Dam55
JF-Expert Member
- Oct 8, 2015
- 5,592
- 11,831
RIWAYA: JANGA
MTUNZI: richard MWAMBE
SEEMU YA 1
I
Saa 5: 7usiku…
DAR ES SALAAM
MVUA ILIYOAMBATANA NA RADI iliendelea kunyesha kwa hasira katika jiji la Dar es salaam, hakukuwa na nyota hata moja iliyong’aa siku hiyo wala mbalamwezi yenye nguvu ya kulishinda wingu zito lililofunga anga la jiji hilo.
Kila mmoja alijifungia ndani ya nyumba yake, kimya, akisikiliza sauti kali za radi na mng’ao mkali wa radi uliongaza ndani na kufukuza giza nene lililovijaza vyumba vya nyumba hizo. Michoro ya kutisha ilionekana angani kana kwamba mbingu ilikuwa ikipasuka, hofu.
“Ngrrrrrrrrrr! Ngrrrrrrrrrrr! Ngrrrrrrrrrr!” kelele ya simu ilisikika katika nyumba moja kubwa ya iliyo kandokando tu mwa barabara na kumkurupusha mwenyenayo toka kitandani, akaiendea meza ndogo na kuinyakuwa simu iliyokuwa ikifanya fujo hizo.
“Hallo!” akaita na kutulia akisubiri upande wa pili uongee. Badala ya kusikia jibu alihisi kupumua kwa nguvu kwa mtu aliye upande wa pili.
“Nilikuahidi kukupigia simu usiku huu kama unakumbuka, nimetimiza ahadi yangu. Nafikiri sasa utakuwa tayari kunisikiliza tofauti na mara zote nilizokuwa nikija ofisini kwako,” sauti ya upande wa pili ikaongea kwa kukwaruza.
“We ni nani? Na mbona unanifuatafuata sana? Nimeshakwambia sitaki na siwezi,” yule mmiliki wa nyumba ile akajibu.
“Sikiliza!” ile sauti ikaendelea kusema, “Huwa hatubahatishi katika kazi yetu, lakini inaonekana unataka kuwa kikwazo. Kwa nini unataka kufa masikini ilhali utajiri unakuja mpaka mlangoni kwako na unaukimbia?
Unataka mwisho wa siku umlaumu Mungu kuwa hakukupa? Acha ujinga! Hii ni nafasi yako ya mwisho,” ile sauti ikasema. Na yule jamaa akatulia na simu yake mkononi alipotupa jicho dirishani alishuhudia tu matone ya mvua yakigonga kioo cha dirisha na kugeuka kuwa michirizi mingi ya maji, hakuweza kuona taswira sahihi ya nje.
“Nisikilize…” akamwambia huyo wa upande wa pili, “kama ninyi mmezoea kufanya hayo, fanyeni na hao. Si kwamba sijui, najua vyema kuwa huo ni mchezo mliouzoea, mnaumiza wananchi kwa sababu ya pesa zenu, mnaua mamia ya watu kwa sababu ya uchu wenu wa utajiri, mnadhulumu na kupora haki ya wananchi kwa sababu yakutaka ufahari wa maisha…”
“E! E! E! E! umekuwa mhubiri siyo? Acha upumbavu, wewe ni mtu muhimu katika hili na unajua, sheria ya nchi katika hili iko juu yako ni kusema neno tu na roho zetu zitapona, unajifanya una shingo ngumu.
Hebu sogea dirishani, sogea kabisa,” ile sauti ilimwomba mwenye nyumba hiyo kusogea, akaitii na kulifikia lile dirisha kubwa la alluminium, “Fungua dirisha,” ile sauti ikamwambia naye akafungua na nje ya nyumba yake akakuta gari imeeegshwa, gari ya kisasa BMW 605 mpya kabisa hata haikuwa na namba bado.
“Umeona hiyo gari? Hiyo ni ya kwako na kesho unaweza kuichukua na kuitumia, nitakuelekeza wapi utapata namba zake,” ile sauti ikamwambia na yule bwana akabaki kapigwa butwaa, akatazama huku na huku hakuona mtu eneo lile, akili yake ikauma kujiuliza yuko wapi huyo anyeongea lakini hakumuona.
“Nimesema sitaki! Sitaki! Sitaki! Nitasimamia haki na haki ndiyo itaamua kila kitu katika hili…” akaongea kwa kelele huku akirudi katika ile meza ndogo.
“Sawa! Swala la mwisho usipokubali hili basi utakuwa umekubali lingine, nenda karibu na mlango wako wa kuingia sebuleni,” ile sauti ilimwamuru lingine, akasukuti na kuitii, akaufikia mlango… “ angalia chini, kuna nini … okota!”
Yule mwenye nyumba akaokota kitu kama broshua, akaigeuza geuza, sasa hiki ni nini? Akajiuliza, mbona sielewi, akahofu.
“Usijiulize, ila hapo una uchaguzi mmoja tu, unaona nini kwenye kurasa ya juu?” ile sauti ikauliza na yule jamaa akaitazama ile broshua ndogo, kulikuwa na picha ya nyumba nzuri , nyumba ya kisasa, nyumba iliyosheheni kila kitu.
“Itakuwa yako hiyo kesho tu ukikubali kutekeleza hili nilitakalo mimi…”
“Sitaki na nitahakikisha nakutia katika mkono wa sheria,” yule jamaa akaongea kwa ukali huku akirudi mahala pale palipokuwa na kile kitako cha simu.
“Basi, kama hutaki na hicho bila shaka umechagua kurasa ya pili, kwa heri,” ile sauti niliposema hayo tu simu ikakatika. Yule bwana akageuza nyuma ile broshua na kukuta picha mtu mwenye fuvu tupu aliyevalia kanzu jeusi na mikononi mwake kashikilia msalaba uliondikwa jina lake yaani la mmiliki wa nyumba hiyo. Hofu ikamwingia, mwili ukamtetema, macho yake yapepesa kama mtu anayetaka kuona kitu kisichoonekana.
Wazo likamjia kupiga simu polisi, alipobofya ile simu na kuweka sikioni hakusikia chochote, simu haifanyi kazi, akakimbilia ile ya mkononi alipoiinua chaji imekwisha na wakati huo umeme umekatika, akabaki kabutwaika huku sura yake ikisawajika kwa mawazo.
Mchoro wa kutisha ukakatiza anga na mng’ao wake ukafanya mwanga mkali ulioangaza hata sisimizi yule ambaye yuko kwenye ardhi akitembea kwa tabu, kisha ukafuata muungurumo mkali na mzito wa radi uliotetemesha nyumba kwa sekunde kadhaa. Kisha mti mkubwa uliokuwa nje ya nyumba hiyo uling’oka na kuanguka na kufanya kishindo kikubwa.
Wazo lililomjia mwenye nyumba ni kutoka nje na kuangalia, maana ile gari aliyoooneshwa pale nje ilikuwa imeegeshwa eneo hilo ulipo huo mti. Itakuwaje kama gari ya watu imeangukiwa na mti? Akawaza huku hofu na mashaka vikimtawala, alipofungua mlango akatanabahi kutoikuta ile gari mahali pale.
Akiwa bado haelewi kinachotukia, akahisi mkono ukimshika begani.
“Eeeeeeeee! Nooooooo!” akapiga kelele na alipogeuka nyuma alikutana uso kwa uso na mke wake kipenzi Bi. Zuhura.
“Nini mume wangu, kimekupata nini? Mbona sikuelewi?” aliingiwa na mashaka na kumuuliza mumewe ambaye bado alikuwa ndani ya pajama.
“Aaaaaah! Aaaaaaah! Mke wangu, aaaaaah! Wanataka kuniua,” akalalama.
“Akina nani? Mbona hapa uko peke yako?” akauliza Bi. Zuhura.
“Siwajui mke wangu ila wanataka kuniua, toa taarifa polisi,” akaendelea kulalama.
Bi. Zuhura akakumbuka kuwa mumewe tangu utoto wake alikuwa na ndoto mbaya za kumfanya atoke chumbani na kutembea peke yake usiku wa manane nje ya nyumba yao, tatizo hili aliambiwa kuwa limekwisha baada ya mumewe huyo kufanyiwa dawa za kienyeji za kwao Tanga lakini akashangaa leo hii kwa mara ya kwanza tangu aoelewe naye anakutana na haya. Atakuwa amerudia ndoto zake za utotoni, akawaza na kumshika mkono mumewe.
“Twende tukalale mume wangu” akamwambia.
“Nimekwambia toa taarifa polisi kuna watu wanataka kuniua,”
“Nitatoa mume wangu subiri pakikucha,” Bi. Zuhura akajibu huku akimkokota mumewe mpaka kitandani na kumliwaza kwa mahaba mazito ili kumsahaulisha masaibu hayo ya ndoto aliyokuwa akiota.
SIKU ILIYOFUATA
JUA TAMU LA ASUBUHI lilipenya kwenye mapazia mazuri ya nyumba ya Jaji Shekibindu na mkewe Bi. Zuhura. Mvua ilikatika usiku wa manane na kuacha mito ya maji ya asili ambayo ilisahaulika na wakazi wa mji huu ikitiririka kuelekea baharini. Ilikuwa ni adha, adha kubwa isiyo kifani. Nje ya dirisha hilo Bi. Zuhura aliweza kuona watu wakitembea viatu mkononi, magari yakiwa yamekwama kwenye madimbwi makubwa ya maji, maduka yakiwa bado hata kufunguliwa.
Akatazama saa ya ukutani, ilikuwa saa moja na nusu ya asubuhi, akarudisha macho kwa mumewe, akakuta bado anakoroma akiwa katikati ya usingizi mzito. Polepole akamwamsha na mtu mzima huyo akaamka pasi na pingamizi lolote.
ITAENDELEA
MTUNZI: richard MWAMBE
SEEMU YA 1
I
Saa 5: 7usiku…
DAR ES SALAAM
MVUA ILIYOAMBATANA NA RADI iliendelea kunyesha kwa hasira katika jiji la Dar es salaam, hakukuwa na nyota hata moja iliyong’aa siku hiyo wala mbalamwezi yenye nguvu ya kulishinda wingu zito lililofunga anga la jiji hilo.
Kila mmoja alijifungia ndani ya nyumba yake, kimya, akisikiliza sauti kali za radi na mng’ao mkali wa radi uliongaza ndani na kufukuza giza nene lililovijaza vyumba vya nyumba hizo. Michoro ya kutisha ilionekana angani kana kwamba mbingu ilikuwa ikipasuka, hofu.
“Ngrrrrrrrrrr! Ngrrrrrrrrrrr! Ngrrrrrrrrrr!” kelele ya simu ilisikika katika nyumba moja kubwa ya iliyo kandokando tu mwa barabara na kumkurupusha mwenyenayo toka kitandani, akaiendea meza ndogo na kuinyakuwa simu iliyokuwa ikifanya fujo hizo.
“Hallo!” akaita na kutulia akisubiri upande wa pili uongee. Badala ya kusikia jibu alihisi kupumua kwa nguvu kwa mtu aliye upande wa pili.
“Nilikuahidi kukupigia simu usiku huu kama unakumbuka, nimetimiza ahadi yangu. Nafikiri sasa utakuwa tayari kunisikiliza tofauti na mara zote nilizokuwa nikija ofisini kwako,” sauti ya upande wa pili ikaongea kwa kukwaruza.
“We ni nani? Na mbona unanifuatafuata sana? Nimeshakwambia sitaki na siwezi,” yule mmiliki wa nyumba ile akajibu.
“Sikiliza!” ile sauti ikaendelea kusema, “Huwa hatubahatishi katika kazi yetu, lakini inaonekana unataka kuwa kikwazo. Kwa nini unataka kufa masikini ilhali utajiri unakuja mpaka mlangoni kwako na unaukimbia?
Unataka mwisho wa siku umlaumu Mungu kuwa hakukupa? Acha ujinga! Hii ni nafasi yako ya mwisho,” ile sauti ikasema. Na yule jamaa akatulia na simu yake mkononi alipotupa jicho dirishani alishuhudia tu matone ya mvua yakigonga kioo cha dirisha na kugeuka kuwa michirizi mingi ya maji, hakuweza kuona taswira sahihi ya nje.
“Nisikilize…” akamwambia huyo wa upande wa pili, “kama ninyi mmezoea kufanya hayo, fanyeni na hao. Si kwamba sijui, najua vyema kuwa huo ni mchezo mliouzoea, mnaumiza wananchi kwa sababu ya pesa zenu, mnaua mamia ya watu kwa sababu ya uchu wenu wa utajiri, mnadhulumu na kupora haki ya wananchi kwa sababu yakutaka ufahari wa maisha…”
“E! E! E! E! umekuwa mhubiri siyo? Acha upumbavu, wewe ni mtu muhimu katika hili na unajua, sheria ya nchi katika hili iko juu yako ni kusema neno tu na roho zetu zitapona, unajifanya una shingo ngumu.
Hebu sogea dirishani, sogea kabisa,” ile sauti ilimwomba mwenye nyumba hiyo kusogea, akaitii na kulifikia lile dirisha kubwa la alluminium, “Fungua dirisha,” ile sauti ikamwambia naye akafungua na nje ya nyumba yake akakuta gari imeeegshwa, gari ya kisasa BMW 605 mpya kabisa hata haikuwa na namba bado.
“Umeona hiyo gari? Hiyo ni ya kwako na kesho unaweza kuichukua na kuitumia, nitakuelekeza wapi utapata namba zake,” ile sauti ikamwambia na yule bwana akabaki kapigwa butwaa, akatazama huku na huku hakuona mtu eneo lile, akili yake ikauma kujiuliza yuko wapi huyo anyeongea lakini hakumuona.
“Nimesema sitaki! Sitaki! Sitaki! Nitasimamia haki na haki ndiyo itaamua kila kitu katika hili…” akaongea kwa kelele huku akirudi katika ile meza ndogo.
“Sawa! Swala la mwisho usipokubali hili basi utakuwa umekubali lingine, nenda karibu na mlango wako wa kuingia sebuleni,” ile sauti ilimwamuru lingine, akasukuti na kuitii, akaufikia mlango… “ angalia chini, kuna nini … okota!”
Yule mwenye nyumba akaokota kitu kama broshua, akaigeuza geuza, sasa hiki ni nini? Akajiuliza, mbona sielewi, akahofu.
“Usijiulize, ila hapo una uchaguzi mmoja tu, unaona nini kwenye kurasa ya juu?” ile sauti ikauliza na yule jamaa akaitazama ile broshua ndogo, kulikuwa na picha ya nyumba nzuri , nyumba ya kisasa, nyumba iliyosheheni kila kitu.
“Itakuwa yako hiyo kesho tu ukikubali kutekeleza hili nilitakalo mimi…”
“Sitaki na nitahakikisha nakutia katika mkono wa sheria,” yule jamaa akaongea kwa ukali huku akirudi mahala pale palipokuwa na kile kitako cha simu.
“Basi, kama hutaki na hicho bila shaka umechagua kurasa ya pili, kwa heri,” ile sauti niliposema hayo tu simu ikakatika. Yule bwana akageuza nyuma ile broshua na kukuta picha mtu mwenye fuvu tupu aliyevalia kanzu jeusi na mikononi mwake kashikilia msalaba uliondikwa jina lake yaani la mmiliki wa nyumba hiyo. Hofu ikamwingia, mwili ukamtetema, macho yake yapepesa kama mtu anayetaka kuona kitu kisichoonekana.
Wazo likamjia kupiga simu polisi, alipobofya ile simu na kuweka sikioni hakusikia chochote, simu haifanyi kazi, akakimbilia ile ya mkononi alipoiinua chaji imekwisha na wakati huo umeme umekatika, akabaki kabutwaika huku sura yake ikisawajika kwa mawazo.
Mchoro wa kutisha ukakatiza anga na mng’ao wake ukafanya mwanga mkali ulioangaza hata sisimizi yule ambaye yuko kwenye ardhi akitembea kwa tabu, kisha ukafuata muungurumo mkali na mzito wa radi uliotetemesha nyumba kwa sekunde kadhaa. Kisha mti mkubwa uliokuwa nje ya nyumba hiyo uling’oka na kuanguka na kufanya kishindo kikubwa.
Wazo lililomjia mwenye nyumba ni kutoka nje na kuangalia, maana ile gari aliyoooneshwa pale nje ilikuwa imeegeshwa eneo hilo ulipo huo mti. Itakuwaje kama gari ya watu imeangukiwa na mti? Akawaza huku hofu na mashaka vikimtawala, alipofungua mlango akatanabahi kutoikuta ile gari mahali pale.
Akiwa bado haelewi kinachotukia, akahisi mkono ukimshika begani.
“Eeeeeeeee! Nooooooo!” akapiga kelele na alipogeuka nyuma alikutana uso kwa uso na mke wake kipenzi Bi. Zuhura.
“Nini mume wangu, kimekupata nini? Mbona sikuelewi?” aliingiwa na mashaka na kumuuliza mumewe ambaye bado alikuwa ndani ya pajama.
“Aaaaaah! Aaaaaaah! Mke wangu, aaaaaah! Wanataka kuniua,” akalalama.
“Akina nani? Mbona hapa uko peke yako?” akauliza Bi. Zuhura.
“Siwajui mke wangu ila wanataka kuniua, toa taarifa polisi,” akaendelea kulalama.
Bi. Zuhura akakumbuka kuwa mumewe tangu utoto wake alikuwa na ndoto mbaya za kumfanya atoke chumbani na kutembea peke yake usiku wa manane nje ya nyumba yao, tatizo hili aliambiwa kuwa limekwisha baada ya mumewe huyo kufanyiwa dawa za kienyeji za kwao Tanga lakini akashangaa leo hii kwa mara ya kwanza tangu aoelewe naye anakutana na haya. Atakuwa amerudia ndoto zake za utotoni, akawaza na kumshika mkono mumewe.
“Twende tukalale mume wangu” akamwambia.
“Nimekwambia toa taarifa polisi kuna watu wanataka kuniua,”
“Nitatoa mume wangu subiri pakikucha,” Bi. Zuhura akajibu huku akimkokota mumewe mpaka kitandani na kumliwaza kwa mahaba mazito ili kumsahaulisha masaibu hayo ya ndoto aliyokuwa akiota.
SIKU ILIYOFUATA
JUA TAMU LA ASUBUHI lilipenya kwenye mapazia mazuri ya nyumba ya Jaji Shekibindu na mkewe Bi. Zuhura. Mvua ilikatika usiku wa manane na kuacha mito ya maji ya asili ambayo ilisahaulika na wakazi wa mji huu ikitiririka kuelekea baharini. Ilikuwa ni adha, adha kubwa isiyo kifani. Nje ya dirisha hilo Bi. Zuhura aliweza kuona watu wakitembea viatu mkononi, magari yakiwa yamekwama kwenye madimbwi makubwa ya maji, maduka yakiwa bado hata kufunguliwa.
Akatazama saa ya ukutani, ilikuwa saa moja na nusu ya asubuhi, akarudisha macho kwa mumewe, akakuta bado anakoroma akiwa katikati ya usingizi mzito. Polepole akamwamsha na mtu mzima huyo akaamka pasi na pingamizi lolote.
ITAENDELEA