Bishop Hiluka
R I P
- Aug 12, 2011
- 7,150
- 14,724
Moyo wa Mama!
Na Bishop Hiluka
ZAWADI, msichana mwembamba mrefu, akiwa na urefu wa futi tano na inchi kumi na mwenye umbile lililovutia mno alikuwa anatembea taratibu kando kando ya barabara ya SUA, barabara inayoelekea katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo.
Zawadi alikuwa anatokea kwenye mzunguko uliokuwa unaziunganisha barabara za Sua, Madaraka na ile inayoelekea eneo la Uwanja wa Ndege katika manispaa ya Morogoro.
Kwa mwonekano tu Zawadi alionekana kuwa na umri wa miaka 25. Nywele zake zilikuwa nyeusi tii zilizotumwa vema sambamba na sura yake iliyokuwa na mvuto wa asilimia mia moja. Nyusi na kope zake zilikuwa ndefu zilizong’ara na kuyafanya macho yake yawe wazi nusu.
Pua yake ilikuwa ndogo kiasi iliyoiacha midomo yake ijidai kwa kuhifadhi meno meupe yaliyojipanga vizuri huku yakiachia kijiuwazi kidogo kwa mbele. Alikuwa mweupe mithili ya chotara, lakini si ule weupe wa mkorogo bali weupe wa asili wenye ung’avu wa kuteleza.
Alikuwa na shingo nzuri iliyokaa vyema katikati ya mabega yake ya kike mazuri na kifua chake kilibeba matiti ya wastani yaliyochongoka mbele na yaliyokuwa na hasira ya kutoboa gauni alilovaa. Tumbo lake lilikuwa flati na kiuno chake kilikuwa chembamba mithili ya dondola.
Katika muda ule wa asubuhi Zawadi alitembea taratibu huku akiwa kainamisha kichwa chake. Alionekana kuchoka sana na mwenye mawazo mengi.
Mkono wake wa kulia alikuwa amebeba kikapu kilichokuwa na bidhaa mbalimbali ndani yake alizotoka kuzinunua katika soko kuu la manispaa ya Morogoro, na mkono wake wa kushoto alikuwa kauzungusha kwa nyuma.
Zawadi alitazama huku na kule na kushusha pumzi ndefu za ndani kwa ndani huku akikunja sura yake kana kwamba alihisi maumivu makali ya kichwa na kutupa macho yake kuwatazama watu wachache aliopishana nao wakiwa katika haraka za kuwahi mishemishe asubuhi ile.
Aliwatazama wale watu kwa makini, wengi walionekana ni wenye furaha katika asubuhi ile, lakini yeye alijiona kuwa mpweke na mnyonge. Hakujua ni kwa nini alijihisi upweke na nini kilikuwa kimemnyang’anya furaha yake katika asubuhi ile! Alitafakari sana lakini hakupata jibu!
Watoto wawili watatu walikuwa wanakimbizana kando kando ya barabara ile ya Sua wakicheza na kumpita. Mmoja wa watoto hao alimkumba Zawadi lakini binti yule alimwangalia tu bila kuonesha hisia zozote za kukerwa, bali aliendelea kutembea taratibu pasipo kujishughulisha na watoto hao.
Alipita jirani na Kambarage Bar and Garden iliyokuwa upande ule wa kushoto kwake kando ya barabara ya SUA na kuwatupia jicho watu wachache waliokuwa wameketi kwenye viti vya plastiki chini ya miti ya vivuli wakiwa na chupa za bia.
Nyuma ya baa hiyo ilionekana mandhali ya uwanda mpana wenye eneo kubwa lenye miti mikubwa kwa midogo na uwanja wa mpira wa Shule ya Msingi Kikundi.
Mbele ya uwanda huo mpana wenye miti kuna mto Kikundi unaokatiza katika soko la Manispaa ya Morogoro na kwenda kumwaga maji yake katika mto Mafisa.
Kwenye mandhali hiyo nzuri ya bustani katika baa ya Kambarage, kijana mmoja mtanashati alikuwa akimwita Zawadi lakini yeye hakumjali. Aliendelea kutembea taratibu pasipo kujihusisha na mtu mwingine.
Mbele kidogo ya baa ya Kambarage upande huohuo wa kushoto alilipita soko dogo la Kikundi lililo kando kando ya barabara ya Sua, soko lile lilikuwa limesambaa katika uwanda mpana wenye miti uliosambaa hadi katika mto Kikundi na Shule ya Msingi Kikundi.
Zawadi aliwapita wachuuzi kadhaa wa mboga, matunda, vitafunwa vya aina mbalimbali na bidhaa zingine kando ya eneo la soko la Kikundi, hakujihusisha nao kabisa, bali alionekana kuzama kwenye lindi mawazo.
Wakati akipita kando ya miti mikubwa aliwaona ndege wa kila aina waliokuwa wakilia kwa namna ya kuisifia asubuhi hiyo na kuifanya kuwa njema, ingawa kwake aliiona haikuwa njema kabisa. Tena ndege hao walionekana kuwa ni wenye furaha kubwa na kulipa uhai eneo lote lililoonekana tulivu mno.
Alijikuta akisimama kwa muda kuwasikiliza ndege hao kwa makini, akajaribu kubashiri nyimbo nzuri walizokuwa wakiimba, akayasikia hadi maneno yaliyotamkwa katika nyimbo hizo ambayo ki ukweli yalibeba ujumbe mzuri wa faraja. Alijikuta akishusha pumzi ndefu akionekana kufarijika kidogo.
Alitabasamu na kuanza kutembea kando kando akiifuata barabara ya Sua inayoelekea Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine, safari hii aliongeza mwendo kidogo akionekana kupata nguvu mpya.
Hakwenda mbali zaidi akasita na kuyakaza macho yake kutazama mbele yake. Kundi la watu, wakubwa kwa wadogo, wake kwa waume walikuwa wakiifuata ngoma ya Vanga iliyokuwa inatokea eneo la Msufini na kuja kwenye uelekeo wake.
Kundi hilo la watu lilimvuka Zawadi huku wakitimua vumbi utadhani ni msafara wa nyumbu wanaohama kutoka mbuga ya Serengeti na kuvuka mpaka wakiingia Kenya. Walikuwa wanarukaruka na kunengua viuno kwa furaha huku wakiimba kufuatisha midundo ya ngoma kubwa iliyokuwa ikipigwa.
Kundi hilo la watu walikuwa wanachutama na kuinuka kila walipokuwa wanaimba kiitikio cha ‘Nimeokota kidude!’
Itaendelea...
Na Bishop Hiluka
ZAWADI, msichana mwembamba mrefu, akiwa na urefu wa futi tano na inchi kumi na mwenye umbile lililovutia mno alikuwa anatembea taratibu kando kando ya barabara ya SUA, barabara inayoelekea katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo.
Zawadi alikuwa anatokea kwenye mzunguko uliokuwa unaziunganisha barabara za Sua, Madaraka na ile inayoelekea eneo la Uwanja wa Ndege katika manispaa ya Morogoro.
Kwa mwonekano tu Zawadi alionekana kuwa na umri wa miaka 25. Nywele zake zilikuwa nyeusi tii zilizotumwa vema sambamba na sura yake iliyokuwa na mvuto wa asilimia mia moja. Nyusi na kope zake zilikuwa ndefu zilizong’ara na kuyafanya macho yake yawe wazi nusu.
Pua yake ilikuwa ndogo kiasi iliyoiacha midomo yake ijidai kwa kuhifadhi meno meupe yaliyojipanga vizuri huku yakiachia kijiuwazi kidogo kwa mbele. Alikuwa mweupe mithili ya chotara, lakini si ule weupe wa mkorogo bali weupe wa asili wenye ung’avu wa kuteleza.
Alikuwa na shingo nzuri iliyokaa vyema katikati ya mabega yake ya kike mazuri na kifua chake kilibeba matiti ya wastani yaliyochongoka mbele na yaliyokuwa na hasira ya kutoboa gauni alilovaa. Tumbo lake lilikuwa flati na kiuno chake kilikuwa chembamba mithili ya dondola.
Katika muda ule wa asubuhi Zawadi alitembea taratibu huku akiwa kainamisha kichwa chake. Alionekana kuchoka sana na mwenye mawazo mengi.
Mkono wake wa kulia alikuwa amebeba kikapu kilichokuwa na bidhaa mbalimbali ndani yake alizotoka kuzinunua katika soko kuu la manispaa ya Morogoro, na mkono wake wa kushoto alikuwa kauzungusha kwa nyuma.
Zawadi alitazama huku na kule na kushusha pumzi ndefu za ndani kwa ndani huku akikunja sura yake kana kwamba alihisi maumivu makali ya kichwa na kutupa macho yake kuwatazama watu wachache aliopishana nao wakiwa katika haraka za kuwahi mishemishe asubuhi ile.
Aliwatazama wale watu kwa makini, wengi walionekana ni wenye furaha katika asubuhi ile, lakini yeye alijiona kuwa mpweke na mnyonge. Hakujua ni kwa nini alijihisi upweke na nini kilikuwa kimemnyang’anya furaha yake katika asubuhi ile! Alitafakari sana lakini hakupata jibu!
Watoto wawili watatu walikuwa wanakimbizana kando kando ya barabara ile ya Sua wakicheza na kumpita. Mmoja wa watoto hao alimkumba Zawadi lakini binti yule alimwangalia tu bila kuonesha hisia zozote za kukerwa, bali aliendelea kutembea taratibu pasipo kujishughulisha na watoto hao.
Alipita jirani na Kambarage Bar and Garden iliyokuwa upande ule wa kushoto kwake kando ya barabara ya SUA na kuwatupia jicho watu wachache waliokuwa wameketi kwenye viti vya plastiki chini ya miti ya vivuli wakiwa na chupa za bia.
Nyuma ya baa hiyo ilionekana mandhali ya uwanda mpana wenye eneo kubwa lenye miti mikubwa kwa midogo na uwanja wa mpira wa Shule ya Msingi Kikundi.
Mbele ya uwanda huo mpana wenye miti kuna mto Kikundi unaokatiza katika soko la Manispaa ya Morogoro na kwenda kumwaga maji yake katika mto Mafisa.
Kwenye mandhali hiyo nzuri ya bustani katika baa ya Kambarage, kijana mmoja mtanashati alikuwa akimwita Zawadi lakini yeye hakumjali. Aliendelea kutembea taratibu pasipo kujihusisha na mtu mwingine.
Mbele kidogo ya baa ya Kambarage upande huohuo wa kushoto alilipita soko dogo la Kikundi lililo kando kando ya barabara ya Sua, soko lile lilikuwa limesambaa katika uwanda mpana wenye miti uliosambaa hadi katika mto Kikundi na Shule ya Msingi Kikundi.
Zawadi aliwapita wachuuzi kadhaa wa mboga, matunda, vitafunwa vya aina mbalimbali na bidhaa zingine kando ya eneo la soko la Kikundi, hakujihusisha nao kabisa, bali alionekana kuzama kwenye lindi mawazo.
Wakati akipita kando ya miti mikubwa aliwaona ndege wa kila aina waliokuwa wakilia kwa namna ya kuisifia asubuhi hiyo na kuifanya kuwa njema, ingawa kwake aliiona haikuwa njema kabisa. Tena ndege hao walionekana kuwa ni wenye furaha kubwa na kulipa uhai eneo lote lililoonekana tulivu mno.
Alijikuta akisimama kwa muda kuwasikiliza ndege hao kwa makini, akajaribu kubashiri nyimbo nzuri walizokuwa wakiimba, akayasikia hadi maneno yaliyotamkwa katika nyimbo hizo ambayo ki ukweli yalibeba ujumbe mzuri wa faraja. Alijikuta akishusha pumzi ndefu akionekana kufarijika kidogo.
Alitabasamu na kuanza kutembea kando kando akiifuata barabara ya Sua inayoelekea Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine, safari hii aliongeza mwendo kidogo akionekana kupata nguvu mpya.
Hakwenda mbali zaidi akasita na kuyakaza macho yake kutazama mbele yake. Kundi la watu, wakubwa kwa wadogo, wake kwa waume walikuwa wakiifuata ngoma ya Vanga iliyokuwa inatokea eneo la Msufini na kuja kwenye uelekeo wake.
Kundi hilo la watu lilimvuka Zawadi huku wakitimua vumbi utadhani ni msafara wa nyumbu wanaohama kutoka mbuga ya Serengeti na kuvuka mpaka wakiingia Kenya. Walikuwa wanarukaruka na kunengua viuno kwa furaha huku wakiimba kufuatisha midundo ya ngoma kubwa iliyokuwa ikipigwa.
Kundi hilo la watu walikuwa wanachutama na kuinuka kila walipokuwa wanaimba kiitikio cha ‘Nimeokota kidude!’
Itaendelea...