Decree Holder
JF-Expert Member
- Jul 19, 2015
- 2,559
- 3,748
Wanabodi karibuni sana twende pamoja kwenye Riwaya hii:
JINA : PENZI HARAMU
MWANDISHi: ZAWADI B LUPELO
Karibu
SEHEMU YA KWANZA
Ndani ya ukumbi wa Black Lord Hall majira ya usiku watu wa kila aina wakiwa wamefurika, wakiwa wamechachawa waliojawa na taharuki,
“Hivi kweli Amani anamwoa Liya?” Aliuliza mmoja wa wageni waalikwa.
Hakuna aliyekuwa anaamini, katika mazingira ya sasa, katika jamii ya sasa ya kitanzania. Jamii inayoshikilia maadili, mila na desturi kama vile mtoto aliye mgongoni amshikiliavyo mama yake, ni jambo la ajabu na isingetegemewa Amani na Liya kuoana. Inawezekanaje? Na nini hatima yake? Hii ndoa itafika wapi? Maswala haya na mengine mengi yaligonga vichwa vya wageni waalikwa waliobahatika kuhudhuria harusi ile ya aina yake.
Watu walikuwa wamekaa kitako mithili ya watu wanaosubiri siku ya unyakuo wa Yesu Kristo, siku ile ambayo tunaambiwa watu wote tutaota mbawa na kupaa kama ndege. Ni watu wenye shauku kuu, furaha, huzuni, mshangao, masikitiko na kila aina ya hisia ziliwagubika wahudhuriaji kila mmoja na hisia yake. Wapo waliosema ndoa ile ni chukizo mbele za Mungu, wakasema Biblia imekataza, Koran hairuhusu, serikali haipendi! Mila zimekiukwa!. Kila mwenye lake lilimtoka kama ilivyo kawaida ya walimwengu.
Baada ya muda mfupi minong'ono ikajaa mule ukumbini sauti zikawa nyingi zikikinzana hakukuwa na shaka kuwa ilikuwa ni mijadala juu ya ile ndoa,
“Hallow! Hallow! Mabibi na mabwana” alisikika mshereheshaji wa sherehe wenyewe wanamwita MC
“Nitaomba tusimame wakati maharusi wakiwa wanaingia ukumbini”
Watu wote walisimama mwenye kigelegele chake alipiga, mwenye kusonya alisonya, mwenye kucheka alicheka mwenye kulaani hivyo hivyo. Ilikuwa ni harusi ya tofauti kwani harusi zilizo nyingi tunatengemea watu kuwa na hisia moja ya furaha na bashasha lakini harusi ya Amani na Liya ilikuwa ya tofauti sana kwani iliwagawa watu kihisia. Muziki uliwashwa kwa sauti ya juu zaidi wakati maharusi wakiwa wanaingia ukumbini. Naam! Amani na Liya wakiwa wameshikana mikono wakicheza taratibu huku wanajongea ndani kwa mwendo wa mnato
“Mabibi na mabwana vigelegele tafadhali!” alisikika mshereheshaji maarufu kwa jina la MC Oscar.
Basi vigelegele vikazidi mle ukumbini kana kwamba kila jambo lipo sawa. Amani na Liya wakiwa wameshaingia ndani walicheza taratibu kuelekea kwenye meza walizoandaliwa maharusi.
Liya alikuwa ni binti mrembo sana mwenye urefu wa wastani, mweupe si mweupe, mweusi si mweusi mwenye rangi iliyotulia. Mnene si mnene mwenye umbo la wastani, anavutia kumtazama, amepambwa akapambika. Wakati wanacheza na kujongea vilipo viti vyao macho ya Amani wakati wote yapo kwa Liya akimwangalia kwa jicho la huba, basi Liya akitabasamu ni raha tupu mithili ya watu waliopo peponi. Wanaonekana ni vijana wadogo wanaofurahia ndoa yao changa ikiwa ina masaa machache toka kufungwa kwake.
Baada ya Amani na Liya wakiwa wameshachukua nafasi na sherehe ikiwa inaendelea, MC aliruhusu burudani kidogo kutoka kwa kikundi cha vichekesho cha Negro Comedians ambao walikuwa ni vijana wanaochipukia kwenye sanaa jijini Dar es salaam chini ya kijana maarufu Amali Said. Wakati sherehe ikiendelea Amani alivitazama viti vilivyokuwa mbele yake ni vitupu ni viti walivyokuwa wameandaliwa wazazi wa maharusi yaani wazazi wa Amani na Liya au tuseme walezi. Viti vilikuwa vitupu hakuna mzazi au mlezi aliyehudhuria ukumbi ulijazwa na ndugu na jamaa na marafiki wengine. Hili jambo lilimshughulisha mno Amani akachukuliwa ghafla na mawazo akatuama mawazoni kwa muda akavuta pumzi
"kwanini lakini?” Alijiuliza Amani hakupata jibu ya maswali yote yaliyokizonga kichwa chake.
“Nimekosa nini kwa Mungu?”
“Eeh Mungu wangu niongoze mimi mwanzo” Amani alisali kimoyomoyo.
Amani akiwa ametuama mawazoni
sherehe ikiwa inaendelea zilisikika kelele zikitokea upande wa mlangoni.
“Kuna nini huko mlangoni?” aling'aka mshereheshaji.
Ilikuwa ni watu wanne waliovalia nguo za kipolisi waking'ang'ania kuingia ndani kwa ulazima. Punde si punde walifanikiwa kuingia ndani baada ya kuishinda kamati ya ulinzi ya sherehe ile pale malangoni mwa ukumbi. “ MC tunaomba maiki DJ zima muziki haraka”aliamrisha kwa ubabe na kwa sauti ya kukoroma Afande Hashimu.
MC Oscar alimkabidhi maiki na baada ya muziki kuwa umezimwa
“Huu ndiyo mwisho wa sherehe hii haramu na maharusi mpo chini ya ulinzi”
Amani alisimama na kusogea akijaribu kutaka kuongea na Hashimu “Afande naomba hao wanandoa haramu wakamatwe mara moja wapo chini ya ulinzi” aliamuru Afande Hashimu.
“Lakini…lakini…Afande…” Amani alikatishwa
“Haya mpo chini ya ulinzi maelezo yote kituoni”Aliongea Afande mmoja huku akimtia pingu Amani.
Amani na Liya walitiwa nguvuni ilikuwa ni usiku wa saa tano ndiyo kwanza sherehe imeanza kuchanganya. Polisi waliwatia pingu mikononi Amani na Liya huku wakiwakokota kama majambazi wa kutumia silaha. Waliwatoa nje na kuwapeleka kwenye gari yao ya polisi. Ndani ya ukumbi tahaluki ikazidi maneno yakawa mengi kila mtu akaongea lake,
“nilijua tu chezeya jamhuri weye hehehe heee!” Alisikika akiongea kwa kebehi moja ya mgeni mwalikwa aliyekuwa amekaa karibu na mlango wenyewe wanamwita “malkia wa kuchamba”
Shoga weee halo haloo! Teeena” alidakia jirani yake maarufu kwa jina la “mama pilikapilika”
Basi hali ndivyo ilivyokuwa mle ndani. Siku zote mambo yakikwendea kombo siyo wote watakaosikitika wengine watafurahi sana. Hivyo ndivyo ilivyokuwa kwa Amani wapo waliosema alikuwa anajidai polisi kiko wapi kakamatwa na polisi wenzie. Wengine wakatoa unabii wakisema “tulijua tu Amani na Liya hii ndoa haramu haitawaacha salama”.
Ikawa ilivyokuwa Mwenye lake alisema, mwenye kusikitika hivyo hivyo mithili ya bahari ya Hindi kila mtu anaogelea kwa namna yake.
ITAENDELEA
JINA : PENZI HARAMU
MWANDISHi: ZAWADI B LUPELO
Karibu
SEHEMU YA KWANZA
Ndani ya ukumbi wa Black Lord Hall majira ya usiku watu wa kila aina wakiwa wamefurika, wakiwa wamechachawa waliojawa na taharuki,
“Hivi kweli Amani anamwoa Liya?” Aliuliza mmoja wa wageni waalikwa.
Hakuna aliyekuwa anaamini, katika mazingira ya sasa, katika jamii ya sasa ya kitanzania. Jamii inayoshikilia maadili, mila na desturi kama vile mtoto aliye mgongoni amshikiliavyo mama yake, ni jambo la ajabu na isingetegemewa Amani na Liya kuoana. Inawezekanaje? Na nini hatima yake? Hii ndoa itafika wapi? Maswala haya na mengine mengi yaligonga vichwa vya wageni waalikwa waliobahatika kuhudhuria harusi ile ya aina yake.
Watu walikuwa wamekaa kitako mithili ya watu wanaosubiri siku ya unyakuo wa Yesu Kristo, siku ile ambayo tunaambiwa watu wote tutaota mbawa na kupaa kama ndege. Ni watu wenye shauku kuu, furaha, huzuni, mshangao, masikitiko na kila aina ya hisia ziliwagubika wahudhuriaji kila mmoja na hisia yake. Wapo waliosema ndoa ile ni chukizo mbele za Mungu, wakasema Biblia imekataza, Koran hairuhusu, serikali haipendi! Mila zimekiukwa!. Kila mwenye lake lilimtoka kama ilivyo kawaida ya walimwengu.
Baada ya muda mfupi minong'ono ikajaa mule ukumbini sauti zikawa nyingi zikikinzana hakukuwa na shaka kuwa ilikuwa ni mijadala juu ya ile ndoa,
“Hallow! Hallow! Mabibi na mabwana” alisikika mshereheshaji wa sherehe wenyewe wanamwita MC
“Nitaomba tusimame wakati maharusi wakiwa wanaingia ukumbini”
Watu wote walisimama mwenye kigelegele chake alipiga, mwenye kusonya alisonya, mwenye kucheka alicheka mwenye kulaani hivyo hivyo. Ilikuwa ni harusi ya tofauti kwani harusi zilizo nyingi tunatengemea watu kuwa na hisia moja ya furaha na bashasha lakini harusi ya Amani na Liya ilikuwa ya tofauti sana kwani iliwagawa watu kihisia. Muziki uliwashwa kwa sauti ya juu zaidi wakati maharusi wakiwa wanaingia ukumbini. Naam! Amani na Liya wakiwa wameshikana mikono wakicheza taratibu huku wanajongea ndani kwa mwendo wa mnato
“Mabibi na mabwana vigelegele tafadhali!” alisikika mshereheshaji maarufu kwa jina la MC Oscar.
Basi vigelegele vikazidi mle ukumbini kana kwamba kila jambo lipo sawa. Amani na Liya wakiwa wameshaingia ndani walicheza taratibu kuelekea kwenye meza walizoandaliwa maharusi.
Liya alikuwa ni binti mrembo sana mwenye urefu wa wastani, mweupe si mweupe, mweusi si mweusi mwenye rangi iliyotulia. Mnene si mnene mwenye umbo la wastani, anavutia kumtazama, amepambwa akapambika. Wakati wanacheza na kujongea vilipo viti vyao macho ya Amani wakati wote yapo kwa Liya akimwangalia kwa jicho la huba, basi Liya akitabasamu ni raha tupu mithili ya watu waliopo peponi. Wanaonekana ni vijana wadogo wanaofurahia ndoa yao changa ikiwa ina masaa machache toka kufungwa kwake.
Baada ya Amani na Liya wakiwa wameshachukua nafasi na sherehe ikiwa inaendelea, MC aliruhusu burudani kidogo kutoka kwa kikundi cha vichekesho cha Negro Comedians ambao walikuwa ni vijana wanaochipukia kwenye sanaa jijini Dar es salaam chini ya kijana maarufu Amali Said. Wakati sherehe ikiendelea Amani alivitazama viti vilivyokuwa mbele yake ni vitupu ni viti walivyokuwa wameandaliwa wazazi wa maharusi yaani wazazi wa Amani na Liya au tuseme walezi. Viti vilikuwa vitupu hakuna mzazi au mlezi aliyehudhuria ukumbi ulijazwa na ndugu na jamaa na marafiki wengine. Hili jambo lilimshughulisha mno Amani akachukuliwa ghafla na mawazo akatuama mawazoni kwa muda akavuta pumzi
"kwanini lakini?” Alijiuliza Amani hakupata jibu ya maswali yote yaliyokizonga kichwa chake.
“Nimekosa nini kwa Mungu?”
“Eeh Mungu wangu niongoze mimi mwanzo” Amani alisali kimoyomoyo.
Amani akiwa ametuama mawazoni
sherehe ikiwa inaendelea zilisikika kelele zikitokea upande wa mlangoni.
“Kuna nini huko mlangoni?” aling'aka mshereheshaji.
Ilikuwa ni watu wanne waliovalia nguo za kipolisi waking'ang'ania kuingia ndani kwa ulazima. Punde si punde walifanikiwa kuingia ndani baada ya kuishinda kamati ya ulinzi ya sherehe ile pale malangoni mwa ukumbi. “ MC tunaomba maiki DJ zima muziki haraka”aliamrisha kwa ubabe na kwa sauti ya kukoroma Afande Hashimu.
MC Oscar alimkabidhi maiki na baada ya muziki kuwa umezimwa
“Huu ndiyo mwisho wa sherehe hii haramu na maharusi mpo chini ya ulinzi”
Amani alisimama na kusogea akijaribu kutaka kuongea na Hashimu “Afande naomba hao wanandoa haramu wakamatwe mara moja wapo chini ya ulinzi” aliamuru Afande Hashimu.
“Lakini…lakini…Afande…” Amani alikatishwa
“Haya mpo chini ya ulinzi maelezo yote kituoni”Aliongea Afande mmoja huku akimtia pingu Amani.
Amani na Liya walitiwa nguvuni ilikuwa ni usiku wa saa tano ndiyo kwanza sherehe imeanza kuchanganya. Polisi waliwatia pingu mikononi Amani na Liya huku wakiwakokota kama majambazi wa kutumia silaha. Waliwatoa nje na kuwapeleka kwenye gari yao ya polisi. Ndani ya ukumbi tahaluki ikazidi maneno yakawa mengi kila mtu akaongea lake,
“nilijua tu chezeya jamhuri weye hehehe heee!” Alisikika akiongea kwa kebehi moja ya mgeni mwalikwa aliyekuwa amekaa karibu na mlango wenyewe wanamwita “malkia wa kuchamba”
Shoga weee halo haloo! Teeena” alidakia jirani yake maarufu kwa jina la “mama pilikapilika”
Basi hali ndivyo ilivyokuwa mle ndani. Siku zote mambo yakikwendea kombo siyo wote watakaosikitika wengine watafurahi sana. Hivyo ndivyo ilivyokuwa kwa Amani wapo waliosema alikuwa anajidai polisi kiko wapi kakamatwa na polisi wenzie. Wengine wakatoa unabii wakisema “tulijua tu Amani na Liya hii ndoa haramu haitawaacha salama”.
Ikawa ilivyokuwa Mwenye lake alisema, mwenye kusikitika hivyo hivyo mithili ya bahari ya Hindi kila mtu anaogelea kwa namna yake.
ITAENDELEA