Willy Gamba 1
JF-Expert Member
- Jan 5, 2015
- 352
- 377
- Thread starter
- #21
SEHEMU YA KUMI NA MBILI
Ole wao hawa mbwa!â niliwaza. Nilizunguka kwa
hasira huku nikipiga ngumi ukuta. Naweza kusema
katika kumbukumbu zangu hakuna siku mbaya
katika maisha yangu kama siku hiyo na sidhani
kama itakuja kutokea siku kama hiyo.
Amewakosea nini? Kwanini makosa yangu yawe
mateso kwa mtu mwingine? Niliikumbuka sana
siku niliyokutana na Betty pale baa. Alikataa,
akakataaâ¦Nikambembeleza, nikambembeleza kwa
maneno ya uungwana. Maskini sikujua kuwa
uhusiano wangu ungemponza kiasi hiki. Bora
ningekutana naye baada ya mkasa huu. Nilijiuliza
swali moja ambalo lilinitisha na kuniongezea hofu.
NANI ATAFUATA?
Bila kujitambua nilikuwa nazunguka zunguka mle
ndani kwa muda wa dakika tano. Nilikuwa nahisi
kichefuchefu, mwili wote ulikuwa wa baridi. Hofu
ilikuwa imenitawala. Nilikuwa nimechanganyikiwa
vibaya, nikasikia sauti ya Ommy.
âVipi mshikaji mbona unapoteza muda?â
âIngia!â Nilimwambia kwa sauti iliyojaa utulivu.
Akaingia.
âHaa! My God, they killed herâ(Mungu wangu
wamemuua).
Akashtuka huku akiwa ameziba mdomo. Ommy
aligwaya vibaya sana. Kwa dakika kadhaa alikuwa
ametumbua macho kwa mshangao.
âTwenzetu Kajuna hii ni kesi nzito!â. Wakati nataka
kuondoka nikauona ujumbe wa karatasi ambao
nilihisi umeachwa na wauaji. Sikutaka kupoteza
muda, nikaichukua ile karatasi na kuiweka mfukoni.
Kabla sijatoka mle ndani nikaanza kuhisi
kichefuchefu kikizidi. Nikaanza kusikia maumivu ya
kichwa ghafla. Ommy hakutaka kuruhusu hali hiyo
akanishika mkono kwa nguvu na kuanza kukimbia.
Nikajikuta nikikimbia bila kutaka.
âKimbia kijana Polisi watakuja hapa muda si
mrefu!â. Tukaingia ndani ya gari kisha akaliondoa
kwa kasi. Baada ya dakika kama tano tukakutana
na gari aina ya 110 defender likiwa na askari
wapatao watano. Wote walikuwa na silaha. Ommy
aliongeza kasi ya gari kitendo kilichonifanya niwe
na hofu zaidi. âUlijuaje kama askari watafika?
Nilimuuliza kwa mshangao.
âMazingira ya ile nyumba yanaonesha kuwa
wanaishi watu wa familia tofauti haiwezekani wote
wawe wameondoka ni hofu tu ndo imewakimbiza
pale na ni lazima watoe taarifa Polisiâ. Alijibu huku
akiendelea kuongeza mwendo wa gari lile. Spidi
ilikuwa inatisha mpaka wakati fulani nilihisi kuwa
tutaingia kwenye mtaro. Kutokana na kasi ile
niliogopa kuendelea kumsemesha kwani angekosea
kitu kidogo tu sidhani kama tungesalimika. Ule
mwendo ungeweza hata kuwashawishi askari wa
usalama barabarani kulitilia mashaka gari letu.
***
Jua lilipochomoza tu, Kitu cha kwanza ilikuwa ni
kukusanya magazeti ya siku ile. Magazeti mengi
yalikuwa na vichwa ambavyo viliyafanya yauzike
kwa siku ile. DAR YATIKISWA KWA MAUAJI
MENGINE YA KUTISHA. Baadhi ya magazeti
yalijinadi. Nilikuwa najua wazi kuwa hakuna jipya
nikachukua gazeti na kuanza kusoma. Kama
nilivyotarajia zilikuwa ni habari za Mauaji ya Betty.
Mwisho habari ilimalizia kwa kusema Polisi
wanaendelea na uchunguzi mkali.
Nikatulia kidogo nikitafakari tukio la jana. Kwa
namna fulani nilianza kujishangaa mwenyewe,
nilishaanza kuzoea matukio ya kutisha kwani
katika hali ya kawaida tukio la Betty lingeniumiza
sana kichwa lakini nikajikuta likinizidishia hasira na
kutamani kukutana tena na Bonge. Sikuwa na
woga tena mbele ya Bonge, nilitamani aingie
kwenye anga zangu nimuonyeshe kazi. Nilikuwa na
hasira kiasi ambacho mtu angekuwa karibu yangu
angeweza kusikia jinsi nilivyokuwa nasaga meno.
âOle wake, ipo siku tu!â¦.â Niliwaza.
Wakati nikiwa kwenye mawazo hayo mazito ndipo
nikakumbuka kile kikaratasi ambacho nilikichukua
eneo la tukio. Huku nikianza kurudiwa na woga
ambao ulishapotea nikaanza kukisoma kile
kikaratasi.
â¦..Tunajua uko hai makosa yalifanyika, uliandaliwa
kifo kitamu tena cha heshima. Ni raha ilioje
kutangazwa kuwa umekufa kwa bomu, je! Huoni
kuwa huo ni ujasiri? Umekataa kifo kileâ¦â¦ safari
hii tunataka kukusamehe lililo muhimu kwako ili
kupata msamaha tunaomba mzigo wetuâ¦. La sivyo
tutakuuwa kinyama kuliko alivyouwawa huyo
malaya wako.Pia lazima ukumbuke kuwa picha
yako tunayo tunaweza kukuweka matatizoni.
Mtemi.
Niliusoma tena ule ujumbe, nikatikisa kichwa.
âEti watanisamehe!â Nilijikuta nikisema kwa sauti
na kumshangaza Ommy ambaye alikuwa anaingia
kutoka bafuni.
âWatakusamehe kina nani!?â Sikumjibu nikampa
kile kikaratasi asome mwenyewe. Akakisoma,
alipomaliza nikamuona akitikisa kichwa.
âWendawazimu kamili, uwape mzigo wakuache
hai!?â Alisema Ommy huku akiwa amekunja sura.
âKifo cha heshima, kifo ambacho kingetawanya
viungo vyangu huku wao wakicheka na kula kuku!â
Nilitamka kwa sauti iliyojaa utulivu.
Walinishangaza sana hawa viumbe ambao
niliwatoa katika kundi la binadamu. Vyovyote
ambavyo ungeweza kuwaita kinyume cha
binadamu na malaika kwangu ilikuwa sahihi.
Ukiwaita mbwa sawa, ukiwaita nguruwe sawa
ukiwaitaâ¦â¦.. jina lolote lile ambalo litawatoa katika
kundi la binadamu wastaarabu wao liliwastahili.
âLeo wapi?â Aliuliza Ommy.
âLeo ilikuwa siku ya kufungua mzigoâ Nilimjibu
nikamuaona ananitazama kwa mshangao.
âUnasema ilikuwa siku ya kufungua Mzigo ina
maana hatufungui tena?â
âMzigo utafunguliwa lakini sioni sababu ya
kufungua leo wakati bado tuko kwenye majonzi ya
kifo cha Betty. Sitaki nisherehekee wakati mbele
yangu kuna tatizo kubwa kiasi hiki.â
âSawa wazo lako ni zuri, kwahiyo leo tutafanya
nini?â
âLeo tuna mambo mawili Ommy, kwanza nahitaji
kuonana na Debora pili nataka kufika eneo la
msiba ili niweze kujua nini kinaendelea.â
âIna maana unataka kuhudhuria mazishi!â
âHapana Ommy, Ingawa majirani walikuwa
wananifahamu lakini ndugu wa marehemu
hawanifahamu.â
âSasa utaenda kufanya nini huko?â
âNataka kujua kilichotokea kama itawezekana.â
âUnataka kuhoji watu msibani?â
âLa, nataka kujaribu kama naweza kupata fununu
kutoka kwa waombolezaji.â
âNa huko kwa Debora?â
âHuko lazima niende kwani kuna mengi nataka
kujua kutoka kwa yule binti!â
âOk, twenzetu.â
***
Watu walikuwa wengi pale msibani. Ndugu jamaa
na marafiki walikusanyika kwa wingi, kingine
ambacho kilisababisha kuvuta zaidi watu bila
shaka ni aina ya tukio lililosababisha kifo. Mauaji
yalikuwa ya aina yake, mtu kukatwa kiungo
kimojakimoja halikuwa jambo la kawaida.
Dakika tano zilipita tukiwa ndani ya gari.
Sikuthubutu kuteremka kwani niliona kuwa ni
hatari kwangu kama wangeniona watu ambao
walikuwa wanafahamu uhusiano wangu na Betty.
Sijui ni kwanini ujasiri wa kwenda pale msibani
uliniishia ghafla.
âKajuna!â
âSema Ommy!â
âTutaganda hapa mpaka saa ngapi?â
âMi nafikiri kuna umuhimu wewe uende kule ukajue
ukweli wa mambo, kwani kila ninavyowaza nahisi
kama kuna hatari inaniandama!â
Ommy akashuka garini na kuelekea kule msibani,
pale nilipokaa nilijitahidi kuinama ili macho ya
watu yasinifikie.
Nilikaa pale kwa muda wa nusu saa nikimsubiri
Ommy ambaye alishapotea katika macho yangu
baada ya kujichanganya kwenye umati ule wa
watu. Mara moja moja niliinua kichwa na
kuchungulia kule msibani lakini sikumuona Ommy.
Nilishangaa baada ya kuona nusu saa inamalizika
bila ya kumuona Ommy.
Niliamua kujilaza kwenye siti, sikutaka kusumbua
tena kichwa changu kujiuliza mambo yanayokuja.
âOyaa vipi tena unalala!â
âSijalala nimeamua kuificha sura yangu si unajua
anaweza kutokea mtu anayenifahamu nikaibua
mambo mengine?â
âVipi una ripoti?â
âRipoti si mzuri.â
âKivipi?â Niliuliza huku kwa mara nyingine kijasho
chembamba kikianza kunitoka.
âUnatakiwa kuendelea kujificha zaidi kuliko
mwanzo.â
âMhhhh!â Nilishusha pumzi nikamuangalia Ommy
ambaye alikuwa anaonesha kutaka kuendelea
kuongea. Kisha akaendelea.
âEti wewe ndio mtuhumiwa namba moja wa mauaji
yale!â Tumbo lilishika joto ghafla baada ya kusikia
kauli hiyo. Nikaganda bila kuongea lolote huku
nikihisi kama midomo yangu imekauka.â
âInawezekana vipi?â Kwa sauti iliyokauka yenye
mikwaruzo nilijikuta nikijikakamua na kuuliza swali
hilo.
âInasemekana mara ya mwisho ulipoondoka kuna
uwezekano mkubwa kuwa mligombana na ndio
maana baada ya wewe kuondoka Betty hakuwa na
furaha mpaka kifo kilipomkuta!â
âDuh, bila shaka ni baada ya kumsimulia mkasa
wangu!â
âSawa lakini kwa majirani hilo hawakulitambua na
ndio maana wameripoti kuwa huenda yale mauaji
yalikuwa ni ya wivu wa kimapenzi!â
âDuh huu msala sasa na kwa jinsi
ninavyowafahamu polisi hawana dogo hizo taarifa
watazishikia bango utafikiri wamethibitisha!â
âLakini ni vizuri tumefahamu hatari iliyoko mbele
yako.â
âNa ndio maana nilihitaji kuja huku.â
***
Jua lilikuwa linawapungia mkono wakazi wa jiji la
Dar es salaam, giza nalo lilikuwa linapiga hodi na
kuwafanya baadhi ya wakazi wa jiji hili kuwa
katika hekaheka tofauti. Wako ambao huo ndio
ulikuwa muda wao wa kuanza shughuli huku
wengine wakiwa wanarejea mapumzikoni baada ya
kumaliza harakati zao za kimaisha.
Palepale ambapo tulisimama siku iliyopita ndipo
tuliposimama siku hii pia. Kama ilivyokuwa na siku
hii pia nilimuacha Ommy kwenye gari nikaelekea
nyumbani kwa Debora. Nilitembea haraka na kwa
kujiamini sana kwani jua lilikuwa limepotea na
hivyo nilifanikiwa kusitirika kwa kigiza chepesi
ambacho kilianza kutawala. Sikugonga kama
nilivyofanya siku ya kwanza kwani nilikuta ule
mlango wa bati la KORIE ukiwa wazi.
Kutoka nyumba kubwa nilikuwa nasikia muziki wa
taarabu ulioimbwa na marehemu Issa Matona.
Sauti ya kiutu uzima ilisikika kwa mbali ikifuatisha
wimbo huo. Taa ilikuwa inawaka chumbani kwa
Debora. Kwa kuwa kazi zake ni za usiku nilihisi
kuwa saa hizo atakuwa anajiandaa kuondoka.
Niliposogea mlangoni nikashtuka baada ya kusikia
mtu akifoka.
âUsitake kuongopa chochote wewe mbwa sema,
Kajuna alifuata nini hapa kwako?â
âMimi simfahamu huyo Kajuna.â Niliisikia sauti ya
Debora ikiwa yenye kwikwi kwa kilio
âUhai wako uko mikononi mwangu, ili uweze
kunusurika unatakiwa kuwa mkweli, yule mtu
aliyeingia hapa kwako jana alifuata nini?â
Kikapita kimya kirefu bila kujibiwa chochote.
Nikaangaza macho pale uani nikayaona matofali
ambayo yalikuwa yamepangwa sehemu moja.
Yalikuwa mengi kiasi bila shaka. Nikajitwisha moja
nakusogea pale mlangoni.
âSasa kwa kuwa hutaki kusema nitakupa kile
unachohitaji.â
âNis..s..samehâ¦. mimi simjui yulâ¦â¦.â
Hakuwahi kumaliza kauli yake niliuusukuma
mlango kwa nguvu na kuingia ndani. Yule mtu
akiwa ameduwazwa na uvamizi huo wa ghafla
alishindwa kufanya lolote licha ya kuwa na bastola
mkononi. Niliitumia Fursa hiyo kwa kumpiga kwa
tofali lile zito kichwani. Nilitumia nguvu zangu zote
nikamshushia kwa nguvu katikati ya paji lake la
uso.
âMungu wangu⦠umeua kaka nitafanya nini mimi?â
Alianza kulia yule binti.
âShhhiiiiiiiiiii!â Nilimtuliza kwa kuweka kidole cha
shahada katikati ya mdomo wangu.
Niliufunga mlango haraka kisha nikamkazia macho
makali.
âTuna maiti humu ndani na muda si mrefu
unaweza kuwa kwenye mikono yas polisi, lazima
ujue kuwa wewe utakuwa mtuhumiwa namba moja
uko tayari?â
Alionesha mshtuko zaidi nilipotoa kauli hiyo lakini
hakujibu kitu.
âNimekusaidia nimemuua mtu aliyetaka kukuua au
ulipenda ufe wewe?â Alikataa kwa kutingisha
kichwa.
âSikia we mwanamke, Chukua kilicho muhimu
kwako haraka sana kwani kuendelea kukaa hapa ni
hatari kwako.â
âNiende wapi?â
âNifuate!â
Akili yake ilionekana kutulia kidogo, akakusanya
vitu ambavyo aliona kuwa muhimu kwake
akaviweka kwenye begi kubwa. Tukaondoka
kuelekea kule aliko Ommy huku tukisaidiana
kushika begi lile kubwa.
âAaah, Shemeji!â Alishtuka Debora baada ya
kumuona Ommy ndani ya gari.
âVipi na huyu?â Aliuliza Ommy huku akionesha
mshangao wa wazi baada ya kuona nimeongozana
na Deborah tena akiwa na begi lake.
âMkuu tuondoke haraka kwani nimeua mtu huko
ndani.â
âUmeua?â Aliuliza Ommy huku akichochea moto
kwenye gari.
âIlibidi!â Nilimjibu kwa mkato.
Nikamsimulia Ommy kilichotokea kisha nikampa
maelekezo tuelekee Ubungo.
âKuna nini Ubungo?â
âNi huyu binti hatakiwi tena ndani ya Dar kwani
usalama wake bado uko hatarini!â
âSasa utampeleka wapi?â
âYeye mwenyewe atasema.â
âShemeji⦠unatakiwa kusafiri utaenda wapi kwani
ni lazima uondoke ndani ya jiji!â
âMusoma kwa mama.â Alijibu Deborah huku
machozi yakitiririka kwenye macho yake.
âYule mtu aliyetaka kukuua unamfahamu?â
âNilikuwa namuonaona tu huko nje.â
âUmeanza kumuona lini!â
âkama sikosei nimeanza kumuona maeneo ya jirani
na nyumbani akiuza kahawa baada ya kifo cha
dada!â
âMh, hawa jamaa wana mpango gani?â Aliuliza
Ommy.
âInashangaza maana kila kona wameweka mtu,
bila shaka ni watu hatari sana.â Niliongea huku
nikihesabu fedha kwa ajili ya nauli ya Debora.
Tulifika Ubumgo saa 3.02, bahati ilikuwa upande
wetu kwani tulipata nafasi kwenye gari ambalo
lilikuwa linaondoka siku ya pili.
***
ITAENDELEA
Ole wao hawa mbwa!â niliwaza. Nilizunguka kwa
hasira huku nikipiga ngumi ukuta. Naweza kusema
katika kumbukumbu zangu hakuna siku mbaya
katika maisha yangu kama siku hiyo na sidhani
kama itakuja kutokea siku kama hiyo.
Amewakosea nini? Kwanini makosa yangu yawe
mateso kwa mtu mwingine? Niliikumbuka sana
siku niliyokutana na Betty pale baa. Alikataa,
akakataaâ¦Nikambembeleza, nikambembeleza kwa
maneno ya uungwana. Maskini sikujua kuwa
uhusiano wangu ungemponza kiasi hiki. Bora
ningekutana naye baada ya mkasa huu. Nilijiuliza
swali moja ambalo lilinitisha na kuniongezea hofu.
NANI ATAFUATA?
Bila kujitambua nilikuwa nazunguka zunguka mle
ndani kwa muda wa dakika tano. Nilikuwa nahisi
kichefuchefu, mwili wote ulikuwa wa baridi. Hofu
ilikuwa imenitawala. Nilikuwa nimechanganyikiwa
vibaya, nikasikia sauti ya Ommy.
âVipi mshikaji mbona unapoteza muda?â
âIngia!â Nilimwambia kwa sauti iliyojaa utulivu.
Akaingia.
âHaa! My God, they killed herâ(Mungu wangu
wamemuua).
Akashtuka huku akiwa ameziba mdomo. Ommy
aligwaya vibaya sana. Kwa dakika kadhaa alikuwa
ametumbua macho kwa mshangao.
âTwenzetu Kajuna hii ni kesi nzito!â. Wakati nataka
kuondoka nikauona ujumbe wa karatasi ambao
nilihisi umeachwa na wauaji. Sikutaka kupoteza
muda, nikaichukua ile karatasi na kuiweka mfukoni.
Kabla sijatoka mle ndani nikaanza kuhisi
kichefuchefu kikizidi. Nikaanza kusikia maumivu ya
kichwa ghafla. Ommy hakutaka kuruhusu hali hiyo
akanishika mkono kwa nguvu na kuanza kukimbia.
Nikajikuta nikikimbia bila kutaka.
âKimbia kijana Polisi watakuja hapa muda si
mrefu!â. Tukaingia ndani ya gari kisha akaliondoa
kwa kasi. Baada ya dakika kama tano tukakutana
na gari aina ya 110 defender likiwa na askari
wapatao watano. Wote walikuwa na silaha. Ommy
aliongeza kasi ya gari kitendo kilichonifanya niwe
na hofu zaidi. âUlijuaje kama askari watafika?
Nilimuuliza kwa mshangao.
âMazingira ya ile nyumba yanaonesha kuwa
wanaishi watu wa familia tofauti haiwezekani wote
wawe wameondoka ni hofu tu ndo imewakimbiza
pale na ni lazima watoe taarifa Polisiâ. Alijibu huku
akiendelea kuongeza mwendo wa gari lile. Spidi
ilikuwa inatisha mpaka wakati fulani nilihisi kuwa
tutaingia kwenye mtaro. Kutokana na kasi ile
niliogopa kuendelea kumsemesha kwani angekosea
kitu kidogo tu sidhani kama tungesalimika. Ule
mwendo ungeweza hata kuwashawishi askari wa
usalama barabarani kulitilia mashaka gari letu.
***
Jua lilipochomoza tu, Kitu cha kwanza ilikuwa ni
kukusanya magazeti ya siku ile. Magazeti mengi
yalikuwa na vichwa ambavyo viliyafanya yauzike
kwa siku ile. DAR YATIKISWA KWA MAUAJI
MENGINE YA KUTISHA. Baadhi ya magazeti
yalijinadi. Nilikuwa najua wazi kuwa hakuna jipya
nikachukua gazeti na kuanza kusoma. Kama
nilivyotarajia zilikuwa ni habari za Mauaji ya Betty.
Mwisho habari ilimalizia kwa kusema Polisi
wanaendelea na uchunguzi mkali.
Nikatulia kidogo nikitafakari tukio la jana. Kwa
namna fulani nilianza kujishangaa mwenyewe,
nilishaanza kuzoea matukio ya kutisha kwani
katika hali ya kawaida tukio la Betty lingeniumiza
sana kichwa lakini nikajikuta likinizidishia hasira na
kutamani kukutana tena na Bonge. Sikuwa na
woga tena mbele ya Bonge, nilitamani aingie
kwenye anga zangu nimuonyeshe kazi. Nilikuwa na
hasira kiasi ambacho mtu angekuwa karibu yangu
angeweza kusikia jinsi nilivyokuwa nasaga meno.
âOle wake, ipo siku tu!â¦.â Niliwaza.
Wakati nikiwa kwenye mawazo hayo mazito ndipo
nikakumbuka kile kikaratasi ambacho nilikichukua
eneo la tukio. Huku nikianza kurudiwa na woga
ambao ulishapotea nikaanza kukisoma kile
kikaratasi.
â¦..Tunajua uko hai makosa yalifanyika, uliandaliwa
kifo kitamu tena cha heshima. Ni raha ilioje
kutangazwa kuwa umekufa kwa bomu, je! Huoni
kuwa huo ni ujasiri? Umekataa kifo kileâ¦â¦ safari
hii tunataka kukusamehe lililo muhimu kwako ili
kupata msamaha tunaomba mzigo wetuâ¦. La sivyo
tutakuuwa kinyama kuliko alivyouwawa huyo
malaya wako.Pia lazima ukumbuke kuwa picha
yako tunayo tunaweza kukuweka matatizoni.
Mtemi.
Niliusoma tena ule ujumbe, nikatikisa kichwa.
âEti watanisamehe!â Nilijikuta nikisema kwa sauti
na kumshangaza Ommy ambaye alikuwa anaingia
kutoka bafuni.
âWatakusamehe kina nani!?â Sikumjibu nikampa
kile kikaratasi asome mwenyewe. Akakisoma,
alipomaliza nikamuona akitikisa kichwa.
âWendawazimu kamili, uwape mzigo wakuache
hai!?â Alisema Ommy huku akiwa amekunja sura.
âKifo cha heshima, kifo ambacho kingetawanya
viungo vyangu huku wao wakicheka na kula kuku!â
Nilitamka kwa sauti iliyojaa utulivu.
Walinishangaza sana hawa viumbe ambao
niliwatoa katika kundi la binadamu. Vyovyote
ambavyo ungeweza kuwaita kinyume cha
binadamu na malaika kwangu ilikuwa sahihi.
Ukiwaita mbwa sawa, ukiwaita nguruwe sawa
ukiwaitaâ¦â¦.. jina lolote lile ambalo litawatoa katika
kundi la binadamu wastaarabu wao liliwastahili.
âLeo wapi?â Aliuliza Ommy.
âLeo ilikuwa siku ya kufungua mzigoâ Nilimjibu
nikamuaona ananitazama kwa mshangao.
âUnasema ilikuwa siku ya kufungua Mzigo ina
maana hatufungui tena?â
âMzigo utafunguliwa lakini sioni sababu ya
kufungua leo wakati bado tuko kwenye majonzi ya
kifo cha Betty. Sitaki nisherehekee wakati mbele
yangu kuna tatizo kubwa kiasi hiki.â
âSawa wazo lako ni zuri, kwahiyo leo tutafanya
nini?â
âLeo tuna mambo mawili Ommy, kwanza nahitaji
kuonana na Debora pili nataka kufika eneo la
msiba ili niweze kujua nini kinaendelea.â
âIna maana unataka kuhudhuria mazishi!â
âHapana Ommy, Ingawa majirani walikuwa
wananifahamu lakini ndugu wa marehemu
hawanifahamu.â
âSasa utaenda kufanya nini huko?â
âNataka kujua kilichotokea kama itawezekana.â
âUnataka kuhoji watu msibani?â
âLa, nataka kujaribu kama naweza kupata fununu
kutoka kwa waombolezaji.â
âNa huko kwa Debora?â
âHuko lazima niende kwani kuna mengi nataka
kujua kutoka kwa yule binti!â
âOk, twenzetu.â
***
Watu walikuwa wengi pale msibani. Ndugu jamaa
na marafiki walikusanyika kwa wingi, kingine
ambacho kilisababisha kuvuta zaidi watu bila
shaka ni aina ya tukio lililosababisha kifo. Mauaji
yalikuwa ya aina yake, mtu kukatwa kiungo
kimojakimoja halikuwa jambo la kawaida.
Dakika tano zilipita tukiwa ndani ya gari.
Sikuthubutu kuteremka kwani niliona kuwa ni
hatari kwangu kama wangeniona watu ambao
walikuwa wanafahamu uhusiano wangu na Betty.
Sijui ni kwanini ujasiri wa kwenda pale msibani
uliniishia ghafla.
âKajuna!â
âSema Ommy!â
âTutaganda hapa mpaka saa ngapi?â
âMi nafikiri kuna umuhimu wewe uende kule ukajue
ukweli wa mambo, kwani kila ninavyowaza nahisi
kama kuna hatari inaniandama!â
Ommy akashuka garini na kuelekea kule msibani,
pale nilipokaa nilijitahidi kuinama ili macho ya
watu yasinifikie.
Nilikaa pale kwa muda wa nusu saa nikimsubiri
Ommy ambaye alishapotea katika macho yangu
baada ya kujichanganya kwenye umati ule wa
watu. Mara moja moja niliinua kichwa na
kuchungulia kule msibani lakini sikumuona Ommy.
Nilishangaa baada ya kuona nusu saa inamalizika
bila ya kumuona Ommy.
Niliamua kujilaza kwenye siti, sikutaka kusumbua
tena kichwa changu kujiuliza mambo yanayokuja.
âOyaa vipi tena unalala!â
âSijalala nimeamua kuificha sura yangu si unajua
anaweza kutokea mtu anayenifahamu nikaibua
mambo mengine?â
âVipi una ripoti?â
âRipoti si mzuri.â
âKivipi?â Niliuliza huku kwa mara nyingine kijasho
chembamba kikianza kunitoka.
âUnatakiwa kuendelea kujificha zaidi kuliko
mwanzo.â
âMhhhh!â Nilishusha pumzi nikamuangalia Ommy
ambaye alikuwa anaonesha kutaka kuendelea
kuongea. Kisha akaendelea.
âEti wewe ndio mtuhumiwa namba moja wa mauaji
yale!â Tumbo lilishika joto ghafla baada ya kusikia
kauli hiyo. Nikaganda bila kuongea lolote huku
nikihisi kama midomo yangu imekauka.â
âInawezekana vipi?â Kwa sauti iliyokauka yenye
mikwaruzo nilijikuta nikijikakamua na kuuliza swali
hilo.
âInasemekana mara ya mwisho ulipoondoka kuna
uwezekano mkubwa kuwa mligombana na ndio
maana baada ya wewe kuondoka Betty hakuwa na
furaha mpaka kifo kilipomkuta!â
âDuh, bila shaka ni baada ya kumsimulia mkasa
wangu!â
âSawa lakini kwa majirani hilo hawakulitambua na
ndio maana wameripoti kuwa huenda yale mauaji
yalikuwa ni ya wivu wa kimapenzi!â
âDuh huu msala sasa na kwa jinsi
ninavyowafahamu polisi hawana dogo hizo taarifa
watazishikia bango utafikiri wamethibitisha!â
âLakini ni vizuri tumefahamu hatari iliyoko mbele
yako.â
âNa ndio maana nilihitaji kuja huku.â
***
Jua lilikuwa linawapungia mkono wakazi wa jiji la
Dar es salaam, giza nalo lilikuwa linapiga hodi na
kuwafanya baadhi ya wakazi wa jiji hili kuwa
katika hekaheka tofauti. Wako ambao huo ndio
ulikuwa muda wao wa kuanza shughuli huku
wengine wakiwa wanarejea mapumzikoni baada ya
kumaliza harakati zao za kimaisha.
Palepale ambapo tulisimama siku iliyopita ndipo
tuliposimama siku hii pia. Kama ilivyokuwa na siku
hii pia nilimuacha Ommy kwenye gari nikaelekea
nyumbani kwa Debora. Nilitembea haraka na kwa
kujiamini sana kwani jua lilikuwa limepotea na
hivyo nilifanikiwa kusitirika kwa kigiza chepesi
ambacho kilianza kutawala. Sikugonga kama
nilivyofanya siku ya kwanza kwani nilikuta ule
mlango wa bati la KORIE ukiwa wazi.
Kutoka nyumba kubwa nilikuwa nasikia muziki wa
taarabu ulioimbwa na marehemu Issa Matona.
Sauti ya kiutu uzima ilisikika kwa mbali ikifuatisha
wimbo huo. Taa ilikuwa inawaka chumbani kwa
Debora. Kwa kuwa kazi zake ni za usiku nilihisi
kuwa saa hizo atakuwa anajiandaa kuondoka.
Niliposogea mlangoni nikashtuka baada ya kusikia
mtu akifoka.
âUsitake kuongopa chochote wewe mbwa sema,
Kajuna alifuata nini hapa kwako?â
âMimi simfahamu huyo Kajuna.â Niliisikia sauti ya
Debora ikiwa yenye kwikwi kwa kilio
âUhai wako uko mikononi mwangu, ili uweze
kunusurika unatakiwa kuwa mkweli, yule mtu
aliyeingia hapa kwako jana alifuata nini?â
Kikapita kimya kirefu bila kujibiwa chochote.
Nikaangaza macho pale uani nikayaona matofali
ambayo yalikuwa yamepangwa sehemu moja.
Yalikuwa mengi kiasi bila shaka. Nikajitwisha moja
nakusogea pale mlangoni.
âSasa kwa kuwa hutaki kusema nitakupa kile
unachohitaji.â
âNis..s..samehâ¦. mimi simjui yulâ¦â¦.â
Hakuwahi kumaliza kauli yake niliuusukuma
mlango kwa nguvu na kuingia ndani. Yule mtu
akiwa ameduwazwa na uvamizi huo wa ghafla
alishindwa kufanya lolote licha ya kuwa na bastola
mkononi. Niliitumia Fursa hiyo kwa kumpiga kwa
tofali lile zito kichwani. Nilitumia nguvu zangu zote
nikamshushia kwa nguvu katikati ya paji lake la
uso.
âMungu wangu⦠umeua kaka nitafanya nini mimi?â
Alianza kulia yule binti.
âShhhiiiiiiiiiii!â Nilimtuliza kwa kuweka kidole cha
shahada katikati ya mdomo wangu.
Niliufunga mlango haraka kisha nikamkazia macho
makali.
âTuna maiti humu ndani na muda si mrefu
unaweza kuwa kwenye mikono yas polisi, lazima
ujue kuwa wewe utakuwa mtuhumiwa namba moja
uko tayari?â
Alionesha mshtuko zaidi nilipotoa kauli hiyo lakini
hakujibu kitu.
âNimekusaidia nimemuua mtu aliyetaka kukuua au
ulipenda ufe wewe?â Alikataa kwa kutingisha
kichwa.
âSikia we mwanamke, Chukua kilicho muhimu
kwako haraka sana kwani kuendelea kukaa hapa ni
hatari kwako.â
âNiende wapi?â
âNifuate!â
Akili yake ilionekana kutulia kidogo, akakusanya
vitu ambavyo aliona kuwa muhimu kwake
akaviweka kwenye begi kubwa. Tukaondoka
kuelekea kule aliko Ommy huku tukisaidiana
kushika begi lile kubwa.
âAaah, Shemeji!â Alishtuka Debora baada ya
kumuona Ommy ndani ya gari.
âVipi na huyu?â Aliuliza Ommy huku akionesha
mshangao wa wazi baada ya kuona nimeongozana
na Deborah tena akiwa na begi lake.
âMkuu tuondoke haraka kwani nimeua mtu huko
ndani.â
âUmeua?â Aliuliza Ommy huku akichochea moto
kwenye gari.
âIlibidi!â Nilimjibu kwa mkato.
Nikamsimulia Ommy kilichotokea kisha nikampa
maelekezo tuelekee Ubungo.
âKuna nini Ubungo?â
âNi huyu binti hatakiwi tena ndani ya Dar kwani
usalama wake bado uko hatarini!â
âSasa utampeleka wapi?â
âYeye mwenyewe atasema.â
âShemeji⦠unatakiwa kusafiri utaenda wapi kwani
ni lazima uondoke ndani ya jiji!â
âMusoma kwa mama.â Alijibu Deborah huku
machozi yakitiririka kwenye macho yake.
âYule mtu aliyetaka kukuua unamfahamu?â
âNilikuwa namuonaona tu huko nje.â
âUmeanza kumuona lini!â
âkama sikosei nimeanza kumuona maeneo ya jirani
na nyumbani akiuza kahawa baada ya kifo cha
dada!â
âMh, hawa jamaa wana mpango gani?â Aliuliza
Ommy.
âInashangaza maana kila kona wameweka mtu,
bila shaka ni watu hatari sana.â Niliongea huku
nikihesabu fedha kwa ajili ya nauli ya Debora.
Tulifika Ubumgo saa 3.02, bahati ilikuwa upande
wetu kwani tulipata nafasi kwenye gari ambalo
lilikuwa linaondoka siku ya pili.
***
ITAENDELEA