RIWAYA: Siku kabla ya leo

RIWAYA: Siku kabla ya leo

Kudo

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2017
Posts
1,821
Reaction score
6,122
Sehemu ya 1*

Dar es laam saa 1:30am
Tarehe 20/07/2017

Doka Joker au maarufu kwa jina Dj alikuwa anawapa tabu ya kucheza wapenzi wa muziki,mara apige nyimbo za Diamond,haijaisha utasikia wimbo wa Alikiba,kila alipopiga wimbo basi watu walilipuka kwa mayowe kuonesha wamekunwa na utalaamu wa Dj kusugua mashine.

Watu wawili walikuwa wamekumbatiana muda wote,huku wakiwa wapo bize na wayazungumzayo,muziki ulipigwa ila hawakuwa na kushangilia au kucheza kulingana midundo ya mziki wao walikutanisha vichwa vyao huku mikono yao ikipita kiunoni mwa kila mmoja,maumbo yao yalikuwa na kazi ya kwenda kushoto na kulia kila mara na kwa mwendo wa taratibu sana.

Mbena alimuuliza Maiga
"Ni lini utakuja nyumbani?"
"Aah nitakuja baada ya mitihani ya kuhitimu chuo kwani umechoka kukaa kwenu?"

"Sio kama nimechoka ila naogopa kuishi mbali na ww Maiga nataka uwe wangu peke yangu,vile visichana vyako visije kunipokonya bwana"

"Mbena mpenzi acha wivu nishakupeleka nyumbani,bado Mimi kwenda kwenu,lakini si unajua wazazi wetu wote wanajua uhusiano wetu afu...."

Maiga hakumalizia kauli yake kuna mtu alipita karibu yake akampiga kikumbo akageuka kutazama hakuona mtu,akayarudisha macho kwa mpenzi wake Mbena aliekuwa akimtizama kwa swali la kulikoni nae pasipo kutoa sauti akanyanyua mabega kwenda juu kuashiria hajui kitu wakaendelea na maongezi yao.

Saa 2:05


Mziki bado ulikuwa umepamba moto huku sasa hali ya hewa mule ukumbini ikianza kuwa na harufu kali ya jasho,.
Maiga alimuaga mpenzi wake Mbena akaelekea vyooni kujisaidia,.
Akapiga hatua mbili na kumgeukia mpenzi wake Mbena akamtazama tena kisha akamkonyeza na kugeuka kuelekea vilipo vyoo vya ukumbi ule wa kuchezea muziki.

Saa 2:20

Alitizama saa yake ikamthibitishia ni zaidi ya dakika kumi na tano tangu Maiga amuage ya kuwa anaelekea chooni na hajarudi,kichwani mwake alihisi ni pengine Maiga anamtu mwingine huko vyooni au atakuwa upande mwingine tofauti na huo akimsaliti,akajenga picha vile usaliti ule unavyoendelea,akajikuta anakabwa koo kwa uchungu na hasira, akaona kukaa bila kufanya kitu ni kujisumbua ngoja amfuate hukohuko akawaadabishe yeye mwenyewe,akasimama kwa hatua za shari akauendea mlango wa kuingilia vyooni kule.

Kwa hatua za kujiamini akaucha mlango wa kuingilia vyoo vya kike na kuingia vyoo vya kiume,akakuta kuko kimya na kumetulia huku kwa mbali,ukisikika mziki ukitoka kwenye sipika za ule ukumbi wa mziki,akaanza kufungua mlango mmoja mmoja na kuangalia,lakini kila alivyokuwa akikagua na ukimya ule akaanza kuogopa lakini kwa nguvu ya wivu akazidi kupiga moyo konde na kuvikagua vyumba vyote ila hakumkuta Maiga.

Milango ya vyoo ilikuwa imepangana na kuacha upande mmoja kama korido ndefu na mwishoni mwa korido ile kulikuwa na uwazi ulioelekea upande wa kulia wa vyoo vile,Mbena akafuata usawa huo na kujikuta sehemu ya kushushia haja ndogo,akaanza kuambaa na uwazi huo,
Hakufika mbali akakutana na damu iliokuwa ikielea ndani ya eneo lilotengenezwa kwa ajili ya kusafirisha mkojo,hofu ikatanda moyoni mwa Mbena lakini akapiga moyo konde na kusogea upande huo hapo hakuamini macho yake alichokiona

Maiga alikuwa amesimama huku mkono mmoja akiwa ameugemeza ukutani na mgongoni mwake kulisimama mpini wa kisu huku damu zikimtililika,Mbena hakuamini macho yake akapiga kelele kubwa na kwa haraka akamkimbilia Maiga na kumvuta akamweka kando huku akilia,akaushika mpini ule wa kisu na kujaribu kuuchomoa,matendo yote aliyafanya huku akiwa hajielewi akipiga kelele na akiliita jina la Maiga.

Wakati akihangaika kumsaidia Maiga punde akaingia mtu mle chooni huku akiwa amejiziba sura yake kwa kofia,alikuwa kashika kamera akampiga picha kadhaa Mbena kisha kwa kasi ya umeme akapotea mle chooni,wakati yeye akiwa akitoka wakaingia watu wanne wakamkamata Mbena,mmoja kati yao akampiga na kitu kizito kisogoni pake kisha wakamchukua na kutokomea nae wanakokujua,

Haikuchukua muda ukumbi wa burudani ukageuka vilio na mikimbio ya huku na huko.....


Asalaam Kudo (Bahati Mwamba)
 
Sehemu ya 2*

Saa 4:15
Tarehe 20/07/2017

Koplo Mina alikuwa yupo katikati ya barabara akitoka moroco akielekea nyumbani kwake Mwananyamala,alitoka kuushuhulisha mwili wake kwa mpenzi wake alieishi maeneo hayo na sasa ni wakati akirudi nyumbani huku mwili wake ukiwa mwepesi ajabu,na kwenye spika za redio yake kulisikika wimbo wa Nyanshisiki Malaika.

Huku akili yake ikimuwaza mpenzi wake simu yake ikaunguruma kutoka mfukoni kwake,akapunguza mwendo na kuitoa kisha akatazama kwenye kioo akakutana na jina la mpigaji Ascp Odeni,akagafirika maana alijua bwana huyo alitaka nini kwake akatukana tusi kubwa kumlaani mkubwa wake huyo wa kazi.
Aliamini kabisa Ascp Odeni amempigia alfajiri yote hiyo kumkumbusha kuhusu ombi lake la kutoka nae kimapenzi,akaingalia simu yake ikiita hadi ikakata.

Punde ikaita tena na mpigaji alikuwa yuleyule,huku akiwa amekunja midomo akaipokea simu ile na bwana Odeni akaunguruma kwa sauti nzito ya kiume
"Koplo Mina!"
"Nakusikia Afande"
"Kuna tukio lipo hapo Masai klabu naomba ufike haraka uungane na Konstebo Tito,ahsubuhi nataka ripoti"
"Nimefika"

Simu upande wa pili ikakatwa akabaki Koplo Mina na gari lake,akaongeza mwendo maana hakuwa mbali na hilo eneo,akakata barabara inayopita papichulo akatokea ilipo mahakama ya kazi,punde akajikuta yupo Masai klabu,akapaki pembeni kulipokuwa na gari za polisi mbili,kwa mwendo wa haraka akasogea hadi kwenye lango la kuingilia Masai klabu,hapo akakutana na kizuizi cha askari polisi akaonyesha kitambulisho chake akaruhisiwa kupita,akajongea hadi ndani,kulikotokea tukio, huko nako akakutana maaskari wengi waliobebelea silaha zao,akapiga hatua na kufika eneo kulipokuwa kumelala mwili wa mtu,huku askari wa kuchukua alama na michoro au kitaalam kitengo chao kiliitwa Investigation crime scene.

Akawapita askari waliosimama pembeni akaufikia mwili ule,hakuamini macho yake alikuwa ni Maiga mtoto wa waziri wa fedha,pia alikuwa ni rais wa chuo kikuu cha Dar es laam,hapo akapata jibu kwanini askari wapo wengi eneo lile,alipokwisha kumtizama akaomba avae mipira akaletewa akavaa.

Aliuchunguza mwili ule kwa hatua hakupata taabu kugundua alichomwa kisu mgongoni maeneo ya uti wa mgongo,lakini hakukawia kugundua marehemu alishangaa kitu kabla ya kufa...

Aliporidhika na uchunguzi wake akasimama kisha akawageukia wataalamu wa michoro na matukio picha,akawauliza
"lolote!?"
"ni mapema kujibu"

Akaachana nao akasogea pepembeni aliposimama raia mmoja na askari wakiteta jambo,akawafikia hakupata taabu kujua yule raia ndie alikuwa meneja wa klabu ile na askari yule ndie Konstebo Tito,.

Akamuuliza meneja tukio lilivyokuwa nae akaeleza ya kuwa yeye alisikia tu kelele zikipigwa kutokea upande wa vyooni na watu kukimbia kutoka vyooni hadi ukumbini jambo lililozua tafrani kwa wapenda burudani wale,yeye kama meneja akawaita walinzi wake wa klabu ile wakaelekea vyooni kule,na kukutana na tukio lile,baada ya maelezo hayo Koplo Mina akauliza tena.
"hakuna mtu alieona?"
Konstebo Tito akaingilia na kusema
"kuna binti pale yeye tangu tumeingia hapa alikuwa analia tu hajasema lolote na kwa mujibu wa mashuhuda wengine wanadai walikuwa wote na marehemu"

Koplo Mina akamfikia binti yule aliekuwa amejikunyata akilia,akamtazama akagundua kisaikolojia hayupo sawa ila akaamua kumuuliza tu
"Unaitwa nani?"
" Nyange"
"unamfahamu vipi Maiga"
"Simfahamu"
"inasemekana mlikuwa wote"
"hatukua wote wala sikuja nae"
"ila?"
"Wakati wanaingia na mimi ndo niliingia"
"wakati wanaingia inamaana zaidi ya mmoja"
"ndio"

Koplo Mina akaona huyo binti anataarifa za mwanzo akamwita Konstebo Tito na kumpa maelekezo machache ya namna ya kumhifadhi yule binti kituoni kisha yeye akaufuata mwili wa Maiga uliokuwa ukipakiwa kwenye gari kwa ajili ya kupelekwa hospital ya mkoa wa Dar es laam kwa ajili ya hatua nyingine zaidi.

Akawasha gari na kutaka kufuata nyuma ya gari iliobeba maiti ile hapo akakumbuka kujitazama akaona mavazi hayamruhusu yeye kama askari,yale yalikuwa ni mavazi aliovaa maalumu kwa ajili ya mpenzi wake,akakata shauri aende kwanza kubadilisha muonekano maana hakuwa mbali na kwake hapo komakoma mita kadhaa kutoka eneo la tukio.

Saa 5:45

Ndani ya suruali ya kitambaa,blauzi yenye mikono mirefu,bastola yake kiunoni na kalamu mkononi,huku nyuma akiacha lawama za matamanio kwa umtazamae,Koplo Mina alivuta hatua zake kikakamavu kuuendea mlango wa Dr Maswe alie kitengo cha utambuzi alama,akaugonga akakuta kimya,ni wakati akijaribu kugonga tena akapita tabibu mmoja karibu yake akampa taarifa kuwa Dr Maswe yupo chumba cha uchunguzi.

Hakutaka kupoteza muda akatembea hadi kilipochumba hicho,hakupata tabu kukiona maana kwa nje walikuwepo maaskari kadhaa,waliokuwa wakilinda chumba kile na ni yeye alietoa maagizo kwa makonstebo wale wahakikishe wanailinda ile maiti.

Lakini hawakuwa peke yao aliongezeka mtu mwingine ambapo alipofika alitambulishwa kuwa ni kaka wa marehemu,akampa pole kisha taratibu akausukuma mlango ule na kuzama ndani ambapo alimkuta Dr Maswe akihangaika na taaluma yake,hakumsemesha akamwacha afanye anayoyafanya yeye anasubiri ripoti.

Dr Maswe alimgeukia Koplo Mina akamtazama kisha kama anaetaka kulia au kucheka akazungumza
"Tena wamekupa kesi wewe ila hii walipaswa kumpa wa hadhi yake"

"kwa hiyo mimi sifai"

"Unafaa ila inaweza kukufukuzisha kazi mtoto wa mkubwa huyu"

Koplo Mina akafikiri kidogo kisha akapuuza maneno ya Dr akamuomba ripoti nae maswe akampa kisha akageuza na kuacha mwili wa Maiga ukipelekwa Mochwari yeye akaelekea kuripoti kwa Ascp Ombeni,maana ishafika ahsubuhi sasa na jua limeanza kuchomoza.

*****
Hakuwa anajua yupo wapi japo mazingira aliokuwa ni chumba kidogo kilichojaa kiza,haikumchukua muda kukumbuka tukio la mpenzi wake kuchomwa na kisu na hakutaka kuamini eti Maiga amekufa,.

Mbena alijikuta akiangua kilio kama mtoto mdogo,pia hakutaka kuamini kuwa pale eti yupo kituoni na anahisishwa na mauaji ya mpenzi wake,alilia pasi kupata msaada wowote,punde kile chumba kikawashwa taa akajikuta yupo sehemu ambayo sio jela kwa uzoefu wa simulizi za mazingira ya jela kutoka kwa watu,.Hapo akili yake ikamwambia tayari ashatekwa au kama ni jela basi amepewa mahali pale kwa kuwa yeye ni mtoto wa waziri wa Afya,.

Mawazo yake yaliyeyuka baada ya mlango kufunguliwa kisha akaingia mwanaume mrefu mwembamba usoni amevalia kinyago mithili ya Ninja,Mbena alijikuta akitetemeka kwa woga,yule mtu nae alipomsogelea akamwambia
"inabidi ukubali wewe ndie umemuua Maiga,sitaki nikwambie kwanini fikiria kwanza nitakuja baadae nikupe utaratibu"
Kisha akaindoka zake.

Mbena alijikuta njia panda asijue kwanini analazimishwa kukubali ameua na inamaana kweli maiga ashaiaga dunia,alijikuta akilia upya alilia hadi akamlaani mtu yule aliingia na kumpa ufikirio wa ndio au hapana,
Hakuwa na namna nafsini akakubali tayari ametekwa na yupo matatizoni hajui ataokoka vipi,akamlaani yule mtu mwenye umbo refu na mwembamba,huku akimpachika jina Mchinjiko...

Asalaam Kudo(Bahati Mwamba)
 
Mkuu utaenda nazo zote2 kwa wakati?? Au unataka kutuletea arosto nyingine?? Kwa nini usingemaliza ile ya kwanza then ndo ikafuata hii?? Kwa nini usimalize KIKOSI CHA PILI kwanza??
 
Mkuu utaenda nazo zote2 kwa wakati?? Au unataka kutuletea arosto nyingine?? Kwa nini usingemaliza ile ya kwanza then ndo ikafuata hii?? Kwa nini usimalize KIKOSI CHA PILI kwanza??
Nadhani ukitizama kule inakoruka Kikosi cha pili utaona lengo langu la kuachia riwaya zote mbili hapa,so usiwe na Shaka zitaisha zote,ila inategemeana na kuruka kila siku maana kuna siku nitakwama kupata bando,ila likiwepo kila siku mzigo utakuwa hewani
 
Sehemu ya 3*

Saa 8:00 ahsubuh

Koplo Mina aligonga mlango wa ofisi ya Ascp Odeni,bila kusubiri karibu akazana ndani,kisha kwa utii akakamaa na kutoa salamu kwa mkuu wake yule,.

Alikuwa ni mwanaume mnene mfupi na mweusi,alikaa nyuma ya meza pana kiasi,Alikuwa ni Odeni akimtizama koplo Mina,kisha pasipo kusubiri sana akamtupia gazeti Mina,Mina akalitazma lile gazeti lilikuwa ni kutoka kampuni ya uchapishaji magazeti ya udaku,

Akalichukua,haikumchukua muda mrefu kubaini kwanini alitupiwa gazeti lile na mkubwa wake,gazeti lilipambwa na picha kubwa ya binti wa waziri wa Afya,akiwa ameshika kisu kilichozama mwilini mwa Maiga.picha ile ilipambwa na maneno makubwa juu yake
"HUYU NDIE MUUAJI WA RAIS WA CHUO KIKUU".

Mina akamtizama Ascp Odeni kisha akamrudishia gazeti lake,akachukua ripoti ya Dr Maswe akamkabidhi Ascp Odeni,.

Odeni akaitazama ripoti ile,kisha kwa upole akamuuliza koplo Mina
"kwa hiyo alama za vidole ni vya mwanamke ambae ndio huyo muaji?"
"Ndio"
Kwa hiyo na wewe unahisi ndie kaua!"
"Mapema kuthibitisha"
"taarifa nyingine!?"
"Hadi sasa hakuna aliethibitisha kumuona muuaji"
"OK angalizo ni kuwa alieua na alieuawa wote watoto wa mawaziri hivyo sitaki niondolewe cheo kisa umefeli kumpata muuaji halisi,hata kama ni huyo binti thibitisha tumtie hatiani"
"sawa mkuu"
"Afu vipi sasa ile inshu"

Mina alimtizama mkuu wake huyo aliekuwa akitabasamu tu kisha akamjibu kimkato
"Ngoja tuzingatie kazi kwanza"
Kisha akaondoka ofisini mule,huku kichwa chake kikivurugwa na mambo yalioanza kujitokeza hadi wakati huo,.
Alipokuwa akitokeza tu nje akakutana na Konstebo Tito,aliekuwa na haraka,walipokutana wakapeana salamu kisha Mina akamwomba wazungumze kwanza,.

Tito alimpeleka hadi chumba alipomhifadhi binti walie amini ni shuhuda wa tukio lile,kisha akamwacha Koplo Mina amhoji yule binti huku yeye akiwa ni mwandishi wa maongezi yao.
"Nyange ndo jina lako sio"
"ndio"
"wakati unaingia ni wewe au wao waliotanguli"
"wao"
"walikuwa Wangapi"
"wawili"
"jinsia?"
"kike na kiume"
"walivaaje? "

Nyange akaelezea wasifu wa watu wale,hapo koplo Mina hakupata taabu kutambua walioongelewa ni Maiga na Mbena,akamgeukia tena
"uliona wakati alikiuawa"
Nyange akasita kujibu kisha kama aliepigwa na shoti ya umeme machozi yakaanza kumtoka na bila kuulizwa tena akajibu kwa kifupi kuwa hakuona mauji yale,.

Koplo Mina hakutaka kumhangaisha akampa ishara konstebo Tito,kwa pamoja wakatoka kwenye chumba kile.
Walipofika nje koplo Mina akamuomba konstebo Tito watumie gari moja la kwake, walipoingia ndani ya gari,koplo Mina akamuuliza Tito amegundua nini hadi sasa,konstebo Tito akamtazama kidogo mwanadada yule kisha akamwambia
"Muuaji sie aliwekwa kwenye gazeti, na hata kama ndie kuna mtu aliona tukio zima au alihusika pia,
Lakini Mbena hajaua muuaji ni aliepeleka picha kwenye vyombo vya habari,kwa hiyo ili tufike kwa muuaji lazima tujue mwandishi wa habari hizo,"

Koplo Mina akakubaliana na konstebo Tito,kisha wakapanga kutawanyika huku konstebo tito akijipa jukumu la kuchukua kuomba kikosi cha maaskari kwenda nyumbani kwa waziri ili kumweka kizuizini Mbena,na asaidie kujibu tuhuma za kuhusika na mauji yale.
Koplo Mina yeye akapanga kurudi kwa Dr Maswe kuna kitu alihitaji kukithibitisha Kwanza kabla hajaendelea na majukumu Mengine,lakini kubwa zaidi alihitaji kubadilisha usafiri maana kwa kutumia gari angejikuta yuko nyuma muda,akapiga hatua kurudi kituoni huku akimwacha Tito akipokea vijana wenzie kwenda nyumbani kwa waziri.

Saa 9:20

Muda huu ulimkuta Koplo Mina akiingia hospital ya mwananyamala,alikuwa juu ya pikipiki kubwa ya kipolisi,akapaki pembeni kwenye maegesho ya pikipiki,kisha kwa mwendo wa mwanafunzi aliechelewa vipindi vya darasani akakifikia chumba cha Dr Maswe,akagonga akaitikiwa na mtu aliendani,akausukuma mlango akaingia ndani akamkuta Dr Maswe akiwa yupo bize na makaratasi kadhaa,alipomwona Koplo Mina,akatabasamu kisha akakaa tayari kupokea swali lolote kutoka kwa koplo.

Koplo Mina akaomba apelekwe ulipo mwili wa Maiga,kuna kitu anahitaji kuona wakiwa wote nae Dr maswe hakubisha akanyanyuka wakaongozana kwenda ilipo mochwari,waliwapita wamama kadhaa waliokua wakilia huku wakiomboleza kifo cha mpendwa wao,watu mbalimbali walikuwa wakifika hospotalini pale,wanafunzi wa chuo nao walikuwa pamoja katika maombolezo yale,.

Dr Maswe na Koplo Mina waliongozana hadi ulipomwili wa Maiga,wakamwamuru mhudumu wa mochwari awatolee mwili ule,
Ulipokwisha kutolewa Mina akausogelea akautazama shingoni,akaona mbinyo wa vidole nyuma ya shingo ya Maiga,akamwita Dr akamwonyesha,nae Dr Maswe akaungana nae kisha bila kuulizwa Dr Maswe akaeleza,
"Kama alikuwa anajisaidia inamaana muuaji alimvizia kwa nyuma,ndo maana kisu kilikita mgongoni,pia muuaji alikuwa mjuzi katika fani hiyo akamchoma ulipo uti wa mgongo,hii inamaana alidhamiria kuua,na asingefanikisha mauji yake bila kutafuta egemeo,ambalo ni shingo ya maiga,ukitazama vizuri sio vidole vya kike hivi ni vipana na virefu,lakini japokuwa ni mbinyo sijafanikiwa kupata alama zake,hii onamaanisha muuaji alivaa mipira,ila alitumia nguvu kumbana nyuma ya shingo ndo maana hata bila vifaa angalizi bado tumeweza kuona kwa macho."

Koplo Mina akashusha pumzi ndefu kisha akaomba watoke mule,wakati wakitoka akapigiwa simu na konstebo Tito aliemfahamisha kuwa kule kwa waziri wa Afya Mbena hayupo,taarifa kutoka kwa mama yake zinasema hakurudi jana tangu aondoke jana na maiga hata wao hawana taarifa nae,na hawajui alipo.

Koplo Mina akaona ugumu katika kazi yake sasa inapaswa ajitahidi kweli ili muuaji apatikane,akawaza aende kwenye moja ya magazeti anunue ili apate kuona mwandishi wa habari ile,.Akavuta hatua hadi kwenye kituo cha kuuzia magazeti kilichokaribu na hospital ile,akanunua moja na kulipitia,akakutana na mwandishi wetu,akaachana nalo,akanunua lingine akakutana tena na mwandishi wetu,na yalikuwa mawili tu yenye habari ile akazubaa kidogo ila hakutaka kulaza damu atamjua mwandishi wetu hukohuko ofisini kwao.

***

Mbena alikuwa amejikunyata,macho mekundu,huku koo likiwa limemkauka kutokana na kilio,mawazo yaliutawala ubongo wake,.
Akiwa katika mawazo ya hatima yake punde akaingia tena yule bwana ambae mbena alimpachika jina Mchinjiko,wakati alikuwa na kamera huku akiwa ameongozana na wanaume wengine wawili walioshiba kimazoezi,kikubwa wale watu walikuwa uchi wa mnyama hakujua lengo lao ni nini,na kwanini wanakamera wanaume wale watatu,akajikuta akitetemeka kwa woga,huku mkojo ukishuka maungoni mwake bila kizuizi ilikuwa fadhaa kwa Mbena na hakuna wakati mgumu katika maisha yake kama aliokuwa nao wakati huo na hiyo ilikuwa ni saa 10:02,tarehe 20/07/2017......


Asalaam Kudo( Bahati Mwamba)




Nb:Kuna hadithi mbili zinaendelea hapa hii na nyingine ambayo ipo sehemu ya 9*
Lengo langu ni kuomba kwa mwenye kupenda kuunga mkono kazi za waandishi,aniunge mkono ili niweze kutoa nakala vitabu vyangu viwili ambavyo vimekwisha kufanyiwa mastering,.

Yeyote atakaenichangai kiasi chochote atapata nakala mbili zote popote atakapo kuwa vitamfikia

No zangu ni hizi
0758573660
0658564341
0624155629
Ahsanteni.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom