RIWAYA: Kikosi cha Pili

RIWAYA: Kikosi cha Pili

Rais alizungumza mengi na hatimae aaksitisha kikao na kuwapa vijana wake wote vibali maalumu vya kuingia kila sehemu lakini pia alitoa amri kwa jeshi la polisi kuacha kumtafuta Zedi ama Meja na waache wafanye kazi.

***

Baada ya kutoka pale walijipanga katika makundi mawili huku kila kundi likiwa na mwanamke mmoja,japo Mwita laikuwa bado hajapona lakini hakukubali kukaa alipanga kufanya jambo gumu kwa yeyote aliehusika katikanjama za kutaka kumuangamiza yeye nataifa lake.

Koplo ziga na makme wao wakawa na kazi moja tu kuhakikisha wanamfikia Zegera siku hiyo nahuko atakipata cha moto huku wakiwa sambamba na sajini Mina. Na Zedi yeye alikuwa na kazi ya kumfimia mnadhimu wa jeshi la wananchi huku akiwa sambamba na koplo mwita na AFsa.

*****

Safari ya koplo ziga na koplo makame pamoja na Mina iliwafikisha mabibo yalipo makazi ya Zegera na baada ya kupaki gari yao ikawa zamu ya kila mmoja kushuka huku wakiwa wamejipanga kuingiandani kwa namna yoyote, kuvamia au wa kukaribishwa hawakuogopa kitu.

Koplo ziga alilifikia geti na kuligonga na punde akatokea kijana mdogo kama miaka ishiri hivi akiwa na bunduki kubwa mkononi,kijana yule hakukumbuuka kuuliza chochote akapokeam pigo tata katikati ya shingo yake na kupasua koo kisha taratibu komando yule akaingia kwa ndani ya geti huku nyuma wakifuatia wababe wengine katika vita ya silaha au mkono.

Wakati wao wanaingia ndio wakti ambao Deepaklipa alikuwa anjiandaa kutoka ndani ya uzio ule na nyuma alikuwa na vijana wengine kama sita hivi.

Deepa alipiga ukulele mmoja tu wa kutoa tahadhari kwa wengine lakini alikuwa kachelewa mbele yake alikuwa kasimama Ziga na hta kumtazma tu uliapaswa ufe kabla hajakufikia lakini Depaklipa alifanya kosa kudhani bado anaubavu wa kupambana na askari yule aliejeruhiwa.

Sidhani kama aliona au kuhisi alifikaje chini ila alichishuhudia ni kuwa yupo chini na Ziga yupo kasimamana bastola mkononi na laipotaka kuinuka alishindwa na hapo alikumbuka teke moja tu alilopigwa nyuma ya uti wa mgongo na hiyop akajua hawezi kusimama katika maisha yake yote,deepklipa alilia na hapo akadhihirisha ana sura mbaya kuliko hata hamorapa nba alipotizamza pembeni akaona vijana wake wote wamewshalala na hiyo ilimanisha hawakuweza japo kupambana na wale wawili na huku mmoja akiwa kasimama mbele yake nakukamilisha idadi ya watu watatu.

“Zegera yuko wapi” swali hilo liliambatana na kofi kali lilompa nyotanyota usoni.,hakuwa na namna zaidi ya kueleza maana hata agekificha bado isingelisaidia akaona mawage mchekle kwa kuku wengi akasema

“yupo kempisk hotel kuna wageni kutoka ufaransa’ baada ya kusema hivyo ni kama vile hawakuwas wakijua ya kuwa amevunjika kiuno wakmbeba mzegamzega na kwenda kumtupa ndani ya buti ya gari kisha safari ya kempisk ikaanza.

Zedi alimpa taarifa Ziga ya kuwa hata wao wamekosa walichokuwa wanakitafuta na safari yao ipo kwelekea kwa mdhimu wa jeshi huku waziri wa michezo wakimweka kiporo na tayari taarifa ilishasambazwa kote ya kuwa viwanja vya ndege havitaruhusu kurusha ndege ya aina yoyote ile hadi hapo taarifa rasimi mitakapotoka ikulu.

K

Hakuna raia aliejua kunanini hadi wakti huo ila kila mmoja alijua tu labda kuna tatizo palhali ila hakuna liekuwa akijua tatizo ni nini.

***

ASALAAAM KUDO


NB;softcopy ipo tayari kama arosto hupendi basi tuwasiliane kwa

no;0758573660
0658564341
0624155629
 
maana watu watatu walishuka na bila kuuliza wakelekea hadi ilipo ofisi ya mapokezi na huko wakuliza chumba namba 50c na wakaelekezwa na bila kuulizwa wakapanda kuelea huko huku sajini mina akiwa makini kuwasindikiza baada ya katika nchi ya ufaransa ulinzi wa dharura.

Aliekuwa wa kwanza kuvamia chumba kile alikuwa ni koplo makame na kwa mtindo wa kujirusha akatangulia kuingia na huko akakutana na wazungu wawili wakiwa wamekaa peke yao na wao walipoona vile hawakukawia kujua hali imechafuka,wakajirusha pembeni huku kila mmoja kaijipanga kivyake,walikuwa wazoefu p[ia katika medani hiyo.

Ziga aliekuwa nyuma ya makame akjipindua kama ninja na kumfikia mmoja wapo na kwa wepesi wa karatsi akamsushia mashambulizi matatu ya nguvu ila mawili yalipanguliwa kiufundi na moja lilimpata mfaransa yule.

Haikuwa kutulia ili amsome yeye akabadili mtindio haraka n akumcharaza ngumi safi usawa wa tumbo na bila kiuliza akamchapa tena teke safi usawa wa mbavu za kulia na kumwacha akigugumia mzungu yule huku akitukana katika lugha isioeleqweka.

Koplo makame nae hakuwa haba akendeleza ubabe kwa baradhuli yule aliejifanya anajua kutandaza mkono lakini hqakujua anacheza na watu wanaopenda kifo na ndani ya dakika ya pili tu tayari alikuwa anaienda kuikata roho baada ya kupigwa numi yenye uzito wa kilo saba hivi kwenye chembe ya moyo na kumpa shida kupumua kisha ikamaliziwa nyinginew ilituia kisogoni na kuharibu mfumo wa ubongo akwa maiti huku akimwacha makame akimgeukia Ziga amabe nae alikua akienda kuua lakini akwahi kumzuia.

“Zegera yuko wapi’ aliuliza makame

“%%@$^” alijibu kilinggala na hapo make akatambua kuwa wapo na kikako huko Malaika hoteli akampasha habari hiyo Ziga na ziga akatoa pigo la mwisho lililoondoka nauhai wa bazazi yule


asalaam Kudo
 
Zedi alikuwa anaingia lugalo na akaonesha kitambulisho chake kutoka ikulu na hapo hakutaka maelezo mengi akamtafuta Meja jenero kisha akampasha habari na ruhusa ikatolewa ya kumkamata mnadhimuwa jeshi laini ajabu walipofika katika makazi yake hawakumkuta na hapo ikawa ni kasheshe jeshi zima likaagizwa kumtafuta msaliti yule.

Zedi akiwa na Mwita wakapata taarifa kuwa kuna ndege itaingia dakika chache ikiwa imebeba Papaa deo Mukamba na hiyo ikawa ni fahari kwao,wakaacha wanajshi wanamtafuta msaliti wao wakelekea uwanja wa ndege kumpokea shetani wa kikongo.

****

Ndege ilitua salama na abiria wakaanza kushuka na haikuchukua muda waliemhitaji wakamwona,alikuwa ni papaa Deo Mukamba.

Zedi alijipamnga kuwakabili walinzi wake huku Mwita akijaribu kuwafuata watu walionda kumpokea bazazi yule.

Ilianza kama mzaha gari jesi likagongwa kioo cha mbele waliomo wakatahamaki wakashuka kwa gadhabu kumkabili mpuuzi wao aliekuwa kafungwa bandeji upande wa kichwa ila hawakujua kwanini Mwita alienda cuba kujifunza ukomando.

Aliekuwa upande wa kulia akawahi kumkwida shati lakini dahmira yake haikufanikiwa akijikuta akichezea ngumi zisizo na idadi na kumwacha akitepeta kama mlenda.

Mwita alimwona yule aliekuwa upnde wakushoto akijaribu kuchomoa bastola na huku akipiga hatua kumfikia yeye akaamua kumrahisishia safari akaruka upande wa mbele wa gari na katua mbele yake na bila kuuliza akanza kumwangushia mvua ya makofi ya miguu na dakika iliofuata tayari alikuwa maiti.

Kile kitendo cha haraka vile kilichukua dakika moja hivi na kilimwacha Afsa akiwa hajui ampe nani hongera kati ya Zedi na mwita maana wote walikuwa wamefanya matukio ndani ya dakika moja na tayri papaa deo mukamba alikuwa mikononi mwao na niyeye tu alipaswa kuwasha gari wapate kuondoka.

*****

Papaa Deo mukamba alikuwa katikati ya watu saba na alitakiwa kusemayote katika mpango tikisa unaoendelea nchini Tanzania.

Aliamua tu kusema ukweli maanahakuwa nanamna na hta shehena ya silaha iliokuwa bandarini alisema pia na alisema muda huo kuna watu wmenda kuzitoa laini pia alisema kuhusu kambi ya mafuzo ya kijehi ilioko kitunda na alisema pia ufadhili wao unafanywa na wafaransa na wanataka kuchimba madini ya Urano na dhahabu huku wakifadhili vita mabayo itakuwa haikomi kama nchini Kongo.laiki pia alisma kuna kikao kinendelea huko kitunda cha mwakilishi wa wafaransa na mabazazi walioko hapa ncini.

Taarifa yake ilifanyiwa kazi haraka na askari jeshi wapatao mia moja walitumwa kwenda bandarini kuzuia shehena ya silaha lakini pia kikosi cha watu saba kiliondoka kwenda kukabiliana na wanajeshi wanafundishwa huko kitunda ambao hawakuzidi miamoja wakiongozwa na Ibra mbaya.

*****

asalaam kudo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom