RIWAYA: R i s a s i 4

RIWAYA: R i s a s i 4

CHAPISHO LA 12
Siku mbili baadae…
JOSEPH Rutashobya alisimama juu ya kilima
kidogo, akatazama eneo lote lililokuwa na kijiji
walichokiishi zamani, mahame, hakukuwa na
nyumba hata moja, hakukuwa na binadamu
aliyeishi, migomba na mibuni vilifanya machaka
ya kutisha. Joru akainama kichwa kwa muda na
kuwaomboleza wapendwa marehemu wote
waliouawa siku hiyo, aliwaombea na wale wote
walijaribu kukipigania kijiji chao. Akamtazama
Kemi aliyekuwa kajifunga lubega, wakaanza
kutelemka kilima kuelekea bondeni. Mkononi
akiwa na upanga na jembe dogo, Kemi alikuwa
na akimfuata kwa nyuma wakati Joru
akikatakata vichaka na kufanya njia.
Haikuchukua muda walikuwa chini kabisa,
kwenye tambarare ya vichaka. Joru alitazama
eneo lile, akakumbuka vipindi vingi sana vya
utoto wake, akamtazama Kemilembe, aktazama
tena eneo lile walilokuwa wakiishi.
‘Joseeeeee, twende tukacheze !!!!’
Aliihisi sauti ya kitoto ya Kemi ikipita masikioni
mwake miaka zaidi ya ishirini iliyopita, hisia kali
zikauteka moyo wake, kumbukumbu ya matukio
mengi ya maisha ikajaa kichwani mwake,
aliwaona mtu mmoja mmoja aliyemkumbuka,
rafiki zake, wazazi wake na memngine mengi.
Machozi ya uchungu yakamtiririka,
akamkumbatia Kemi kwa uchungu.
“Kemi, kijiji kilichotulea, kijiji kilichotukutanisha
duniani, kijiji kilichotujengea mapenzi yetu, kijiji
tulichokipenda sana, leo hii si kijiji tena,
mahame na ukiwa…” Joru alimwambia Kemi.
Kemi akaegama kifuani mwa Joru.
“…Wewe ni mali ya Mungu na mimi ni Mali ya
Mungu…”
Sauti iliyofuatiwa na mwangwi, sauti mbaya
iliyomchukiza Joru, na kutia hasira mpya katika
moyo wake, donge lilimshika, Joru alianza
kutetemeka na kupumua kwa nguvu. Kemi
aliyaona mabadiliko hayo ya Joru, akamtazama
kwa woga kijana huyo aliyekuwa na mwili
unaotisha pindi awapo hasirani.
“Nini Joru?” Kemi aliuliza.
“Lazima nilipe kisasi, lazima nimuue kwa mkono
wangu, damu ya Rutashobya na Watanzania
haiwezi kupotea hivi hivi,” Joru alimjibu Kemi,
kisha akasogea taratibu kwenye eneo ambalo
alihisi kabisa ndipo alipouawa baba na mama
yake
“………Aaaaaaaaiiiigghhh!!!!.........”
Sauti ya mama wa Joru ilirudi kwa kishindo
moyoni mwa Joru, akashtuka, moyo ukawa
unamwenda mbio, akasimama na kutazama
chini taratibu, akaondoa mguu wake uliokuwa
umevikwa buti la kijeshi, buti la Muamerika,
akaona kitu kinachong’aa kwa jua lile la saa
nane mchana, akainama na kufukua udongo ule
kidogo tu, kidani, akakivuta, kikajifukua kutoka
udongoni. Joru alikikumbuka kidani kile,
akakigeuzageauza, kidani cha mama yake.
Alikisafisha kwa nguo yake, kilikuwa na kutu
lakini hazikuwa za kutisha, Joru akamtazama
Kemi, akaitazama shingo ile ya upanga, akampa
ishara ya kuwa asogee, naye akafanya hivyo
aliposogea akamvisha kidani kile shingoni
mwake.
“Sasa wewe ndiye mama Rutashobya!” Joru
akamwambia, kisha wakaendelea kuelekea eneo
husika.
“Asante Joru,” Kemi alijibu huku akiendelea
kumfuata nyuma Joru mpaka walipofika eneo
walilohisi ni lenyewe ambalo lilikuwa na choo.
Kemi akavuta hatua chahe, akasimama mbele
kidogo ya Joru, palikuwa na udongo uliodidimia
kiasi na nyasi kavu zilizokuwa eneo hilo.
Akasimama na kutazama mbele, akauona mti
ambao alijificha akimtazama mzee Rutashobya
alipokuwa akifukia mfuko ule, kisha akarudisha
macho yak echini tena na kuonesha kidole.
“Joru, ni hapa bila shaka, siku ile mimi nilijificha
pale kwenye ule mti na ndoo yangu kichwani,”
Kemi akamwambia Joru. Macho ya joru
yalimtazama Kemi kwa upendo mkubwa.
“Wewe ni mtu wa pekee sana kwangu,” Joru
akasema, kisha akainua kijembe chake na
kuchimba taratibu. Joru alichimba huku Kemi
akiwa pembeni kuangalia kinachotokea.
Haikuchukua muda, Joru aliunasa mfuko wa
plastiki, akatupa kijembe pembeni, akaushika ule
mfuko mchafu na kuuvuta taratibu kuja nje.
‘Kesho na keshokutwa utakua kijana mwanangu,
hakikisha unalipa kisasi kwa damu hii
inayomwagika, damu ya familia yako, damu ya
wazazi wako,’
Sauti ya baba wa Joru ilimrudia mwanawe
alipokuwa akivuta mfuko ule, wakati mfuko ule
ukichomoka taratibu ardhini, Joru aliukumbuka,
aliukumbuka bila shaka.
‘Jose, usiutupe mfuko huo una kazi kubwa
baadae,’
Maneno hayo yalipata maana siku hiyo kwa
Joru, mawazo yalikuwa lukuki, hakuna
aliyeongea wala kumuuliza mwenzake, kila
mmoja alitaka kuona tu nini kilikuwa kwenye
mfuko huo.
“Joru, kuna sumu humo ndani” Kemi
alimwambia Joru.
“Hakuna sumu, baba alikuwa anakutisha tu,
hakutaka uje uchezee, ngoja uone,” joru akajibu
na kumalizia kuuvuta ule mfuko nje kabisa ya
shimo lile, ulikuwa umefungwa vizuri,
umefungwa kifundo. Joru akaupapasa, sasa
alikuwa mtu mzima alielewa nini kilikuwa katika
mfuko huo, akaufungua na kukitoa, bastola ya
kizamani na risasi nne. Tabasamu pana
likaupamba uso wa Joru. Akaigeuzageuza
bastola ile, ilikuwa ya kizamanai kwelikweli, na
risasi zake nne ambazo hazikuwamo katika
magazine, ila pembeni katika kikasha cha
chuma. Kemi alishangaa sana aliijua bastola
kwa kuwa aliwahi kuiona katika senema za
kizungu, na aliiona kwa askari wakati alipokuwa
gerezani.
Joru akaitazama ile bastola iliyokula kutu za
kutosha, hakika ilikuwa ya kizamani. Alipokuwa
mtoto alikiona kitu hiki mara kadhaa ndani kwao
lakini hakuwahi kujua kazi au matumizi yake,
lakini sasa anajua hata kwamba ilitumika katika
vita kuu ya pili ya dunia ambayo kwa simulizi,
baba yake mzee Rutashobya alishiriki, baba
ambaye hata yeye alizoea kumwita babu.
Akachomoa risasi zile nne ailizokuwa ndani ya
kibweta kile cha chuma, ni nne tu na si zaidi,
alizitazama kwa makini, hakujua lengo la baba
yeke kuzifukia, labda hakutaka mtu azione au
hakutaka watu wabaya kama Malyamungu
kuzipata kwa maana wangetumia kwa matumizi
mabaya vilevile.
“Kemi, turudi, hakuna la zaidi,” Joru
akamwambia Kemi kisha wakageuza na kurudi
walikotoka wakiwa wameshikana mikono.
Joru alifika nyumbani, kazi ya kwanza aliyoanza
nayo ni kuisafisha ile bastola kwa kutumia
mafuta maalumu ili iweze kufanya kazi upya.
Alikuwa kaka peke yake nyumba ya nyumba
wakati Kemi akiendelea na kazi nyingine kwa
mama Shibagenda ikiwamo kumlea Joru mtoto.
Masaa matatu, yaliirudisha ile bastola katika
uhai mpya, ilikuwa iking’aa, iking’aa mpaka
inaumiza macho. Mtutu wake wa chuma
king’avu ulirudi katika uhai, kitako chake cha
mbao ya mpingo kiling’azwa kwa mafuta, kila
kitu kilirudi kati uhai. Joru aliziweka sawa
risasui na akahakikisha kuwa zipo sawa kwa
kazi zitakayotumwa, akavuta kikasha kingine
ambacho risasi zake zinaingiliana na ile bastola,
akajaribu kuipachika katika magazine ikakaa
sawa akapachika nay a pili nayo ikawa sawa,
akaichukua ile magazine na kupichika mahala
pake, akajaribu hiki na kile. Joru aliziheshimu
zile risasi nne, hakutaka kuziharibu kwani alijua
sasa kuwa zina kazi maalumu, kazi ngumu ya
kisasi. Akaishika bastola, akafanya kama
analenga, akabana jicho moja, bahati nzuri
kulikuwa na mwewe aliyekuwa anapita,
akaondoa usalama na kufyatua bastola hiyo.
Kwa mara ya kwanzaq alipata ladha ya mlio wa
bastola ya kale, Yule mwewe alijilaumu kwa nini
alipita eneo hilo, kwani ni manyoya tu
yaliyoonekana angani, alipotua chini
hakujulikana ndani ni wapi na nje ni wapi. Joru
akatikisa kichwa kuonesha haamini
kinachotokea.
“Asante Rutashobya, risasi hizi nne zitaishia
kichwani mwa Mali ya Mungu kama amekufa
basi nitazifyatua juu ya kaburi lake,” Joru
alijiseme kwa sauti ya utulivu, akachukua zile
risasi nne na kuzisweka katika kibweta chake
kama kwanza, akakiweka katika mkoba wake
mdogo wa kijeshi kisha akaiweka ile bastola na
kunyanyuka kutoka pale alipoketi kwa muda
mrefu. Alipogeuka akakutana uso kwa uso na
mama Shibangeda.
“Vipi Joru mbona watushtua?” Mama
Shibagenda akauliza.
“Pole na samahani mama, nilikuwa nafanyia
mazoezi kifaa change maalumu, maana
natakiwa kwenda Uganda siku nne zijazo,” Joru
akajibu.
“Kikazi au binafsi?” mamaShibagenda akauliza.
“Kikazi mama, na ni kazi ya hatari sana kuliko
unavyofikiria,” Joru akajibu kwa kirefu.
“Kazi gani mwanangu?” mama Shibagenda
akazidi kuhoji.
“Mama, wakati wa vita vya Uganda. Jeshi la
Tanzania lilifanya kazi kubwa sana ya
kumfurusha nduli Idd Amin, lakini kuna kitu
walikuwa hawajamaliza, nimetumwa kwenda
kumaliza hicho kimoja, ila ni hatari, kuna mawili,
kurudi au kuzikiwa huko huko,” Joru alimwambia
mama Shibagenda.
“Joru!” Mama Shibagenda aliita kwa mshangao,
akajishika kiuno na kumtazama mwanajeshi
huyo kijana.
“Mbona unashtuka mama?” Joru akauliza na
kusimama kutoka pale alipokuwa.
“Mimi hiyo kazi yenu inaniuzi, yaani baba yako
angejua unataka kwenda huko angeshakukataza,
bora ulienda kwa kutoroka, ila we Joru ni dume
huogopi,” Mama Shibagenda akamwambia Joru.
Kisha wote wawili wakafuatana kurudi upande
wa pili wa nyuma, mwendo wa hatua ishirini,
mama Shibagenda akasimama na kumzuia Joru.
“Enhe, nambie, kuhusu Kemi, nimependa sana
stori yenu, sasa unaoa au unaenda kumtafuta
Yule uliyezaa naye?” Mama shibagenda
akauliza.
“Mama, mimi sijazaa na mtu, Yule kazaa
mwenyewe, kwanza kaniuzi sana, mwanamke
gani mwenye roho mbaya ya kuniletea mtoto na
lkisha yeye kuondoka, je kama asingeniona, si
angeweza hata kumtumbukiza chooni?
Wanawake wa mtindo huu hawafai katika jamii,
wajirekebishe. Lakini nakushukuru mama kwa
kunilelea mtoto, na Mungu alikuongoza
ukampata mpenzi wangu kipenzi, Kemilembe,
huyo ndiye mama wa Joru, nampenda sana
Kemi,” Joru aliongea kwa hisia na masikitiko.
Joru akamuona mwanawe akicheza kibarazani
pamoja na mtoto wa Shibagenda.
“Kuna watu wamezaliwa na wema wa ajabu na
upendo wa kupindukia, nah ii ni familia ya
Shibagenda, asanteni sana kwa ukarimu wenu
mmenilea, mkatulea mpaka sasa, muendelee
kutulea mpaka tutakaposimama kwa miguu yetu
wenyewe, nitamuoa Kemi pindi nikitoka kwenye
Operesheni Mali ya Mungu huko Uganda,” Joru
akamwambia mama Shibagenda na kumnyanyua
mwanawe.
“Yalivyofanana basi!!!” Kemi akazungumza
kutokea mlangoni alikokuwa amejificha.
Joseph Rutashobya aliitazama kalenda ya
ukutani kwenye ukuta wa nyumba ya
Shibagenda, akahesabu siku zilizobaki kwa
mapumziko yake, hazikuwa haba, zilikuwa saba,
akatikisa kichwa, akaamua moyoni kesho
naanza oparesheni yangu, naipa siku tatu iwe
imekamilika,” akajisemea.
‘….Hakikisha unatimiza hilo kama ulivyosema…!’
Alihisi sauti kama ya baba yake ikimwambia.
‘Nitatimiza,’ aliijibu.
Siku hiyo usiku Joru hakulala vizuri,
alisumbuliwa na ndoto za kutisha, ndoto za
kuogofya na kumkatisha tama, mara kwa mara
alishtuka na kuketi kitandani. Kemi naye alimka
mara zote hizo na kumtuliza Joru, kumfariji
katika mahangaiko yake. Ilipofika saa tisa usiku
Joru akachuku begi lake la kawaida tu sio la
kijeshi, akapanga baadhi ya vitu vyake muhimu.
Aliitazama sana bastola ile aliyoichimba porini,
sasa iking’aa kana kwamba ni mpya lakini
utaijua kwa umbo lake kuwa ni ya kizamanai
sana, Smith and Wesson, hakuwa na uhakika
kwa hilo.
“Kemi nakwenda Uganda kufanya kazi
aliyonituma mzee Rutashobya, usimwambie mtu,
lakini nitarudi baada ya siku tatu,” Joru
akamwambia Kemi aliyekua amejivuta jirani
naye kabisa.
“Joru mpenzi, naamini kabisa utarudi na
utafanikisha kazi yako, sina kinyongo na safari
yako, lakini utuletee zawadi wenzako,”Kemi
alimwambia Joru.
“Usijali, baba akitoka safari ni vizuri kuleta
zawadi, name nitawaletea zawadi, zawadi ya
ushindi,” Joru akamwambia Kemi.
“Baba usiende hivi hivi, japo tupeane Baraka
maana nitakukosa kwa muda wa siku kadhaa,”
Kemi alisema huku akisimama na kukiacha
kitenge chake kikiuacha mwili nay eye kubaki
kama alivyo, akamfuata Joru pale aliposimama
alipokuwa akiweka vizuri mambo yake,
akamfungua taulo naye akabaki vilevile, wawili
hao wakaingia upya mapenzini, kitanda kikubwa
kikawapokea na blanketi pana likawasitiri.

JOSEPH RUTASHOBYA ANAKUTA BASTOLA YA
KALE IULIYOFICHWA NA MZEE WAKE, SIRI HIYO
ALIIJUA KEMI PEKEE....
RISASI NNE ZINAAMBATANA NA BASTOLA HIYO,
SASA JORU ANAPANGA SAFARI YA KWENDA
UGANDA....
NINI KITAJIRI UGANDA? USIKOSE CHAPISHO LA
13
 
CHAPISHO LA 13
8 Kulipokucha, Joru akamuacha Kemi na
mtoto akabeba kibegi chake na kutokomea
kwenye giza la nje. Alipofika eneo la sokoni,
alikuta Landrover 109 inayoelekea mpakani
katika daraja kubwa la mto Kagera, hakusita bali
alilipanda na kuanza safari yake. Mida kama ya
saa mbili asubuhi hivi, alifika mpakani, Joru
hakuwa na hati ya kusafuria lakini kwake hilo
halikuwa tatizo, aliingia kenye mgahawa na
kutafuta madereva wa malori, akampata mmoja,
Kibinda.
“Mambo vipi?” Joru alimsalimia jamaa huyo
mfupi, mnene anayeonekana kuwa na ukorofi
mwingi machoni mwake.
“Poa, vipi brotherman, mbona kifurushi?”
alimuuliza huku akiendela kunywa bia yake.
“Wewe ndio Kibinda?” Joru akauliza.
“Mi sipendi mtu anyeuliza majibu ujue, ee haya
sema ndio mimi,” Kibinda akajiubu kwa nyodo.
Mara mhudumu wa hapo akaja na chupa
nyingine kwenye chano akamletea Joru. Joru
akaitazama na kumtazama Yule binti, kisha
macho yake akayarudisha kwa Kibinda.
“Situmii kilevi,” akamwambia.
“We mwanaume gani wewe, kilevi hutumii na
huyo binti je humtumii? Chagua kimoja, hapa
kuna sheria, ukikutana na Kibinda lazima ufanye
kile anachokifanya yeye kwa wakati huo, ndiyo
mtaenda sawa, kama la, potea nisikuone,”
Kibinda aliongea kwa sauti yake ya kilevi.
Joru alimtazama kijana huyo aliyekuwa
akijimiminia bia kama baba yake ndiye
aliyetengeneza kampuni hiyo, safari .
“Kazi yangu hairuhusu mimi kutumia chochote
kati ya ulivyovitaja,” Joru akamwambia Kibinda.
“Kazi yako kazi gani? We una kazi wewe?
Lonyalonya hivi utakuwa na kazi wewe! Basi we
hunifai katika ufalme wangu, potea hapa,”
Kibinda akaongea kwa sauti ya juu na kuitisha
bia nyiongine.
“Mimi kazi yangu ni kuua! Na leo ni zamu yako,”
Joru akamwambia Kibinda.
“The the the the, wewe unaweza kuua wewe?
Nikikuletea mende hapa unaweza kuua wewe?”
Kibinda akacheka sana, hali hii ikamletea hasira
Joru, akasimama na kusogea pale alipoketi
Kibinda. Kofi moja, kofi la pili, pombe zikamtoka
Kibinda, akamkwida na kumuinua pamoja na
unene wake, Kibinda aliinuliwa juu, miguu
ikamning’inia chini.
“Sikiliza we mpumbavu!” Joru akaanza kwa
kusema, “Sasa ukitaka nisikuuwe utafanya lile
ninalotaka, maana nilitaka nitumie lugha laini
sasa wewe umenitaka nitumie lugha ya ukali,”
Joru akamaliza.
“Sawa kaka, hamna shida! Hamna Shida,”
Kibinda alijibu, watu walianza kujaa kwenye kile
kimgahawa kushuhudia kinachotokea. Joru
alimuachia ghafla na Kibinda akajibwaga chini
kama gunia la chumvi.
“Twende kwenye gari yako,” Joru alimuamuru na
Kibinda akafuata kama alivyoahidi.
International , lilikuwa ni lori kubwa lenye tela la
urefu wa futi arobaini limeegesha nje ya
mgahawa huo, Kibinda akapanda na Joru
akafuatia.
“Unaijua Uganda vizuri?” Joru akamuuliza
Kibinda.
“Ndiyo naijua sana tu kuliko unavyofikiria,”
Kibinda akajibu.
“Nataka unifikishe hapa,” Joru akamuonesha
eneo analotaka kwenda, akiwa mkononi
kakamata kipande cha karatasi chenye ramani
ya Uganda.
Kibinda badala ya kujibu akatoa macho kama
mjusi aliyebanwa na mlango. Akachukua ile
karatasi ambayo Joru alimuonesha, hakuielewa
hata ni nini kinachoonekana zaidi ya kuona
vijimistari vilivyopita huku na kule, alichokielewa
tu ni kuwa alikuwa ameshika ramani.
“Umepaona hapa?” Joru akamuonesha kwa eneo
Fulani katika ramani hiyo kwa kutumia kidole
chake.
“Nimepaona,” akajibu.
“Unapajua?”
“Ndiyo napajua,”
“Nataka nifike hapa,” Joru akasisitiza.
“Sasa kaka hapa ni mbali, na mimi siendi huku,
mi naenda Mbalala, we unataka nikupeleke Jinja
wapi na wapi?” Kibinda akalalamika.
“Nitakulipa pesa nyingi,” Joru akamwambia.
“Pesa sio tatizo kaka, hata mi nanazo, fikiria hii
gari ninayoendesha ina mtambo wa GPS popote
ninapoenda wananiona, unataka kibarua kiote
nyasi?” Kibinda akazidi kulalamika.
“Sawa nimekuelewa, we unataka kuniacha
wapi?” Joru akahoji.
“Mi ntakupeleka mpaka hapa njiapanda,
umepaona, pale we utakwenda Jinja na mi
nitakwenda Mbalala,” Kibinda akajibu huku
akiwasha gari yake tayari kuvuka daraja la mto
Kagera.
…Uganda, Joseph Rutashobya anakuja, hata
kama sikuweza kuja kupigana nawe, lakini
nakuja kumalizia kile kilichobaki…
Joru aliongea moyoni akiiambia maneno nchi
hiyo ya Uganda wakati gari ile ilipokuwa
ikilianza daraja la mto Kagera ambalo ndio
mpaka mkubwa wan chi hizi mbili zilizowahi
kuingia katika vita miaka ya nyuma lakini bado
zote zipo katika shirikisho la Jumuia ya Afrika
Mashariki.
…Maiti nyingi za wasio na hatia zilipita katika
mto huu zikipelekwa na maji pasipojulikana,
watoto wakabaki yatima, wamama wakabaki
wajane…
Joru aliangusha machozi, akayatazama maji
yaliyokuwa yakitirirka kuelekea Ziwa Victoria,
mto Kagera ukaachwa nyuma, Joru akaendelea
na safari ndani ya nchi ya Uganda akiwa na
mawazo lukuki. Kibinda aliendelea kuliendesha
lori lake lililokuwa likivuta mzigo mzito. Joru
alikuwa akiwaza mengi sana akifikiria wapi
ataanzia katika kazi yake hiyo, atajuaje mahali
alipo huyo anayemtaka, alijipa moyo, ‘nitampata
tu, kama kafa nitahani msiba,’ akajiwazia zaidi
na zaidi.
“Vipi kaka mbona huongei?” Kibinda aliuliza.
“Aaa nna mambo mengi sana kichwani,” Joru
akajibu.
“Sema bwana unaweza ukakuta mi ndo
nakusaidia kutatua shida yako, ushawahi kufika
Uganda wewe au mara ya kwanza sasa?”
Kibinda akaongea.
“Hapana sijafika kabla, ni mara ya kwanza,”
Joru akajibu.
“Sasa Jinja unaenda kufanya nini au kwa nani?”
Kibinda akauliza.
“Naenda kumtafuta kaka yangu, nasikia ni
mwnajeshi huku Uganda ila sijui yupo wapi,”
Joru akadanganya.
“Aaaa ok, pole sana, sasa huku kambi ni nyingi
lakini utampata tu, mi nina rafiki yangu
mwanajeshi hapo Kampala, lakini lazima
tutamkuta Masaka, nitakuunganisha naye kisha
yeye atakusaidia kwa mapana na marefu, kama
hutojali lakini,” Kibinda aliongea kwa sauti na
kumalizia na cheko kubwa sana kama ilivyo
kawaida yake.
“Asante ntashukuru sana nikikutana na rafiki
yako,” Joru akajibu.
“Tena pale utafurahia maisha maana kuna totoz
za ukweli kaka, kama unatumia ulevi huo
mwenyewe utanitafuta kunipa mrejesho,
wasichana wa Kiganda wako poa, si wachoyo,
hawawezi kukunyima tena wewe mgeni,
utawafaidi kikwelikweli,” Kibinda alikuwa
akiendelea kuongea huku akiwa kang’ang’ani
usukani wa lori kama mtu aendeshavyo baiskeli.
§§§§§
9 Kanali Malyamungu. Nani asiyemjua
kanali Malyamungu katika Uganda? Mwanajeshi
aliyekuwa na cheo cha chini lakini mara tu,
ghafla akapandishwa mpaka kuwa kanali wa
jeshi, cheo alichopewa Rais wa kipindi hicho,
dikteta Idd Amin na kumfanya kuwa mtu wake
wa karibu sana. Mauaji mengi ya Waganda
wenye vyeo mbalimbali wakiwemo maofisa wa
jeshi, mawaziri, mabalozi ni yeye aliyeyatekeleza
kwa amri yake, wakati mwingine kwa kutumia
ajali za kutengeneza.
Kabla ya kuwa mwanajeshi, Malyamungu
alikuwa mlinzi katika lango la kiwanda Fulani na
baadae alipojiunga na jeshi alipandishwa cheo
haraka mpaka kufikia ngazi ya Kanali. Alikuwa
ni afisa wa jeshi ambaye kila mtu alimwogopa,
kila aliyemwona alitetemeka kwa hofu,
alipendwa na Idd Amin na aliaminiwa katika
mipango mingi hasa mipango ya siri kama ule
wa kumuua askofu mkuu uliotokea miaka mingia
nyuma kwa kisingizio kuwa askofu huyo alikuwa
akihifadhi silaha nzito za kivita kwa lengo la
kuipindua serikali iliyopo madarakani, lakini
haikuwa kweli. Askofu huyo na mawaziri
wengine waliuawa kwa siku moja kwa ajali ya
kutengeneza lakini miili yao ilipofanyiwa
uchunguzi waligundulika kuwa na matundu ya
risasi. Kanali Malyamungu, aliyekuwa kiongozi
wa kikosi kinachotekeleza mauaji ya aina hiyo
aliutangazia umma asubuhi ya saa tano kuwa
imethibitika kuwa askofu huyo alikuwa na silaha
akishirikiana na Rais aliyepita, Milton Obote kutekeleza uasi dhidi ya serikali iliyopo madarakani, akaonesha na ushahidi wa silaha
mbalimbali walizozikamata, lakini ilikuwa ni
mchezo mchafu dhidi ya watu hao.Baada ya kulitumikia jeshi hilo kwa miaka mingi,
akiwa amekoswakoswa na mapigano ya vita vya
Kagera, Malyamungu alistahafu jeshi na kuamua
kurudi kwake alikozaliwa katika eneo la Mutibwa, Jinja na kuanza maisha ya kilimo na
ufugaji akiwa na mkewe na watoto wao wawili.
Hakuwa hi kufikiri hata mara moja kuwa kuna
mtu au watu watakaokuja kuulipa uovu wake,
aliamini eti uovu haulipwi. Umri ulikwenda,
alipostahafu, serikali ikampa na ulinzi wa
kumlinda. Eneo la nyumba yake lilikuwa
haliingiliki kirahisi, kamera za usalama
zilitapakaa kila kona ukiachana na mbwa na
walinzi waliopo katika eneo hilo.LORI alilopanda Joru lilifika Masaka, hapo
walikutana na barabara inayotoka Kampala
kuelekea Mbalala mpaka Rwanda. Kibinda
akaegesha lori pembenikaribu kabisa na kituo
cha mafuta cha Shell, akateremka kuliacha gari
likiunguruma.
“Oe!” akamwita Joru na kumpa ishara ya kuwa
amfuate, naye akafanya hivyo. Wakafuatana na
kuingia kwenye klabu moja ya usiku, klabu
maarufu sana eneo la Masaka. Ndani ya klabu
hiyo kulikuwa na muziki mkubwa, watu wa kila
aina, wahuni na wasio wastaarabu, Malaya na
makahaba waliovalia nguo na wengine kutembea
na chupi tu huku wakitomaswa makalio na
vijana waliokuwa humo. Joru akamfuata Kibinda
mpaka katika meza moja iliyokaliwa na watu
wane, Kibinda akaketi na Joru akafanya vivyo
hivyo.
“Jackson Mutebezi, kutana na jamaa yangu
Joru,” Kibinda aliwatambulisha wawili hao.
Wakapeana mikono, “Sasa mi si mkaaji nipo
kwenye ruti zangu za kawaida, Jackson, huyu
jamaa ana shida atakueleza mwenyewe kisha
umsaidie mi nitapita wiki ijayo, tafadhali,”
Kibinda alimaliza na tayari akawa
amekwishanyanyuka.
“Hamna tabu pal, mimi na wewe tumetoka
mbali, nitampa msaada anaoutaka,” Jackson
Mutebezi alimjibu Kibinda na kuagana.
Jackson Mutebezi alimtazama Joru juu mpaka
chini.
“Unatoka wapi?” akamwuliza.
“Tanzania, Mutukula,” Joru akajimjubu.
“Oh good, (vizuri) napafahamu sana hapo,”
Jackson akajibu.
“Umepafamuje?” Joru akauliza.
“Joru, ni stori ndefu sana yaani ndefu sana,
sitaki kuikumbuka,” Jackson akajibu.
“Napenda kuifahamu siku moja hiyo stori,” Joru
akasisitiza.
Jackson akamtazama Joru na kumkazia macho.
Joru naye akabaki kumtazama kijana huyu
aliyeonekana tayari yuko na pombe nyingi
kichwani.
“Sikia,” Joru akamwambia, “Mimi natoka wapi
na wewe unatoka wapi havina nafasi kwa sasa
cha maana ni kile kilichonileta mpaka leo niko
na wewe, najua utanisaidia,” Joru alimaliza.
Jackson Mutebezi akaingiza mkono mfukoni na
kutoa sigara yake, akaipachika kinywani na
kuibana kwa midomo yake.
“Ngoja nivute nipate akili, maana nikikutazama
naona wewe waweza kunisaidia katika mkakati
wangu Fulani,” Jackson aliyasema hayo huku
akijipapasa mifukoni kutafuta kiberiti. Joru
akalielewa hilo, akachomoa kiberiti chake cha
gesi na kukiwasha mbele ya kijana huyo, mlio
wa kiberiti uliyarejesha macho ya Jackson kwa
Joru.
“Hutakiwi kusumbuka wakati mimi nipo, vivyo
hivyo sitakiwi kusumbuka wakati wewe upo,”
Joru alimwambia Jackson, Jackson alimtazama
Joru na kuiwasha sigara yake.
“Asante rafiki, lete stori,” Jackson alimwambia
Joru.
“Umenambia unaijua Mtukula, niambie
unaijuaje?” Joru alimwuliza Jackson. Jackson
akainama kwa muda kisha akainua kichwa
chake na uso wake akamuelekezea Joru.
“Niliokota maiti ya baba yangu katika mto
Kagera na tulishindwa kuirudisha Uganda
tukaamua kumzika Mtukula,” Jackson aliongea
kwa uchungu.

JORU ANAFIKISHWA MASAKA, ANAKUTANA NA
JACK, JE ; UNAFIKIRI WATARANDANA KATIKA
TABIA?
NINI KITATOKEA JORU AKIMWABIA AZMA
YAKE?
 
willy gamba senki yu sana, kitu kitam sana hikiila naomba uimalizie na UCHU
 
CHAPISHO LA 14
“Pole sana Jack, hastahili kuishi yeyote
aliyeyafanya haya,” Joru akamsindikiza kwa
maneno.
“Any way, tuyaache hayo, una shida gani
nikusaidie kabla jua halijawia?” Jackson
akamuuliza Joru.
“Sina haja ya kujificha, nataka habari ya mtu
mmoja tu, Kanali Malyamungu, anaishi wapi au
kazikwa wapi bas! Nahitaji kumsalimu,” Joru
aliongea huku akipumua kwa nguvu. Jacskon
akamkazia macho Joru.
“Unamjua mtu huyo?” akamwuliza Joru.
“Simjui,” joru akajibu.
“Ndio maana unamtafuta, kwa sababu humjui,
yupo, yupo hai, wala hajafa, lakini si rahisi
kumuona kwa sasa, amestahafu jeshi miaka
kama saba iliyopita,” Jackson akajibu. Joru
akasikiliza kwa makini sana habari hiyo iliyotolewa kwa ufupi na kijana huyo anayeonekana tangu machoni kuwa yupoyupo
tu, kijana asiyejali, aliyechoka maisha.
“Joru, we hunijui wala mi sikujui, lakini wewe ni
kijana mwenzangu wote sisi tunasaka maisha,
achana na huyo mtu, kabla hujafika anapoishi
utakuwa marehemu tayari,” Jackson alimuonya
Joru. Joru alifikiria kwa kina shauri hilo lakini
hakuona umaana wake.
“Wacha aniue, lazima niende, nipe ramani hata
kama ni usiku huu, nina siku mbili tu ya
kukutana na mtu huyu ili nimpe kile alichokisahau Mtukula,” Joru aliongea kwa jazba
akimtazama Jackson usoni. Jackson naye
macho yake aliyakaza kwa Joru, wote
walitazamana kama majogoo yanayotaka
kupigana, kisha Jackson akanyanyuka na
kuelekea mahali Fulani akipenya penya kwenye
kundi la vijana wa kike kwa wa kiume waliokuwa
wakicheza muziki. Joru nae akasimama na
kumfuata kwa njia hiyohiyo mpaka wote
wakajikuta nje ya club hiyo, Jorru akaongeza
mwendo na kumfikia Jack, akamsimamisha na
Jack akatii.
“Sikiliza kaka, mi yatima sina baba sina mama
na huyo ninaye mtafuta ndiye aliyenifanya niwe
hivi, nikpo tayari kwa lolote, akiniwa au
nikimuwahi yote sawa,” Joru alisisitiza.
Jackson akamtazama Joru na kutikisa kichwa,
kisha akainama na kuivuta suruali yake, akaacha
mguu mmoja wazi.
“Tazama huu mguu,” akamwonesha Joru.
“Una nini? Au umekuwaje?” Joru akauliza.
“Huuoni? Sio mguu halisi ni wa bandia huu,”
Jack akamjibu huku akimuonesha ule mguu.
Joru akainama na kuupapasa na kuugongagonga, kweli ulikuwa ni mguu wa
bandia, mguu uliotengenezwa kwa plastiki ngumu.
“Haya yalinipata kwa sababu ya huyo mtu, huyo
mtu alimuua baba yangu, baba yangu alikuwa ni
mtu wa juu sana serikalini wakati wa Idd Amin
lakini alimchinja kama kuku, nilipokuwa mtu
mzima nikaamua kulipiza kisasi kama usemevyo
wewe lakini sikufika popote, nilikamata na
kuvunjwa mguu huu na kuambiwa nisirudie tena,
sasa wewe Joru unajiamini nini kupambana na
shetani Yule?” Jack akaongea kwa uchungu.
Kisha akamuwacha Joru na kuondoka akaingia
kwenye gari yake na uiwasha akaondoka
taratibu. Mwendo kama wa mita mia moja hivi
akasimamisha gari, akafungua mlango na
kutoka nje, akasimama na kumtazama Joru.
Baada ya dakika tano za kutazamana, Jack
akaiacha ile gari na kumuelekea Joru,
akasimama na kumtazama tena kana kwamba
ndiyo mara ya kwanza akimuona.
“Twende zetu, nikauoneshe unalolitaka,” Jack
akamwambia Joru, kisha wote wawili wakaingia
garini na kutokomea.
“Sasa sikiliza, huyu jamaa siku hizi ana
mtandao mkubwa sana wa ujambazi, na ndiyo
maisha anayoishi baada ya kustahafu jeshi,
lazima ujue kluwa ana masikio mengi sana, sasa
we ulitakiwa tukaongee pembeni pale
uliporopoka ndio maana nikaondoka,
wameshasikia sasa tuko matatani,” Jack
alimwambia Joru huku akikunja kona kuingia
mtaa Fulani hivi. Baada ya mwendo mfupio hivi,
Jack aliona gari nyingine ikiingia mtaa ule.
“Joru geuka nyuma!,” Jack akamwambia, Joru
akageuka na kuiona ile gari inayokuja.
“Vipi?” akauliza.
“Wanatufuata, wameshasikia tunamzungumzia
boss wao, sijui hata tufanye nini maana hapa
mni mawili lazima watuue, au watupeleke kwa
bosi wao, Malyamungu, tumekwisha,” Jack
akamwambia Joru.
“Simama unishuhe, halafu wewe kanisubiri
mbele kule,” Joru alimwambia Jack.
“Kaka hiyo troop sio ya kuichezea au kucheka
nayo, hapa cha kufanya mimi ni kufukuzana nao
mpaka niwapoteze,” Jack akamwambia Joru.
“Hapana Jack, simama mi nitawatuliza hata
kama wako hamsini,” Joru alisisitiza. Jacka
hakuwa na linguine alisimamisha gari na Joru
akasuka garini akasimama nje kwenye kagiza
hafifu kalilkokuwa kakififishwa kwa mbalamwezi
pevu. Ile gari ikaja na kusimama mita chache
kutoka aliposimama Joru, milango ikafunguliwa
na wale jamaa wakashuka, walikuwa watatu tu,
wawili wakamsogelea Joru, na mmoja akabaki
nyuma akiwa na gongo la kuchezea mcjezo wa
baseball , akilipigapiga mkononi kana kwamba
anasubiri amri tu alitumie gongo hilo. Wale
wawili waliomsogelea Joru mmoja alikuwa na
bastola na mwingine alionekana kiongozi wao
alikuwa mikono mitupu.
“We ni nani, na umekuja kufanya nini?” Yule
kiongozi aliyevalia suti nyeusi na kofia nyeusi pia
alimuuliza Joru huku akipuliza moshi wa mtemba wake.
“Huna hadhi ya kuniuliza swali la namna hiyo,unataka kunijua mimi?” joru aklamjibu na
kumuuliza.
“Inaonekana we tafu sana ee? Unadiriki kunijibu
hivyo mimi?” Yule mtu akauliza huku akimsogelea pale alipo.
“Nimezaliwa ili niwe tafu, niweze kuwajibu hivi
watu kama ninyi, vibaraka,” Joru alimjibu kwa
dharau akisindikiza na sonyo refu lisha
akageuka kama anaondoka kuelekea kwenye
gari kumbe ilikuwa ni mbinu ya kuwaweka sawa.
“Wewe! Simama kabla sijakutawanya ubongo
wako,” Yule mwenye bastola alisema kwa sauti
huku akivuta hatua kumfuata Joru na bastola
mkononi. Ilikuwa ni nafasi hiyo anayoisubiri,
Joru aligeuka kwa kasi na kuipiga teke nile
bastola, ikatoka mikononi mwa Yule mtu, kisha
mguu wa pili ukatua shavuni mwa Yule jamaa
aliyekuwa na bastola akayumba na kwenda chini
moja kwa moja. Kwa harakaharaka Joru
alimuona Yule mwenye gongo akaija kasi na
gongo lake juu, akampiga teke moja la mbavu
Yule kiongozi wao mpaka akatema mtemba
wake na kugeuka kwa Joru ndipo Joru
alipomkamata suti yake na kumgeuza haraka
upande wa pili na kumfaya ngao dhidi ya lile
gongo lililokuwa linashuka kichwani mwake.
Paaaaa! Gongo likatua kwenye paji la uso la Yule
kiongozi na kumpasua vibaya fuvu la kichwa
chake. Joru akamsukuma Yule kiongozi ambaye
sasa alikuwa ni marahemu akambwaga chini
kwa mbele, akaruka sarakasi na kuokota
bastola, alipokaa sawa tu tayari alishafyatu na
kufumua kifua cha Yule aliyekuwa na gongo,
akapaishwa juu na gongo likichomoka mikononi
mwake, akajibwaga kwenye boneti ya gari, hana
uhai. Joru alimtazama Yule mmoja aliyebaki
pale chini.
“Nenda kamwambie bosi wako, nipo, nimekuja,
akikuuliza nani, mwambie Israel mtoa roho
katumwa na roho zote alizozitoa kwamba sasa
zamu yake imefika,” Joru akafyatua risasi moja
na kumvunja mkono Yule aliyebaki kisha
akaisweka ile bastola kiunoni mwake na kuingia
kwenye gari ya Jack.
“Dah, kaka Joru, uko poa yaani upo kama Van
Damme, vipi wamekwisha?” Jack akauliza.
“Wamekwisha wawili ila mmoja nimemuacha
apelike ujumbe kwa bosi wake,” Joru akajibu
huku akijiweka vizuri kitini na Jack akiondoa lile
gari kutoka eneo lile.
§§§§§

Haikuchukua muda taarifa zilifika kwa mhusika,
mtu wa mawasiliano ambaye ni yeye tu mwenye
uwezo wa kuonana na Malyamungu,
akastaajabu sana kwa ushupavu wa huyo mtu
aliyeweza kukisambaratisha kikosi hicho, kikosi
tata. Akajishauri jinsi ya kumwambia bosi wake
habarti hiyo mbaya, lakini aliposhauriana na
vijana wake wengine juu ya hilo, walimshauri
asimweleze, ila wafanye juu chini kumpata huyo
kiumbe haraka iwezekanavyo. Uamuazi
ukapitishwa na vijana wakaanza msako wa
kumsaka Joru kwa hali na mali, wakihakikisha
Joru haingii katika mji wa Jinja, wakati huo
wengine wakipangwa kuhakikisha anakamatika
hukohuko Masaka alikofanya unyama huo.
Ilikuwa kazi, kazi ngumu.
Mtoto wa kwanza wa Malyamungu ndiye
aliyeipata habari hiyo kuwa kikosi chake, kikosi
tata kimesambaratishwa na kijana huyo huko
Masaka kikiwa katika moja ya majukumu yake
ya kila mara.
Kalosi Malyamungu alihisi kuchanganyikiwa,
hakuwahi kusikia vijana wa baba yake
wakishindwa kirahisi namna hiyo, kila alipokaa
alikuwa akiwaza jinsi ya kuongeza nguvu katika
kumdhibiti mtu huyo ambaye bado alikuwa
hajamjua uwezo na nini hasa anachokitaka.
Wakati Kalosi akisumbuka kichwa kwa hilo
akiwapanga vijana wake kule Masaka, Joru na
Jack walikuwa njiani kuelekea Kampala,
wakisogea kabisa na mji wa Jinja ambako
Malyamungu ndipo alikuwa ameweka makao
yake, serikali ikimpa ulinzi lakini haikujua nini
kinafanyika chini ya zuria, Malyamungu alikuwa
na kikosi cha vijana wa kulinda karibu sehemu
mbalimbali za Uganda na hii ni kwa sababu
alijua wazi kuwa ana maadui wengi aliowajenga
wakati wa utawala wa nduli Idd Amin, hivyo
kuona mtu anataka kulipa kisasi kwa jinsi yoyote
kwake halikuwa jambo la kushangaza. Silaha
alizokuwa akiziiba wakati akiwa mwanajeshi
huko nyuma zilimtosha kujiwekea ulinzi wake
mwenyewe dhidi ya ule wa serikali wa askari
mmoja getini. Aliishi maisha ya kuwa ndani tu,
ni mara chache sana alitoka nje, kila kitu
alikipata akiwa ndani, alihakikisha dunia yote
anayo katika sebule yake na kujua kila
kinachojiri nje kuliko wewe uliye nje.
§§§§§
KAMPALA

SAA kumi na moja alfajiri, Joru na Jack waliingia
Kampala, mji mkuu wa Uganda, si mbali sana na
Jinja. Joru na jack walifikia katika nyumba ya
akina Jack kwa mapumziko mafupi kabla ya
kutimiza azma yao kwa Yule wanayemhitaji, wao
waliona kuwa hapo ni mahali salama na
panapowafaa sana kwa shughuli yao hiyo.
Joru na Jack walijipumzisha vya kutosha,
mchana wa saa saba wote wawili pamoja
walikuwa mezani kwa chakula, wakibadilishana
hili na lile.
“Sasa Joru, we umejipangaje katika kautimiza
hili ulilonambia?” Jack aliuliza wakiwa
chakulani.
“Nimejipanga vya kutosha, nimechukua miaka
ishirini kujiandaa kwa ajili ya hili na lazima
nilitimize leo hii usiku,” Joru akajibu.
“Sikia Joru,” Jack akamwambia.
“Unasemaje?” Joru akamuuliza na kuacha kula
akimsikiliza kijana huyo.
“Malyamungu, ni mtu anayeogopwa sana tangu
enzi zile mpaka sasa ijpaokuwa umri
umemuacha, na kwa sababu anajua hilo,
amejipanga sana, kuivamia ngome yake inahitaji
askari au watu wenye ujuzi mkubwa sana na mb
inu za kutosha za uvamizi,” Jack alimwambia
Joru.
“Niko tayari nina uwezo wa kuingia katika hiyo
ngome kwa jinsi ambayo wewe mwenyewe
hautodhani, na ni lazima nimmalize Malyamungu
kwa mkono wangu, nitahakikisha na nina uwezo
wa kuwadhibiti wale wote watakaokuwa
wamemzunguka,” Joru alijigamba.
Jack aliinama chini kwa muda, kisha akainua
uso wake na kumtazama Joru kwa macho
makali.
“Napenda unavyojiamini, kubali kuniahidi kitu
kimoja tu,” Jack akasema.
“Niambie na nitakuahidi,” Joru alimwambia
Jack.
“Mimi ni mwanajeshi katika jeshi la Uganda,
nilijaribu kulipiza kisasi kwa mtu huyu dhidi ya
mauaji ya baba yangu ambaye alikuwa na cheo
cha juu sana serikalini, lakini nilikamatwa, mtoto
wake mkubwa, Kalosi, alinipiga risasi ya goti
ambayo ilipelekea mimi kukatwa mguu, kwa
huruma na hisani ya Rais Museveni, nikaachwa
jeshini nikitumia mguu wa bandia kitu ambacho
si rahisi popote pale duniani, lakini najua kwa
kuwa mimi nimesomea zaidi maswali ya ICT,”
akasita kidogo, akakohoa na kuendelea, “naomba
unilipizie kisasi kwa Kalosi pia, lakini nina
wasiwasi, umejiandaaje, nikimaanisha silaha?”
Jack akamuuliza Joru.
Joru akasogeza kibegi chake kidogo na kupekua
ndani yake kisha akatoa bastola ya kizamani,
ambayo ilikuwa iking’azwa sana na mwanga wa
jua lililokuwa likipenya kupitia dirisha lililokuwa
katika chumba hicho cha kulia chakula.
“Ha! Joru, hiki nini?” Jack aliuliza kwa
mshangao.
“Wesson and Smith, bastola ambayo baba
yangu aliipata vitani mwaka 1944, baba yangu
kapigana vita ya pili ya dunia, bastola hii na
risasi nne, (akazitoa zile risasi na kuziweka
mezani) hizi ndizo za kulipia kisasi, lazima
zitafune kichwa cha Malyamungu,” Joru
akamaliza kuongea na kuinua kikombe cha
kahawa na kukiweka kinywani kabla ya kuvuta
kwa hisia kahawa hiyo.
“Joru, usifanye mchezo na kazi inayokukabili,
kwa risasi hizi nne utamuua nani umwache
nani?” Jack akauliza tena.
“Jack, sihitaji kuua mtu zaidi ya Malyamungu na
sasa wewe umeniongezea mwingine, kuua watu
wawili kwa risasi nne kwangu mimi sio shida,
nitatumia risasi mbili na mbili zitabaki,” Joru
aliongea kwa kujiamini.
“Inabidi uwe na shabaha ya kutosha,” Jack
alimwambia Joru.
“Sio shabaha ya kutosha tu, ila nina shabaha ya
ajabu,” Joru aliongeza huku kikombe cha
kahawa bado kikiwa mkononi mwake, bado
hakijashuka chini. Jack alinyanyuka kutoka
katika kiti chake akavuta hatua chache mpaka
katika kabati kubwa akatoa bastola moja ya
kisasa na kuja nayo mpaka mezani, akaiweka
mbele ya Joru na kikasha cha risasi.
“Nataka kuona shabaha yako ya ajabu,” Jack
akamwambia Joru. Joru akaitazama ile bastola
na kuinyanyua kwa mkono wake wa kulia mara
tu baada ya kukiweka kikombe cha kahawa
mezani, akavuta kile kikasha cha risasi
akazipakua na kupakia risasi kumi ndani ya ile
bastola, akavuta kiwambo cha sauti na
kukifunga mbele ya mtutu wa bastola hiyo.
Akainua macho na kutazama dirishani, dirisha la
vioo, vioo ishirini na nane vilivyokuwa
vimepangwa kwa ustadi, vilikuwa wazi vikiwa
vimefunguliwa, kati ya kioo na kioo kulikuwa na
uwazi wa sentimita zipatazo ishirini. Nje ya
nyumba kulikuwa na mti mkubwa juu yake
kulitua kungulu mmoja aliyekuwa akipiga kelele,
Joru akaiweka vizuri ile bastola na kuinyanyua
sekunde moja ilitosha kumlenga na kumfumua
Yule kungulu.
“Shiiiit, Impossible!!!” (haiwezekani!) Jack
alishangaa kwa maana hakujua kama tayari
Joru alikuwa akilenga kitu Fulani, hakuna kioo
kilichovunjika lakini alishuhudia manyonya ya
kungulu pale kwenye mti yakipukutika kwa fujo.

JORU NA JACK WANAUNGANISHA NGUVU,
WANAINGIA KAMPALA, VIBARAKA WA
MALYAMUNGU WANAFUATILIA NYENDO ZAO...
MISHENI ITAFANIKIWA?
 
CHAPISHO LA 15
“Shiiiit, Impossible!!!” (haiwezekani!) Jack
alishangaa kwa maana hakujua kama tayari
Joru alikuwa akilenga kitu Fulani, hakuna kioo
kilichovunjika lakini alishuhudia manyonya ya
kungulu pale kwenye mti yakipukutika kwa fujo.
“Naitwa Joseph Rutashobya, the point man ,”
Joru akajigamba. Jack alitikisa kichwa,
akacheka kidogo na kugonganisha viganja vyake.
“Basi sina shaka na wewe! Naamini unaweza
kumlenga Malyamungu hata kutokea nje ya wigo
wake, ijapokuwa tu umekiona kidole cha mguu
wake,” Jack akasema na wawili hao wakacheka sana.
§§§§§

“Mtoto wa Mutebezi ndiye aliyemkaribisha kijana
huyo,” mtu mmoja alikuwa akimwambia kibaraka
wa Malyamungu, ambaye mara tu alipopata
taarifa hiyo alipiga simu kwa Kalosi kule Jinja.
Kalosi akatoa amri ya Jack Mutebezi
kukamatwa ikiwezekana kuuawa pamoja na
mgeni wake.
Franko Besije, akatazama watu wake wapatao
kumi aliofuatana nao kutoka Jinja kuja Masaka.
“Inabidi twende Kampala, tukamuue Jack na
mgeni wake, kazi inatakiwa ifanywe kwa ustadi
wa hali ya juu sana, inasemekana Yule kijana ni
hatari sana, kwa vyovyote Jack atakuwa
kamkodi kwa ajili ya kisasi, bila kuchelewa,
tayari kule kuna mtu anayewafuatilia nyendo zao
na kila nukta ananipa taarifa, anasema bado
wapo ndani ya nyumba mzee Mutebezi
hawajatoka, sasa tusipoteze muda twendeni,”
Franko aliwaambia wenzake, wote wakatoka na
kuingia kwenye gari zao kisha kuondoka kwa
kasi kutoka Masaka kuelekea Kampala.
§§§§§

Joru na Jack walitoka nje pamoja, wakaingia
kwenye gari yao na kufunga milango, mbele yao
kulikuwa na maduka mengi ya vitu mbalimbali.
Jack alikuwa nyuma ya usukani, akatazama
huku na huku na kisha taratibu akaitoa ile gari
na kuiingiza barabarani. Safari ilikuwa ni kwenye
nyumba ya Jack, nyumba iliyo mafichoni zaidi,
kwani Jack alijenga mashambani. Ulikuwa ni
mwendo mrefu kidogo barabara ya kuelekea
Jinja. Jack kwa kuwa alikuwa mzoefu wa
barabara hizo za Kampala alikuwa akipita
vichochoroni.
“Vipi, mbona unapita kwenye hizi njia mbovu,
utaua gari yako,” Joru alimwambia Jack.
“Kumbuka nilikwambia Malyamungu ana macho
na masikio mengi, si ajabu hapa tunafuatailiwa,”
Jack alisema.
“Sio si ajabu, tazama kwenye kioo chako cha
ndani, kuna gari nyeusi inakuja nyuma na
nimeiona muda mrefu sana kila tunapokunja
nayo inakunja papo hapo,” Joru akamwambia
Jack. Jack akaendesha gari mpaka kwenye bar
moja kubwa ya wazi, akaegesha hapo nje.
“Chukua hii,” Jack akampa bastola Joru nay eye
akachukua nyingine, “Tuketi hapa kama dakika
kumi tumsome huyo mshenzi,” Jack alimwambia
Joru na Joru akahafiki, wakateremka na
kufunga milango bila kuweka lock wakaingia
kwenye wigo wa bar hiyo na kuchagua viti vya
pembeni, wakaketi. Wakaiona ile gari ikipunguza
mwendo na kupita kidogo ile bar, Joru akaikazia
macho kuona itasimama wapi, lakini
hakufanikiwa. Ilipita dakika mbili, watu wawili
waliovalia miwani nyeusi waliingia kwenye bar
hiyo wakaketi karibu na mlango wa kuingilia.
Jack na Joru wakawa wakiwatazama kwa chati
wakijifanya hawana muda nao, wakiongea
mambo yao. Mmoja wa watu wale alikuwa
akaiandika ujumbe wa simu mara kwa mara.
“Kaa mkao wa kula,” Jack alimwambia Joru.
“Kwa nini?” Joru aliuliza.
“Hawa maza faka nitawaanzishia msinambe
sasa hivi,” Jack akamwambia Joru kwa
kumnong’oneza.
“Tufanye hivi, tuwaache kwa vyovyote watakuwa
wanawapa taarifa wenzao, sasa unaonaje
wakijikusanya ili tukiwaanzishia tunapukutisha
wengi, unasemaje?” Joru alitoa pendekezo
lingine. Jack alitulia kimya kwa sekunde kadhaa
kisha akatikisa kichwa kuashiria kuwa
amekubaliana na Joru. Wakaagiza vinywaji na
vilaji wakawa wakinywa taratibu huku
wakiendelea kuwatazama wale watu kwa makini,
wakihakikisha hawawapotezi.
§§§§§

Franko na kundi lake walikuwa wakikaribia
Kampala walipopata taarifa kuwa Jack na mgeni
wake wapo katika The Great Nile Bar iliyopo
katika viunga vya mji wa Kampala. Franko
akawasisitizia kuhakikisha Jack na mgeni wake
hawaondoki katika eneo hilo, na kama
wakiondoka basi waendelee kufuatiliwa ili
wanalizwe kabla hawajaleta madhara zaidi.
Wale jamaa wakaendelea kunywa wakiwalinda
Jack na Joru, wao kwa mawazo yao ni kwamba
Jack na Joru hawajui lolote juu yao, kumbe
hawakujua kama wanacheza na mwanajeshi wa
Tanzania aliyekomaa katika medani za vita
ijapokuwa hakuwahi kupigana vita ila hiyo
ilitakiwa iwe ya kwanza, labda mwenyewe aliita
‘Kagera War II’ .
Saa kadhaa zikapita na ile bar bikazidi
kuchangamka, watu walijaa na kujaa, madada
wa kujiuza nao walikuwa wakiingia na vinguo
vya ajabu ajabu, jua lilikuwa likituwa upande wa
magaharibi na kufanya dhambi za Kampala
kuchukua nafasi yake.
“Joru, twende turudi, wewe ni sawa na kaka
yangu au niseme ndugu yangu,” Jacj alianzisha
mazungumzo.
“Kwa nini Jack?” Joru akauliza.
“Baba yangu mzee Mutebezi asili yake kabisa ni
Kagera, Tanzania, alikuja huku miaka mingi sana
wakati wa Obote, si unajua tena Wahaya na
Waganda hatuna tofauti sana, na mwenyewe
aliwahi kunambia kuwa kwao ni Mutukula” Jack
alieleza.
“Oh, Mutukula, home sweet home ,” Joru
alimalizia kwa kusema hayo, “Idd Amin alituma
watu wake wakiongozwa na Malyamungu
wakaua na kuchoma kijiji chetu chote hata sasa
hakuna kijiji bali ni mapori na vichaka,
Malyamungu alimuuwa mama yangu na baba
yangu kwa bunduki aina ya Riffle, nakumbuka
nilikuwa nimejificha kwenye vichaka na kisha
hapo nilikimbia msituni,” akamalizia na machozi
yakamtoka na kuyapamba mashavu yake, “Leo,
jack Leo jua halitakuchwa bila kuishika roho ya
Malyamungu mkononi mwangu,” akamaliza.
“Joru, niliokota maiti ya baba yangu katika mto
Kagera nikisaidiwa na wasamalia wema
wachache, sikupenda kuitazama sana kwa
sababu aliuawa kinyama sana, mkono wa
Malyamungu ulifanya kazi hiyo akishirikiana na
vibaraka wake, sote tunania mamoja, sote tuna
kitu kimoja, sote tuna roho moja, sote tuna lugha
moja,” Jack alimaliza kuongea na kugonga mikono yao.
Joru aliziona gari mbili, land cruiser zikifika eneo
lile, moja ilisimama upande wa kulia wa bar na
nyingine ilipitiliza mpaka upande wa pili wa bar
ile. Baada ya zote kusimama, watu kama kumi
hivi waliteremka, kuna wale waliobaki nje na
wengine wakaingia ndani na kuchukua nafasi
sehemu mbalimbali na kuketi kisha wakaagiza
vinywaji.
“Kagera War II has to began,” (vita ya pili ya
Kagera itaanza punde) alisema Jack huku
akimtazama Joru. Joru akambania jicho moja
kaushiria kuwa amemuelewa kwa lile alilosema.
Dakika mbili zilikuwa nyingi sana, Joru na Jack
wakagundua kuwa wamezingirwa pande zote na
hao adui zao, Joru aliwatazama mmoja mmoja
kisha akarudisha macho yake mezani.
“Bila shaka kikosi chote cha Malyamungu ndiyo
hichi!” Joru alisema.
“Kwa ninavyoelewa mimi hawa wako kama kumi
kuna wachache sana kule nyumbani,” Jack
akamwambia Joru.
“Safi, sasa hawa tunawafanyia hapa na
kuwapunguza kadiri ya uwezo kisha
tunaunganisha mpaka Jinja leo hii, lazima kazi
imalizike na mi kesho nirudi Mutukula kabla
hawajanikamata kwa maana nimevunja sheri ya
kutoka nchini bila ruhusa ya mkuu wangu,” Joru.
“Haina shaka mkuu,” Jack akaitikia na
kunyanyuka kuelekea chooni, hiyo ilikuwa ni
mbinu mojawapo ya kuanzisha mashambulizi
katika eneo hilo, Joru alitazama vizuri na
kujaribu kuona kama atalazimika kutumia silaha
basi asiwazuru raia wengine, lakini alipenda
atumie mikono yake zaidi.
Baada ya Jack kutoka kwenda chooni, wawili wa
wale jamaa nao walinyanyuka kuelekea upande
ule, Joru alikuwa akiwaangalia jinsi wanavyojipanga na kunong’onezana hili na lile.
Mmoja wao akaingia chooni na mwingine
akasubiri mlangoni.
Jack akiwa anajisaidia alihisi kushikwa bega,
akageuka akakutana na mmoja wa wale vijana.
“We vipi mbona? Mbona unakatisha watu
starehe zao?” Jack akauliza.
“Starehe?! Starehe we unaijua?” Yule kijana
akauliza tena kwa kejeli. Jack akageuka ghafla
na kiwiko cha mkono wake kikatua katika tumbo
la Yule jamaa.
“Aaaaaaaaiighhh!” akatoa yowe hafifu la
uchungu huku akiwa kajishika tumbo na
kujiinamia, Jack hakupoteza muda alimpiga
kifuti kwa ule mguu wake mzima katika paji la
uso na yule jamaa akahamisha mikono kutoka
tumboni na kushika paji lake. Hakujibu
shambulizi lolote, alikubali kufa kikondoo,
aliposimama akakutana na uso mbaya wa Jack
uliojikunja ndita za kutisha.
“Kwa nini mnanifatafata sana hayawani nyie?
Leo nakumaliza bila wenzako kujua ----
mkubwa,” Jack alikoroma kwa sauti nzito huku
jamaa akibaki kato macho, Yule jamaa aliingiza
mkono nwenye kiuno cha suruali yake kwa
haraka lakini Jack akamuahi, alimpiga kichwa
kimoja maridadi, jamaa akayumba na kujibamiza
ukutani, kabla hajajipanga na bastola yake
mkononi, Jack aliruka na kuipiga teke ile
bastola, ikamtoka mkononi na kuanguka
pembeni. Yule jamaa kajirusha mzimamzima
kuiwahi, lo, alikutana uso kwa uso na teke kali la
mguu wa bandia likampasua katika paji la uso,
kisha Jack akamkamata ukosi wa shati lake na
kumnyanyua, hakuongea lolote, almtumbukiza
kichwa katika singi la kunawia mikono na
kulijaza maji. Yule jamaa alihangaika ili ajinasue
lakini wapi. Akiwa katika purukushani hizo. Yule
wanje alishangaa mwenzake anachelewa kurudi,
tayari ilikuwa dakika tatu zimepita, akaamua
kuingia chooni akipishana na watu wachache
wanaoingia vyoo vingine bila kujua nini
kinaendelea kwenye choio cha VIP, mlango
ulibamizwa na Yule kijana wa pilia akaingia na
kukuta jamaa yake tayari akiwa hana uwezo wa
lolote. Akiwa katika kutahamaki tayari Jack
alitoa bastola yake kwa haraka na kuifyatua
moja kwa moja katika moyo wa kijana Yule,
akapaishwa na kubamizwa ukutani kisha akatua
chini kama gunia.
“Wasalimie kuzimu,” Jack akajisemea kwa sauti
ya chini, kisha akajiweka sawa na kutoka ndani
ya choo kile.
Joru alishangaa Jack anachelewa kutoka, akajua
kwa vyovyote watakuwa wamembananisha,
alitamani anyanyuke amfuate lakini mpango
haukua hivyo. Lakini aliona hakuna jinsi ni bora
anyanyuke akamsaidie mwenzake. Alipoinuka tu
watu wawili waliokaa nyuma yake wakamdaka
na kumshika kutoka nae nje. Bila fujo Joru
alitulia na kukubali kuswagwa nje kama
ng’ombe aendaye machinjioni.
“Umekamatika leo!” Franko alimwambia Joru
pindi alipofikishwa mbele yake, “Mpakieni
kwenye gari tukamuue mbele,” akaongezea kisha
yeye akageuka na kutangulia garini. Joru
aliongozwa akiwa ameshikwa huku na huku
kuelekea kwenye gari. Kama kuna kitu alikuwa
anakisubiria basi ilikuwa ni hicho cha kulikaribia
gari, akiwa ameshikwa na vijana wawili
wakakamavu, nyuma tena kulikua na wengine
wawili wenye silaha za moto ndani ya makoti
yao wakati wengine bado walikuwa wakiendelea
kuangalia hili na lile kama kuna shida yoyote
itakayojitokeza. Joru kwa kutumia miguu yake
miwili aliikanyaga bodi ya gari na kutembeza
miguu yake kama mtu anayepanda juu kisha
akaruka sarakasi kwa mtindo wa back wale
waliomshika wakajikuta akiatoka mikononi,
wakamuona akipita juu ya o na kutua nyuma
kabisa ya wote wanne.
Mmoja wa nyuma mwenye silaha aligeuka
haraka lakini si matarajio yake alikutana na
konde moja zito la kulia kutoka kwa Joru, bila
kupinga akaenda chini mchangani, Yule
mwingine alikuwa akijiandaa kutoa bunduki
yake, ‘too late’ Joru alimsukuma kwa kanyagio
la mguu wake tuymboni akarudi nyuma kama
mita moja kisha teke kali lilimtoka Joru na kutua
shavuni kwa Yule jamaa naye bila kipingamizi
alitua chini.
Sasa wale vijana walikuwa kama mbogo
aliyejeruhiwa. Joru alijirusha juu na kuichanua
miguu yake yote miwili, mateke hayo yaliwapata
sawia waliokuja kusaidia, Joru akajidondosha
chini na mara juu yake akaanguka mtu mfu
aliyekuwa akivujwa damu kichwani, alipopepesa
macho haraka alimuona Jack akiwa na bastola
mkononi. Joru akabingirika na kupita uvungu wa
gari, lakini alipoibuka upande wa pili, guu la
Franko lilimkanyaga tumboni kwa nguvu.
“Mende wewe unajifanya unajua kupigana sio?
Haya pigana na mimi marehemu niliyeshindikana
kuzimu mpaka shetani akanirudisha duniani,”
Franko alimwambia Joru aliyekuwa kabana
meno kwa maumivu.
“Wapiganaji huwa hatuna maneno mengi,” Joru
akamwambia Franko na muda huo huo, Joru
akajizungusha kiufundi na kuchomoka katika
mguu wa Franko, kisha akiwa bdo yuko chini
hajajiinuwa alipiga teke moja kali lililotua
kwenye visigino vya Franko, ilikuwa ni ngwala
moja maridadi ambayo Joru tangu aanze
mafunzo yake hakuwa kuitumia. Franko
alinyanyuliwa mzimamzima kwa nguvu ya
ngwala ile kabla hajafika chini Joru aliinuka
haraka na kumdaka kisha akamshusha kwa
nguvu katika goti lake na kuuvunja uti wa
mgongo wa Franko. Bado jamaa waliobaki
walikuwa wakimuandama Joru.
Joru akatazama huku na huko kulikuwa na
kijana mwingine aliyekuwa akija kwa kasi, kwa
nguvu zake zote Joru aliinuka na Franko
mikononi mwake na kumrusha kwa Yule jamaa
lakini jamaa alikuwa makini sana akaukwepa
mwili wa Franko kwa kuruka sama soti safi kwa
maana alikuwa akijua mbinu ya Joru, lakini Joru
alishangaa kumuona jamaa akitua chini akiwa
mfu damu zikichurizika katika kisogo chake.
“Brotherrrrrr!!!!!” ilikuwa sauti ya Jack ikimwita
Joru, Joru alipogeuka aliona Jack akiwa kwenye
wakati mgumu, sasa muda wa mikono haukuwa
na nafasi, aliichomoa bastola aliyopewa na Jack,
kwa kupitia uvungu wa gari, alifyatu risasi tatu
zilizowatosha vijana haoa na kuwasambaratisha
chini, Jack akachomoka akiwa anachechemea,
watu walijaa eneo lile kuangalia mapambano
hayo, ving’ora vya polisi vilisikika baada ya
kupata taarifa ya uhalifu kutoka kwa meneja wa
bar ile. Joru alimsaidia Jack na kumpakia
kwenye gari la wale jamaa, kumbe dereva muda
wote kajificha ndani hakutoka, Joru alipotaka
kuingia kwenye usukani akamkuta dereva huyo
kajikunyata kimya.
“Endesha gari mpaka kwa Malyamungu,” Joru
alimwamuru kisha akaingia upande wa pili,
“Endesha haraka,” Joru aling’aka huku akimpa
mbata moja kali iliyomfanya Yule dereva
kujigonga katika usukani na gari ikapiga honi.
Dreva akaiondoa ile cruiser kwa kasi kutoka
eneo la ile bar kuingia barabara ya vumbi
iliyowatolea Barbara kuu kisha wakaambaa zao
na barabara ielekeayo Jinja.
“Ongeza mwendo!!!!” Joru alimkaripia Yule kijana
naye akaongeza mwendo kuelekea huko
wanakotaka watekaji wake.
“Pole Jack, nilijua wamekuweza wale, maana
nilipoinuka tu wakanibana,” Jiru alimwambia Jack.
“Hapana, niliwadhibiti wote wawili, wale mende
tu, mtu niyemhofia ni Franko pekee kwani Yule
jamaa mtata katika mapigano lakini nimeshangaa umemmaliza kama unavunja
chawa,”
“Nililijua hilo ndo maana nikatumia ujanja
kummaliza,” Joru alijibu.
§§§§§

Kalosi alikuwa katulia juu ya kiti chake cha
magurudumu ndani ya ofisi nyeti ya baba yake,
aliitazama saa ya ukutani ilimwambia inakaribia
saa mbili kamili, akawasha televisheni UBC ili
kupata habari za siku hiyo, lakini kabla hajaanza
hata kuangali, simu ya mezani iliita, ilimtaka
akajumuike na wenzake wa familia kwa chakula
cha jioni.
Dakika kumi baadae katika nyumba ya
Malyamungu ambayo ilikuwa na ulinzi mkali na
ilifungwa kamera za usalama zilizoweza kuona
kila kitokacho na kuingia, Kalosi alikjiunga na
wenzake, wakaketi mezani na mhudumu wa
nyumba alikuwa akiwahudumia kwa vyakula na
mapochopocho mbalimbali. Meza ilikuwa na
watu wane, Malyamungu, mkewe na vijana wao
wawili, Kalosi na Mark.
Kalosi na Mark walikuwa najeshi tangu mwanzo,
ila Kalosi aliamua kuacha baada ya baba yake
kumdokeza lile analotaka kufanya, lakini Mark
yeye alibaki jeshini akilitumikia taifa. Siku hiyo
wote walikuwa nyumbani mezani wakisehereheke
siku kumbukumbu ya siku ya ndoa ya baba na
mama yao. Ilikuwa ni furaha kwa wane hao,
vinywaji na nyama za kila aina zilikuwa zikiishia
katika matumbo yao. Kupitia kamera za
usalama waliona ile Cruiser ikiingia getini.
“Mbona iko moja?” Mark aliuliza.
“Ngoja tusubiri ripoti, kalosi alijibu na wote
wakaendelea kuburudika,”
Gari iliyowabeba Jack na Joru ilifika getini, Yule
askari bila kuangalia akafungua geti na ile gari
ikaingia ndani bila tabu, ikajivuta polepole
kuelekea eneo la maegesho.
“Simama hapa!” Joru aliamuru, ile gari ikasimama. Joru akatazama huku na kule.
“Nyumba ya Malyamungu ipo wapi kati ya hizi?”
Joru akauliza.
“Inayowaka taa ndani,” akajibu Yule dereva. Joru
akateremka na kumwamuru Jack aende na
dereva Yule mpaka maegeshoni. Ikawa hivyo,
Joru akapita kwa kuinama kufuata seng’enge
iliyofunikwa vizuri kwa maua ya bugamvili akiwa
kainama na bastola yake ileile ailiyopewa na
Jack ikiwa mkononi.
Mbwa wakaanza kubweka baada ya kupata
harufu ngeni katika eneo lao. Joru hakupenda
kelele za mbwa hao kwani alitaka kuingia kimya
kimya katika nyumba hiyo, aliangalia kule sauti
ya mbwa inakotokea na kuwaona mbwa wawili
wakubwa wakija upande wake bila kuchelewa
wala hakuwapa muda wa kumfikia risasi mbili
kila mmoja ya kwake zilifanikisha kuwazima bila
kelele, wakajibwaga katika nyasi na kupumzika
kwa amani.
Joru aliendelea kutembea taratibu kwa hadhari
kubwa akitazama huku na kule.
‘…Damu ya Rutashobya haiwezi kupotea
hivihivi…’
Sauti ya baba yake ilianza kumrudia kichwani
mwake nakumfanya Joru kushikwa na hasira
zilizojaa gadhabu, akaongeza kasi ya miguu
yake kuielekea nyumba ile akihakikisha kuwa
hakuna anayemwona.
‘…Aaaaaaaaiiiiggghhhh, kimbia Joseph kimbia…’

JORU NA JACK WANAPAMBANA NA
KUWASHINDA MAADUI WAO, SASA WANAIKABILI
NGOME YA MALYAMUNGU, NINI KITAJIRI...
USIKOSE CHAPISHO LIJALO UJUE MBIVU NA
MBICHI
 
CHAPISHO LA MWISHO
10 JACK MUTEBEZI akiwa bado
kamuwekea bastola Yule dereva alimuamuru
kuegesha gari mahali pa kila siku anapoegesha.
Hii ilikuwa ni kutaka kutowashtua wale walio
ndani ya eneo hilo, kuanzia na walinzi mpaka
malyamungu mwenyewe. Yule dereva akaegesha
gari mahali pake na kutulia palepale kwenye
usukani, Jack alizungusha macho yake huku na
kule akatzama mazingira hayo yaliyokuwa
yakimulikwa na taa zenye mwanga mithili ya
mbalamwezi. Hakumuona Joru, lakini aliamini
kijana huyo hawezi fanya makosa, Jack
hakuweza kushuka na kufanya lolote kutokana
na maumivu aliyokuwa akiyasikia katika mguu
wake ambao ameuunganisha na ule wa bandia
kutokana na mikikimikiki aliyokumbana nayo
siku hiyo. Alitulia katika siti ya nyuma akijaribu
kufanya kitu ambacho ama kitakuwa msaada
kwa Joru au kitasogeza mbele azma yao. Jack
akageuka kwa dereva na kumkuta akiwa
kakodoa macho yake mbele ya usukani.
“Zaidi ya walinzi, kitu gani hapa kinasaidia
ulinzi?” Jack akmuuliza Yule dereva.
“Aaah mbwa na kamera za usalama,” akajibu
kwa kitetemeshi.
“Wapi ambapo kamera hizi zinongozwa?”
akahoji.
“Kuna sehemu mbili, moja ni nyumba kubwa na
nyingine ni kibanda kile kule,” akajibu na
kuoneshea mkono katika kibanda kilichopo
umbali kama wa mita mia na hamsini hivi. Jack
akaona hapo patakuwa pagumu kwa Joru
kuifikia nyumba ile kama kamera hizo
zitaendelea kufanya kazi. Akamwamuru Yule
dereva ampeleke mpaka kwenye kile kibanda.
“Kwa muda huu ni hatari kaka, watatuona tu
halafu hawatatuacha hai,” Yule dereva akasema.
“Kwa hiyo we unaogopa kufa?” Jack
akamuuliza.
“Ha! Kuna mtu asiyeogopa kufa?” Yule dereva
akauliza.
Jack akamuamuru kuteremka na kumtaka
amuongoze mpaka kwenye kile kibanda,
akimuoneshea bastola Yule dereva akateremka
nje ya ile gari huku mikono yake ikiwa kichwani
na kuongoza njia, Jack alikuwa nyuma yake
akiwa na bastola yenye kiwambo cha sauti,
walijaribu kupita kwa kujificha ili kamera isiweze
kupata picha yao. Mahala Fulani hawakuwa na
ujanja, kwani juu ya ule mlango wa kile kibanda
kulikuwa na kamera inayaotazama mbele na
hakukuwa na njia nyingine isipokuwa hiyo tu.
Jack alipoinua macho akakutana uso kwa uso
na kamera hiyo.
“Shabash!” akajikuta akitamka neno hilo kwa
hasira. Kwa kuwa alishajua kuwa ameonekana,
akavuta hatua za haraka huku akimsukuma Yule
dereva mpaka mlangoni, akatulia na kutazama
huku na kule kama kuna alam yoyote endapo
atagusa mlango huo.
“We! Fungua mlango,” alimwamuru Yule dereva.
Yule dereva akasita hakuufungua ule mlango,
“Hutaki? Nakufumua kichwa chako sasa hivi,”
Jack alimpa kitisho Yule dereva, lakini jamaa
alionesha ununda wake. Jack akashikwa na
hasira, akairudisha bastola kiunoni mwake,
kitendo hicho kikamfanya Yule dereva kuanzisha
shambulizi la ghafla, aligeuka na kumtandika
ngumi moja kali Jack, Jack hakutegemea pigo
hilo, hakuwa amejiandaa, kabla hajajiweka sawa,
konde la pili na la tatu yakamuishia, akatema
damu. Alipotaka kuchukua bastola yake
ikamponyika na kuanguka chini, Yule dereva
akaipiga teke ikaenda mbali kidogo, hakuna
ujanja.
“Nalipiza kisasi cha rafiki zangu uliowaua kule
The Great Nile Bar, na nakuhakikishi hamuwezi
kufanikisha azma yenu kwani hivi sasa kamera
zimekwishakuona wewe na mwenzio, zitazame
hii, ile, na ile kule,” yule dereva alikuwa
akimwambia Jack, ijapokuwa Jack aliambiwa
atazame kamera hizo lakini aliujua ujanja huo,
akajifanya anageuka ili atazame, Yule dereva
aliachia konde zito, Jack aliliona akaepa na
kuudaka ule mkono akageuka nao na kuuvunja
kwa kuupinda begani mwake.
“Utajutia uamuzi wako!” alimwambia Yule
dereva, akambeba na kumbwaga chini kwa
mbele, hakumchelewesha alimkanyaga kwenye
koo lake, “Ulifikiri mi ni wa kuchezewa?” Jack
aliuliza. Kabla hajakaa sawa kummaliza Yule
jamaa alisikia michakacho ya miguu inayokuja
upande huo. Mara risasi kama tatu zikasikika
upande wake, kajirusha na kuinyakuwa bastola
yake kisha kwa samasoti moja akatua nyuma ya
maua marefu akatulia kimya.
“Kadondokea wapi?” mmoja wa walinzi
akauliza.
“Simuoni, atakuwa kajificha,” mwingine akajibu
huki akichomoa simu ya upepo na kutaka kuita
malindo mengine. Jack akaona sasa mambo
yataharibika, akaruka juu kama mzimu na kutua
juu ya wote wawili na kwenda nao mpaka chini
kisha akajinyanyua haraka na kutua pembeni,
risasi moja ikafumua ile kamera ya mlangoni.
Alipojaribu kupiga risasi nyingine, lo, bastola
imeishiwa, hamna risasi katika chemba yake.
Akaipachika kiunoni mwake na kumkabili mmoja
wao aliyekuwa karibu kwa mikono. Makonde
matatu ya nguvu yalivunja shingo ya askari Yule,
wakati huo Yule wa pili alikuwa akija kasi, kwa
umbali aliomfikia asingeweza kumshambulia na
alishindwa kurudi nyuma ili atengeneze nafasi
hiyo, akatumia mbinu ya kijinga, akamrukia na
kuanguka nae chini kisha akajiviringa pembeni,
lakini Yule mlinzi aliyeonekana hodari kwa
michezo hiyo alijinyanyu kiufundi na kuwa wa
kwanza kusimama. Jack kabla hajajiinua teke
moja la mbavu lilimfanya agune kwa maumivu,
akajitupa mbali na kujifanya kaelelemewa na
maumivu, Yule mlinzi akaona tayari ushindi
wake umeonekana akamjia taratibu kwa
madaha. Jack akajifanya anajiinua kwa tabu na
kujirudisha chini, kumbe alikuwa anasubiri
akaribie.
Jack alifuta mguu wake mzima kwa kasi na
nguvu na kumpiga jamaa ngwala moja maridadi,
Yule mlinzi bila kipingamizi alijibwaga chini na
kukutana na bisu kali lililodidimia kifuani mwake,
macho yakamtoka, roho ikatengana na mwili.
Joru akaamka na kuchukua risasi akaijaza
bastola yake, mara nyuma yake akasikia mlio
wa bastola inayoondolewa usalama.
“Tulia hapo ng’ombe wewe! Weka bastola chini
na unitazame ili nikurarue vizuri,” alikuwa ni Yule
dereva aliyevunjwa mkono akiwa ameshika
shotgun ya mmoja wa wale walinzi ambao
tayari walikuwa marehemu. Jack akaweka
bastola yak echini, kisha akageuka kwa kasi na
kurusha kisu kilichokuwa kimebanwa katika
kizibao chake alichovaa juu, Yule dereva alijikuta
koromeo lake likichanwa vibaya na kisu hicho,
akarudi ardhini alikokuwa amelala tangu
mwanzo na kuyaingia mauti. Jack akaokota
bastola yake na kuwasachi wale jamaa mmoja
kwa mwingine, hakuna cha maana isipokuwa
alikuta kila mmoja akiwa na kidubwasha kidogo
kilichokuwa kikiwaka taa nyekundu,
alipokichunguza aligundua ni maalum kwa
dharura na msaada, akagundua kuwa Yule
dereva atakuwa alikibonyeza muda Fulani ndio
maana wale walinzi wakaja kumsaidi. Jack
akavikusanya vyote na kuvivunjavunja kisha
akauendea mlango nwa kile kibanda na
kuufungua kwa risasi moja, alikuwa
amekwishachanganyikiwa, hakujua kama Joru
mzima au la.
Akaingia ndani ya kile kibanda na kukutana na
mitambo ya usalama, luninga ndogondogo
zilizokuwa zikionesha kila kona ya eneo lile,
akatazama zote hakuna hata moja ambayo
ilimuonesha Joru wala mtu yeyote. Hakuna
linguine, aliifuata switch kubwa na kuizima,
kamera zote zikazimika. Pembeni akaona
kikabati cha chuma, kikabati kama cha kuwekea
pesa benki ambacho komeo lake ni kama
usukani wa boti, akakiendea, alipotaka kukigusa
moyo wake ukasita, akafikiri mara mbili na
kuamua kujipanga kwenda nyumba kubwa yeye
mwenyewe.
§§§§§

Tafrija ya familia iliyokuwa ikiendelea ndani ya
nyumba ya Malyamungu, ilisita ghafla, Kalosi
aliona kama kivuli kimepita katika moja ya
vijiluninga vilivyopo katika sehemu maalumu ya
sebule kubwa ya Malyamungu. Kila mtu akatulia,
Kalosi akaziendea zile luninga kutazama ni kitu
gani. Sheria ya eneo hilo ilikuwa ni kutotembea
usiku hata kwa walinzi labda kwa ruhusa
maalumu, hii ilikuwa ni kuruhusu wale wasio
wahusika kuonekana kiurahisi na kamera hizo.
Alipokaribia zile runinga mara ghafla zikazimika
zote kumi na mbili.
“Shiiitttt!” akang’aka.
“Vipi?” mdogo wake akauliza, alipozitazama zile
runinga zilikuwa giza, akachomoa bastola yake
na kuiweka sawa.
“Wazee, tulieni hapahapa, ulinzi dhidi yenu upo
imara,” aliongea mdogo wa Kalosi ambaye ni
mwanajeshi katika jeshi la Uganda, UPDF.
Akajiweka tayari kwa lolote ili kuwalinda wazazi
wake, bastola mkononi, akawa akichungulia nje
kupitia dirisha moja baada ya jingine. Kalosi
akatoa sonyo refu na kuuendea mlango mkubwa
wa nyuma hiyo.
“Mark, weka ulinzi nakuja, ngoja niende control
room ,” Kalosi akamwambia mdogo wake Mark
aliyekuwa bado anaangalia angalia nje kupitia
madirisha ya nyumba hiyo. Akamuonesha ishara
ya dole gumba kaka yake akimaanisha ‘poa’.
“Hapohapo ulipo tulia, hutoki kwenda popote,
rudi ndani,” ilikuwa sauti kavu ya Joru
ikimwamuru Kalosi. Kalosi alitazamana na domo
pana la bastola aina ya Smith and Wesson ,
akatulia hana la kufanya. Joru akampa ishara ya
kurudi alikotoka. Mkono wa kushoto Joru
alikamata bastola nyingine iliyofungwa kiwambo
cha sauti.
“Rudi ndani,” akamwamuru tena Kalosi,
“Usigeuke, rudi kinyumenyume mpaka
nitakapokwambia,” Joru aliendeleza amri. Kalosi
hakuwa na ujanja alianza kuvuta hatua kwa
nyuma huku mikono yake ikiwa hewani.
Mark aliposikia amri hiyo akajua tayari
kumekucha, akajificha nyuma yan pazia kubwa
ambalo lilikuwa kama mita tano kwa umbali
tokea pale mlangoni, hivyo angeweza kumuona
kwa uzuri Joru atakapoingia, aliiweka tayari
bastola yake na kuikamata vyema kabisa,
alianza kumuona Kalosi akiingia akiwa anarudi
kinyumenyume. Akasubiri zamu ya Joru kuingia
ili ammalize palepale, akaiinua bastola yake na
kuielekeza kule mlangoni.
§§§§§

Jack aliendelea kutazama lile kabati la chuma,
akapiga moyo konde na kuinua bastola yake,
risasi mbili tu alikuwa amekwishafumua kitasa
imara kabisa cha kabati hilo akaukamata
mlango na kuuvuta, likabaki wazi, Jack
hakuamini macho yake, mabunda ya noti
yalikuwa yamepangwa kwa ustadi wa hali ya juu
kabisa, akatazama huku na kule akachukua box
la ukubwa wa wastani akayasunda ya manoti
pamoja na kuliweka mezani. Chini kabisa ya zile
noti alikutana na mabomu ya kurusha kwa
mkono, guruneti, akatikisa kichwa.
‘Hivi hawa walikuwa wanajua siku moja
kutakuwa na vita au vipi?’ akajiuliza Jack, ‘Sasa
leo haya yatafanya kazi maalum hapahapa,’
akajijibu kisha akanyanyua lile boxi na kuiendea
switch ya umeme, akazima taa zote za nje, giza
likatawala. Jack akakenua kwa furaha ya kupata
uficho huo. Akatoka na kutembea taratibu na lile
box mikononi mwake mpaka kwenye ile gari,
akatazama ndani hakuna funguo, akasonya,
hakujua nini cha kufanya, akaamua kulitupia
ndani lile box na kisha yeye mwenyewe kuamua
kuikabili nyumba kubwa, akawa akitembea
polepole mkono wa kulia akiwa na bastola yake
na kushoto akiwa kakamatia bisu lenye hasira.
Akazifikia ngazi na kuzikwea taratibu. Kitu cha
kustusha kilimtokea, mbele yake alikutana na
damu inayotiririka kwenye ngazi ikitokea ndani
ya hiyo. ‘Joru!’ akajiwazia kwa mshtuko na
kuongeza nguvu kuzipanda zile ngazi kuielekea
ile nyumba.
§§§§§
§§§§§
Mark alijiweka tayari kwa shambulizi la ghafla
lakini kabla hajafanya lolote, mfanyakazi wa
ndani aliyekuwa akitokeas kwenye korido kuja
sebuleni alikuta hali ile ya hatari, akapiga kelele
za kushtukiza, kelele za woga, ambazo
zilimvuruga kila mtu mle ndani. Mark alipoteza
umakini kutokana na kelele hizo, akafyatua risasi
lakini alipokuwa akiondoa usalama wa bastola
ile Joru alikwishajua kuna hatari, tayari akajitupa
chini huku bastola yake ngangari mkononi, ile
risasi ikakosa shabaha na kuchimba ukuta. Yule
binti akakimbia kutoka nje, hakuumaliza mlango
kwani risasi nyingine ya Mark aliyomlenga Joru
iliishia kwa Yule binti, akabwagwa chini chale
damu zikitiririka kwa kasi. Joru muda huo huo
akiwa chini hakupoteza nafasi, teke moja kali
likamwangusha Kalosi kabla hajafanya lolote,
kisha yeye akajiinua na haraka kugeuka kule
ilikotokea ile risasi, nyuma ya pazia, bastola
zote mbili mkononi, moja ikimtazama Kalosi
aliyekua akijiinua na nyingine ikimtazama Mark
pale dirishani alipokuwa kapigwa na butwaa
baada ya kuona mwili wa msichana wa kazi
ukimalizia tone la mwisho la uhai wake.
Kwa kutumia bastola yake akamuonesha ishara
Mark ya kuungana na mwenzake. Nukta
hiyohiyo mlango ukasukumwa, Jack akajitoma
ndani huku akijirusha sarakasi ili kupoteza
shabaha ya yeyote aliyekusudia kumlenga,
alipotua na kusimama tu, Mark alichomoa
bastola nyingine na kuifyatua.
“Aaaaaaaiiiiggghhhhh!!!!!” yowe la uchungu
likamtoka Jack.
Kitendo cha Jack kuanguka chini kilimuuma
sana Joru, lakini hakuona haja kwanza ya
kumsaidia wakati pembeni yake ana adui
waliomzunguka. Aliuma meno na kuikamata
sawia bastola yake aina Smith and Wesson,
aliifyatua trigger na bastola ile ya kizamani ikato
mbanjo wa aina yake, risasi yake ikmfikia Mark
usawa wa moyo na kumpaisha mpaka kwenye
kioo cha dirisha, alijipigiza na kutoka nacho nje,
chali bila uhai. Joru akatikisa kichwa kwa kazi
murua iliyoonesha na bastola hiyo ya kizamani.
Kalosi alitaka atumie nafasi hiyo kumshambulia
Joru, akachelewa, Joru alikuwa tayari amegeuka
na kumzuia kwa teke moja kali lililotua tumboni
na kumfanya Kalosi kujiinamia. Joru
akamwamuru kuinuka.
“Mfunge huyo kitambaa zuia damu” Joru
akamwamuru Kalosi, amri hiyo ilimfanya Kalosi
kujisikia vibaya sana akakaidi, kwa kumwangalia
Joru kwa jicho la dharau.
“Wewe ni nani?” sauti ya Malyamungu iliyafikia
masikio ya Joru pale aliposimama.
“Unataka kunijua? Subiri dakika moja tu,” Kisha
akamtazama Kalosi na kumuamuru aelekee pale
alipoketi baba yake. Kalosi akatii.
“Kaka vipi?” Joru alimuuliza Jack.
“Niko sawa, ni mkwaruzo tu begani,” Jack
akajibu. Joru akiwa kamuweka kwenye shabaha
Malyamungu na Kalosi alianza kunagusha
machozi.
Vilio vya uchungu vilimrudia masikioni mwake,
alimkumbuka babaye na mamaye, jinsi
walivyouawa kikatili na mtu huyo aliketi mbele
yake.
“Laiti ungejua kuwa siku hii inakuja basi
ungeomba Mungu akuchukue mapema, wewe ni
Malyamungu na mimi ni mali ya Mungu,” Joru
aliongea kwa uchungu sana, “Sipendi kukuua
lakini baba yangu uliyemuua pamoja na mama
yangu na wanakijiji wengine, wamenituma, tangu
mwaka ule wa 1977 leo hii nimekuja kutimiza
azma hiyo, naitwa Joseph Rutashobya kutoka
Tanzania, Mtukula ndani ya mkoa wa Kagera,
Malyamungu huna haja ya kuishi kwa sasa, sina
haja ya kukupa nafasi ya kusali kwa mara ya
mwisho,” Joru aliongea kwa uchungu sana.
“Joru, shoot them,” (Joru walipue hao!) ilikuwa
sauti ya Jack kutoka pale chini. Joru aliisikia
sauti ya Jack, akainua bastola yake na kulenga
paji la uso wa Malyamungu, kisha akamwambia
Joru.
“Mimi nilishuhudia baba yako akimuua mama
yangu na baba yangu, na wewe sasa ni dhamu
yako kushuhudia hay ohayo,” Joru alimaliza na
kuiweka tayari bastola yake ya kizamani
iliyokuwa na risasi tatu tu baada ya ile moja
kumuua Mark. Akaifyatua kwa hasira, na risasi
moja ikatawanya kichwa cha Malyamungu.
“Noooooooooo!!!!!!” ilikuwa sauti kali ya kike,
mama wa Kalosi aliibuka kutoka uvungu wa
meza akiwa na shotgun mkononi mwake,
akairusha kumrushia kalosi ili afanye yake.
Kakutana na shabaha kali ya ajabu kutoka kwa
Joru, ile shotgun ilipigwa risasi kwa kutumia
bastola ya kisasa ambayo Joru aliikamatia
mkono wake wa kushoto, na kudondoshea
pembeni. Kisha mkono wake wa kulia ukafyatua
tena bastola ile ya kizamani na mama wa Kalosi
akatupwa chini akiwa hana uhai.
Kalosi alishaindwa kuvumilia kushuhudia wazazi
wake wakiuawa namna hiyo ilhali yeye yuko
kando akitazama. Akamvamia Joru na kuanza
kumshambulia, teke la kwanza lilitoa ile bastola
mkononi mwa Joru, teke la pili likampata joru
ubavuni, Joru akajipinda kutokana na maumivu
aliyoyapata, akatema kipande cha damu. Kalosi
akainua chupa ya pombe kali na kumrushia
Joru, Joru akaruka hewani na kuipiga teke
maridadi ikamrudia Kalosi na kumpiga usoni.
Kalosi kabla hajajiweka sawa na bunduki
nyingine mkononi, alijikuta akipaishwa na
kujipigiza ukutani kisha akajibwaga chini bila
uhai. Joru akageuka na kumuona Jack akiwa na
bastola ile aliyoidondosha, bastola ya kale,
Smith and Wesson.
“Asta la vista Kalosi,” Jack alisema kisha
akaanguka sakafuni mzima mzima.
“Jack, Jack, Jaaaaaaccckkkk!!!!” Joru aliita kwa nguvu. Baada ya sekunde kadhaa, akaamua
kumuinua, na kumuweka begani, akakusanya na
bastola zao akatoka nje na kuikuta ile gari ikiwa
palepale, akambwaga katika kiti cha nyuma na
kuingia katika kiti cha dereva, akatazama gari
haina ufunguo. Akabomoa mahali pa kuwekea
ufunguo akaunganaisha viwayawaya mpaka gari
ile ikawaka, akatia gia akaigeuza na kuondoka
kwa kasi kuelekea geti kubwa la nyumba hiyo,
hakujali kufunguliwa alipita na kugonga vyuma
vya geti hilo kisha akakunja kona kali na kuingia
barabara iliyokuwa ikienda kutokea barabara
kuu.Mlipuko mkubwa ukatokea nyuma yake, bomu
alilolitega Jack katika mtindo anaoujua yeye
lililipuka na kufumua kibada chote kilichojaa
mitambo ya mawasiano na usalama. Mara tena
mlipuko mwingine ukatoakea katika nyumba ya
Malyamungu. Joru akakanyaga mafuta na
kuipata barabara kuu ya kuja Kampala.
Akaendesha gari kama mwizi mpaka umbali wa
kilomita hamsini, nje ya mji, akatafuta mahali
kwenye kijiji ambapo kuna watu kidogo,
akaegesha gari na kurudi kwa mguu mpaka
sehemu iliyokuwa na vijana waliokuwa katika
ulinzi wa sungusungu, akawauliza kama eneo
lile kuna zahanati, wakamuonesha zahanati ya
misheni, akaenda na kukuta iko wazi, akaomba
vifaa vichache akapewa na kurudi ndani ya gari.
Akampaka iodine katika jeraha lake na kumfunga
kwa bandeji kisha akamchoma sindano ya
Diclofenac na kuondoa gari kwa kasi.
Saa kumi alfajiri ilimkuta Joru na majeruhi wake
katika eneo la Masaka, katika bar ileile
waliyokutana mwanzo. Joru, akazimamaisha
gari katika maegesho ya bar hiyo, akaicha pale,
akachukua mfuko na kuzisunda zile pesa zote,
akambeba Jack mpaka kwenye moja malori
yaliyokuwa hapo, akamsaka dereva akampata,
akamwomba amfikishe mpakani, ikawa hivyo.
Saa nne asubuhi Jack alipata fahamu, akainua
kichwa lakini kilikuwa kizito sana, akakikuridisha
kitandani.
“Joru,” akaita. Joru alipatwa na furaha sana
kuona swahiba wake amerudiwa na fahamu.
“Jack, Jack, umeamka, asante Mungu,” Joru
hakuamini kama mtu huyoi amekwisha amka.
“Hapa ni wapi?” Jack akauliza.
“ Tuko mpakani upande wa Tanzania, tuko
salama,” Joru alimwambia Jack.
“Oh, asante sana,” Jack alishukuru. Baada ya
masaa mawili, Jack alikuwa akifanya mazoezi
ya kutembea, ndipo alipojigundua kuwa ana
jeraha katika ubavu wake. Jack alipigwa risasi
mbili, moja begani lakini haikumwingia
sawasawa na nyingine ilipiga ubavuni na kunasa
ndani yake. Joru baada ya kumfikisha hospitali
hiyo ya serikali alijitambulisha na kupatiwa
msaada wa haraka.
§§§§§

Polisi walifika katika nyumba ya Malyamungu na
kukuta maafa wasiyoyategemea, walikusanya
miili isiyi na uhai kama nane hivi, wakati huo
nyumba ya Malyamungu ilikuwa ikiteketea kwa
moto.
“The bastard has gone,” (Mwanaharamu
amekwenda) , kiongozi aliyekuwa akiongoza
polisi hao katika operesheni ile alitamka maneno
hayo wakati akitazama mwili wa Malyamungu
ukifunikwa kwa mfuko maalumu wa plastiki.
Akarejea katika gari yake kisha akaketi kimya
akitafakari jambo, “Natamani kama ningemuua
mimi vile lo,” Yule polisi akaendelea kujiseme
kwa masikitiko, kisha wakaondoka na gari zao
wakiwaacha kikosi cha zimamoto kikitimiza
majukumu yake.
Kama kuna habari ilifurahiwa na watu huko
Uganda basi waliposikia kifo cha Malyamungu
redioni. Walitamani kupiga vigelegele lakini
haikuwa hivyo. Wengi wao waliachwa na
makovu yasiyofutika, machozi ya kumbukumbu
mbaya ya mtu huyo, ama aliwaua ndugu zao au
alichoma moto nyumba zao.
“Hakuna marefu yasiyo na ncha,” mwananchi
mmoja alikuwa akiwaambia wenziwake pindi
alipokuwa akiiacha luninga iliyokuwa ikionesha
habari hiyo mapema asubuhi.
§§§§§

BAADA YA SIKU 2

Joru na Jack walirudi katika hali zao za
kawaida, wote walikuwa na furaha hasa baada
ya kuitimiza azma hiyo iliyokuwa ikimtesa kila
mmoja moyoni kwa jinsi zake. Jack alihesabu
pesa zilizokuwa ndani ya fuko lile, si haba pesa
ilikuwa ni nyingi ya kutosha. Akamwambia Joru
jinsi alivyoipata pesa hiyo nyumbani kwa
Malyamungu.
“Safi sana Jack, pesa hii itajenga maisha yako,
usirudi tena Uganda, tafuta ardhi na kujenga
hapa kisha fanya miradi yako, mke na mtoto
utawafuata au utawaita waje waungane nawe
katika maisha mapya,” Jack alimtazama Joru
kwa kumkazia macho. Akasimama na
kumkumbatia rafikiye huyo ambaye urafiki wao
ulikuwa ni wa siku sita tu mpaka hapo lakini
tayari walikwishafanya mambo makubwa.
Baada ya siku hiyo Joru alirudi nyumbani na
kuungana tena na family ya Shibagenda, Kemi
hakuamini kama mpenziwe huyo karudi salama.
Siku hiyo alimkuta mzee Shibagenda mwenyewe
nyumbani.
“Joru, wewe ni mwanaume sasa, ulilolifanya
nimelisikia, hongera sana, umekomaa,”
Shibagenda akampongeza Joru.
Haikupita muda mrefu, mipango ya ndoa na ya
Joru na Kemi ikaanza ndani ya familia ya
Shibagenda. Kabla ya ndoa hiyo Joru akiwa na
Kemi pamoja na mtoto wao walikwenda kuzuru
eneo ambalo kijiji chao kilikuwapo. Joru
alisimama juu ya kilima kidogo akitazama
vichaka vya migomba na mikahawa
vilivyobadilisha taswira ya eneo hilo. Joru
akaangukwa na machozi, akamtazama Kemi,
akamtazama mwanawe.
“Baba, uliniachia risasi 4, nimezitumia kama
ulivyofikiri, nimekuja hapa kukwambia wewe,
mama yangu pamoja na majirani wote ambao
roho zao zilidhurumiwa na Malyamungu, Kazi
mliyonituma nimeimaliza”.

«««« MWISHO »»»»
 
CHAPISHO LA 11
§§§§§

Rejea JORU na KEMI
JORU alimkumbati Kemi kwa nguvu, wote wawili
waliangusha machozi. Mama Shibagenda alibaki
kuwaangalia vijana hao. Wakati wakiwa katika
kukumbatiana huko Kemi alihisi mwili
ukimtekenya sana, alihisi raha ya ajabu, alizidi
kumkumbatia Joru. Baada ya dakika kama tano
za kumatiano hilo, Joru alimuachia Kemi,
akamfuata machozi.
“Ina maana ninyi mnafahamiana?” Mama
Shibagenda akauliza.
“Mama tunafahamiana tangu utoto wetui,
tumelelewa kijiji kimoja na tulikuwa marafiki wa
kweli, sikutegemea kama mrembo wangu yuko
hai,” Joru akaeleza, ndipo mama Shibagenda
alipopata kujua mkasa mzima wa Joru na Kemi
kila mtu kwa upande wake.
“Poleni, sana sasa mmeamini kuwa milima
haikutani ee? Haya basi Joru, kama kawaida
nyumba yako ipo daima inakusubiri,
ukajipumzishe kidogo,” mama Shibagenda
akamwambia Joru, kisha akamgeukia Kemi
aliyekua akionekana na aibu kidogo, “Nani, Kemi!
Mchukulie mzigo umuongoze, usijali ni siku
nyingi hamjaonana basi mkaongee vizuri na
kusalimiana, kazi za huku mi nitafanya tu,”
alimaliza mama Shibagenda, Kemi akamchukua
begi la Joru na kuelekea kule kunako nyumba ya
uani, wakimuacha mtoto akirudishwa kulala.
Kama kuna kitu ambacho Kemi alikuwa
akikifikiria kitafika lini na vipi ni hicho, tangu
avunje ungo hakuwahi kukutana na mwanaume.
Upendo wake wa kweli kwa Joru ulimfanya Kemi
kuuhifadhi usichana wake mpaka huyo
aliyetamani kumpa afike, ijapokuwa alikuwa
hajui kama yupo hai au amekwishakufa, lakini
upendo wa kweli ulimwongoza katika hili. Kemi
alikuwa mtu wa kuweka ahadi bila kuvunja,
alimpenda Joru, alimpaenda sana, siku zote
alikuwa akimfikiria kijana huyo, haja yake hata
kama asipoolewa na Joru lakini Joru awe wa
kwanza kufungua njia hiyo inayotamaniwa na
wengi.
Walifika kwenye nyumba ambayo Joru alikuwa
akiitumia tangu kwanza, akakuta kila kitu kipo
kama kilivyo.
“Hapa ndio kwako?” akauliza Kemi.
“Ndiyo, nyumba hii nilikabidhiwa na baba
mwenye nyumba, mzee Shibagenda, niishi muda
wote wa maisha yangu, wamekuwa kama
wazazi kwangu, wamenipenda kwa upendo wote.
Kemi nalikutafuta sana katika nafsi na moyo
wangu nisikuone, hakika nilijuwa kuwa labda
umekufa miaka ile ya mauaji yaliyotokea pale
kijijini,” Joru alimjibu Kemi na kuongezea na
mazungumzo mengine. Kemi akatua begi chini,
akamtazama kijana Yule aliyekuwa ndani ya
sare nadhifu ya jeshi, aliyejaa katika umbo la
kiuwanaume haswa, kemi akainamisha uso wake
hakupenda kumwangalia usoni.
“Joru siamini kama ni wewe, siamini kabisa,
sikujua kama mtoto Yule ni wako, lakini jina lake
lilinifanya nimpende kama mwanangu, kwangu
nilimuona kama mume, hata nilipolala naye
kitandani nilihisi niko na Joru wangu, nakupenda
sana Joru,” Kemi alimweleza Joru kisha machozi
yakafuata na kutiririka juu ya mashavu yake
meusi, yanayopendeza kwa rangi hiyo
aliyojaliwa na Mungu, akamtazama Joru usoni,
huku akiwa amejawa na uchungu, “Joru,
nimekutunzia usichana wangu mpaka sasa
ingawaje sikujua kama upo hai au umekufa,
niliapa sintompa mwanaume yoyote penzi langu
isipokuwa wewe, nilitaka kubkwa lakini
nikapigania mwili wangu mpaka nikajinasua
mikononi mwa nunda, ijapokuwa nilimuua bila
kukusudia na kufungwa jela miaka miwili, bado
nilikukumbuka Joru, sasa moyo wangu unauma
sana kuona kuwa mtoto Yule ni wako, najua
huwezi kupata mtoto bila mwanamke, ijapokuwa
hautakuwa tayari kunioa lakini kabla sijampa
penzi mwanaume mwingine nilitaka wewe uwe
wa kwanza, wewe uondoe kizinda cha uke
wangu, niko tayari hata kama umepata ugonjwa
huko ulikopita,” Kemi akaangusha chozi.
Joru akamsika mbega na kumvutia kwake,
akamkumbatia katika kifua chake kipana,
akamsaidia kulia kwa sekunde kadhaa, kisha
akamtoa, mikono yake ikiwa katika mabega ya
Kemi alimtazama usoni.
“Kemilembe, daima umekuwa ndani ya moyo
wangu, kiukweli kabisa siwezi kubishana na
moyo, ninakupenda kipepeo, nimekuwa nikikulilia
daima, nikikuomboleza kama umekufa lakini
bado Mungu alikuwa na mpango na sisi.
Nimeishi kwa taabu sana Kemi, porini na katika
maeneo hatarishi, nimefanya kazi kwa bwana
mmoja nikidhulumiwa ujira karibu mwaka
mzima, kwa hasira ili kulipiza kisasi kwa bwana
huyo aliyekuwa akinilaza pamoja na kuku ndani
ya banda lililojaa utitiri, nikaamua kumbaka binti
yake, Koku, kumbe siku hiyo inaoneka alikuwa
katika siku za uzazi, akashika mimba pa si mi
kujua, siku ya mwisho ya kuhitimu kozi yangu
ya jeshi ndipo aliponilete mtoto huyu, akanambia
kuwa yeye amechumbiwa na bwana mwingine
hivyo mimi nilee mwanangu, nikamchukua.” Joru
akaeleza, akameza mate kisha akaendelea,
“Hakuna mwanamke nampenda kama Kemi,
daima sikuona thamani ya maisha bila wewe,
daima nilikuwa naomba Mungu kama upo hai
tukutane tena na sasa limetimia, nisamehe
mpenzi, nisamehe sana, lakini elewa kuwa wewe
si ubavu wangu bali ni moyo wangu, nakupenda
Kemi, uwe mama wa watoto wangu, tuishi,
tutulie, tujenge familia,” Joru akamaliza na
kumtaza Kemi usoni. Machozi ya Kemi
yalikauka, tabasamu likachanua kama ua la
yugiyugi.
Kemi akamsogelea Joru, akashika kifungo cha
gwanda lake na kukifungua, kisha cha pili, mara
cha tatu mpaka vyote vikaisha, akamvua
gwanda lile na kuliweka kochini, Kemi hakuishia
hapo, akaufyatua mkanda mnene wa suruari ya
Joru, akalegeza zipu, jicho lake likapenya ndani
ya eneo nyeti la Joru, akaona jinsi gani kijana
huyo alikuwa kwenye hari, kwani alituna
kiukweli. Kemi akamkalisha Joru kochini,
akamvua buti zake na kuziweka kando akamtoa
na suruali akaiweka kando na kumuacha akiwa
na vesti na boxer pekee, kifua chake kilichokuwa
kikipanda na kushuka kilimhamasisha Kemi,
akawa akikaukiwa mate kila sekunde,
akasimama. Joru akaelewa nini maana ya Kemi
kusimama, naye akasimama na kumkumbatia
akambusu kwa bashasha, kama alivyokuwa
akiona kwenye sinema, akaupitisha ulimi wake
kinywani mwa binti huyo, Kemi nae hakuwa
nyuma akakubaliana na hilo, ndimi zao
zikaogelea katika kinywa cha kila mmoja. Joru
akaishusha zipu ya blauzi ya Kemi kabla
hajaitupa pembeani na kukutana na kifua mororo
cha binti huyo, matiti mawili ya ukubwa wa
wastani yalikipamba kifua hicho kilichopendeza,
kilikuwa kikipanda na kushuka kikionesha ni jinsi
gani kilitamani. Joru akacheza na mtiti hayo,
akiyaminya kwa ustadi na kuyanyonyanyonya,
akaona Kemi akilalamika kwa raha,
akamnyanyua na kuingia naye chumbani,
akambwaga kitandani kisha akamalizia kuitoa
sketi ya binti huyo.
Baada ya dakika kama kumi na tano za
kuliwazana kwa kushikana hapa na pale kimya
bila yeyote kuongea, sasa kila mtu akawa kama
alivyozaliwa akishuhudia umbo la mwenzie,
wawili hao wakazama katika mapenzi mazito,
Kemi alikuwa akilalamika hasa kwa kusikia
maumivu kwa kuwa ilikuwa ni mara yake ya
kwanza, shughuli ilikuwa pevu, Joru akiwa ni
mara moja katika maisha yake kufanya tendo
hilo, hapo kwa Kemi alifurahia, kila mtu akawa
anaongea lugha yake, lugha iliyojulikana na wao
wenyewe.
Baada ya saa nzima ya mapenzi mazito, tayari
Joru alikuwa ameshafungua njia kama Kemi
alivyomuahidi, usingizi ukawapitia wote wawili,
waliposhtuka ilikuwa saa nane mchana, kila
mmoja akakimbilia bafuni kujiswafi, lakini bado
kila mmoja alikuwa na hamu na mwenzake,
hivyo wakatumia muda mwingine kujuliana hali
ndani ya bafu hilo lililojengwa kwa ndani ya
nyumba hiyo. Ilikuwa ni furaha ya watu wawili
kukutana tena.
Baada ya wiki moja
“Joru mpenzi, ijapokuwa tumeonana baada ya
miaka mingi, lakini unaonekana huna furaha”
Kemi alimwuliza Joru, wakiwa wameketi kwenye
jiwe nje ya nyumba ya Shibagenda pamoja na
mtoto wao.
“Ni kweli usemalo mpenzi, sina raha hata kidogo,
kuna jambo natakiwa kulifanya lakini sijajua ni
wapi pa kuanzia,” Joru akajibu.
“Niambie nitakusaidia, kama tumekutana tena
na jambo hilo hujaweza kulitatua basi amini
kwamba ni mimi wa kukusaidia ili ulitatue sasa,”
Kemi aliongea kwa lugha ya ushawishi.
“Kemi, kabla baba yangu hajafa aliniambia
maneno machache lakini pia hakuyamaliza,
akakata roho,” Joru akamwambia Kemi.
“Maneno gani?” Kemi akahoji.
“Aliniambia nilipize kisasi kwa mtu aliyemwaga
damu ya wanakijiji na damu ya Rutashobya,
sasa hili ni deni ambnalo liko moyoni mwangu
kwa miongo miwili sasa, nitaaniza wapi, sijajua,
kabla hajafa ilionekana kuna kitu anataka
kuniambia, aliishia tu kusema neno ‘nyuma ya
choo’ lakini hakunambia nini alimaanisha,” Joru
akamueleza Kemi kile kinachomsumbua akilini
mwake.
“Nyuma ya choo?” Kemi akauliza.
“Ndiyo, nyuma ya choo,” Joru akajibu. Kemi
akatulia kimya akitafakari jambo, kisha
akamtazama Joru aliyekuwa akicheza na
mwanawe, akatabasamu kuwaona hao Joru
wawili wakicheza kwa furaha.
“Joru, huna budi kufanya uloambiwa, kuna kitu
nakumbuka sasa, nafikiri kitakuwa na maana
kwako, nafikiri, labda ni jibu la swala lako,” Kemi
alimweleza Joru, akaketi vizuri na kumtazama.

1977
kijijini kwa JORU na
KEMI

JIONI ya siku moja, mzee Rutashobya, aliingia
chumbani mwake na kufungua mkoba ambao
una kitu alichokihifadhi kwa miaka mingi sana,
akakitoa na kukitia katika mfuko wa plastiki
kisha akatoka nacho nje, nyuma ya nyumba
akihakikisha hakuna anayemwona katika kufanya
hilo. Akachukua jembe na kuzunguka nyuma ya
choo, akachimba shimo la kina cha nusu mita na
kutumbukiza ule mfuko, kisha akafukia vizuri na
kutandaza nyasi juu yake. Akaangalia sana
kama kuna mtu aliyemuona hakuona kitu.
Wakati huo mzee Rutashobya akafanya hayo,
Kemilembe alikuwa akitoka kuteka maji,
akamuona baba wa Joseph akifukia kitu chini.
Kemi akasimama kwenye nyasi ndefu ili kuona
nini kinatukia, alishuhudia kila kitu mpaka Yule
mzee alipomaliza. Kwa kuwa Kemi alijuwa kuwa
hayamhusu, alaiendelea na safari ya kuingia
nyumbani. Mzee Rutashobwa akamuona Kemi,
akajiuliza kama atakuwa amemuona wakati
akilifanya hilo, akamwita Kemi, akimtaka kwanza
aweke ndoo ya maji nyumbani kwao. Baada ya
hapoi Kemi alikuja mpaka pale nyuma ya choo.
“Kemi, ulikuwa unatoka wapi?” akauliza
Rutashobya.
“Kuteka maji,” Kemi akajibu kwa lafudhi ya
Kihaya.
“Umeniona hapa nilikuwa nafanya nini?”
akauliza tena.
“Ndiyo babu nimekuona, umefukia mufuko,”
akamjibu kwa ustadi sana.
“Sasa sikiliza, hapa nimefukia sumu, sumu
mbaya kabisa ambayo ukiishika lazima ufe, usije
kucheza hapa na wenzako, sawa?” Rutashobya
akatoa onyo.
“Sawa babu!” Kemi akajibu. Watoto wa kijiji
hicho walizoea kumwita mzee Rutashobya
‘babu’ kutokana na uchezhi wake kwa watoto,
akiwatania kila kukicha, hivyo daima
walimpenda sana mzee huyu.
“Usimwambie mchumba wako Jose, sawa?”
akamsisitizia. Kemi akaitikia na kukiri kuwa
hatomwambia mtu. Kemi alipoondoka mzee
Rutashobya nae akatoka eneo lile, alijua wazi
kuwa baada ya siku chache tu Kemi atasahau
juu ya tukio lile na ndivyo ilivyokuwa.
Kemi hakukumbuka tena hata kama alimuona
mzee huyo akiwa pale, siku, miezi ikapita. Lakini
yeye tu Rutashobya aliyejua kuwa amefukia kitu
gani, malengo yake si kumpa mtu yeyote kitu
hicho bali aliamua kukitupa kwa kuwa ni sumu
mbaya kabisa, alikitupa kwa mtindo huo kwani
aliona wazi kama akitupa kwa njia ya kawaida,
watoto na watu wengine wangezurika nacho.
Siku alipokuwa anakufa baada ya mateso makali
ya vibaraka wa nduli Idd Amin, aliona kuwa ni
wakati wa kumwambia mwanawe, japokuwa
haikuwa dhamira yake tangu kwanza, kabla
hajamwambia ni nini kipo mzee Rutashobya
akakata roho, Joru akabaki gizani, hakujua ni
nini baba yake alitaka kumwambia.
Rejea Joru na KEMI
JORU alisisimkwa mwili kwa habari hiyo ya
Kemi, hakuwahi kuisikia hata mara moja katika
maisha yake, alimkumbatia Kemi kwa nguvu.
“Kemi, twende kijijini, nikachimbe hapo nione
kuna nini!” joru alisisitiza. Kemi akamtazama
Joru, akatikisa kichwa.
“Joru, hakuna kijiji kule ni mapori na machaka
ya kutisha!” Kemi akamwambia Joru.

KEMI NA JORU MAPENZINI..... KEMI
ANAMSIMULIA JORU JUU YA TUKIO LA ZAMANI
SANA AMBALO YEYE ALILISHUHUDIA KIJIJINI
KWAO..... JE LITAKUWA NA MATIKI KATIK
MKASA HUU?

Mkuu sana Willy Gamba 1, hili chapisho ndo kwanza page ya mwisho riwaya kwa kutumia laptop. Ningekuwa natumia simu labda ningekuwa page ya tatu hivi hata sijui. Ili kuingia page ya pili ktk laptop hii, kamata like kwanza, kisha mention na tatu ni qoutation mkuu Willy Gamba 1.

hakika naiona raha ya kusoma riwaya kwa mfufululizo. Ile uchu siku ikiisha itanilazimu kuisoma upya ili kuielewa japo imevamiwa na story za kulalamikia uletaji wake. comments za wafuatiliaji nyingi kuliko za mletaji bwana?:embarrassed1::embarrassed1:
 
CHAPISHO LA MWISHO
10 JACK MUTEBEZI akiwa bado
kamuwekea bastola Yule dereva alimuamuru
kuegesha gari mahali pa kila siku anapoegesha.
Hii ilikuwa ni kutaka kutowashtua wale walio
ndani ya eneo hilo, kuanzia na walinzi mpaka
malyamungu mwenyewe. Yule dereva akaegesha
gari mahali pake na kutulia palepale kwenye
usukani, Jack alizungusha macho yake huku na
kule akatzama mazingira hayo yaliyokuwa
yakimulikwa na taa zenye mwanga mithili ya
mbalamwezi. Hakumuona Joru, lakini aliamini
kijana huyo hawezi fanya makosa, Jack
hakuweza kushuka na kufanya lolote kutokana
na maumivu aliyokuwa akiyasikia katika mguu
wake ambao ameuunganisha na ule wa bandia
kutokana na mikikimikiki aliyokumbana nayo
siku hiyo. Alitulia katika siti ya nyuma akijaribu
kufanya kitu ambacho ama kitakuwa msaada
kwa Joru au kitasogeza mbele azma yao. Jack
akageuka kwa dereva na kumkuta akiwa
kakodoa macho yake mbele ya usukani.
“Zaidi ya walinzi, kitu gani hapa kinasaidia
ulinzi?” Jack akmuuliza Yule dereva.
“Aaah mbwa na kamera za usalama,” akajibu
kwa kitetemeshi.
“Wapi ambapo kamera hizi zinongozwa?”
akahoji.
“Kuna sehemu mbili, moja ni nyumba kubwa na
nyingine ni kibanda kile kule,” akajibu na
kuoneshea mkono katika kibanda kilichopo
umbali kama wa mita mia na hamsini hivi. Jack
akaona hapo patakuwa pagumu kwa Joru
kuifikia nyumba ile kama kamera hizo
zitaendelea kufanya kazi. Akamwamuru Yule
dereva ampeleke mpaka kwenye kile kibanda.
“Kwa muda huu ni hatari kaka, watatuona tu
halafu hawatatuacha hai,” Yule dereva akasema.
“Kwa hiyo we unaogopa kufa?” Jack
akamuuliza.
“Ha! Kuna mtu asiyeogopa kufa?” Yule dereva
akauliza.
Jack akamuamuru kuteremka na kumtaka
amuongoze mpaka kwenye kile kibanda,
akimuoneshea bastola Yule dereva akateremka
nje ya ile gari huku mikono yake ikiwa kichwani
na kuongoza njia, Jack alikuwa nyuma yake
akiwa na bastola yenye kiwambo cha sauti,
walijaribu kupita kwa kujificha ili kamera isiweze
kupata picha yao. Mahala Fulani hawakuwa na
ujanja, kwani juu ya ule mlango wa kile kibanda
kulikuwa na kamera inayaotazama mbele na
hakukuwa na njia nyingine isipokuwa hiyo tu.
Jack alipoinua macho akakutana uso kwa uso
na kamera hiyo.
“Shabash!” akajikuta akitamka neno hilo kwa
hasira. Kwa kuwa alishajua kuwa ameonekana,
akavuta hatua za haraka huku akimsukuma Yule
dereva mpaka mlangoni, akatulia na kutazama
huku na kule kama kuna alam yoyote endapo
atagusa mlango huo.
“We! Fungua mlango,” alimwamuru Yule dereva.
Yule dereva akasita hakuufungua ule mlango,
“Hutaki? Nakufumua kichwa chako sasa hivi,”
Jack alimpa kitisho Yule dereva, lakini jamaa
alionesha ununda wake. Jack akashikwa na
hasira, akairudisha bastola kiunoni mwake,
kitendo hicho kikamfanya Yule dereva kuanzisha
shambulizi la ghafla, aligeuka na kumtandika
ngumi moja kali Jack, Jack hakutegemea pigo
hilo, hakuwa amejiandaa, kabla hajajiweka sawa,
konde la pili na la tatu yakamuishia, akatema
damu. Alipotaka kuchukua bastola yake
ikamponyika na kuanguka chini, Yule dereva
akaipiga teke ikaenda mbali kidogo, hakuna
ujanja.
“Nalipiza kisasi cha rafiki zangu uliowaua kule
The Great Nile Bar, na nakuhakikishi hamuwezi
kufanikisha azma yenu kwani hivi sasa kamera
zimekwishakuona wewe na mwenzio, zitazame
hii, ile, na ile kule,” yule dereva alikuwa
akimwambia Jack, ijapokuwa Jack aliambiwa
atazame kamera hizo lakini aliujua ujanja huo,
akajifanya anageuka ili atazame, Yule dereva
aliachia konde zito, Jack aliliona akaepa na
kuudaka ule mkono akageuka nao na kuuvunja
kwa kuupinda begani mwake.
“Utajutia uamuzi wako!” alimwambia Yule
dereva, akambeba na kumbwaga chini kwa
mbele, hakumchelewesha alimkanyaga kwenye
koo lake, “Ulifikiri mi ni wa kuchezewa?” Jack
aliuliza. Kabla hajakaa sawa kummaliza Yule
jamaa alisikia michakacho ya miguu inayokuja
upande huo. Mara risasi kama tatu zikasikika
upande wake, kajirusha na kuinyakuwa bastola
yake kisha kwa samasoti moja akatua nyuma ya
maua marefu akatulia kimya.
“Kadondokea wapi?” mmoja wa walinzi
akauliza.
“Simuoni, atakuwa kajificha,” mwingine akajibu
huki akichomoa simu ya upepo na kutaka kuita
malindo mengine. Jack akaona sasa mambo
yataharibika, akaruka juu kama mzimu na kutua
juu ya wote wawili na kwenda nao mpaka chini
kisha akajinyanyua haraka na kutua pembeni,
risasi moja ikafumua ile kamera ya mlangoni.
Alipojaribu kupiga risasi nyingine, lo, bastola
imeishiwa, hamna risasi katika chemba yake.
Akaipachika kiunoni mwake na kumkabili mmoja
wao aliyekuwa karibu kwa mikono. Makonde
matatu ya nguvu yalivunja shingo ya askari Yule,
wakati huo Yule wa pili alikuwa akija kasi, kwa
umbali aliomfikia asingeweza kumshambulia na
alishindwa kurudi nyuma ili atengeneze nafasi
hiyo, akatumia mbinu ya kijinga, akamrukia na
kuanguka nae chini kisha akajiviringa pembeni,
lakini Yule mlinzi aliyeonekana hodari kwa
michezo hiyo alijinyanyu kiufundi na kuwa wa
kwanza kusimama. Jack kabla hajajiinua teke
moja la mbavu lilimfanya agune kwa maumivu,
akajitupa mbali na kujifanya kaelelemewa na
maumivu, Yule mlinzi akaona tayari ushindi
wake umeonekana akamjia taratibu kwa
madaha. Jack akajifanya anajiinua kwa tabu na
kujirudisha chini, kumbe alikuwa anasubiri
akaribie.
Jack alifuta mguu wake mzima kwa kasi na
nguvu na kumpiga jamaa ngwala moja maridadi,
Yule mlinzi bila kipingamizi alijibwaga chini na
kukutana na bisu kali lililodidimia kifuani mwake,
macho yakamtoka, roho ikatengana na mwili.
Joru akaamka na kuchukua risasi akaijaza
bastola yake, mara nyuma yake akasikia mlio
wa bastola inayoondolewa usalama.
“Tulia hapo ng’ombe wewe! Weka bastola chini
na unitazame ili nikurarue vizuri,” alikuwa ni Yule
dereva aliyevunjwa mkono akiwa ameshika
shotgun ya mmoja wa wale walinzi ambao
tayari walikuwa marehemu. Jack akaweka
bastola yak echini, kisha akageuka kwa kasi na
kurusha kisu kilichokuwa kimebanwa katika
kizibao chake alichovaa juu, Yule dereva alijikuta
koromeo lake likichanwa vibaya na kisu hicho,
akarudi ardhini alikokuwa amelala tangu
mwanzo na kuyaingia mauti. Jack akaokota
bastola yake na kuwasachi wale jamaa mmoja
kwa mwingine, hakuna cha maana isipokuwa
alikuta kila mmoja akiwa na kidubwasha kidogo
kilichokuwa kikiwaka taa nyekundu,
alipokichunguza aligundua ni maalum kwa
dharura na msaada, akagundua kuwa Yule
dereva atakuwa alikibonyeza muda Fulani ndio
maana wale walinzi wakaja kumsaidi. Jack
akavikusanya vyote na kuvivunjavunja kisha
akauendea mlango nwa kile kibanda na
kuufungua kwa risasi moja, alikuwa
amekwishachanganyikiwa, hakujua kama Joru
mzima au la.
Akaingia ndani ya kile kibanda na kukutana na
mitambo ya usalama, luninga ndogondogo
zilizokuwa zikionesha kila kona ya eneo lile,
akatazama zote hakuna hata moja ambayo
ilimuonesha Joru wala mtu yeyote. Hakuna
linguine, aliifuata switch kubwa na kuizima,
kamera zote zikazimika. Pembeni akaona
kikabati cha chuma, kikabati kama cha kuwekea
pesa benki ambacho komeo lake ni kama
usukani wa boti, akakiendea, alipotaka kukigusa
moyo wake ukasita, akafikiri mara mbili na
kuamua kujipanga kwenda nyumba kubwa yeye
mwenyewe.
§§§§§

Tafrija ya familia iliyokuwa ikiendelea ndani ya
nyumba ya Malyamungu, ilisita ghafla, Kalosi
aliona kama kivuli kimepita katika moja ya
vijiluninga vilivyopo katika sehemu maalumu ya
sebule kubwa ya Malyamungu. Kila mtu akatulia,
Kalosi akaziendea zile luninga kutazama ni kitu
gani. Sheria ya eneo hilo ilikuwa ni kutotembea
usiku hata kwa walinzi labda kwa ruhusa
maalumu, hii ilikuwa ni kuruhusu wale wasio
wahusika kuonekana kiurahisi na kamera hizo.
Alipokaribia zile runinga mara ghafla zikazimika
zote kumi na mbili.
“Shiiitttt!” akang’aka.
“Vipi?” mdogo wake akauliza, alipozitazama zile
runinga zilikuwa giza, akachomoa bastola yake
na kuiweka sawa.
“Wazee, tulieni hapahapa, ulinzi dhidi yenu upo
imara,” aliongea mdogo wa Kalosi ambaye ni
mwanajeshi katika jeshi la Uganda, UPDF.
Akajiweka tayari kwa lolote ili kuwalinda wazazi
wake, bastola mkononi, akawa akichungulia nje
kupitia dirisha moja baada ya jingine. Kalosi
akatoa sonyo refu na kuuendea mlango mkubwa
wa nyuma hiyo.
“Mark, weka ulinzi nakuja, ngoja niende control
room ,” Kalosi akamwambia mdogo wake Mark
aliyekuwa bado anaangalia angalia nje kupitia
madirisha ya nyumba hiyo. Akamuonesha ishara
ya dole gumba kaka yake akimaanisha ‘poa’.
“Hapohapo ulipo tulia, hutoki kwenda popote,
rudi ndani,” ilikuwa sauti kavu ya Joru
ikimwamuru Kalosi. Kalosi alitazamana na domo
pana la bastola aina ya Smith and Wesson ,
akatulia hana la kufanya. Joru akampa ishara ya
kurudi alikotoka. Mkono wa kushoto Joru
alikamata bastola nyingine iliyofungwa kiwambo
cha sauti.
“Rudi ndani,” akamwamuru tena Kalosi,
“Usigeuke, rudi kinyumenyume mpaka
nitakapokwambia,” Joru aliendeleza amri. Kalosi
hakuwa na ujanja alianza kuvuta hatua kwa
nyuma huku mikono yake ikiwa hewani.
Mark aliposikia amri hiyo akajua tayari
kumekucha, akajificha nyuma yan pazia kubwa
ambalo lilikuwa kama mita tano kwa umbali
tokea pale mlangoni, hivyo angeweza kumuona
kwa uzuri Joru atakapoingia, aliiweka tayari
bastola yake na kuikamata vyema kabisa,
alianza kumuona Kalosi akiingia akiwa anarudi
kinyumenyume. Akasubiri zamu ya Joru kuingia
ili ammalize palepale, akaiinua bastola yake na
kuielekeza kule mlangoni.
§§§§§

Jack aliendelea kutazama lile kabati la chuma,
akapiga moyo konde na kuinua bastola yake,
risasi mbili tu alikuwa amekwishafumua kitasa
imara kabisa cha kabati hilo akaukamata
mlango na kuuvuta, likabaki wazi, Jack
hakuamini macho yake, mabunda ya noti
yalikuwa yamepangwa kwa ustadi wa hali ya juu
kabisa, akatazama huku na kule akachukua box
la ukubwa wa wastani akayasunda ya manoti
pamoja na kuliweka mezani. Chini kabisa ya zile
noti alikutana na mabomu ya kurusha kwa
mkono, guruneti, akatikisa kichwa.
‘Hivi hawa walikuwa wanajua siku moja
kutakuwa na vita au vipi?’ akajiuliza Jack, ‘Sasa
leo haya yatafanya kazi maalum hapahapa,’
akajijibu kisha akanyanyua lile boxi na kuiendea
switch ya umeme, akazima taa zote za nje, giza
likatawala. Jack akakenua kwa furaha ya kupata
uficho huo. Akatoka na kutembea taratibu na lile
box mikononi mwake mpaka kwenye ile gari,
akatazama ndani hakuna funguo, akasonya,
hakujua nini cha kufanya, akaamua kulitupia
ndani lile box na kisha yeye mwenyewe kuamua
kuikabili nyumba kubwa, akawa akitembea
polepole mkono wa kulia akiwa na bastola yake
na kushoto akiwa kakamatia bisu lenye hasira.
Akazifikia ngazi na kuzikwea taratibu. Kitu cha
kustusha kilimtokea, mbele yake alikutana na
damu inayotiririka kwenye ngazi ikitokea ndani
ya hiyo. ‘Joru!’ akajiwazia kwa mshtuko na
kuongeza nguvu kuzipanda zile ngazi kuielekea
ile nyumba.
§§§§§
§§§§§
Mark alijiweka tayari kwa shambulizi la ghafla
lakini kabla hajafanya lolote, mfanyakazi wa
ndani aliyekuwa akitokeas kwenye korido kuja
sebuleni alikuta hali ile ya hatari, akapiga kelele
za kushtukiza, kelele za woga, ambazo
zilimvuruga kila mtu mle ndani. Mark alipoteza
umakini kutokana na kelele hizo, akafyatua risasi
lakini alipokuwa akiondoa usalama wa bastola
ile Joru alikwishajua kuna hatari, tayari akajitupa
chini huku bastola yake ngangari mkononi, ile
risasi ikakosa shabaha na kuchimba ukuta. Yule
binti akakimbia kutoka nje, hakuumaliza mlango
kwani risasi nyingine ya Mark aliyomlenga Joru
iliishia kwa Yule binti, akabwagwa chini chale
damu zikitiririka kwa kasi. Joru muda huo huo
akiwa chini hakupoteza nafasi, teke moja kali
likamwangusha Kalosi kabla hajafanya lolote,
kisha yeye akajiinua na haraka kugeuka kule
ilikotokea ile risasi, nyuma ya pazia, bastola
zote mbili mkononi, moja ikimtazama Kalosi
aliyekua akijiinua na nyingine ikimtazama Mark
pale dirishani alipokuwa kapigwa na butwaa
baada ya kuona mwili wa msichana wa kazi
ukimalizia tone la mwisho la uhai wake.
Kwa kutumia bastola yake akamuonesha ishara
Mark ya kuungana na mwenzake. Nukta
hiyohiyo mlango ukasukumwa, Jack akajitoma
ndani huku akijirusha sarakasi ili kupoteza
shabaha ya yeyote aliyekusudia kumlenga,
alipotua na kusimama tu, Mark alichomoa
bastola nyingine na kuifyatua.
“Aaaaaaaiiiiggghhhhh!!!!!” yowe la uchungu
likamtoka Jack.
Kitendo cha Jack kuanguka chini kilimuuma
sana Joru, lakini hakuona haja kwanza ya
kumsaidia wakati pembeni yake ana adui
waliomzunguka. Aliuma meno na kuikamata
sawia bastola yake aina Smith and Wesson,
aliifyatua trigger na bastola ile ya kizamani ikato
mbanjo wa aina yake, risasi yake ikmfikia Mark
usawa wa moyo na kumpaisha mpaka kwenye
kioo cha dirisha, alijipigiza na kutoka nacho nje,
chali bila uhai. Joru akatikisa kichwa kwa kazi
murua iliyoonesha na bastola hiyo ya kizamani.
Kalosi alitaka atumie nafasi hiyo kumshambulia
Joru, akachelewa, Joru alikuwa tayari amegeuka
na kumzuia kwa teke moja kali lililotua tumboni
na kumfanya Kalosi kujiinamia. Joru
akamwamuru kuinuka.
“Mfunge huyo kitambaa zuia damu” Joru
akamwamuru Kalosi, amri hiyo ilimfanya Kalosi
kujisikia vibaya sana akakaidi, kwa kumwangalia
Joru kwa jicho la dharau.
“Wewe ni nani?” sauti ya Malyamungu iliyafikia
masikio ya Joru pale aliposimama.
“Unataka kunijua? Subiri dakika moja tu,” Kisha
akamtazama Kalosi na kumuamuru aelekee pale
alipoketi baba yake. Kalosi akatii.
“Kaka vipi?” Joru alimuuliza Jack.
“Niko sawa, ni mkwaruzo tu begani,” Jack
akajibu. Joru akiwa kamuweka kwenye shabaha
Malyamungu na Kalosi alianza kunagusha
machozi.
Vilio vya uchungu vilimrudia masikioni mwake,
alimkumbuka babaye na mamaye, jinsi
walivyouawa kikatili na mtu huyo aliketi mbele
yake.
“Laiti ungejua kuwa siku hii inakuja basi
ungeomba Mungu akuchukue mapema, wewe ni
Malyamungu na mimi ni mali ya Mungu,” Joru
aliongea kwa uchungu sana, “Sipendi kukuua
lakini baba yangu uliyemuua pamoja na mama
yangu na wanakijiji wengine, wamenituma, tangu
mwaka ule wa 1977 leo hii nimekuja kutimiza
azma hiyo, naitwa Joseph Rutashobya kutoka
Tanzania, Mtukula ndani ya mkoa wa Kagera,
Malyamungu huna haja ya kuishi kwa sasa, sina
haja ya kukupa nafasi ya kusali kwa mara ya
mwisho,” Joru aliongea kwa uchungu sana.
“Joru, shoot them,” (Joru walipue hao!) ilikuwa
sauti ya Jack kutoka pale chini. Joru aliisikia
sauti ya Jack, akainua bastola yake na kulenga
paji la uso wa Malyamungu, kisha akamwambia
Joru.
“Mimi nilishuhudia baba yako akimuua mama
yangu na baba yangu, na wewe sasa ni dhamu
yako kushuhudia hay ohayo,” Joru alimaliza na
kuiweka tayari bastola yake ya kizamani
iliyokuwa na risasi tatu tu baada ya ile moja
kumuua Mark. Akaifyatua kwa hasira, na risasi
moja ikatawanya kichwa cha Malyamungu.
“Noooooooooo!!!!!!” ilikuwa sauti kali ya kike,
mama wa Kalosi aliibuka kutoka uvungu wa
meza akiwa na shotgun mkononi mwake,
akairusha kumrushia kalosi ili afanye yake.
Kakutana na shabaha kali ya ajabu kutoka kwa
Joru, ile shotgun ilipigwa risasi kwa kutumia
bastola ya kisasa ambayo Joru aliikamatia
mkono wake wa kushoto, na kudondoshea
pembeni. Kisha mkono wake wa kulia ukafyatua
tena bastola ile ya kizamani na mama wa Kalosi
akatupwa chini akiwa hana uhai.
Kalosi alishaindwa kuvumilia kushuhudia wazazi
wake wakiuawa namna hiyo ilhali yeye yuko
kando akitazama. Akamvamia Joru na kuanza
kumshambulia, teke la kwanza lilitoa ile bastola
mkononi mwa Joru, teke la pili likampata joru
ubavuni, Joru akajipinda kutokana na maumivu
aliyoyapata, akatema kipande cha damu. Kalosi
akainua chupa ya pombe kali na kumrushia
Joru, Joru akaruka hewani na kuipiga teke
maridadi ikamrudia Kalosi na kumpiga usoni.
Kalosi kabla hajajiweka sawa na bunduki
nyingine mkononi, alijikuta akipaishwa na
kujipigiza ukutani kisha akajibwaga chini bila
uhai. Joru akageuka na kumuona Jack akiwa na
bastola ile aliyoidondosha, bastola ya kale,
Smith and Wesson.
“Asta la vista Kalosi,” Jack alisema kisha
akaanguka sakafuni mzima mzima.
“Jack, Jack, Jaaaaaaccckkkk!!!!” Joru aliita kwa nguvu. Baada ya sekunde kadhaa, akaamua
kumuinua, na kumuweka begani, akakusanya na
bastola zao akatoka nje na kuikuta ile gari ikiwa
palepale, akambwaga katika kiti cha nyuma na
kuingia katika kiti cha dereva, akatazama gari
haina ufunguo. Akabomoa mahali pa kuwekea
ufunguo akaunganaisha viwayawaya mpaka gari
ile ikawaka, akatia gia akaigeuza na kuondoka
kwa kasi kuelekea geti kubwa la nyumba hiyo,
hakujali kufunguliwa alipita na kugonga vyuma
vya geti hilo kisha akakunja kona kali na kuingia
barabara iliyokuwa ikienda kutokea barabara
kuu.Mlipuko mkubwa ukatokea nyuma yake, bomu
alilolitega Jack katika mtindo anaoujua yeye
lililipuka na kufumua kibada chote kilichojaa
mitambo ya mawasiano na usalama. Mara tena
mlipuko mwingine ukatoakea katika nyumba ya
Malyamungu. Joru akakanyaga mafuta na
kuipata barabara kuu ya kuja Kampala.
Akaendesha gari kama mwizi mpaka umbali wa
kilomita hamsini, nje ya mji, akatafuta mahali
kwenye kijiji ambapo kuna watu kidogo,
akaegesha gari na kurudi kwa mguu mpaka
sehemu iliyokuwa na vijana waliokuwa katika
ulinzi wa sungusungu, akawauliza kama eneo
lile kuna zahanati, wakamuonesha zahanati ya
misheni, akaenda na kukuta iko wazi, akaomba
vifaa vichache akapewa na kurudi ndani ya gari.
Akampaka iodine katika jeraha lake na kumfunga
kwa bandeji kisha akamchoma sindano ya
Diclofenac na kuondoa gari kwa kasi.
Saa kumi alfajiri ilimkuta Joru na majeruhi wake
katika eneo la Masaka, katika bar ileile
waliyokutana mwanzo. Joru, akazimamaisha
gari katika maegesho ya bar hiyo, akaicha pale,
akachukua mfuko na kuzisunda zile pesa zote,
akambeba Jack mpaka kwenye moja malori
yaliyokuwa hapo, akamsaka dereva akampata,
akamwomba amfikishe mpakani, ikawa hivyo.
Saa nne asubuhi Jack alipata fahamu, akainua
kichwa lakini kilikuwa kizito sana, akakikuridisha
kitandani.
“Joru,” akaita. Joru alipatwa na furaha sana
kuona swahiba wake amerudiwa na fahamu.
“Jack, Jack, umeamka, asante Mungu,” Joru
hakuamini kama mtu huyoi amekwisha amka.
“Hapa ni wapi?” Jack akauliza.
“ Tuko mpakani upande wa Tanzania, tuko
salama,” Joru alimwambia Jack.
“Oh, asante sana,” Jack alishukuru. Baada ya
masaa mawili, Jack alikuwa akifanya mazoezi
ya kutembea, ndipo alipojigundua kuwa ana
jeraha katika ubavu wake. Jack alipigwa risasi
mbili, moja begani lakini haikumwingia
sawasawa na nyingine ilipiga ubavuni na kunasa
ndani yake. Joru baada ya kumfikisha hospitali
hiyo ya serikali alijitambulisha na kupatiwa
msaada wa haraka.
§§§§§

Polisi walifika katika nyumba ya Malyamungu na
kukuta maafa wasiyoyategemea, walikusanya
miili isiyi na uhai kama nane hivi, wakati huo
nyumba ya Malyamungu ilikuwa ikiteketea kwa
moto.
“The bastard has gone,” (Mwanaharamu
amekwenda) , kiongozi aliyekuwa akiongoza
polisi hao katika operesheni ile alitamka maneno
hayo wakati akitazama mwili wa Malyamungu
ukifunikwa kwa mfuko maalumu wa plastiki.
Akarejea katika gari yake kisha akaketi kimya
akitafakari jambo, “Natamani kama ningemuua
mimi vile lo,” Yule polisi akaendelea kujiseme
kwa masikitiko, kisha wakaondoka na gari zao
wakiwaacha kikosi cha zimamoto kikitimiza
majukumu yake.
Kama kuna habari ilifurahiwa na watu huko
Uganda basi waliposikia kifo cha Malyamungu
redioni. Walitamani kupiga vigelegele lakini
haikuwa hivyo. Wengi wao waliachwa na
makovu yasiyofutika, machozi ya kumbukumbu
mbaya ya mtu huyo, ama aliwaua ndugu zao au
alichoma moto nyumba zao.
“Hakuna marefu yasiyo na ncha,” mwananchi
mmoja alikuwa akiwaambia wenziwake pindi
alipokuwa akiiacha luninga iliyokuwa ikionesha
habari hiyo mapema asubuhi.
§§§§§

BAADA YA SIKU 2

Joru na Jack walirudi katika hali zao za
kawaida, wote walikuwa na furaha hasa baada
ya kuitimiza azma hiyo iliyokuwa ikimtesa kila
mmoja moyoni kwa jinsi zake. Jack alihesabu
pesa zilizokuwa ndani ya fuko lile, si haba pesa
ilikuwa ni nyingi ya kutosha. Akamwambia Joru
jinsi alivyoipata pesa hiyo nyumbani kwa
Malyamungu.
“Safi sana Jack, pesa hii itajenga maisha yako,
usirudi tena Uganda, tafuta ardhi na kujenga
hapa kisha fanya miradi yako, mke na mtoto
utawafuata au utawaita waje waungane nawe
katika maisha mapya,” Jack alimtazama Joru
kwa kumkazia macho. Akasimama na
kumkumbatia rafikiye huyo ambaye urafiki wao
ulikuwa ni wa siku sita tu mpaka hapo lakini
tayari walikwishafanya mambo makubwa.
Baada ya siku hiyo Joru alirudi nyumbani na
kuungana tena na family ya Shibagenda, Kemi
hakuamini kama mpenziwe huyo karudi salama.
Siku hiyo alimkuta mzee Shibagenda mwenyewe
nyumbani.
“Joru, wewe ni mwanaume sasa, ulilolifanya
nimelisikia, hongera sana, umekomaa,”
Shibagenda akampongeza Joru.
Haikupita muda mrefu, mipango ya ndoa na ya
Joru na Kemi ikaanza ndani ya familia ya
Shibagenda. Kabla ya ndoa hiyo Joru akiwa na
Kemi pamoja na mtoto wao walikwenda kuzuru
eneo ambalo kijiji chao kilikuwapo. Joru
alisimama juu ya kilima kidogo akitazama
vichaka vya migomba na mikahawa
vilivyobadilisha taswira ya eneo hilo. Joru
akaangukwa na machozi, akamtazama Kemi,
akamtazama mwanawe.
“Baba, uliniachia risasi 4, nimezitumia kama
ulivyofikiri, nimekuja hapa kukwambia wewe,
mama yangu pamoja na majirani wote ambao
roho zao zilidhurumiwa na Malyamungu, Kazi
mliyonituma nimeimaliza”.

«««« MWISHO »»»»

Mkuu Willy Gamba 1, tayri nimemaliza riwaya hii. kuna jamaa yetu kwenye jukwa hili aliahidi kutuletea nyingine ya Kijasho na nini vile? naisubiria.

kuna raha ya ajabu kusoma riwaya kwa mfululizo hadi kuimaliza. visa vimejipanga vema na inasisimua.

baada ya liike mkuu, nikupongeze kwa kutuletea burudani mkuu Willy Gamba 1
 
Back
Top Bottom