwanamke kweli shusha bastola yak echini tupambane”
Mrs Sanga alizungumza kwa kujiamini huku akisikilizia maumivu ya mguu wake wenye jeraha la kisu. Magreth akamtazama mrs Sanga na nabii Sanga kisha akachomoa magazine ya bastola yake na akavitupa pembeni. Nabii Sanga akamsogeza mke wake pembeni na akajiweka sawa kwa ajili ya kupambana na Magreth.
β€œYaani siamini nime kutao matopeni alafu leo hii una simama kwenye njia yangu. Hakika nita kuua leo hapa”
Nabii Sanga alizungumza huku akikunja ngumi.
β€œMke wangu endelea kuingiza namba za siri.”
Nabii Sanga akarusha ngumi mbili ambazo moja Magreth akaikwepa ila ya pili ikampiga kifuani mwake na kumteresha kidogo na akarudi nyuma huku akisikilizia maumivu hayo.
β€œMuue huyo mume wangu”
Mrs Sanga alishabikia. Nabii Sanga akaanza kurusha mashambulizi ya ngumi mfululizo, Magreth kazi yake ikawa ni kuzuia kwa maana nabii Sanga wa leo sio yule ambaye alipigana naye akiwa na mke wake siku walipo kuja kwake. Nabii Sanga huyu ana onyesha ana mazoezi makali na mafunzo mazuri ya kupigana kung fu. Hakika mashambulizi ya nabii Sanga yakaanza kumzidi Magreth aliye choka kwa kupigana na pande la mwanaume. Kabali aliyo kabwa na nabii Sanga hakika ikaanza kumfanya ahisi ana poteza maisha. Japo amevalia nguo zake za kazi ambazo haziingizi risasi ila hazizuii kuingiza maumivu ya ngumi nzito zinto alizo pigwa na nabii Sanga. Magreth taratibu akajikaza kutoa kabali hiyo ila ikawa ni ngumu sana kwake. Mrs Sanga akafungua mlango unao inga katike eneo ambalo lina manohari ndogo.
β€œMume wangu mmalizie tuondoke.”
Mrs Sanga alizungumza huku akiwa amesimama mlangoni hapo. Magreth akampiga nabii Sanga visukusuku viwili vya tumbani na kumfanya alegeze mkono wake, Magreth akajitoa kwenye mikono ya nabii Sanga. Akachomoa upanga wake mrefu na wenye makali yanayo kata pande zote mbili. Akamtazama mrs Sanga aliye simama mlangoni kisha akamtazama nabii Sanga anaye jiweka tayari kwa mashambulizi. Magreth kwa nguvu zake zote akamrushia mrs Sanga upanda huo ambao kwa kasi ya ajabu ukakita tumboni kwa mrs Sanga na kutokea upande wa pili.


β€œNOOOOOOOOO….!!!!”
Nabii Sanga alizungumza kwa hasira huku macho yakimtoka. Akamrukia Magreth na wakaanguka chini. Akamshindilia Magreth ngumi mbili ambazo zote Magreth akazizuia kwa mikono wake. Magreth akambinua nabii Sanga na kumlaza chini akaushika mkono wake wa kulia wa nabii Sanga, akaupitisha katikati ya miguu yake na kuuvunja. Nabii Sanga akapiga yowe la maumivu makali sana. Mrs Sanga taratibu akapiga magoti chini huku damu zikimtoka mdomoni mwake pamoja eneo ambalo upanga huo wenye ncha kali ume mtoboa. Hakika hakuamini kama ipo siku ana weza kukumbana na tukio kama hilo ambalo kwa asilimia mia moja lina kwenda kumaliza maisha yake.


Nabii akajitahidi kunyanyuka ila Magreth akampiga na visigino kifuani mwake na kumfanya nabii Sanga kutema damu kwa maana pigo hilo lime vunja mbavu za kifuani mwake. Taratibu Magreth akasimama huku akiweweseka.


β€œMumekuwa ni watu wa kuishi katika DHAMBI. Mume danganya maelefu ya watu kwamba nyinyi ni wema kumbe hamuna lolote. Sasa leo muna kufa”
Magreth alizungumza huku akimtazama nabii Sanga pamoja mke wake.
β€œWee….malaya”
Mrs Sanga alizungumza huku akimnyooshea Magreth kidole. Magreth amasogelea mrs Sanga hadi sehemu alipo piga magoti. Akavua kofia ya vazi lake hilo la kuzuia risasi na akakitingisha kichwa chake na kuziweka sawa nywele zake.


β€œNdio mimi ni malaya niliye tembea na mume wako na akanipatia mali zake. Sasa leo ni mwisho wa dhambi zako kunguni wewe”
Magreth akauchomoa upanga huo na kumfanya mrs Sanga aanguke na kulala chali hukua kishikilia tumbo lake na damu zikizidi kumwagika.
β€œMage please usimuue mke wangu”
Nabii Sanga aliomba huku akijiburuta chini kumsogelea mke wake ambaye ana hali mbaya kuliko ya kwake.
β€œKifo ni haki yenu, mukindelea kuishi hapa duniani muta zidi kufanya DHAMBI nyingi”
β€œMage hata wewe una dhambi usituhukumu, wewe sio Mungu”
β€œOoohoo kumbe una jua kuna Mungu, basi leo nime kua malaika mtoa roho”
Magreth akanyanyua upanga wake juu ya kuukita katika eneo la moyo wa mrs Sanga na kumfanya mrs Sanga kutoa ukelele wa maumivu makali. Magreth akazungusha upanga huo na kuuchangua changua moyo wa mrs Sanga na taratibu akakata roho. Nabii Sanga akazidi kulia kama mtoto mdogo kwa maana hakuamini kama mke wake anakufa mbele yake.
β€œKutokana na biashara yako ya madawa ya kulevya. Ulisababisha maelfu ya watu jijini Dar es Salamaa kushambuliwa na kufa kwa mabomu ya Al-Shabab. Mulijipenda nyinyi wenyewe na sio kuwapenda watu wengine. Vijana wengi wameathirika kwa madawa ya kulevya kwa ajili ya nyinyi kujipatia mali zenu. Sanga wewe ni nabii wa aina gani? Una hisi Mungu ana weza kumuweka roho wake mtakatifu kwenye hekalu chafu kama hilo. Unatumia nguvu za giza kuwaponya watu ambao sio Mungu huyu ninaye mjua mimi ni Mungu wako wa ajabu ndio ana fanya miujiza. Sasa siwezi kukuacha ukaendelea kuitesa jamii kwa DHAMBI zako Sanga”
Magreth alizungumza kwa uchungu huku machozi yakimwagika usoni mwake. Japo yupo kazini ila nabii Sanga ndio mwanaume wake kumuingilia kimwili na ndio mwanaume aliye mpa mafanikio ya kiuchumi.
β€œOkay nipo tayari ku….fa…a kwa ajili ya DHAMBI zangu. Ila nina ombi moja”
β€œOmbi gani?”
β€œTafadhali usimuue mwanangu Julieth. Muacheni aishi maisha yake salama na mume wake. Mimi na mke wangu ndio tuna ongoza hili gende lote, Julieth hausiki chochote”
Nabii Sanga alizungumza huku akiwa amepiga magoti mbele ya Magreth.


β€œTafadhali Mage nina kuomba sana iwe hivyo”
β€œNime kuelewa, nita muacha aishi salama, niambie yupo ndani ya hii meli?”
β€œHapana wamesha ondoka ila sinto kuambia ni wapi wame kwenda ila muache awe salama”
β€œKama hawapo ni jambo la heri. Sihitaji mikono yangu ikuue ila jimalize mwenyewe?”
Magreth alizungumza huku akimkabidhi nabii Sanga upanga huo. Nabii Sanga akautazama upanda huo, akatazama damu ya mke wake iliyo tapakaa katika upanga huo. Taratibu akaushika vizuri mkononi mwake. Akamtazama Magreth aliye simama mita kadhaa kutoka alipo piga magoti. Kwa kasi ya ajabu nabii Sanga akamshambulia Magreth kwa upanga huo, ila Magreth akawahi kuruka sarakasi ya kinyume na shambulizi hilo kikapita. Magreth akaruka hewanu na kumruka nabii Sanga na kutua nyuma yake, akaushika mkono wa nabii Sanga ulio shika upanga huo na kwa nguvu zake zote akisaidiana na mkono wa nabii Sanga akapitisha upanga huo shingoni mwa nabii Sanga na kukata koromea la nabii Sanga na damu nyingi zikaanza kumwagika. Nabii Sanga hakika hakuamini kama ipo siku Magreth ata muua. Magreth akayafumba macho yake kwa sekunde kadhaa huku mwili mzima ukimsisimka. Akafumbua macho yake na kumkuta nabii Sanga akiwa amelala chini huku damu yake na mke wake kizikaribiana kisha zikagusana na kusababisha dimbwi kubwa la damu. Magreth machozi yakanza kumwagika, huku taratibu akianza kukumbuka mambo mema aliyo fanyiwa na nabii Sanga kuanzia alipo kuwa kanisani kwa nabii Sanga akiimba kama mwana kwaya, akakumbuka jinsi alivyo muokoa nabii Sanga kutoka kwa watekaji. Akakumbuka hata siku alipo lala naye nyumbani kwake na kumpatia zawadi ya usichana wake. Taratibu Magreth akaa chini huku akihisi nguvu za mwili zikimuishia. Hakika japo nabii Sanga alifanya mambo mengi maovu ila ukwelini kwamba kuna mazuri ambayo ameyafanya kwa jamii ya watu wanao mzunguka. Magreth akazidi kulia kama mtoto mdogo, uchungu mwingi ukamtawala.


β€˜Ehee Mungu kwa nini umenipa nafasi kama hii ya kumua huyu baba wa watu na mke wake?’


Magreth alizungumza kimoyo moyo huku akitazama maiti ya nabii Sanga na mke wake. Wanajeshi wanne wa nchi ya Tanzania wakiwa wameongozana na Evans wakafika eneo hilo, kila mmoja hakuamini kuona kilicho tokea eneo hilo. Taratibu Evans akachuchumaa na kwa nguvu zote wakakumbatiana na Magreth.
β€œIme kwisha baby, ime kwisha”
Evans alizungumza huku akimfariji Magreth aliye zidisha kilio chake.
β€œNabii Sanga na mke wake wame uwawa. Nina rudia nabii Sanga na mke wake wamekwisha uwawa”
Mwanajeshi mmoja alizungumza huku katika kofia yake ngumu ikiwa ime fungwa kamera inayo peleka mawasiliano ya video moja kwa moja ikulu kwenye commanding room. Taratibu Evans akaanza kumnyonya denda Magreth na kumfanya atulize kilio chake na mwisho wake akanyamaza.
β€œNina kupenda Magreth. Nipo tayari kuwa nawe kwenye hali yoyote”
Evans alizungumza huku akimmshika Magreth mashavuni mwake.


β€œNina kupenda pia Evans, nahitaji urudi kwenye sura yako halisi sasa.’


β€œTukifika nyumbani nita rudi kwenye sura yangu halisi”
Taratibu Evans akambeba Magreth na wakaanza kuondoka eneo hilo.
β€œEvans nishushe bwana, tuna weza kukutana na adui?”
β€œUsijali hakuna adui yoyote ambaye ana weza kutokea kwa maana meli kwa sasa imesha tekwa na jeshi letu na wanajeshi wote wa nabii Sanga wameuwawa na miili yao kutupiwa baharini”
Evans alizungumza huku akiwa amejawa na tabasamu pana. Magreth akamtazama Evans kisha taratibu akaipitisha mikono yake yake shinoni mwa Evans na wakaanza kunyonyana denda.
β€œEvans niahidi kitu”
β€œKitu gani?”
β€œAchana na kale kademu kako kwa manaa nita kaua?”
β€œUsijali mke wangu, amesha ondolewa hapa kwenye meli na helicopter na sinto kuwa naye tena”
β€œKweli?”
β€œHaki ya Mungu vile. Nina kupenda sana mke wangu na kwa maana haya yote yamesha kwisha basi nita hakikisha kwamba nina kuoa harusi kubwa ya kifahari ambayo hapa Tanzania haijawahi kutokea”
β€œKweli?”
β€œYaa ita kuwa ni harusi kubwa zaidi ya Jery na mke wake”
β€œNashukuru mume wangu”
Evans na Magreth wakafika katika moja ya helicopter ya jeshi. Wakaingia pamoja na wanajeshi walio jeruhiwa katika mapambano hayo na kuianza safari ya kurudi nchini Tanzania.


***


Jenerali Mollel, Josephine, Samson pamoja na wafanyakazi wengine wa ikulu. Wapo kwenye kambi ya jeshi la anga kuwasubiria wanajeshi mashujaa walio weza kumuondoka nabii Sanga. Helicopter waliyo panda Magreth na Evans pamoja na wanajeshi wengine walio jeruhiwa, ikatua taratibu kwenye kiwanja cha ndege katika kambi hiyo. Madaktari wa jeshi wakwa tayari kuwapokea majeruhusi huku Evans akimbebea Magreth taratibu na wakanaza kutembea kuelekea eneo alipo jenerali Mollel. Josephine akashindwa kujizuia na kuanza kuwakimbilia kwa kasi sana na alipo wakaribia Evans akamshusha Magreth na wakakumbatiana kwa nguvu na Josephine. Evans akatabasamu huku akimtazama Magreth na Josephine jinsi wanavyo lia kwa furaha.
β€œKazi nzuri Mage”
β€œNashukuru nina imani kwamba maombi yako yame weza kunisaidia”
Wakaachiana taratibu na kutembea hadi sehemu alipo simama jenerali Mollel. Wakapeana mikono na jenerali Mollel ikiwa ni ishara ya kuwapongeza.
β€œKazi nzri vijana wangu”
β€œNina shukuru mkuu. Kuna huu ushahidi ambao dunia ikihitaji kuupata basi uta waonyesha”
Evans alizungumza huku akifungua mfuko wa suruali yake ya jeshi aliyo vaa akatoa fauli alilo likunja kwa mfumo wa duara na akamkabidhi jenerali Mollel.
β€œNi faili la nini?”
β€œLina onyesha DHAMBI zote alizo zifanya nabii Sanga na familia yake. Nilihakiksiha kwamba sitoki ndani ya ile meli pasipo hili faili na nina shukuru Mungu nime lipata.”
Jenerali Mollel akafungua ukurusaha wa kwanza wa faili hilo na kupitisha macho na kujikuta akiachia misunyo kwa maana aliyo yaona katika faili hilo yana mstahili nabii Sanga kufa vifo walivyo kufa.


β€œNina washukuru nyinyi timu ya watu wanne. Pasipo nyinyi hili jambo lisinge fika hapa”
β€œTuna kushukuru na wewe. Pia shukrani zetu kwa RPC Karata kwa maana yeye ndio aliye weza kutusaidia na kutuamini kipindi ambacho hata wewe nina imani usinge weza kutulewa. Nina ombi moja kwako jenerali”
Magreth alizungumza huku akimtazama jenerali Mollel usoni mwake.
β€œNiombe tu”
β€œNina kuomba upandishe cheo RPC Karata”
β€œUsijali nitalifanyia kazi. Atakuwa IGP, au nitakua nime muoea?”
β€œHapana ana stahili”
Josephine alizungumza kwa furaha.
β€œNina jambo moja nina hitaji kuwaambia nyinyi nyote wanne”
Jenerali Mollel akaka kimya kwa sekunde thelathini kisha akendelea kuzungumza.
β€œRaisi Mtenzi atunaye tena duniani, amejiua kwa kujikata mshipa mkuu wa damu katika mkono wake. Amefariki usiku wa kuamkia leo. Hivyo mimi sina kipingamizi cha kuwa raisi siku tisini kisha baada ya hapo uchaguzi uta fanyika na nina imani nita kuwa raisi kabisa”
β€œMasikini weee, ila ana stahili kwa maana yeye ndio amemuua mzee Mbogo”
Josephine alizungumza kawaida.
β€œKweli?”
Magreth aliyliza kwa mshangao.
β€œNdio”
Josephine akatoa simu mfukoni mwake na kuiweka video ya jinsi raisi Mtenzi akimuua mzee Mbogo kwa kumpiga raisi. Magreth, Samson na Evans wakajikuta wakiumia sana kwa ajili ya kifo cha mzee Mbogo kwa maana wame uwawa kikatili sana.


β€œMkuu kuna hadhina kubwa sana ambayo ukisha apishwa kuwa raisi tuta hitaji tuitafute kwa ajili ya kuindeleza nchi yetu. Ukisha apishwa tu nita kuambia ni wapi ilipo”


Josephine alizungumza huku akimtazama jenerali Mollel usoni mwake.
β€œNime kuelewa Josephine”


Evans, Magreth, Josephine na Samson wakaondoka uwanjani hapo na kuelekea nyumbani kwa Magreth kwa ajili ya kujipumzisha asubuhi hiyo.


Ilipo timu saa tisa alasiri jenerali Mollel akatangaza juu ya kifo cha raisi Mtenzi na akaelezea jinsi kilivyo tokea. Hakika haikuwa habari nzuri kwa wananchi wa nchi ya Tanzania. Wengi wao walijawa na majonzi na bendera zote zikashushwa nusu mlingoti na ikatangazwa ni wiki nzima ya majonzi. Baada ya siku nne baada ya Tangazo raisi Mtenzi akazikwa huku Jery na mke wake wakiyafwatilia mazishi ya raisi Mtenzi kupitia luninga wakiwa nchini Marekeni.


β€œBaba alistahili kufa”
β€œKwa nini una sema hivyo mume wangu”
Jery akamuonyesha Julieth video ya jinsi baba yake alivyo kuwa akimuua mzee Mbogo na Julieth akajikuta akijawa na mshangao mkubwa sana kwa maana ana yafahamu mahusiano ya raisi Mtenzi na mzee Mbogo jinsi yalivyo kuwa.


β€œNime sikia meli ya baba ime kamatwa na wanajeshi wa nchi ya Tanzania. Nina imani kwamba baba na mama watakuwa wame uwawa?”
β€œUsisehem hivyo mke wangu”
β€œNo hata wakiuwawa, nita umia kama mtoto ila sinto weza kulipiza kisasi kwa maana baba na mama ni watu walio fanya DHAMBI nyingi sana kwa muamvuali wa dini”
Julieth alizungumza kwa sauti ya upole huku usoni mwake akiwa amejawa na huzuni. Akamuadhithia Jery siri zote za familia yake na hata kuolewa na Jery na yeye kuwa mshauri wa raisi na yeye ndio aliye kuwa ana husika katika kuzitoa siri nyeti za taifa.
β€œNina kuomba unisamehe mume wangu mimi na familia yangu”
Julieth alizungumza huku akimwagika na machozi usoni mwake.
β€œUsijali nime kusamehe. Na mimi nina kuomba unisamehe kwa maana hili jambo halito endelea kudumi milele ni lazima ipo siku uta lifahamu”


Jery alizungumza kwa sauti ya upole.
β€œJambo gani mume wangu?”


Akamueleza Julieth kila kitu kuhusiana na mahusiano yake na Shani na akaeleza jinsi baba yake alivyo kuwa ana pinga mimba hiyo.
β€œBaba alikuwa ana fanya makosa. Nime furahi sana mume wangu kwa kuweza kumpatia Shani ujauzito, muambie tu akaishi kwenye hiyo nyumba uliyo nunua mfungulie miradi na endeshe maisha yake. Nita mpenda mwanaye na nita mpenda na yeye pia.”
Maneno ya Julieth yakamfurahisha Jery na akamkumbatia kwa nguvu mke wake. Gafla Julieth akaanza kujihisi kichefuchefu na akakimbilia bafuni na kutapika. Ishara hiyo ikaanza kumfurahisha Jery, kwa haraka akatafuta kipimo cha kupima ujauzito na Julieth akapima ujauzito na kujikuta akiwa ni mjamzito jambo lililo futa huzuni ya kufiwa na wazazi wao na sasa wakaanza kufikiria juu ya maisha ya kuwakuza watoto hao wataoa kwenda kuzaliwa. Jery akawasiliana na Shani na akamueleza kila kitu kuhisana na maamuzi ya Julieth na akamtumia kiasi cha dola milioni mbili kwa ajili ya kufungua miradi mbalimbali kwa ajili ya mtoto wake huyo atakaye zaliwa.
***


β€œSamahani sana Evans kwa hili nitakalo zungumza”
Sauti ya Baby Al ilisika vizuri masikini mwa Evans aliye iweka simu yake upande wa kulia wa sikio lake.


β€œZungumza tu”
β€œBaba amenitafutia mwanaume wa kuona naye. Sina budi kufunga naye ndoa, nina kuomba unisamehe sana Evans.”
β€œUsijali nina elewa hilo. Kuwa na amani”
β€œKweli?”
β€œNdio nina tambua kabisa baba yako hapendi ngozi nyeusi hivyo ingeleta shida kwenye furaha ya maish ayako ikiwa una una mpenda sana baba yako. Ila Baby Al nina kushukuru kwa kila jambo ulilo nifanyia mimi”
β€œNashukuru nawe pia ila upendo wangu kwako hauto kufa uta endelea kuishi”
β€œAsante sana kwa hilo Baby Al nikutakie maisha mema ya ndoa yako”
β€œNina shukuru, nina kuomba umtafute mwamke utakaye mpenda sawa baby”
β€œNashukuru Mungu atanisaidia katika hilo”
β€œAmen bye”
Simu ikakatwa na kumfanya Evans kushusha pumzi huku akiwa amejawa na furaha sana. Isitoshe amerudi kwenye sura yake ya kawaida sasa. Akarudi ndani na kumkumbatia Magreth kwa furaha zote kwa maana kwa sasa hakuna kipingamizi kwenye ndoa yao na isitoshe Leila alisha mueleza ukweli na akampatia shilingi milioni moja kwa ajili ya kufungua biashara yake mwenyewe.
β€œNita kupelekea kukutambulisha kwa maama mara baada ya jenerali Mollel kuapishwa”
β€œSawa mume wangu.”
β€œMume pendaza sana”
Josephine alizungumza huku akimtazama Magreth pamoja Evans. Baada ya siku mbili jenerali Mollel akaapishwa na kuwa raisi wa Tanzania kwa miezi mitatu kabla ya uchaguzi kufanyika. Kila mwananchi alifurahi juu ya uongozi wa jenerali Mollel ambaye kwa sasa ni raisi Mollel. Baada ya wiki tatu za uongozi wake kama raisi. Wakaanza harakati za kuitafuta adhina hiyo ambayo ilitamaniwa sana na nchi ya Marekeni. Kiongozi wa kuisaka hadhina hiyo ni Josephine huku akisaidiana na wanajeshi wa jeshi la kujenga taifa. Wakafanikiwa kuipata hadhina hiyo iliyo chini ya ardhi. Vito vya thamani viliyo kuwa vina tumiwa na wafalme wa zamani vilivyo tengenezwa kwa dhahabu tu, vime jaa katika pango hilo ambalo pasipo damu ya Josephine pango hilo lisinge weza kufunguka.


Ulinzi mkali ukaimarishwa na wanajeshi hao na hadhina yote ikatolewa na kuhifadhiwa kwenye glala kubwa la taifa. Hadhina hiyo ikaanza kuuzwa kwa bei kubwa sana na kusababisha uchumi wa nchi ya Tanzania kupanda kwa kasi ndani ya mwenzi mmoja tu na kuwa taifa tajiri duniani. Raisi Mollel akaanzisha utaratibu wa kila mwananchi wa Tanzania kuanzia miaka kumi na nane ana lipwa kiwango cha laki mbili na nusu kila mwenzi, uwe una kazi au hauna kazi ila una lipwa. Pia akaanzisha utaratibu wa kila kijana anaye hitaji kuoa basi harusi yake ina garamiwa na serikali. Hakika kila mwananchi hakuhitaji kuikwepesha kura yake kwa uchaguzi ulio fwata amapo raisi Mollel akapita bila kupingwa kwa kura asilimia tisini na nane.


Harusi ya Evans na Magreth ikwa ndio harusi ya kwanza kuhudumiwa na serikali ya nchi ya Tanzania. Mamia ya watu kutoka ndani na nje ya nchi wakahudhuria harusi hiyo ya kifahari kupita harusi zote zilizo wahi kutokea katika nchi ya Tanzania. Kila mgeni aliye hudhuria anakula, kunywa na kusaza. Raisi Mollel naye ni miongoni mwa wageni waalikwa huku ulinzi ukiwa ni mkali kupitakawaida.


β€œKweli Mungu akiamua kukunyanyua hakuna binadamu anaye weza kuwashusha. Nina wapenda sana Mage na Evans”
Josephine alizungumza huku akiwa amewakumbatia maharusi.


β€œTuna kupenda pia Josephine”
β€œJosephine”
Samson aliita mara baada ya Josephine kuachiana na maharusi hao.
β€œNiambie Samson”
Taratibu Samson akapiga goti moja chini kisha akatoa kisanduku kidogo cha pete ya dhababu.
β€œJe upo tayari kuoana na mimi?”
Josephine akashangaa sana. Ila Evans na Magreth hawakuweza kushangaa kwa maana wana tambua Samson alisha achana na mpenzi wake na aliweza kuziweka hisia zake wazi kwa Magreth akimueleza namna jinsi anavyo mpenda Josephine.
β€œSamson una mchumba wako kwa nini una nivisha pete mimi tena mbele za wageni waalikwa?”
Josephine alizungumza kwa sauti ya chini chini.


β€œHapana alisha muacha na alinieleza mimi”
Magreth alizungumza kwa sauti ya chini huku ukumbi ukiwa kimya ukisikilizia jibu la Josephine. Tataratibu Josephine akatazama wageni waalikwa walipo ukumbini hapo. Taratibu akamkabidhi Samson kiganja cha mkono wake wa kushoto na Samson akamvisha Josephine pete hiyo kisha akasimama na wakaanza kunyonyana denda na kuwafanya watu wote ndani ya ukumbi huo kuanza kushangilia kwa furaha sana kwa maana tukio hilo ni la kusisimua sana.


β€œNina kupenda sana Samson”
Josephine alizungumza huku akimwagikwa na machozi.
β€œNina kupenda pia Josephine. Nita kulinda, nita kuheshimu, nita zidi kukupenda na kukuthamini hadi mwisho wa maisha yangu.”
Maneno ya Samson yakamfanya Josephine kuipitisha mikono yake shingoni mwa Samson na wakaanza kupeana denda takatifu.


Baada ya wiki moja Samson na Josephine wakafunga ndoa ambayo walihitaji iudhuriwe na watu wachache sana japo ni ya kifarahi sana. Furaha ikazidi kutawala katika maisha ya Josephien, Samson, Evans naMagreth.


β€œNina ombi la mwisho kwenu”
Raisi Mollel alizungumza huku akiwatazama Samson, Evans Magreth pamoja na Josephine mara baada ya kumaliza mapumziko ya harusi zao na kukaribishwa ikulu na raisi Molle.


β€œZungumza tu muheshimiwa”
β€œNina waomba mue washauri wangu wa hapa ikulu.”
Josephine akawazaama wezake na wote wakaonekana kukubaliana na ombi hilo.
β€œTupo tayari kukusaidia muheshimiwa raisi. Kwa maana nchi hii kwa sasa ipo mikononi mwako”
β€œNina shukuru sana tena sana, pia Cleopatra ata kuwa miongoni mwa washauri wangu. Amerudi Marekeni kukusanaya kila kilicho chake na kurudi hapa nchini Tanzania kwa ajili ya kufanya kazi aliyo iacha baba yake”
β€œNi jambo jema hilo ila muheshimiwa usije ukabadilika na uka fanya DHAMBI kama raisi Mtenzi”
Josephine alizungumza huku akimtazama raisi Mollel machoni mwake.


β€œKwa msaada wa mwenyezi Mungu nina imani sinto fanya DHAMBI yoyote ya kuigarimu taifa na dhambi zitakazo baki ni ndogo ndogo ambazo binadamu hatuwezi kuziepuka”
β€œAmen na Mungu ana niambie wewe ndio raisi utakaye tufikisha kwenye nchi ya ahadi. Kuwa yenye nguvu duaniani”
Josephine alizungumza kwa furaha na wote watano wakaumbatiana ofisini hapo kwa raisi Mollel.
β€œJambo jengine mali zote za nabii Sanga zime taifishwa na serikali na kwa sasa zipo nchini ya serikali ya Tanzania”
Raisi Mollel alizungumza kwa furaha na kusababisha kila mtu kufuraia ushindi huo walio upate wa kumuondoa adui aliye jivisha ngozi ya kondoo. Nabii Sanga.


Ndani ya miaka miwili ya raisi Mollel toka aichukue nchi ya Tanzania mikoni mwake, uchumi, viwanda, nguvu ya kisilaha pamoja na tecnolojia ikakuta sana nchini Tanzania. Mataifa mengine kama Marekeni, Ujerumani na China yakaanza kuiogopa Tanzania, kwani nchi ya Tanzania ime wapiti kwenye kila nyanda. Mamilioni ya wananchi wa Tanzania maisha yao yakazidi kupanda huku wananchi wakiwa na uzalendo wa nchi yao kuhakikisha kwamba nchi hauridi tena kwenye umasikini kama hapo awali na kila mwananchi ana furahia kuishi Tanzania na kuwa Mtanzania halisi na hata wale walio kuwa wame kimbia nchi kwa ajili ya kwenda kutafuta maisha katika nchi tajiri duniani, wakaanza kurudi mmoja baada ya mwengine kwa maana Tanzania ndio nchi namba moja tajiri na yenye nguvu ya kisilaha duniani na kuingusha nchi ya Marekeni iliyo kuwa ina ongoza kuwa tajiri na yenye nguvu hapa duniani.


MWISHO


(Funzo| Dhambi(SIN) ya kujivisha ngozi ya kondoo, kuonekana mwema mbele za watu na nyuma ukiwa na mambo machafu, tambua ipo siku kila jambo lita kuwa hadharani na uta kosa wa kukusaidia kukusafishia dhambi hiyo. Uzalendo wa kuipenda nchi yetu ndio jambo kubwa kuliko yote kwa maana hatuna nchi nyingine zaidi ya Tanzania. Hivyo tuna paswa kuilinda kwa ajili yetu na vizazi yetu)


Leo 27/12/2018 Nina anza kumshukuru Mungu kwa kunisaida kuimaliza hadithi hii niliyo iandika kuanzia 13/01/2018 na kuimaliza salama. Pia nipende kutoa shukrani zangu kwa wasomaji wangu wa ndani na nje ya nchi ya Tanzania. Mume kuwa ni watu muhimu sana wa kunipa support kwenye kazi yangu hii na kunifanya niwe nina jitahidi siku hadi siku kuhakikisha kwamba nina kikuza kipaji changu na kuandika hadithi ambazo ni nzuri zaidi ya hizi. Nina waahidi kwa mwaka 2019 pajapo majaliwa ya mwenyezi Mungu sinto waangusha nita hakikisha kwamba nina fanya kazi bora zaidi ya hizi. Nikisema niwaaje majina wasomaji wangu wote, wapo nitakao wakumbuka na wengine nita wasahau, ila kiukweli mume kuwa zaidi ya familia kwangu kwa mana siku hadi siku mume endelea kuwa nami kwenye kutekeleza majukumu yangu ya kuandika hadithi hii. Pia niishukuru familia yangu kwa kunipa support hata pale nilipo jihisi kushindwa na kukata tamaa, walinifariji na nika simama tena na kuandika zaidi na zaidi. Basi tukutane tena tarehe 10/01/2018 nitakapo anza hadithi nyingine mpya katika website yangu pamoja na group langu jipya la whatsapp kwa mwaka 2019 ambapo msomaji wangu uta kuwa una lipa ada ya shilingi 4000 tu kila mwenzi. Namba za group la whatsapp ni 0657072588 au 0742334453. Nina wapenda sana, nina wajali sana na nina waheshimu sana na Mungu atubariki na kutuongoza kwa mwaka mwengine mpya wa STORY ZA EDDY 2019. I LOVE YOU ALL MY FANS AND GOD BLESS YOU ALL.Z
 
Kama nilivyoahidi nimetekeleza stori imefika mwisho sasa kwa wanaopenda kusoma stori za huyu mwandishi wanaweza mcheck kwenye namba yake ndio legendary aliyeandika story ya asss you kill me kama mnaikumbuka ilikuaga humu kipindi flani
 
Mimi nimemaliza kuisoma leo tar 22/04/2025 umetisha mzee baba kazi nzuri
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…