HaMachiach
JF-Expert Member
- Dec 15, 2015
- 3,444
- 6,201
MTUNZI Amata Gaimba
Sehemu 1
SEHEMU FULANI HUKO AFRIKA MAGAHARIBI
MACHO YANGU yalikuwa mazito sana kiasi kwamba iliniwia ngumu kuyafumbua. Haikuwa rahisi kwangu, nilijaribu kutumia nguvu ya mwisho niliyonayo kuona japo nuru, haikuwezekana. Fahamu zilipokaa sawa nikahisi maumivu makali sana kisogoni, nikajaribu kuinua mkono ili japo kushika eneo hilo la mwili. Damu! Damu iliyoanza kuganda na kufanya kama buja zito iligandamana na nywele zangu, nilipopapasa zaidi nikagundua kuwa nina mpasuko au niite mchaniko.
Bado giza nene liliyafanya macho yangu yashindwe kuona chochote, mboni zilifunguka na kufunguka lakini kuiona nuru ilikuwa ndoto.
Niko wapi? Nikajiuliza, hakukuwa na wa kunijibu zaidi ya mvumo wa giza kuyapa taabu masikio yangu. Maumivu ya jeraha langu la kisogoni yakaanza kuhisika kwa mbali, nikahisi kama moyo umehamia hapo kwa jinsi ulivyokuwa ukipwita. Kila nukta ya sekunde iliyopita, maumivu yake yalizidi nikaanza kuhisi kero, nikajaribu kujigeuza, kichwa kizito, nilipotumia nguvu zote kujigeuza nikahisi kugonga vitu vigumu kama kuni zilizorundikwa lakini kwa mpangilio maalumu. Nikatulia kwa sekunde chache huku nikijaribu kuvuta hisia kutambua ni nini nimekigonga. Nikainua mkono na kupapasa, sikujua kama nimeshika fimbo au kota la kutungulia embe. Nikapapasa ka sentimeta kadhaa, mara nikahisi kitu ambacho sikukitegemea, mwisho wa kile nilichokipapasa nikahisi nimeshika kitanga cha mkono wa mwanadamu, nikakipapasa vyema nikajiridhisha kuwa ndiyo ni kitanga cha mkono lakini kimebaki mifupa tupu.
Nikachezesha mguu wangu nao ukagonga vitu vingine kama hivyo, ndipo nikagundua kuwa hata maumivu mengine ninayoyasikia ni kwa sababu nimelalia mifupa ya binadamu iliyojaa katika eneo hilo.
“Shiiiit!!!!” nikang’aka kwa sauti, kisha nikajiinua kuketi, kiuno changu nacho kikagosha kwa nguvu. Hapo nikagundua kuwa hta kiuno nacho kimepata tabu kidogo. Nikavumilia na kufanikiwa kuketi, kila nilipogusa na kushika kulikuwa na mifupa tu, mafuvu nayo niliyapapasa kama vifuu vya nazi. Sikuweza kuona kwa macho yangu kutokana na giza nene katika eneo hilo. Kila sekunde iliyopita nilizidi kuipata hali halisi ya ndani humo, harufu ya mauti ilitapakaa.
Wakiua huwa wanatupa maiti humu! Nikawaza.
Ina maana hata mimi walijua nimekufa? Nikajiuliza. Zaidi ya hapo sikuwa na lingine la kufanya zaidi ya kuutafuta kama ni ukuta au ni kitu gani kinachofanya miimo ya eneo hilo. Maumivu yalinizidi katika kisogo change kiasi kwamba iliniwia ngumu kuvumilia. Nikatambaa kwa shida nikiparamia mifupa na skeleton za binadamu, na kwa sababu nilikuwa sioni niendako nikajikuta na jigonga kwenye ukuta. Nikatulia na kuanza kuupapasa huku nikiugulia kwa maumivu. Ukuta ulikuwa laini na wa kutereza, wenye vitu kama marumaru kwa jinsi vilivyounganishwa, nikaupapasa na kufanikiwa kusimama lakini sikufikia juu, parefu.
Kaburi! Nikawaza na hapo nikaanza kupata kizunguzungu kwa sababu sikuwahi kuingia kaburini tangu nizaliwe, lakini mara hii nimezikwa mzima mzima? Nikajikuta naanguka kwa nguvu na kufikia juu ya miili iliyooza zamani maumivu yake hasa sehemu za kisogo changu yalizidi lakini nikazidi kuidhihirishia hali hiyo kuwa mimi ni mwanaume.
“Chwaaaa!!!! Chwaaaa!!!!” nikasikia mtu akipiga chafya, hii sasa ikanifanya nishikwe na hofu kuu. Pamoja na ukakamavu wangu na ujuvi wa upiganaji na kujilinda, nilijikuta Napata woga wa ajabu uliotiririka kutoka utosini mpaka unyayoni, moyo wangu ulikwenda mpio kama saa mbovu, macho ya kanitoka pima maana sikujua kama ni maiti imepata uhai, au ndiyo moja ya vitisho vya humu ndani au inakuaje, maana kwa mtindo huu mtu unaweza kufa kihoro. Tatizo kubwa sikuwa namwona mtu huyo au kiumbe hicho maana giza lilikuwa nene sana, joto nalo lilikuwa kali mno, nikajiinua na kutafuta kona ya ukuta huo kwa taabu nikaipata na kujiegama hapo nikisubiri hatima yangu.
“Kheeeee!!!!!” ile sauti ikakoroma, nikajiweka sawa, sasa nilijua nipo kwenye kona ya kaburi hilo, hata kama nitashambuliwa, basi shambulizi litatoka ndani ya nyuzi arobaini na tano tu, ningeweza kukabiliana nalo hata kama ni giza. Nilianza kuvuta hisia ambazo nilifundishwa na Master wangu wakati nipo Japan kwenye mafunzo magumu sana ya Karate huku nikiwa nimefungwa kitambaa usoni, jinsi ya kumhisi adui yuko upande gani, kusikiliza mgongano wa hewa na kujua adui anatumia pigo gani, kumwona adui ndani ya hisia ya sita.
“Chwaaaa! Khaaaaa!!!!” chafya nikasisikia tena na mkhoromo ukafuatia, safari hii sikuogopa, ila nilikuwa nimelowa jasho na hewa nzito ndani humo ilianza kunishinda taratibu na kujihisi kuchoka. Njaa nayo ikaendelea kuleta upinzani mkubwa. Mara ule mkhoromo ukaendelea sasa ukaanza kuyasumbua masikio yangu, nikagundua huyo ni mwanadamu ambaye amefika dakika za mwisho za uhai wake.
Anakufa? Nikajiuliza, kwa kuwa nilishajua ni upande gani alipo huyo akoromaye, nikainuka haraka na kaukanyaga mifupa na miili mikavu mpaka pale nilipohisi, naam ndipo. Nikajikuta nimepiga magoti na kuanza kumtikisa huyo mtu, mikono yangu nikahisi imeshika kitu kama koti la suti, nikamtikisa na kumtikisa, yeye akazidi kukoroma tu. Nikampapasa usoni nikahisi kuwa ana majeraha mengi na ya kutisha kani nilihisi nashika mtu asiye na macho. Yule mtu aliye kufani akanishika mkono kwa nguvu zake zote na kuupachika katika mkanda wa suruali yake kisha yeye mwenyewe akatulia kimya kabisa, mkono wake ukalegea, nikajua tayari andipela.
Hapo nikajikuta kwenye hofu kuu, hofu ya kifo, nikajikuta nimesahahu mateso yangu yote, na mawazo yangu yakawa juu ya mtu huyo. Akili iliporudi, nikaanza kumsachi kuanzia mifuko ya koti, shati lake na suruali. Katika mfuko wa ndani wa shati nikatoa kijitabu kidogo sana, sikuweza kukisoma kwani hapa nilikuwa natumia hisia tu kutambua vitu, katika viatu vyake baada ya kumvua nikatoa karatasi ambayo sikuweza kujua ni karatasi ya nini au gani. Nikakumbuka kuwa mtu huyu alipoushika mkono wangu kwa nguvu aliuweka kwenye mkanda wa kiunoni.
Inawezekana kuna ujumbe katika mkanda huo! Nikawaza na kuanza kuufungua kiunoni mwake nikautoa na kuushika mkononi. Ni mkanda tu wa ngozi wenye chuma kikubwa cha kuufungia kutoka upande huu kwenda huu.
Ujumbe gani upon a mkanda huu? Nikajiuliza, sikuwa na jibu, ambaye ningemuuliza, ameshakufa, sasa nafanyaje. Maumivu niliyoyasahau ghafla nikaanza kuyahisi upya kwa nguvu, joto kali, shati lote likawa chapachapa kwa jasho na suruali pia ikaanza kuwa katika hali hiyo. Nikatia kile kijitabu mfukoni na ile karatasi.
Vitanisaidia nini sasa, labda kama ningepata nuru ya kusoma au kuona ni vitu gani… nikajiambia kwa sauti ya moyoni kisha nikajiegemeza katika ukuta upande mwingine. Hapo nikahisi naishiwa nguvu kabisa, pumzi nazipata kwa taabu sana nikajua sasa muda wangu umekwisha, nikafunga mikono na kuanza kusali sala zangu za mwisho. Nikaomba kwa Mungu wangu, msamaha kwa yote niliyoyakosa, lakini nikamwachia kila kitu aamue yeye kwani yeye anajua kuwa yepi nimeyafanya kimakosa na yepi nilikuwa kazini. Japokuwa sikuwa nawaona wengine, kupitia sala zangu hizi nikawaomba msamaha wote.
Joto lilizidi kuwa kali, harufu nzito ya mauti ikaanza kuzisumbua upya pua zangu, giza nalo likawa adui mkubwa. Nikatulia kimya nikiwa nimejikunyata huku mikononi nikiwa nimeukamata mkanda wa yule marehemu aliyenitangulia. Kutoka moyoni nikahisi sauti ikinitaka kuufunga mkanda ule kiunoni, nikaipuuzia lakini baadae ikazidi kunisumbua, nikaamua kuitii hisia hii kwani ni moja ya kazi yetu kutii hisia ya sita na ndiyo intelijensia yenyewe. Nilikuwa naishiwa nguvu, nikaupachika kiunoni tu bila kuuweka kwenye lupsi za suruali kwani sikuwa na muda na nguvu hizo. Nikachuku mwisho huu na huu na kuukutanisha kisha nikaupachika kwa nguvu ili meno yake yaumane. Sekunde ileile nilipoupachika na yale meno kuumana, nikasikia mlipuko kutoka upande mmoja wa ukuta, vumbi likatawala ndani ya kaburi hilo, nikakohoa kwa nguvu sana, hali ilipotulia nikaona tundu la ukubwa wa mdomo wa pipa katika ukuta wa kushoto kwangu. Mwanga hafifu ukapenya ndani nikajua kuwa kwa hapo ningeweza
Sehemu 1
SEHEMU FULANI HUKO AFRIKA MAGAHARIBI
MACHO YANGU yalikuwa mazito sana kiasi kwamba iliniwia ngumu kuyafumbua. Haikuwa rahisi kwangu, nilijaribu kutumia nguvu ya mwisho niliyonayo kuona japo nuru, haikuwezekana. Fahamu zilipokaa sawa nikahisi maumivu makali sana kisogoni, nikajaribu kuinua mkono ili japo kushika eneo hilo la mwili. Damu! Damu iliyoanza kuganda na kufanya kama buja zito iligandamana na nywele zangu, nilipopapasa zaidi nikagundua kuwa nina mpasuko au niite mchaniko.
Bado giza nene liliyafanya macho yangu yashindwe kuona chochote, mboni zilifunguka na kufunguka lakini kuiona nuru ilikuwa ndoto.
Niko wapi? Nikajiuliza, hakukuwa na wa kunijibu zaidi ya mvumo wa giza kuyapa taabu masikio yangu. Maumivu ya jeraha langu la kisogoni yakaanza kuhisika kwa mbali, nikahisi kama moyo umehamia hapo kwa jinsi ulivyokuwa ukipwita. Kila nukta ya sekunde iliyopita, maumivu yake yalizidi nikaanza kuhisi kero, nikajaribu kujigeuza, kichwa kizito, nilipotumia nguvu zote kujigeuza nikahisi kugonga vitu vigumu kama kuni zilizorundikwa lakini kwa mpangilio maalumu. Nikatulia kwa sekunde chache huku nikijaribu kuvuta hisia kutambua ni nini nimekigonga. Nikainua mkono na kupapasa, sikujua kama nimeshika fimbo au kota la kutungulia embe. Nikapapasa ka sentimeta kadhaa, mara nikahisi kitu ambacho sikukitegemea, mwisho wa kile nilichokipapasa nikahisi nimeshika kitanga cha mkono wa mwanadamu, nikakipapasa vyema nikajiridhisha kuwa ndiyo ni kitanga cha mkono lakini kimebaki mifupa tupu.
Nikachezesha mguu wangu nao ukagonga vitu vingine kama hivyo, ndipo nikagundua kuwa hata maumivu mengine ninayoyasikia ni kwa sababu nimelalia mifupa ya binadamu iliyojaa katika eneo hilo.
“Shiiiit!!!!” nikang’aka kwa sauti, kisha nikajiinua kuketi, kiuno changu nacho kikagosha kwa nguvu. Hapo nikagundua kuwa hta kiuno nacho kimepata tabu kidogo. Nikavumilia na kufanikiwa kuketi, kila nilipogusa na kushika kulikuwa na mifupa tu, mafuvu nayo niliyapapasa kama vifuu vya nazi. Sikuweza kuona kwa macho yangu kutokana na giza nene katika eneo hilo. Kila sekunde iliyopita nilizidi kuipata hali halisi ya ndani humo, harufu ya mauti ilitapakaa.
Wakiua huwa wanatupa maiti humu! Nikawaza.
Ina maana hata mimi walijua nimekufa? Nikajiuliza. Zaidi ya hapo sikuwa na lingine la kufanya zaidi ya kuutafuta kama ni ukuta au ni kitu gani kinachofanya miimo ya eneo hilo. Maumivu yalinizidi katika kisogo change kiasi kwamba iliniwia ngumu kuvumilia. Nikatambaa kwa shida nikiparamia mifupa na skeleton za binadamu, na kwa sababu nilikuwa sioni niendako nikajikuta na jigonga kwenye ukuta. Nikatulia na kuanza kuupapasa huku nikiugulia kwa maumivu. Ukuta ulikuwa laini na wa kutereza, wenye vitu kama marumaru kwa jinsi vilivyounganishwa, nikaupapasa na kufanikiwa kusimama lakini sikufikia juu, parefu.
Kaburi! Nikawaza na hapo nikaanza kupata kizunguzungu kwa sababu sikuwahi kuingia kaburini tangu nizaliwe, lakini mara hii nimezikwa mzima mzima? Nikajikuta naanguka kwa nguvu na kufikia juu ya miili iliyooza zamani maumivu yake hasa sehemu za kisogo changu yalizidi lakini nikazidi kuidhihirishia hali hiyo kuwa mimi ni mwanaume.
“Chwaaaa!!!! Chwaaaa!!!!” nikasikia mtu akipiga chafya, hii sasa ikanifanya nishikwe na hofu kuu. Pamoja na ukakamavu wangu na ujuvi wa upiganaji na kujilinda, nilijikuta Napata woga wa ajabu uliotiririka kutoka utosini mpaka unyayoni, moyo wangu ulikwenda mpio kama saa mbovu, macho ya kanitoka pima maana sikujua kama ni maiti imepata uhai, au ndiyo moja ya vitisho vya humu ndani au inakuaje, maana kwa mtindo huu mtu unaweza kufa kihoro. Tatizo kubwa sikuwa namwona mtu huyo au kiumbe hicho maana giza lilikuwa nene sana, joto nalo lilikuwa kali mno, nikajiinua na kutafuta kona ya ukuta huo kwa taabu nikaipata na kujiegama hapo nikisubiri hatima yangu.
“Kheeeee!!!!!” ile sauti ikakoroma, nikajiweka sawa, sasa nilijua nipo kwenye kona ya kaburi hilo, hata kama nitashambuliwa, basi shambulizi litatoka ndani ya nyuzi arobaini na tano tu, ningeweza kukabiliana nalo hata kama ni giza. Nilianza kuvuta hisia ambazo nilifundishwa na Master wangu wakati nipo Japan kwenye mafunzo magumu sana ya Karate huku nikiwa nimefungwa kitambaa usoni, jinsi ya kumhisi adui yuko upande gani, kusikiliza mgongano wa hewa na kujua adui anatumia pigo gani, kumwona adui ndani ya hisia ya sita.
“Chwaaaa! Khaaaaa!!!!” chafya nikasisikia tena na mkhoromo ukafuatia, safari hii sikuogopa, ila nilikuwa nimelowa jasho na hewa nzito ndani humo ilianza kunishinda taratibu na kujihisi kuchoka. Njaa nayo ikaendelea kuleta upinzani mkubwa. Mara ule mkhoromo ukaendelea sasa ukaanza kuyasumbua masikio yangu, nikagundua huyo ni mwanadamu ambaye amefika dakika za mwisho za uhai wake.
Anakufa? Nikajiuliza, kwa kuwa nilishajua ni upande gani alipo huyo akoromaye, nikainuka haraka na kaukanyaga mifupa na miili mikavu mpaka pale nilipohisi, naam ndipo. Nikajikuta nimepiga magoti na kuanza kumtikisa huyo mtu, mikono yangu nikahisi imeshika kitu kama koti la suti, nikamtikisa na kumtikisa, yeye akazidi kukoroma tu. Nikampapasa usoni nikahisi kuwa ana majeraha mengi na ya kutisha kani nilihisi nashika mtu asiye na macho. Yule mtu aliye kufani akanishika mkono kwa nguvu zake zote na kuupachika katika mkanda wa suruali yake kisha yeye mwenyewe akatulia kimya kabisa, mkono wake ukalegea, nikajua tayari andipela.
Hapo nikajikuta kwenye hofu kuu, hofu ya kifo, nikajikuta nimesahahu mateso yangu yote, na mawazo yangu yakawa juu ya mtu huyo. Akili iliporudi, nikaanza kumsachi kuanzia mifuko ya koti, shati lake na suruali. Katika mfuko wa ndani wa shati nikatoa kijitabu kidogo sana, sikuweza kukisoma kwani hapa nilikuwa natumia hisia tu kutambua vitu, katika viatu vyake baada ya kumvua nikatoa karatasi ambayo sikuweza kujua ni karatasi ya nini au gani. Nikakumbuka kuwa mtu huyu alipoushika mkono wangu kwa nguvu aliuweka kwenye mkanda wa kiunoni.
Inawezekana kuna ujumbe katika mkanda huo! Nikawaza na kuanza kuufungua kiunoni mwake nikautoa na kuushika mkononi. Ni mkanda tu wa ngozi wenye chuma kikubwa cha kuufungia kutoka upande huu kwenda huu.
Ujumbe gani upon a mkanda huu? Nikajiuliza, sikuwa na jibu, ambaye ningemuuliza, ameshakufa, sasa nafanyaje. Maumivu niliyoyasahau ghafla nikaanza kuyahisi upya kwa nguvu, joto kali, shati lote likawa chapachapa kwa jasho na suruali pia ikaanza kuwa katika hali hiyo. Nikatia kile kijitabu mfukoni na ile karatasi.
Vitanisaidia nini sasa, labda kama ningepata nuru ya kusoma au kuona ni vitu gani… nikajiambia kwa sauti ya moyoni kisha nikajiegemeza katika ukuta upande mwingine. Hapo nikahisi naishiwa nguvu kabisa, pumzi nazipata kwa taabu sana nikajua sasa muda wangu umekwisha, nikafunga mikono na kuanza kusali sala zangu za mwisho. Nikaomba kwa Mungu wangu, msamaha kwa yote niliyoyakosa, lakini nikamwachia kila kitu aamue yeye kwani yeye anajua kuwa yepi nimeyafanya kimakosa na yepi nilikuwa kazini. Japokuwa sikuwa nawaona wengine, kupitia sala zangu hizi nikawaomba msamaha wote.
Joto lilizidi kuwa kali, harufu nzito ya mauti ikaanza kuzisumbua upya pua zangu, giza nalo likawa adui mkubwa. Nikatulia kimya nikiwa nimejikunyata huku mikononi nikiwa nimeukamata mkanda wa yule marehemu aliyenitangulia. Kutoka moyoni nikahisi sauti ikinitaka kuufunga mkanda ule kiunoni, nikaipuuzia lakini baadae ikazidi kunisumbua, nikaamua kuitii hisia hii kwani ni moja ya kazi yetu kutii hisia ya sita na ndiyo intelijensia yenyewe. Nilikuwa naishiwa nguvu, nikaupachika kiunoni tu bila kuuweka kwenye lupsi za suruali kwani sikuwa na muda na nguvu hizo. Nikachuku mwisho huu na huu na kuukutanisha kisha nikaupachika kwa nguvu ili meno yake yaumane. Sekunde ileile nilipoupachika na yale meno kuumana, nikasikia mlipuko kutoka upande mmoja wa ukuta, vumbi likatawala ndani ya kaburi hilo, nikakohoa kwa nguvu sana, hali ilipotulia nikaona tundu la ukubwa wa mdomo wa pipa katika ukuta wa kushoto kwangu. Mwanga hafifu ukapenya ndani nikajua kuwa kwa hapo ningeweza
