Willy Gamba 1
JF-Expert Member
- Jan 5, 2015
- 352
- 376
RIWAYA; MZIGO
MTUNZI; AHMAD MNIACHI
SEHEMU YA KWANZA
Niliwasili Dar es salaam saa tisa na nusu alasiri,
ilikuwa ni mapema zaidi kuliko nilivyotarajia. Mvua
ambayo ilinyesha masaa kadhaa yaliyopita ilisaidia
kupunguza vumbi ingawa ilisababisha fukuto la
joto kuzidi.
Watu walikuwa wametawanyika ovyo pale kituo
kikuu cha mabasi Ubungo kana kwamba ni siafu
walioangukiwa na kaa la moto. Miongoni mwao
walikuwa ni abiria ambao wanasafiri huku wengine
wakiwasili. Pia walikuwepo wapiga debe ambao
walileta kero kubwa kwa abiria.
Bonge alinionya kuwa nisipitie sehemu nyingine
kabla ya kumfikishia mzigo wake. Pia alinitisha
kuwa iwapo sitatekeleza maagizo yake, basi
asingenipa malipo yangu kwa kazi ya kusafirisha
mzigo ule. Vile vile alinikumbusha kuhusu ile picha
ambayo ilikuwa inaniweka katika wakati mgumu.
Ni picha ambayo leo inanifanya niwe mtumwa
inanifanya pia nishindwe kuamua iwapo nitekeleze
au nisitekeleze kile nitakachotumwa. Ndiyo ni hii
picha ambayo imenifanya nijikute nakuwa mtumwa
wa Bonge, huku nikitekeleza maagizo yake kana
kwamba yeye ni rimoti na mimi ni runinga.
Kwa sababu ambazo mpaka leo sijazielewa
nikaamua kuvunja maagizo yake kwa kupitia
nyumbani kwangu Yombo buza. Sifahamu kama
kuna nguvu ya ziada kutoka nje ya nafsi yangu
ilinituma kufanya uamuzi huo wa aina yake;
Kuvunja maagizo ya mtu kama Bonge halikuwa
jambo la kawaida. Pengine chuki yangu juu ya
Bonge ilinipa ujasiri wa kufanya hayo yote, lakini
pia inawezekana ni ujasiri wa nafsi yangu ambao
nimetunukiwa na Muumba.
Ilikuwa siku ya tatu toka nikabidhiwe begi lile.
Sikujua kilichokuwamo ndani yake ingawa hisia
zilinituma kuwa huenda ni almasi au dhahabu.
Nilijikuta nikianza kuingiwa na mashaka kwani
nilitishwa kuwa iwapo nitathubutu kufungua tu
basi adhabu yangu itakuwa kifo!
Hivi kweli nikiufikisha huu mzigo nitaweza
kuepukana na hicho kifo? Lilikuwa ni swali gumu
ambalo nilijiuliza bila kupata jibu.
Lazima nifungue kwani Martin na Bonge watajuaje
kuwa mzigo umefunguliwa?
Nilipofika chumbani nikalitua begi lile kitandani,
moyo wangu ulikuwa unaenda mbio kama mtoto
aliyemuona daktari akiwa na sindano mkononi.
Martin alikuwa miongoni mwa watu ambao
niliwafikiria sana kila liliponijia wazo la kufungua
begi, huyu ndiye aliyenitisha zaidi, jinsi alivyo!
Ana umbo kubwa lenye misuli iliyojengeka kama
mnyanyua vitu vizito, macho yake ni makubwa
kama kurunzi huku uso wake ukipambwa na kovu
kubwa lililopita katikati ya uso wake likionyesha
kila dalili kuwa kilikuwa kidonda kikubwa ambacho
kilishonwa kwa nyuzi kadhaa kabla ya kuwa kovu
la kutisha. Kwa jinsi alivyo alitosha kabisa
kumnyamazisha mtoto anaelia kwa neno moja,
huyo Martin anakuja, labda awe hajawahi
kumuona.
Pale alipokuwa ananitazama nilikuwa sijamkosea
chochote lakini alikuwa anatisha kama yule nyoka
anayeshambulia kwa kurusha mate ya sumu.
Macho yake yalionesha wazi dalili zote za mtu
muovu kama si muuaji kamili, ni bora kusimuliwa
kuliko kukutana na mtu kama huyo usiku. swali
kubwa nililo jiuliza lilikuwa atanifanya nini
akigundua kuwa nimefungua ule mzigo? Iwapo
alikuwa ananitazama kwa sura ambayo kwake
ilikuwa ya upole lakini kijasho chembamba
kilinitoka, vipi nikutane naye siku ambayo
amekasirika? Halafu ajue kuwa maagizo
waliyonipa nimeyavunja, nini kitatokea?
Bila shaka atanifanya kama alivyofanyiwa yule
mwanamke kule guest. Nilikuwa sijawahi kuona
mtu aliyeuwawa kikatili namna ile. Taswira yake
ilinijia kichwani mara kwa mara, mwili ulisisimka
na kufanya vipele vidogovidogo kama mtu
anayehisi baridi kali.
Maskini Merina, Mungu amlaze mahali pema
peponi.
Shauku yangu ya kutaka kujua kuhusu mzigo ule
ilisababishwa na vitisho vya Martin na Bonge.
Adhabu ya kifo kwa kufungua mzigo tu? Woga
niliokuwa nao ulimezwa kabisa na hamu ya kujua
kilichomo ndani yake, na sasa nilikuwa nimeamua
kuchagua kufuata maelekezo ya nafsi yangu na si
yale ya Bonge.
Laiti wasingenionya kiasi kile nisingekuwa na wazo
lolote juu ya mzigo wao. Ningeufikisha kama
walivyotarajia bila hata kuwa na chembe ya wazo
juu ya kutaka kujua kilichomo ndani.
Kwa mara nyingine nikalikazia macho begi lile
jeusi, lilikuwa kama refarii katika maisha yangu.
Nifungue niishi kwa mashaka au niache niishi kwa
amani. Kwangu lilikuwa jambo zito sana kwani
sijawahi kubeba kitu ambacho sikifahamu.
Jambo moja ambalo lilinikosesha raha ni kuwa
iwapo sitafungua basi nitakuwa na fumbo moyoni,
fumbo ambalo sitaweza kulifumbua maisha yangu
yote. Nakumbuka sana nilipokuwa mwanafunzi
jinsi nilivyoumiza kichwa kwenye mafumbo.
Nilikuwa sikubali kushindwa. Lakini kwa mara ya
kwanza leo nakabiliana na fumbo ambalo gharama
ya kufumbua kwake ni kifo.
Nikubali kushindwa?
Kweli nilikuwa naelekea kushindwa. Lakini kwa nini
nishindwe?
Nikiwa mtaalamu wa mafumbo nilikuwa na kazi
mbili, kwanza mzigo halafu uhai wangu. Lengo
lilikuwa ni kujua kuhusu ule mzigo bila kupata
matatizo, yaani nilitaka kuuwa ndege wawili kwa
jiwe moja.
Nikatabasamu huku nikiwa nalitazama vizuri begi
lile ambalo niliahidiwa pesa nyingi kwa kulifikisha
kwa muhusika bila kuvunja masharti. Fedha
nilizoahidiwa sijawahi kufikiria hata siku moja
kuwa ipo siku nitakuja kuzihesabu achilia mbali
kuzimiliki.
Kwanini kusafirisha lile begi kutoka Mwanza
nilipwe pesa zote hizo? Kutatua fumbo lile kwangu
lilikuwa jambo kubwa kuliko zawadi ambayo
ningepewa na bonge huku fumbo likiendelea kubaki
kama maisha ya kaburini ambayo maiti tu ndiye
anayejua yalivyo.
Haiwezekani! Lazima begi lifunguliwe.
Kabla sijafungua nikapata wazo muruwa kabisa.
Nikatabasamu, Lilikuwa wazo kabambe sana.
Nilitaka niue ndege wawili kwa jiwe moja.
Nilidhamiria kulifumbua fumbo lile bila kupata
matatizo yoyote. Nilianza kujihisi kuwa mshindi
ingawa bado niliendelea kujionya juu ya hatari
ninayokabiliana nayo. Bonge hajawahi kuliona lile
begi likoje kwani lilionekana wazi kuwa ni jipya, hii
ilinifanya niamini kuwa wazo langu litakuwa
muruwa.
Kabla sijafanya lolote nikakaa kitandani kwanza
kisha nikaegemea ukuta nikavuta pumzi kwa nguvu
na kuzishusha, taratibu zikaanza kunijia fikra juu
ya mambo ya ajabu ambayo yanatokea katika
maisha yangu.
Muda huu mfupi ambao nilikaa hapo uliweza
kunifanya niyatazame maisha yangu kama mtu
anayetazama filamu ndefu ya kusisimua. Nilikuwa
kama mtu ninayejitazama mwenyewe kwenye kioo.
Ilikuwa kana kwamba ninajisimulia kitu fulani.
Kabla sijaendelea naomba nikusimulie mwanzo wa
yote mpaka kufikia hapa, kwanza ingekuwa vema
unifahamu mimi ni nani?
***
Naitwa Kajuna Daudi Kazakamba, ni mtoto wa
kwanza katika familia yenye watoto watatu, mimi
na wadogo zangu wawili wote wa kike Koku na
Waridi
***
Baadhi ya watu wanaoishi Dar es salaam wana
akili za ajabu sana. Hawapendi kuishi maeneo
yenye nafasi na hewa nzuri. Hupenda sehemu
zenye misongamano ya watu na hususani zile
zilizoko kando ya barabara. Mfano mzuri maeneo
kama Kinondoni na Manzese. Hilo ndilo jambo
lililomfanya baba yangu kununua kiwanja eneo
ambalo liko karibu na barabara. Madhara yake
yalikuwa makubwa kwa baba na familia kwa
ujumla.
Ikiwa ni miaka kumi na mitano toka ajenge
nyumba hiyo akapokea barua kutoka serikalini
ikimtaka kuhama eneo hilo. Katika barua hiyo
serikali ilidai kuwa baba amejenga katika eneo
ambalo linatambuliwa kisheria kuwa ni hifadhi ya
barabara. Kwa masikitiko makubwa kabisa
nikashuhudia nyumba yetu ikibomolewa. Hakuna
fidia iliyotolewa ingawa vyombo vya habari
vikiwanukuu viongozi husika vilitoa taarifa kuwa
waathirika wote wamelipwa fidia zao.
Ukawa mwanzo mpya wa maisha ya kupanga na
kuhamahama, mpaka pale baba alipojenga nyumba
nyingine Mwananyamala baada ya kupata fedha
zake za mafao kutoka shirika la reli Tanzania
ambako alifanyia kazi. Fedha hizi zilipatikana kwa
mbinde, iliwalazimu wazee kuandamana na kulala
barabarani wakati wa kudai mafao hayo. Wakati
mwingine polisi walilazimika kutumia nguvu za
ziada kuwadhibiti wazee hao.
Fedha zote za kiinua mgongo ziliishia kwenye
ujenzi wa nyumba hiyo. Mwaka huo nilikuwa
kidato cha sita shule ya sekondari Tambaza.
Mapema mwaka uliofuata nikahitimu masomo
yangu.
Kama zilivyo hadithi za watoto wengine wanaotoka
kwenye familia kama zetu hapo ndio ikawa tamati
sikuweza kuendelea.
Nikaanza kutangatanga kutafuta maisha.
Nikahama Mwananyamala kwa wazazi wangu
nikahamia Yombo buza. Huko nilihama nyumba
kadhaa hatimaye nikapata sehemu ambayo nilikaa
muda mrefu kuliko nyumba nyingine.
Chumba kimoja, kitanda, ndoo na vyombo vidogo
vidogo vilikuwa vinaonesha taswira halisi ya
maisha yangu. Ulikuwa mkusanyiko usiovutia ndani
ya chumba hicho cha kupanga, hakukuwa na
tofauti kubwa na sehemu inayouziwa pombe za
kienyeji. Niliridhika kuishi maisha hayo kuliko
kumuongezea baba mzigo, kwani biashara yake
kubwa kipindi hicho ilikuwa ni samaki ambao
alikuwa anawauza katika mitaa ya Mwananyamala
na Kinondoni, pale inapotokea hali ya hewa si nzuri
alikuwa anachoma mahindi na kuyauza. Baba
yangu hakuwa mtu anayependa kukaa bila kazi
mwenyewe alijisifu kwa kusema yeye ni zao la
Tanu Youth league.
***
Ilikuwa saa 12.37 jioni. Nilivua sare zangu za kazi
nikazitia kwenye boksi. Nikachagua nguo safi
kutoka kwenye kamba ya nguo. Kamba hiyo
niliifunga kwenye misumari ambayo niliigongea
ukutani. Baadhi ya wenye nyumba hawapendi
mtindo huu wa kutoboa ovyo nyumba zao kwa
misumari. Nyumba niliyoishi haikuwa na masharti
kama hayo, vyumba vyote vilikuwa vimetobolewa
kwa misumari. Kimsingi ulikuwa ni uharibifu ambao
wakati mwingine uliweza hata kusababisha nyufa
ndio maana baadhi ya wenye nyumba walikuwa
hawaridhishwi na hilo. Sisi tulikuwa na bahati
kwani mwenye nyumba alikuwa mlevi hivyo wewe
fanya lolote lakini siku ikifika mpe chake akalewe.
Hakuwa na uchungu sana na nyumba yake labda
kwa kuwa ni nyumba ya urithi. Nilikuwa naamini
kuwa kitu ambacho mtu hukipata bila kukitolea
jasho mara nyingi hakionei uchungu na wala
hakithamini kama kile ambacho amekifanyia kazi.
Niliitazama kalenda ya kampuni ambayo nilikuwa
nafanyia kazi, nikagundua kuwa ilikuwa ni ya
miaka miwili iliyopita. Niliziangalia kwa hasira
picha za watu ambao walikuwa wanacheka kwenye
kalenda ile. Walikuwa na matumbo makubwa
ambayo bila shaka yalikuwa yanawapa shida
wakati wa kupumua na kulala. Hivi hawa
wanakumbuka kweli kuwa kuna watu wanapata
shida duniani au wanajali matumbo yao tu?
Kwenye picha ile kulikuwa na Watanzania wenye
asili ya kiasia na wale weusi kama sisi.
Nikaitazama tena kwa uchungu kalenda ile.
Kalenda mpya zilikuwa zinatoka kila mwaka, ili
uweze kupata kalenda hizo ulitakiwa
kuwabembeleza waajiri waweze kukupatia. Wengi
wao walikuwa ni watu wenye majivuno. Sikuwa na
muda wa kumbembeleza mtu, kazi yenyewe
sikuipenda, tatizo kubwa sikuwa na kazi nyingine
ya kufanya. Kilichonikera zaidi kazi zenyewe
hazikuwa za kila siku huku siku nenda rudi
tukiendelea kuwa vibarua.
Tulikuwa tunarushiwa vikaratasi ambavyo
vimekunjwa, ukifungua unakuta idadi ya siku
utakazofanya kazi kwa mwezi pamoja na malipo
utakayolipwa. Ilikuwa ni kampuni inayojishughuli
sha na utengenezaji wa juisi za aina mbalimbali,
biskuti na mikate. Ilikuwa ni miongoni mwa
makampuni yanayosifika sana kwa kusamehewa
kodi. Nilipata kusikia tetesi kuwa ni ya shemeji
yake kigogo mkubwa wa wizara ya viwanda na
biashara. Roho iliniuma sana, Mungu
ametuzawadia sote hii nchi, lakini kuna watu
wanaoifanya kuwa mali yao.
ITAENDELEA
MTUNZI; AHMAD MNIACHI
SEHEMU YA KWANZA
Niliwasili Dar es salaam saa tisa na nusu alasiri,
ilikuwa ni mapema zaidi kuliko nilivyotarajia. Mvua
ambayo ilinyesha masaa kadhaa yaliyopita ilisaidia
kupunguza vumbi ingawa ilisababisha fukuto la
joto kuzidi.
Watu walikuwa wametawanyika ovyo pale kituo
kikuu cha mabasi Ubungo kana kwamba ni siafu
walioangukiwa na kaa la moto. Miongoni mwao
walikuwa ni abiria ambao wanasafiri huku wengine
wakiwasili. Pia walikuwepo wapiga debe ambao
walileta kero kubwa kwa abiria.
Bonge alinionya kuwa nisipitie sehemu nyingine
kabla ya kumfikishia mzigo wake. Pia alinitisha
kuwa iwapo sitatekeleza maagizo yake, basi
asingenipa malipo yangu kwa kazi ya kusafirisha
mzigo ule. Vile vile alinikumbusha kuhusu ile picha
ambayo ilikuwa inaniweka katika wakati mgumu.
Ni picha ambayo leo inanifanya niwe mtumwa
inanifanya pia nishindwe kuamua iwapo nitekeleze
au nisitekeleze kile nitakachotumwa. Ndiyo ni hii
picha ambayo imenifanya nijikute nakuwa mtumwa
wa Bonge, huku nikitekeleza maagizo yake kana
kwamba yeye ni rimoti na mimi ni runinga.
Kwa sababu ambazo mpaka leo sijazielewa
nikaamua kuvunja maagizo yake kwa kupitia
nyumbani kwangu Yombo buza. Sifahamu kama
kuna nguvu ya ziada kutoka nje ya nafsi yangu
ilinituma kufanya uamuzi huo wa aina yake;
Kuvunja maagizo ya mtu kama Bonge halikuwa
jambo la kawaida. Pengine chuki yangu juu ya
Bonge ilinipa ujasiri wa kufanya hayo yote, lakini
pia inawezekana ni ujasiri wa nafsi yangu ambao
nimetunukiwa na Muumba.
Ilikuwa siku ya tatu toka nikabidhiwe begi lile.
Sikujua kilichokuwamo ndani yake ingawa hisia
zilinituma kuwa huenda ni almasi au dhahabu.
Nilijikuta nikianza kuingiwa na mashaka kwani
nilitishwa kuwa iwapo nitathubutu kufungua tu
basi adhabu yangu itakuwa kifo!
Hivi kweli nikiufikisha huu mzigo nitaweza
kuepukana na hicho kifo? Lilikuwa ni swali gumu
ambalo nilijiuliza bila kupata jibu.
Lazima nifungue kwani Martin na Bonge watajuaje
kuwa mzigo umefunguliwa?
Nilipofika chumbani nikalitua begi lile kitandani,
moyo wangu ulikuwa unaenda mbio kama mtoto
aliyemuona daktari akiwa na sindano mkononi.
Martin alikuwa miongoni mwa watu ambao
niliwafikiria sana kila liliponijia wazo la kufungua
begi, huyu ndiye aliyenitisha zaidi, jinsi alivyo!
Ana umbo kubwa lenye misuli iliyojengeka kama
mnyanyua vitu vizito, macho yake ni makubwa
kama kurunzi huku uso wake ukipambwa na kovu
kubwa lililopita katikati ya uso wake likionyesha
kila dalili kuwa kilikuwa kidonda kikubwa ambacho
kilishonwa kwa nyuzi kadhaa kabla ya kuwa kovu
la kutisha. Kwa jinsi alivyo alitosha kabisa
kumnyamazisha mtoto anaelia kwa neno moja,
huyo Martin anakuja, labda awe hajawahi
kumuona.
Pale alipokuwa ananitazama nilikuwa sijamkosea
chochote lakini alikuwa anatisha kama yule nyoka
anayeshambulia kwa kurusha mate ya sumu.
Macho yake yalionesha wazi dalili zote za mtu
muovu kama si muuaji kamili, ni bora kusimuliwa
kuliko kukutana na mtu kama huyo usiku. swali
kubwa nililo jiuliza lilikuwa atanifanya nini
akigundua kuwa nimefungua ule mzigo? Iwapo
alikuwa ananitazama kwa sura ambayo kwake
ilikuwa ya upole lakini kijasho chembamba
kilinitoka, vipi nikutane naye siku ambayo
amekasirika? Halafu ajue kuwa maagizo
waliyonipa nimeyavunja, nini kitatokea?
Bila shaka atanifanya kama alivyofanyiwa yule
mwanamke kule guest. Nilikuwa sijawahi kuona
mtu aliyeuwawa kikatili namna ile. Taswira yake
ilinijia kichwani mara kwa mara, mwili ulisisimka
na kufanya vipele vidogovidogo kama mtu
anayehisi baridi kali.
Maskini Merina, Mungu amlaze mahali pema
peponi.
Shauku yangu ya kutaka kujua kuhusu mzigo ule
ilisababishwa na vitisho vya Martin na Bonge.
Adhabu ya kifo kwa kufungua mzigo tu? Woga
niliokuwa nao ulimezwa kabisa na hamu ya kujua
kilichomo ndani yake, na sasa nilikuwa nimeamua
kuchagua kufuata maelekezo ya nafsi yangu na si
yale ya Bonge.
Laiti wasingenionya kiasi kile nisingekuwa na wazo
lolote juu ya mzigo wao. Ningeufikisha kama
walivyotarajia bila hata kuwa na chembe ya wazo
juu ya kutaka kujua kilichomo ndani.
Kwa mara nyingine nikalikazia macho begi lile
jeusi, lilikuwa kama refarii katika maisha yangu.
Nifungue niishi kwa mashaka au niache niishi kwa
amani. Kwangu lilikuwa jambo zito sana kwani
sijawahi kubeba kitu ambacho sikifahamu.
Jambo moja ambalo lilinikosesha raha ni kuwa
iwapo sitafungua basi nitakuwa na fumbo moyoni,
fumbo ambalo sitaweza kulifumbua maisha yangu
yote. Nakumbuka sana nilipokuwa mwanafunzi
jinsi nilivyoumiza kichwa kwenye mafumbo.
Nilikuwa sikubali kushindwa. Lakini kwa mara ya
kwanza leo nakabiliana na fumbo ambalo gharama
ya kufumbua kwake ni kifo.
Nikubali kushindwa?
Kweli nilikuwa naelekea kushindwa. Lakini kwa nini
nishindwe?
Nikiwa mtaalamu wa mafumbo nilikuwa na kazi
mbili, kwanza mzigo halafu uhai wangu. Lengo
lilikuwa ni kujua kuhusu ule mzigo bila kupata
matatizo, yaani nilitaka kuuwa ndege wawili kwa
jiwe moja.
Nikatabasamu huku nikiwa nalitazama vizuri begi
lile ambalo niliahidiwa pesa nyingi kwa kulifikisha
kwa muhusika bila kuvunja masharti. Fedha
nilizoahidiwa sijawahi kufikiria hata siku moja
kuwa ipo siku nitakuja kuzihesabu achilia mbali
kuzimiliki.
Kwanini kusafirisha lile begi kutoka Mwanza
nilipwe pesa zote hizo? Kutatua fumbo lile kwangu
lilikuwa jambo kubwa kuliko zawadi ambayo
ningepewa na bonge huku fumbo likiendelea kubaki
kama maisha ya kaburini ambayo maiti tu ndiye
anayejua yalivyo.
Haiwezekani! Lazima begi lifunguliwe.
Kabla sijafungua nikapata wazo muruwa kabisa.
Nikatabasamu, Lilikuwa wazo kabambe sana.
Nilitaka niue ndege wawili kwa jiwe moja.
Nilidhamiria kulifumbua fumbo lile bila kupata
matatizo yoyote. Nilianza kujihisi kuwa mshindi
ingawa bado niliendelea kujionya juu ya hatari
ninayokabiliana nayo. Bonge hajawahi kuliona lile
begi likoje kwani lilionekana wazi kuwa ni jipya, hii
ilinifanya niamini kuwa wazo langu litakuwa
muruwa.
Kabla sijafanya lolote nikakaa kitandani kwanza
kisha nikaegemea ukuta nikavuta pumzi kwa nguvu
na kuzishusha, taratibu zikaanza kunijia fikra juu
ya mambo ya ajabu ambayo yanatokea katika
maisha yangu.
Muda huu mfupi ambao nilikaa hapo uliweza
kunifanya niyatazame maisha yangu kama mtu
anayetazama filamu ndefu ya kusisimua. Nilikuwa
kama mtu ninayejitazama mwenyewe kwenye kioo.
Ilikuwa kana kwamba ninajisimulia kitu fulani.
Kabla sijaendelea naomba nikusimulie mwanzo wa
yote mpaka kufikia hapa, kwanza ingekuwa vema
unifahamu mimi ni nani?
***
Naitwa Kajuna Daudi Kazakamba, ni mtoto wa
kwanza katika familia yenye watoto watatu, mimi
na wadogo zangu wawili wote wa kike Koku na
Waridi
***
Baadhi ya watu wanaoishi Dar es salaam wana
akili za ajabu sana. Hawapendi kuishi maeneo
yenye nafasi na hewa nzuri. Hupenda sehemu
zenye misongamano ya watu na hususani zile
zilizoko kando ya barabara. Mfano mzuri maeneo
kama Kinondoni na Manzese. Hilo ndilo jambo
lililomfanya baba yangu kununua kiwanja eneo
ambalo liko karibu na barabara. Madhara yake
yalikuwa makubwa kwa baba na familia kwa
ujumla.
Ikiwa ni miaka kumi na mitano toka ajenge
nyumba hiyo akapokea barua kutoka serikalini
ikimtaka kuhama eneo hilo. Katika barua hiyo
serikali ilidai kuwa baba amejenga katika eneo
ambalo linatambuliwa kisheria kuwa ni hifadhi ya
barabara. Kwa masikitiko makubwa kabisa
nikashuhudia nyumba yetu ikibomolewa. Hakuna
fidia iliyotolewa ingawa vyombo vya habari
vikiwanukuu viongozi husika vilitoa taarifa kuwa
waathirika wote wamelipwa fidia zao.
Ukawa mwanzo mpya wa maisha ya kupanga na
kuhamahama, mpaka pale baba alipojenga nyumba
nyingine Mwananyamala baada ya kupata fedha
zake za mafao kutoka shirika la reli Tanzania
ambako alifanyia kazi. Fedha hizi zilipatikana kwa
mbinde, iliwalazimu wazee kuandamana na kulala
barabarani wakati wa kudai mafao hayo. Wakati
mwingine polisi walilazimika kutumia nguvu za
ziada kuwadhibiti wazee hao.
Fedha zote za kiinua mgongo ziliishia kwenye
ujenzi wa nyumba hiyo. Mwaka huo nilikuwa
kidato cha sita shule ya sekondari Tambaza.
Mapema mwaka uliofuata nikahitimu masomo
yangu.
Kama zilivyo hadithi za watoto wengine wanaotoka
kwenye familia kama zetu hapo ndio ikawa tamati
sikuweza kuendelea.
Nikaanza kutangatanga kutafuta maisha.
Nikahama Mwananyamala kwa wazazi wangu
nikahamia Yombo buza. Huko nilihama nyumba
kadhaa hatimaye nikapata sehemu ambayo nilikaa
muda mrefu kuliko nyumba nyingine.
Chumba kimoja, kitanda, ndoo na vyombo vidogo
vidogo vilikuwa vinaonesha taswira halisi ya
maisha yangu. Ulikuwa mkusanyiko usiovutia ndani
ya chumba hicho cha kupanga, hakukuwa na
tofauti kubwa na sehemu inayouziwa pombe za
kienyeji. Niliridhika kuishi maisha hayo kuliko
kumuongezea baba mzigo, kwani biashara yake
kubwa kipindi hicho ilikuwa ni samaki ambao
alikuwa anawauza katika mitaa ya Mwananyamala
na Kinondoni, pale inapotokea hali ya hewa si nzuri
alikuwa anachoma mahindi na kuyauza. Baba
yangu hakuwa mtu anayependa kukaa bila kazi
mwenyewe alijisifu kwa kusema yeye ni zao la
Tanu Youth league.
***
Ilikuwa saa 12.37 jioni. Nilivua sare zangu za kazi
nikazitia kwenye boksi. Nikachagua nguo safi
kutoka kwenye kamba ya nguo. Kamba hiyo
niliifunga kwenye misumari ambayo niliigongea
ukutani. Baadhi ya wenye nyumba hawapendi
mtindo huu wa kutoboa ovyo nyumba zao kwa
misumari. Nyumba niliyoishi haikuwa na masharti
kama hayo, vyumba vyote vilikuwa vimetobolewa
kwa misumari. Kimsingi ulikuwa ni uharibifu ambao
wakati mwingine uliweza hata kusababisha nyufa
ndio maana baadhi ya wenye nyumba walikuwa
hawaridhishwi na hilo. Sisi tulikuwa na bahati
kwani mwenye nyumba alikuwa mlevi hivyo wewe
fanya lolote lakini siku ikifika mpe chake akalewe.
Hakuwa na uchungu sana na nyumba yake labda
kwa kuwa ni nyumba ya urithi. Nilikuwa naamini
kuwa kitu ambacho mtu hukipata bila kukitolea
jasho mara nyingi hakionei uchungu na wala
hakithamini kama kile ambacho amekifanyia kazi.
Niliitazama kalenda ya kampuni ambayo nilikuwa
nafanyia kazi, nikagundua kuwa ilikuwa ni ya
miaka miwili iliyopita. Niliziangalia kwa hasira
picha za watu ambao walikuwa wanacheka kwenye
kalenda ile. Walikuwa na matumbo makubwa
ambayo bila shaka yalikuwa yanawapa shida
wakati wa kupumua na kulala. Hivi hawa
wanakumbuka kweli kuwa kuna watu wanapata
shida duniani au wanajali matumbo yao tu?
Kwenye picha ile kulikuwa na Watanzania wenye
asili ya kiasia na wale weusi kama sisi.
Nikaitazama tena kwa uchungu kalenda ile.
Kalenda mpya zilikuwa zinatoka kila mwaka, ili
uweze kupata kalenda hizo ulitakiwa
kuwabembeleza waajiri waweze kukupatia. Wengi
wao walikuwa ni watu wenye majivuno. Sikuwa na
muda wa kumbembeleza mtu, kazi yenyewe
sikuipenda, tatizo kubwa sikuwa na kazi nyingine
ya kufanya. Kilichonikera zaidi kazi zenyewe
hazikuwa za kila siku huku siku nenda rudi
tukiendelea kuwa vibarua.
Tulikuwa tunarushiwa vikaratasi ambavyo
vimekunjwa, ukifungua unakuta idadi ya siku
utakazofanya kazi kwa mwezi pamoja na malipo
utakayolipwa. Ilikuwa ni kampuni inayojishughuli
sha na utengenezaji wa juisi za aina mbalimbali,
biskuti na mikate. Ilikuwa ni miongoni mwa
makampuni yanayosifika sana kwa kusamehewa
kodi. Nilipata kusikia tetesi kuwa ni ya shemeji
yake kigogo mkubwa wa wizara ya viwanda na
biashara. Roho iliniuma sana, Mungu
ametuzawadia sote hii nchi, lakini kuna watu
wanaoifanya kuwa mali yao.
ITAENDELEA