Riwaya: Hekaheka za Komando Zedi Wimba na Jasusi Honda huko Somalia

Hiv huyu remi si ndiye yule mdada alietokea Rwanda akafikia nyegezi mwanza
RIWAYA; URITHI WA GAIDI

NA; BAHATI MWAMBA

SIMU; 0758573660

SEHEMU YA KUMI NA NNE




“hakuna mlinzi anaeweza kutembea katikati ya mvua kubwa hii” Alijisemea!!

Ndipo alipoamka na pia akahisi kitu kikiwaka na kuzima kichwani kwake.

Akakitoa kifaa kile na kukibonyeza kikaacha kumweka.

“tatatata…ti….tatatata..ti..”
Bado aliendelea kusikia sauti ile na sasa ilizidi kukaribia kwenye hema lake.

Roho ikamdunda!!

Kule nje yule bwana aliendelea kuhangaika kutafuta mwelekeo wa mawimbi na bado alijua mawimbi yale yalitokea kwenye moja ya mahema aliokuwa amesimama kati yake.

Akawa anapiga hatua moja mbele na hatua moja nyuma,yani bila kutoka pale alipokua lengo likiwa ni kujua mweleko sahihi wa mawimbi mageni.

Hatimae alijua ni upande gani mawimbi yale yalikuwa.

Honda nae kule ndani alikuwa amesimama karibu kabisa na mlango na kwa kusaidiwa na mwanga wa radi, aliweza kuona mtu akiwa hatua chache kutoka mlangoni kwake na alikuwa anahangaika huku na huko.

Honda akili ikamjia na haraka akawasha kidubwasha kile na kukirudisha ndani ya kikasha cha risasi kisha akaruka hatua kubwa na kuangukia kitandani na kulala.

“Aisee hawa watu wana mitambo yenye nguvu sana” Alijiwazia huku akimalizia kujifunika shuka.

Dakika moja badae, yule bwana aliingia mule ndani na bila kujali kama alikuta mtu au la, yeye aliendelea kukagua hapa na pale.
Hatimae kile kifaa kilianza kutoa mlio mkubwa mfululizo na Honda akaamka na kukutana na kisu kikiwa shingoni mwake.

“ulikuja kutupepeleza sio? Alihoji yule bwana huku akitumia mkono mwingine kuwasiliana kwa simu ya upepo.

Hazikupita dakika tatu wapiganaji zaidi ya sita wenye mitutu waliingia mle ndani na kumweka kati Honda.

Isa nae akaingia.

Yule bwana akampa maelekezo kwa lugha ya kienyeji na kisha akamwonesha kifaa kile chenye muundo wa risasi alichokikuta kwenye viatu vya Honda.

“Hii si ni ile ya kule melini?” Alihoji Isa huku akimtizama Honda.

“Ndo yenyewe! Kwani kuna nini mbona navamiwa usiku huu? Alihoji Honda.

“Aah ni usalama tu unazingatiwa ila usijali” Alisema Isa huku akiwapa ishara wapiganaji wake nao wakashusha silaha zao.

“Wale wazungu walikuwa ni mamluki na tulikuwa sahihi kuwapoteza, walituwekea mtego wa kujua tulipo aisee” Alisema Isa huku akimwangalia Honda ambae wakati huo alikuwa anafanya jitihada za kunyanyuka kitandani.

Isa aliongea na vijana wake kuwaelesha na kisha wakasambaratika mle hemani na kukiharibu kifaa kile.

Honda alipumua kwa afueni na kurudi kujilaza na hakulapua lau tone la usingizi hadi ilipotimu ahsubuhi.

***
Ahsubuhi ilikuwa na mengi ya kufanya kwa pande zaidi ya tatu.

Honda na wapiganaji wa AIAI waliamka wakiwa na lengo moja la kufanya mauaji katikati ya Mogadishu huku wadunguaji wakifanya zoezi kwa ajili ya kukamilisha kazi yao mida ya jioni ya siku hiyo.

Upande mwingine ulikuwa ni ule wa Zedi Wimba na Haji Makame ambao wao lengo lao lilikuwa ni kuvuruga mipango ya wauaji na kumuokoa Rais bila uwepo wao kujulikana popote.

Kundi lingine lilikuwa ni kundi la ulinzi na usalama wa viongozi wote watakao hudhuria mkutano huo na bila kujua lolote linalopangwa, wao waliendelea na taratibu zao kama kawaida kuhakikisha usalama upo kwa asilimia zote.

Hatimae wakati uliwadia!!

Maeneo yote yalikuwa na ulinzi wa kutosha kuhakikisha eneo la Lamada na viunga vyake lipo salama.

Misafara ya viongozi mbalimbali ilianza kuwasili kwenye hotel Lamada.

Aliingia Rais wa Somalia kisha akafuatia Rais wa Kenya na wajumbe wake.

Katika majengo matatu yaliokuwa yanatazamana na hotel ile, kulikuwa kuna makundi mawili yenye malengo tofauti.

Kundi la kwanza lilikuwa lile la wadunguaji ambao kila mmoja alikuwa amekaa sehemu yake kuhakikisha mlengwa wao hawamkosi na walitaka kufanikisha azima yao hiyo wakati rais huyo atakapokuwa akitoka ndani ya hotel.

Kundi lingine lilikuwa ni lile ambalo lilikuwa na watu wawili tu na wao walikuwa kwenye chumba cha hotel nyingine wakiwa na chupa yao iliokuwa na unga wa chupa nyingine na vitu vingine kadhaa ambavyo vingehakikisha sauti iliokusudiwa inatoka.

Walikaa wakihakikisha kabisa kila tukio linaloendelea kule chini linatazamwa na wao mubashara bila kukosa hata nukta.

Muda wa kuanza kikao ulianza na watu mbalimbali walikuwa wapo na radio zao wakisikiliza.

Waliongea viongozi kadhaa na hatimae wakati rais wa Kenya anataka kuzungumza; Zedi na Haji walikonyezana.

Na hatua iliofuata ilikuwa ni kufungua dirisha kisha wakapachika chupa ya bia kwenye mdomo wa bunduki aina ya gobole kisha wakafyatua kuelekea kule ilipokuwa Lamada hotel na kilichofuata ni sauti kubwa ilioambatana na moshi mzito.

Ilikuwa ni taharuki iliozuka,walinzi wa viongozi hawakujua kimetokea nini na harakati zao zilikuwa ni kuhakikisha hakuna madhara yanayotokea kwa viongozi hao.

Wadunguaji nao walibaki wakiwa wamebutwaika wasijue kilichotokea.

Isa ambae alikuwa karibu ya eneo la tukio na Honda; walishuhudia mtafaruku usiosemekana.
“Shukeni wote, na msiache alama” Isa alitahadharisha vijana wake kisha akaondoa gari na wakarejea porini huku wakiwa wameshindwa kuekeleza mpango wao.

Zedi na Haji nao walikuwa wako mbali na eneo lile huku wakiwa wanashingilia ushindi wao kwa kuvuruga mpango ule ambao hawakuwa na hakika kama walikuwa sahihi,ila walijua wamefanya kile walichopaswa kufanya.

Na kazi ikabaki ni kumtafuta Imamu Shafi’I wa msikiti wa Masjid nuur.


***

- TANZANIA-

Ahsubuhi ile ilikuwa ni ahsubuhi mbaya kabisa kwa Remi.

Alilia peke yake na kulikuwa hakuna wa kumsaidia wala kumuonea huruma.

Alilia na Mungu wake.

Nchi nzima kulitapakaa taarifa zake na picha zake, mitandao ya kijamii ilikuwa ndio taarifa kuu.

Alikuwa amesahau kuzima simu yake na mara ikaita.

Namba zilikuwa ni za Kagoshima.

“Nadhani kuna haja ya wewe kujisalimisha kituoni”
Alisema Kagoshima.

“Muda ukifika nitafanya hivyo ila sio sasa” Alijibu kinyonge Remi.

“Ila tambua serikali ina mkono mrefu itakufikia tu” Alisema Kagoshima.

“Haina shida” Alijibu Remi na kukata simu.

Alishusha pumzi na kuzishusha, alihitaji kuhama pale mana si pahali salama tena kwake.

Walikuwa na nyumba nyingine mwananyamala kisiwani.

Wakati anatoka kwenye ile nyumba alihisi hayuko peke yake,licha ya kujifunika kanga juu hadi chini.
Licha ya kuhisi huko lakini kamwe hakuona mtu mwenyewe yupo umbali gani nae mana watu walikuwa ni wengi nyuma yake.

Alichukua bodaboda na kwenda kushukia komakoma na kuanza kutupa tena miguu yake kwa hatua za mashaka tele.

Hakufika hata mbali, alihisi kitu kidogo kikipenya kwenye shingo yake na kilichofuata hakujua licha ya kuhisi akiangukia mikononi mwa mtu.

Remi mbio zake ziliishia ukingoni.

***

Tukutane wakati mwingine

Sent using Jamii Forums mobile app
 
RIWAYA; URITHI WA GAIDI

NA; BAHATI MWAMBA

SIMU; 0758573660


SEHEMU YA KUMI NA TANO



***

- TANZANIA-

Ahsubuhi ile ilikuwa ni ahsubuhi mbaya kabisa kwa Remi.

Alilia peke yake na kulikuwa hakuna wa kumsaidia wala kumuonea huruma.

Alilia na Mungu wake.

Nchi nzima kulitapakaa taarifa zake na picha zake, mitandao ya kijamii ilikuwa ndio taarifa kuu.

Alikuwa amesahau kuzima simu yake na mara ikaita.

Namba zilikuwa ni za Kagoshima.

“Nadhani kuna haja ya wewe kujisalimisha kituoni”
Alisema Kagoshima.

“Muda ukifika nitafanya hivyo ila sio sasa” Alijibu kinyonge Remi.

“Ila tambua serikali ina mkono mrefu itakufikia tu” Alisema Kagoshima.

“Haina shida” Alijibu Remi na kukata simu.

Alishusha pumzi na kuzishusha, alihitaji kuhama pale mana si pahali salama tena kwake.

Walikuwa na nyumba nyingine mwananyamala kisiwani.

Wakati anatoka kwenye ile nyumba alihisi hayuko peke yake,licha ya kujifunika kanga juu hadi chini.
Licha ya kuhisi huko lakini kamwe hakuona mtu mwenyewe yupo umbali gani nae mana watu walikuwa ni wengi nyuma yake.

Alichukua bodaboda na kwenda kushukia komakoma na kuanza kutupa tena miguu yake kwa hatua za mashaka tele.

Hakufika hata mbali, alihisi kitu kidogo kikipenya kwenye shingo yake na kilichofuata hakujua licha ya kuhisi akiangukia mikononi mwa mtu.

Remi mbio zake ziliishia ukingoni.

***

Sajenti Kobelo; aliegesha gari kwenye uwanja wa ccm mwinjuma kisha akatembea kwa miguu kuelekea kilipokuwa kituo cha polisi.

Baada ya kufanya taratibu zote za kujitambulisha na kueleza nia yake pale kituoni, hatimae alielekezwa ilipokuwa ofisi ya marehemu Vengu ambayo ilikuwa inakaimiwa na mtu mwingine wakati huo.

Aliingia na kumkuta mtu yule ambae alikuwa na cheo sawa na chake.

Itifaki ilizingatiwa kisha akasema kilichompeleka pale.

Alipewa faili ambalo alikuwa akilitumia Sajini Vengu.

Alianza kuyakagua kwa umakini wa hali ya juu sana.

Alikutana na maelezo yaliokuwa yameandikwa na Remi. Pia alisoma namna tukio la kutekwa kwa mwandishi lilivyomhusanisha na ofisi za uchunguzi wa mambo kale na pia ni kwanini mtuhumiwa alitakiwa kuwa Remi.

Alitoa kitabu chake kidogi a kuanza kuandika yale alioona ni muhimu kwake na pia alikutana na namba za simu za Remi.

Alizinakili pia kisha akawa ametoka na picha mbili tofauti.

Remi anahusika na pia Remi hahusiki.

Kwanini?

Kwa sababu Remi aliwasiliana na Davis Minja na kumwelekeza jambo hivyo anahusika kwa asilimia kadhaa kujua alipo mwandishi yule.

Lakini pia Remi anaweza kuwa hahusiki kwa sababu asingeweza kufanya tukio akiwa ofisini kwake.
Hoja ya mwisho ilikuwa na mashiko kidogo.

Lakini kuna kitu kingine kilimpa maswali…
Kwa nini Davis afuatiliwe na kisha atekwe kwenye ofisi za Remi?

Remi Haji Makame!!
Aliliandika jina lile kwenye kitabu chake kisha akaaga na kuondoka.

Lakini kabla hajatoka mle ofisini akamgeukia ofisa aliemkuta mle ndani.

“Kama kuna mtu atakuja kujitambulisha kwako kwa jina la Kenge; basi mwambie lolote ila sio hizo kablasha nilizokagua” Alisema sajenti Kobelo.

Ofisa yule alikubali.

Sajenti alitoka na kuelekea alikokuwa amepaki gari lake, akapanda na kuondoka lengo likiwa ni kuelekea nyumbani kwa Sajini Vengu ambae msiba ulikuwa umewekwa kwao kimara na yeye alikuwa anaishi mwananyamala kwa Bibi titi.

Njiani yalipita maswali kadhaa kichwani kwake.

Alihitaji kumjua kwanza Remi.
Haji Makame ni jina la watu wa Pemba na kiasili ni waislam na Remi ni jina ambalo halijasidifu imani yoyote ila si jina lenye asili ya huko Pemba; sasa vije tena Remi iungane na Makame?

Hata!!

Kuna walakini katika jina hilo.

Lakini kulikuwa kuna haja gani ya kumuua Sajini Vengu?

Kuna jambo si bure.

Alipiga ngeta baada ya mwili wake kumsisimka.

Moja ya vitu alivyokuwa amejaliwa Sajenti kobelo; ni hisia.
Kila anapokuwa katikati ya jambo zito, mwili wake huamsha msisimko usiokifani na hapo hujiandaa kukabiliana na hatari.

Kwa maelekezo ya ananuani alioikuta ndani ya kituo cha mwinjuma ni kuwa Vengu aliishi nyumba namba kumi na tano.

Njia haikuruhusu gari kupita, alitafuta sehemu alioona inafaa akapaki gari kisha akaanza kutafuta namba ya nyumba hiyo.

Hakukawia kuiona!

Kulikuwa kuna geti jekundu na nyumba ilionekana kuwa pweke.

Akasukuma geti na kuingia ndani kisha akageuka na kulitazama lile geti.

Inamaana hakuwa amelifunga hili geti?

Hakukuwa na wa kumjibu.

Akapiga hatua zake ndogo ndogo huku akijaribu kutazama mazingira ya nje ya nyumba ile ambayo haikuwa kubwa licha ya kuwa na geti.

Kulia kwake kulikuwa kuna kibanda ambacho kwa ndani kulikuwa kuna pikipiki kubwa ya Baja.

Akarudisha macho kutazama mlangoni mwa nyumba.

Mmmh!!

Aliguna baada ya kuhisi kuchunguliwa na mtu kutokea ndani upande ambao alihisi kuna chumba kulingana na dirisha lilivyokuwa limekaa.

Alihisi kabisa kuna mtu alikuwa amesogeza pazia na kumtazama.

Ni nan na anafanya nini?

Akaongeza tahadhari!!

Akasukuma mlango.

Nao ulikuwa wazi.

Ala!!

Akaingia kwa tahadhari kubwa huku akiwa makini kuliko makini yenyewe.

Mezani alikuta kuna kompyuta mpakato iliokuwa imefungwa nusu yani kama vile mfungaji alikuwa na haraka sana.

Akaikunja kompyuta ile kisha akaiacha pale mezani na kuanza kupiga hatua kuelekea kwenye chumba alichohisi kuona mtu akimtizama.

Alipokaribia mlangoni tu akajikuta akirushwa sebuleni kwa teke zito lilitua sawia kifuani mwake na kwenda kumsambaratisha chini kama mzigo.

Akakataka kusimama ila alijikuta akijaa kwenye mikono ya mvamizi na kupigwa double hit kifuani kwa lengo la kumvunja mifupa ya kifua ila akawahi kujua hila hiyo hivyo kwa tabu akajitahidi kurudi nyuma kwa mtindo wa aina yake na kujikuta akipamia kabati ambalo alisambaratika nalo chini.

Bado mvamizi hakumwacha, akamzoa chini kwa mikono miwili kisha akamtwisha kichwa katikati ya paji la uso na Kobelo akabweka kama mbwa dume aliepokonywa mwanamke wake.

Maumivu yakamsambaa mwili mzima.

Kobelo akaona akizubaa nae ataitwa maiti.

Kwa nguvu zilizosalia akajiachia na kufyatuka kichwa kikali kilichoenda kutua kifuani mwa mvamizi na kisha kumrusha nyuma kwa kasi na kumbwaga chini akasambaratika kama gunia la nyanya mbichi huku akilia kama mbwa jike aliezidiwa na mkuyenge.

Sajenti kobelo aligundua kitu wakati akijipanga kumkabili adui.
Alihisi kichwa chake kimekutana na nyama laini hivi lakini kilio kilichotoka kilikuwa cha kike.

Ebana e!

Mvamizi alisimama,alikuwa ni mwanamke.

Kila mmoja alijipanga kumkabili mwenzie.

Mvamizi akanesa kidogo na kuachia ngumi za harakaharaka lakini zote zilienda kupiga hewa na alijikuta akipokea makonde mawili ya nguvu mbavuni mwake.

Akabweka kama bwege.

Akajaribu tena kurusha mateke, lakini yalipanguliwa kistadi na sajenti kisha akamwachia konde zito kwenye mbavu za kulia.

Mvamizi alimanusura atapike dagaa aliokula.

Alipojaribu kuhema akashindwa na alipotaka kusimama pia alishindwa.

“Mwanamke waacha kuoelewa unakuja kupambana na waume zako pumbavu wewe” Alisema Sajenti Kobelo huku akiwa anamtazama mvamizi akijaribu kujiinua bila mafanikio.

Mara likatokea tukio ambalo Kobelo hakulitarajia.

Mvamizi kwa kasi ya ajabu alitoa kitu mifukoni kwake na kupiga chini na kuzuka moshi mzito ambao ulimchanganya Kobelo na alichosikia ni sauti ya mgongano wa mtu na mlango na alioojaribu kufuata nyuma hakuna alichoambulia zaidi ya sauti za mgongano wa milango ya geti.

“ooh shit” alimaka Sajenti huku akirudi ndani na kuikwapua kompyuta kisha akatoka haraka eneo lile.

Kitu ambacho hakujua ni kuwa kompyuta ile ilienda kuzua utata.

Utata ambao ulizidi kuwa utata!!

***

Nb: hakuna kitu kinachokatisha tamaa Kama kuona uposti zaidi ya vipande sita kwa siku tatu afu unakutana na komenti nne tu na pale unapokuwa na majukumu mengine usipoposit siku mbili kuna watu wanatokea na kukuvurumishia majina ya kila aina mara unalinga mara hivi mara vile,wakati ukipost huwaoni.

Ni wambie kitu!!

Hakuna kitu ambacho mwandishi anapenda na kupata moyo kuendelea na kazi yake kama kuona anapata sapoti na ushauri wa watu kuhusu kazi anayoipost kwa sababu unapoandika huwa upo peke yako na unapopost unabaki kuwa peke yako dah lazima ukate tamaa au hata ule mzuka wa kutupia kila siku unaweza kuisha na usijali.

Sapoti yako ni muhimu kuliko matusi yako!!

Tukutane kesho

Tuko pamoja kaka


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
RIWAYA; URITHI WA GAIDI

NA; BAHATI MWAMBA

SIMU; 0758573660

SEHEMU YA KUMI NA SITA



Mvamizi kwa kasi ya ajabu alitoa kitu mifukoni kwake na kupiga chini na kuzuka moshi mzito ambao ulimchanganya Kobelo na alichosikia ni sauti ya mgongano wa mtu na mlango na alioojaribu kufuata nyuma hakuna alichoambulia zaidi ya sauti za mgongano wa milango ya geti.

“ooh shit” alimaka Sajenti huku akirudi ndani na kuikwapua kompyuta kisha akatoka haraka eneo lile.

Kitu ambacho hakujua ni kuwa kompyuta ile ilienda kuzua utata.

Utata ambao ulizidi kuwa utata!!

***

Sajenti Kobelo alizidi kuona ugumu wa kazi ile hasa baada ya kupambana na mwanamke aliekuwa amejiziba uso wake kuanzia juu hadi chini.

“Alifuata nini nyumbani pale?” Alijiuliza bila kupata majibu na alizidi kuendesha gari kurejea nyumbani kwake.

“Kuna tatizo pahali kuhusu inshu hii” Alijisemea tena huku macho yake akiyatupa kwenye kompyuta mpakato iliokuwa kwenye kiti cha kushoto kwake.

Safari yake ilimfikisha nyumbani kwake na alishuka moja kwa moja alielekea ndani na kupitiliza hadi kwenye chumba kidogo kilichokuwa kimesheheni vifaa vingi vya mawasiliano.
Alikaa kwenye kiti kisha akachukua waya uliokuwa umeungwa kwenye umeme na kuchomeka kwenye kompyuta alioingia nayo mule ndani.

Akaiwasha na kuanza kupekuwa mafaili yaliokuwa yamehifadhiwa mule na hakuna la maana alilolipata.

Alipokuwa mbioni kukata tamaa akaona kwa chini kuna faili limeandikwa “REMI”

Akalifungua!!

Akakutana na maneno “inawezekana vipi?” kisha yakafuatia maneno mengine kwa chini “kwanini askari?” Alizidi kushuka na maneno mengine kadhaa ambayo yalikuwa na viulizo vingi.

Hatimae alifika kwenye ujumbe wa picha na kuufungua.

Video ile ilionesha gari likiwa linakimbia kwa kasi sana na ilivyoonesha picha zilizpigwa kutoka kwenye gari lililokuwa mbele na ilionekana ni mfukuzano uliokuwa baina ya gari zile.
Kuna kitu kilimshangaza kwenye gari ile iliokuwa nyuma ya gari la mbele.

Namba za gari!!

Namba alizoziona ni zile zile namba zilizokuwa kwenye gari aliloliona kule alikofia Sajini Vengu.

Aliguna!!

Kisha akachukua kalamu na kutaka kuandika ila akakumbuka karatasi alioichukua mfukoni mwa marehemu, akaitoa.

Alikutana na maneno yale yale ya viulizo na kisha kufuatiwa na namba za gari zilezile alizokuwa akizitazama kwenye picha mjongeo.

Video ilifika wakati ambao kuna tukio liliendelea ila kwa kuwa kamera ilikuwa inachukua kwa nyuma tu, hakuweza kuona ila alisikia purukushani kisha ikafuatiwa na mlipuko wa risasi na miguno na kisha akaona tena watu waliovalia sare za jeshi la polisi na kilichofuatia hapo ni video kuzima.

“ina maana polisi walihusika katika utekaji huu? Sasa kwa nini walitumia gari lenye namba sawa na za lile lililokuwa kwa Remi?”

Akaguna tena!!

Lakini kwanini Remi na Remi ni nani hasa?

Akajiuliza huku akihamia kwenye kompyuta kubwa iliokuwa mezani na kuiwasha kisha akawasha data na kuanza kuperuzi kuhusu Remi.

Alichokutana nacho ndicho kilichomshangaza.

Kweli Remi alikuwa ni mkimbizi ila alishatunukiwa uraia kwa ushujaa wake katika mkasa wa Congo sasa vije tena aitwe mkimbizi? Na vipi wale waliomtunuku nishani ya ushujaa wapo wapi wakati huu.

Aliguna tena na kisha akachukua kitabu chake na kurejea yale aliokuwa ameyaandika wakati alipokuwa anautazama mwili wa marehemu Vengu.

“Huyu binti hakuuwa bwana!!” Alijikatalia peke yake.

Hili tundu sio la mpigo wa bunduki ndogo” Alijisemea tena huku akiwa anazidi kupitia hiki na kile kuhakikisha anapata picha kamili ya tukio lilivyokuwa.

Bado nafsi yake ilimwambia Remi hawezi kuwa mhusika.

Akakumbuka kitu

Alikumbuka kachumbari ya jina la Remi.

Remi Haji Makame!

Akalitaja tena lile jina na kuliandika kwenye kompyuta na kufuta lile la Remi na kubaki Haji Makame.

Ex soldier? Alijiuliza baada ya kuona tovuti moja ikimtaja kama ni mwanajeshi zamani, lakini pia alitajwa kama aliwahi kuwa askari polisi wa cheo cha juu na hivi sasa hatambuliki baada ya kuwa anajihusisha na ugaidi na sasa anatafutwa na serikali ya marekani.

Mmh!! Inawezekana vipi hii! Alijiuliza tena.

Mambo yalizidi kumchanganya.

Haji tayari alikuwa ameshafutwa katika utumishi na alinasibishwa kama mtu hatari.

Hapo akawa amepata jibu ya kuwa Haji alikuwa ni mume wa Remi na walioana miaka kadhaa nyuma.


Alihitaji kumpata Remi.

Alichukua namba za simu zilizokuwa zimeandikwa kwenye vitabu vya Vengu na kuzipiga ila hazikuwa zikipatikana.

Alishusha pumzi nyingi na kuzishusha, hakujua aanzie wapi kudadavua jambo lile.

Wanataka nini kwa huyu mwanamke?

Alikumbuka kitu, akatoka na kuelekea kwenye gari lake na kuchukua gazeti lililokuwa limeandika habari za mauaji ya Vengu.

Alikuwa anatafuta mwandishi wa habari ile ila kama kawaida katika habari kama hizo huwa kunakuwa na neno “Na mwandishi wetu”

Alifyonza!!

Akapiga tena namba iliompigia kumpa taarifa ya mauaji ya Vengu; nayo haikupatikana.

Alirudi tena kwenye sifuri.

Akaigemea kiti na kushika kichwa huku akitizama kompyuta yake.

Hakupata jibu!!

Akainuka na kurejea tena kwenye kitabu chake, akarudia kusoma baadhi ya mambo alionukuu kutoka kwenye kablasha la Vengu kule kituoni.

Akasoma tena muda uliokisiwa kutumika katika utekaji na mauaji ofisini kwa Remi.

Akafikiria kwa zaidi ya dakika sita bila kupata cha kumuongoza katika sakata lile.

Mara akawaza jambo ambalo hakuwa na hakika nalo, akachukua simu yake na kutafuta namba fulani kisha akapiga.

“nambie kipanga!!” Sauti ya kike ilipokea kwa uchangamfu.

“Acha zako Habiba” Alisema kwa masihala Kobelo.

“Aah kipanga; vipi leo tena mmepigana na shoga angu?” Alihoji huku akicheka.

Yalikuwa ni masihala ya Habiba na Kobelo.

“aah umekariri tu, sikia leo naomba unisaidie jambo fulani hivi” Kobelo alisema.

Habiba aliguna kisha akasema
“Shida gani tena naweza kukusaidia mimi?” Alihoji Habiba kwa mshangao kidogo.

“Hivi inawezekana kupata mawasiliano ya mtu akiwa hayuko kwenye eneo alillopo wakati huo” Alisema Kobelo.

“Sijakwelewa kipanga”

“Ok yani namaanisha unaweza kujua mawasiliano ya simu katika eneo fulani hata kama akiwa ametoka kwenye hilo eneo?” Alifafanua Kobelo.

“eeh mbona rahisi tu” Alijibu Habiba.

“Sasa subiri kidogo nitakutaarifu kwa ujumbe mfupi sasa hivi unisaidie hiyo kazi”

“Sawa”

Kobelo akakata simu na kuanza kutafuta anuani ya ofisi za Remi na alipozipata akazituma kwa Habiba huku akiambatanisha na ujumbe mfupi wa maneno.

“Nitafutie mawasiliano yaliokuwa karibu na eneo hilo au ndani ya eneo hilo mida ya alfajiri”

Kama alijua kupokea jibu lile na kulifanyia kazi ni kazi nyepesi, alikosea sana Sajenti Kobelo.

**+
 
RIWAYA; URITHI WA GAIDI

NA; BAHATI MWAMBA

SIMU; 0758573660

SEHEMU YA KUMI NA SITA



Mvamizi kwa kasi ya ajabu alitoa kitu mifukoni kwake na kupiga chini na kuzuka moshi mzito ambao ulimchanganya Kobelo na alichosikia ni sauti ya mgongano wa mtu na mlango na alioojaribu kufuata nyuma hakuna alichoambulia zaidi ya sauti za mgongano wa milango ya geti.

“ooh shit” alimaka Sajenti huku akirudi ndani na kuikwapua kompyuta kisha akatoka haraka eneo lile.

Kitu ambacho hakujua ni kuwa kompyuta ile ilienda kuzua utata.

Utata ambao ulizidi kuwa utata!!

***

Sajenti Kobelo alizidi kuona ugumu wa kazi ile hasa baada ya kupambana na mwanamke aliekuwa amejiziba uso wake kuanzia juu hadi chini.

“Alifuata nini nyumbani pale?” Alijiuliza bila kupata majibu na alizidi kuendesha gari kurejea nyumbani kwake.

“Kuna tatizo pahali kuhusu inshu hii” Alijisemea tena huku macho yake akiyatupa kwenye kompyuta mpakato iliokuwa kwenye kiti cha kushoto kwake.

Safari yake ilimfikisha nyumbani kwake na alishuka moja kwa moja alielekea ndani na kupitiliza hadi kwenye chumba kidogo kilichokuwa kimesheheni vifaa vingi vya mawasiliano.
Alikaa kwenye kiti kisha akachukua waya uliokuwa umeungwa kwenye umeme na kuchomeka kwenye kompyuta alioingia nayo mule ndani.

Akaiwasha na kuanza kupekuwa mafaili yaliokuwa yamehifadhiwa mule na hakuna la maana alilolipata.

Alipokuwa mbioni kukata tamaa akaona kwa chini kuna faili limeandikwa “REMI”

Akalifungua!!

Akakutana na maneno “inawezekana vipi?” kisha yakafuatia maneno mengine kwa chini “kwanini askari?” Alizidi kushuka na maneno mengine kadhaa ambayo yalikuwa na viulizo vingi.

Hatimae alifika kwenye ujumbe wa picha na kuufungua.

Video ile ilionesha gari likiwa linakimbia kwa kasi sana na ilivyoonesha picha zilizpigwa kutoka kwenye gari lililokuwa mbele na ilionekana ni mfukuzano uliokuwa baina ya gari zile.
Kuna kitu kilimshangaza kwenye gari ile iliokuwa nyuma ya gari la mbele.

Namba za gari!!

Namba alizoziona ni zile zile namba zilizokuwa kwenye gari aliloliona kule alikofia Sajini Vengu.

Aliguna!!

Kisha akachukua kalamu na kutaka kuandika ila akakumbuka karatasi alioichukua mfukoni mwa marehemu, akaitoa.

Alikutana na maneno yale yale ya viulizo na kisha kufuatiwa na namba za gari zilezile alizokuwa akizitazama kwenye picha mjongeo.

Video ilifika wakati ambao kuna tukio liliendelea ila kwa kuwa kamera ilikuwa inachukua kwa nyuma tu, hakuweza kuona ila alisikia purukushani kisha ikafuatiwa na mlipuko wa risasi na miguno na kisha akaona tena watu waliovalia sare za jeshi la polisi na kilichofuatia hapo ni video kuzima.

“ina maana polisi walihusika katika utekaji huu? Sasa kwa nini walitumia gari lenye namba sawa na za lile lililokuwa kwa Remi?”

Akaguna tena!!

Lakini kwanini Remi na Remi ni nani hasa?

Akajiuliza huku akihamia kwenye kompyuta kubwa iliokuwa mezani na kuiwasha kisha akawasha data na kuanza kuperuzi kuhusu Remi.

Alichokutana nacho ndicho kilichomshangaza.

Kweli Remi alikuwa ni mkimbizi ila alishatunukiwa uraia kwa ushujaa wake katika mkasa wa Congo sasa vije tena aitwe mkimbizi? Na vipi wale waliomtunuku nishani ya ushujaa wapo wapi wakati huu.

Aliguna tena na kisha akachukua kitabu chake na kurejea yale aliokuwa ameyaandika wakati alipokuwa anautazama mwili wa marehemu Vengu.

“Huyu binti hakuuwa bwana!!” Alijikatalia peke yake.

Hili tundu sio la mpigo wa bunduki ndogo” Alijisemea tena huku akiwa anazidi kupitia hiki na kile kuhakikisha anapata picha kamili ya tukio lilivyokuwa.

Bado nafsi yake ilimwambia Remi hawezi kuwa mhusika.

Akakumbuka kitu

Alikumbuka kachumbari ya jina la Remi.

Remi Haji Makame!

Akalitaja tena lile jina na kuliandika kwenye kompyuta na kufuta lile la Remi na kubaki Haji Makame.

Ex soldier? Alijiuliza baada ya kuona tovuti moja ikimtaja kama ni mwanajeshi zamani, lakini pia alitajwa kama aliwahi kuwa askari polisi wa cheo cha juu na hivi sasa hatambuliki baada ya kuwa anajihusisha na ugaidi na sasa anatafutwa na serikali ya marekani.

Mmh!! Inawezekana vipi hii! Alijiuliza tena.

Mambo yalizidi kumchanganya.

Haji tayari alikuwa ameshafutwa katika utumishi na alinasibishwa kama mtu hatari.

Hapo akawa amepata jibu ya kuwa Haji alikuwa ni mume wa Remi na walioana miaka kadhaa nyuma.


Alihitaji kumpata Remi.

Alichukua namba za simu zilizokuwa zimeandikwa kwenye vitabu vya Vengu na kuzipiga ila hazikuwa zikipatikana.

Alishusha pumzi nyingi na kuzishusha, hakujua aanzie wapi kudadavua jambo lile.

Wanataka nini kwa huyu mwanamke?

Alikumbuka kitu, akatoka na kuelekea kwenye gari lake na kuchukua gazeti lililokuwa limeandika habari za mauaji ya Vengu.

Alikuwa anatafuta mwandishi wa habari ile ila kama kawaida katika habari kama hizo huwa kunakuwa na neno “Na mwandishi wetu”

Alifyonza!!

Akapiga tena namba iliompigia kumpa taarifa ya mauaji ya Vengu; nayo haikupatikana.

Alirudi tena kwenye sifuri.

Akaigemea kiti na kushika kichwa huku akitizama kompyuta yake.

Hakupata jibu!!

Akainuka na kurejea tena kwenye kitabu chake, akarudia kusoma baadhi ya mambo alionukuu kutoka kwenye kablasha la Vengu kule kituoni.

Akasoma tena muda uliokisiwa kutumika katika utekaji na mauaji ofisini kwa Remi.

Akafikiria kwa zaidi ya dakika sita bila kupata cha kumuongoza katika sakata lile.

Mara akawaza jambo ambalo hakuwa na hakika nalo, akachukua simu yake na kutafuta namba fulani kisha akapiga.

“nambie kipanga!!” Sauti ya kike ilipokea kwa uchangamfu.

“Acha zako Habiba” Alisema kwa masihala Kobelo.

“Aah kipanga; vipi leo tena mmepigana na shoga angu?” Alihoji huku akicheka.

Yalikuwa ni masihala ya Habiba na Kobelo.

“aah umekariri tu, sikia leo naomba unisaidie jambo fulani hivi” Kobelo alisema.

Habiba aliguna kisha akasema
“Shida gani tena naweza kukusaidia mimi?” Alihoji Habiba kwa mshangao kidogo.

“Hivi inawezekana kupata mawasiliano ya mtu akiwa hayuko kwenye eneo alillopo wakati huo” Alisema Kobelo.

“Sijakwelewa kipanga”

“Ok yani namaanisha unaweza kujua mawasiliano ya simu katika eneo fulani hata kama akiwa ametoka kwenye hilo eneo?” Alifafanua Kobelo.

“eeh mbona rahisi tu” Alijibu Habiba.

“Sasa subiri kidogo nitakutaarifu kwa ujumbe mfupi sasa hivi unisaidie hiyo kazi”

“Sawa”

Kobelo akakata simu na kuanza kutafuta anuani ya ofisi za Remi na alipozipata akazituma kwa Habiba huku akiambatanisha na ujumbe mfupi wa maneno.

“Nitafutie mawasiliano yaliokuwa karibu na eneo hilo au ndani ya eneo hilo mida ya alfajiri”

Kama alijua kupokea jibu lile na kulifanyia kazi ni kazi nyepesi, alikosea sana Sajenti Kobelo.

**+
Bomba sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom