winston20
JF-Expert Member
- Jun 21, 2020
- 1,117
- 2,256
- Thread starter
- #21
GENGE
EP20
KICHWA CHA MADAM S hakikupata wasaa wa kutulia. Jambo gumu na kubwa liliendelea kumsumbua kichwani.
Tunakwama wapi? Akajiuliza. Usiku huo alilala chali kitandani, akiwa na vazi la kulalia tu. Taa yenye mwanga wa rangi ya orange iliyowekwa kwenye meza ndogo ilikijaza chumba hicho kwa uhafifu wake. Ungeweza kumletea usingizi, lakini kwake haikuwa hivyo, tuli, alitulia. Alihakikisha ananyamazisha kelele zote ubongoni mwake ili achambue kimoja baada ya kingine.
Mwanamama huyu alikuwa mbobevu sana katika maswala ya kijasusi, daima alijua anachofanya. Uongozi wake katika kitengo cha siri cha serikali ulitambulika vyema na Mkuu wan chi, aliheshimika kwa siri vilevile. Kazi yake ilionesha matunda. Vijana wake hawakumwangusha. Mpaka siku hii alipojilaza kitandani, uzee ulikuwa unapiga hodi. Mvi zilikijaza kichwa chake na kumfanya awe mrembo maradufu. Hakuwahi kuolewa. Ijapokuwa alikuwa na mabwana wa hapa na pale ili kukata kiu yake ya kike, bado hakuwahi kupata mtoto. Si kwamba alikuwa tasa, la, ila majukumua na kazi yake vilimfanya aepuke kushika mimba. Haya yote yalimpa mawazo mengi kadiri umri ulivyokuwa ukienda. Watoto pekee aliyewaona ni wake ni vijana wa TSA na si wengine. Aliwaita wanangu, nao wakamwita mama.
Akili ya Madam S ilizimika na kuacha giza nene katika ubongo wake. Hii alijifunza huko Mongolia katika pitapita zake za mafunzo ya Kiintelijensia. Akarudisha kumbukumbu moja moja za nyuma. Kumbukumbu zake zikamrudisha alipokuwa na umri wa wastani. Siku alipopokea barua ya kutakiwa kuripoti Ikulu katika kitengo cha usalama.
Alipokelewa na watu wawili wacheshi ambao aneweza kumwita mmoja baba na mwingine baba mdogo. James Msambamagoya na Chameleone, walimpokea, wakampa ofisi na kumsimamia kwa ukaribu sana katika kazi waliyompa. Selina akafanya vizuri, aliweza kuratibu vyema safari za ndani za Rais, kupanga makabrasha na mambo mengine ya kiitifaki. Alimheshimu sana Chameleone kwa jinsi alivyokuwa akipanga mambo yake. Akajitahidi kujifunza na kuiba mambo kadhaa. Akafanikiwa. ‘Binti Chameleone’ wakampa jina. Kwa sababu mwishowe alikuwa na tabia kama za mzee huyo. Hakuwa na ukaribu sana na James Msambamagoya, kwa kuwa alimtaka kimapenzi mara kadhaa.
“Sikiliza binti… nakupa kazi ya siri, na uifanye kwa umakini”. Sauti ya Chameleone ilimrudia kwenye kumbukumbu zake.
“Nahitaji umfuatilie au umchunguze James… ila uwe makini sana asijue hili. Nataka unambie, akimaliza kazi hupendelea kwenda wapi, na nani ikiwezekana nipe hata orodha ya marafiki zake anaokutana nao mara kwa mara.” Agizo.
Madam S aliikumbuka siku hii, jinsi alivyoweza kumfuatilia mwanausalama huyo. Aligundua kuwa, baa aipendayo ni Banana. Aliwatambua marafiki zake, aliokuwa anakunywa nao. Wanajeshi. Sura zao aliziona mara kadhaa walipokuwa wakija Ikulu kwa kazi maalumu. Alivuta sura ya mmoja mmoja, alikumbuka wapo waliofungwa kwa kesi ya uhaini, wengine walitoroka. Kati ya waliotoroka alikumbuka Mwanachia aliyejulikana kwa jina la Chatu, alikwishauawa. Alimkumbuka Mwakibinga naye alikwishauawa kwa mkono wa TSA. Bado wawili.
Yuko wapi aliyekuwa waziri wa mambo ya nje wakati ule? Ambaye iligundulika kuwa ndiye mpanga mipango, anayeitaka nchi, aitwe rais. Uchu wa madaraka.
Madam S alikuwa bado kitandani, chali. Akili yake ilikuwa imepaa mbingu ya saba, nje ya upeo wake wa kawaida. Iliitaji utulivu mkubwa kuweza kuwasha sakiti mpya ya umeme katika ubongo, kucukua tafutishi kutoka kwenye memori za muda za wakati huo. Kutafuta wapi zilitupa kumbukumbu hizo na kuzirudisha kwenye mfumo wa LTM yaani Long Time Memory. Ni zoezi gumu ambalo majasusi ujifunza. Katika zoezi hili mfumo wa kumbukumbu wa Madam S ulirudi kwa Chameleone.
“Nina ofisi yangu ya siri ambayo taarifa nyingi zinapatikana…” sauti ya Chameleone ilimrudia kichwani.
Hospitali ya Ocean Road! Akajikuta akiwaza.
Ding! Dong! Sauti ya kengele ilimgutua. Akafumbua macho na kushusha pumzi kwa nguvu.
Ding! Dong! Ikajirudia tena. Haraka haraka, akachukua kitabu chake cha kumbukumbu. Akafyatua kalamu na kuandika mambo machache muhimu. Akakiacha kitanda na kuliendea kabati la nguo. Akachojoa na kuchukua koti refu na kujitupia mwilini. Akafunga zipu yake mpaka chini. Akaenda sebuleni na kuwasha taa. Alielewa ni nani anayegonga mlangoni kutokana na jinsi alivyoibonya kengele hiyo.
Kabla hajafungua geti akatazama saa yake. Saa sita kasoro robo usiku. Akafungua geti.
Kamanda Amata akajitoma ndani na Madam S akafunga geti lile. Hatua chache wakafika sebuleni, pombe kali ikawekwa kati. Wote wawili, kila mmoja, akajitupa kitini.
“Yes Kamanda!” Madam S akamsabahi kwa namna hiyo mara baada ya kushusha bilauri yenye kinywaji.
“Madam, akili yangu haijatulia kabisa…” akasema na kupiga tena funda moja la kinywaji kile.
“Nini unafikiri?” Madam akamrudishia swali.
“Madam nimetoka kuachana na mtoto wa Mtokambali, nililoambiwa sijalitegemea,”
“Nambie mwanangu…”
“Kibwana Mtokambali alikwishafariki na amezikwa huko Kiev,”
“Nani amekwambia?”
“Mtoto wake wa kwanza, Bwana Onesmo anaishi Mwananyamala,”
“Umeonana naye?”
“Ndiyo, nilimtafuta nikampata nyumbani kwake, nikazungumza naye mengi sana. Anailaumu serikali kwa kutomjali baba yake. Anauliza, ukiachana na kosa alilohukumiwa kama mhaini mbona mmeusahau utumishi wake kwa miaka yote?” Amata akaeleza. Kutoka mfukoni mwake akachomoa rekoda ndogo, akawasha. Wote wawili wakaanza kusikiliza mazungumzo yale kutoka Alfa hadi Omega.
* * *
KIEV 1980
Katika Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Boryspil Kyiv, Kibwana Mtokambali alipokelewa na swahiba wake Colonel Ivan Chernyakhovsky. Colonel huyu alimfahamu vyema Kibwana Mtokambali kwa kuwa walikutana kwenye mafunzo ya kijeshi mwaka 1968 huko katika Akademia ya Kijeshi ya Kiev. Ivan alijua fika nini dhamira ya swahiba wake. Tangu wakiwa katika academia hiyo, Mtokambali hakuweza kuficha hisia yake.
“Utakuwa mwanaume kamili ukifanikiwa hilo, hata ukishindwa, utakuwa umejaribu pakubwa…” Ivan alimwambia mara kadhaa wakiwa katika mafunzo yao. Tofauti na Kibwana, Ivan yeye akili yake yote ilikuwa ni kuanzisha chuo cha maswala ya usalama katika Kiev. Ndoto yake haikufa mpaka alipofanikiwa kwa asilimia kubwa na serikali kumsaidia.
Siku hii, ndani ya uwanja wa ndege alimpokea shujaa wake huyu.
“Tovarishch, ya ne smog…” Kibwana akamwambia Ivan kwa Kirusia kuwa ameshindwa jaribio lake.
“Ne volnuysya, moy pokazhu tebe drugoy put,” brat. YA Ivan akamtoa wasiwasi na kumwahidi kumwonesha njia nyingine ya kufanikisha lengo hilo. Wakakumbatiana kwa sekunde kadhaa kisha wakaelekea garini ambako mizigo yote ilikuwa tayari imekwisha pakiwa.
“Karibu tena Kiev komredi…”Ivan akamwambia Mtokambali.
“Nimekaribia, asante sana…”
Wote wawili wakaondoka uwanjani hapo kwa gari maalum la kijeshi. Baada ya mwendo wa takribani dakika arobaini na tano, waliwasili katika kitongoji kimoja mashambani. Lile Fiat likaingizwa ndani ya wigo mkubwa uliuzungukwa na kila aina ya ulinzi. Jumba la kifahari lilikuwa katikati ya wigo huo. Mara tu alipokanyaga ardhi, Kibwana akapokelewa na mwaDanada mrefu wa wastani, mwenye nywele nyeupe zilizomwagika mgongoni mwake. Suruali yake ya kijeshi ilimkaa vyema na kumpendezesha haswa.
“Kutana na Barbier Saratov,” Ivan akamwambia mgeni wake.
 “Nafurahi kukutana nawe Barbier…”wakasalimiana na kuzungumza machache kisha wakaelekea ndani ya jumba hilo. Moja kwa moja walifikia katika meza kubwa ya chakula, iliyopambwa na pombe kali kali. Kijindoo kidogo chenye barafu kilikuwa kikifuka mvuke. Kibwana Mtokambali aliitazama ile meza na kukumbuka miaka ya nyuma alipokuwa katika nchi hiyo kwa mafunzo ya kijeshi. Katika meza hiyo kulikuwa na watu watatu tu, Ivan, Barbier na Mtokamba. Akukuwa na mtu mwingine na wala hakukuonesha dalili ya kuwa na mtu wa ziada katika jumba hilo, ukiachana na walinzi wa nje.
Baada ya glasi mbili tatu kumiminiwa tumboni, ukimya ulivunjwa.
“Kwa katiba ya nchi yetu, nitahukumiwa kifo,” Kibwana alimweleza Ivan.
“Kamanda haogopi kufa, kwa kuwa ni sehemu ya maisha yake hasa anapopigania taifa lake,” Ivan akajibu.
“Najua comrade!”
“Sasa wasiwasi wako ni nini?” Ivan akamuuliza swahiba wake.
“Sina wasiwasi,”
“Hayo ndiyo maneno. By the way, utakuwa na Barbier kwa takriban wiki tatu au mwezi hivi. Yeye atakupitisha katika michakato tofauti ya kukubadili na kukurudisha tena kwenye uwanja wa vita,” Ivana akamwambia Mtokambali.
“Kunibadili?” akauliza.
“Naam, wewe utahukumiwa kufa, na utakufa, sasa sisi tunakuua mapema na kukurejesha vitani,” akamweleza, “Barbier!” akaita.
“Yes Sir!”
“Mweleze kinachoendelea kwa ajili yake,” Ivan akamwambia yule mwanamke. Barbier akavuta droo kubwa chini ya meza hiyo, akatoa kabrasha moja na kuliweka mezani. Alipoifunga ile droo, akalifungua lile kabrasha. Ndani yake kulikuwa na karatasi kama kumi hivi zote zikiwa na sura za watu, wazungu na majina yao. Zaidi ya hapo kuliokuwa na tarakimu nyingi sana.
“Nani unampenda kati ya hawa?” Barbier akamuuliza Mtokambali huku akimsogezea lile kabrasha. Mgeni huyo akachukua lile kabrasha na kuanza kulipekuapekua. Picha namba kumi na moja, akaipenda. Akamrudishia Barbier lila kabrasha kama alivyopewa, yaani kwa kulisukuma.
“Ok!” Barbier akatamka. Akaitatua ile karatasi na kuondoka pale mezani akiwaacha Mtokambali na Ivan, marafiki wawili.
“Don’t worry Kibwana. Hakuna linaloshindikana chini ya jua, utaona tu. Mimi na watu wangu tutakupa kila kitu ili ufanikishe lengo. Mafanikio yako ndiyo yetu kama tulivyopanga,” Ivan akamtoa wasiwasi.
Dakika kumi baadae, Barbier alirudi na kuketi katika kiti kilekile.
“Kila kitu sawa?” Ivan akamuuliza.
“Ndiyo! Kinachofuata ni kujiandaa kwa safari wiki moja ijayo. Dakta Punchkunel yuko tayari na atakuwa kwa ajili yetu siku hiyo,” Babier akatoa maelezo. Wakati yuote haya yakionelewa, Kibwana alikuwa kimya akigugumia vodka yake. Hakuna alichokielewa zaidi ya kusikia tu.
ITAENDELEA
EP20
KICHWA CHA MADAM S hakikupata wasaa wa kutulia. Jambo gumu na kubwa liliendelea kumsumbua kichwani.
Tunakwama wapi? Akajiuliza. Usiku huo alilala chali kitandani, akiwa na vazi la kulalia tu. Taa yenye mwanga wa rangi ya orange iliyowekwa kwenye meza ndogo ilikijaza chumba hicho kwa uhafifu wake. Ungeweza kumletea usingizi, lakini kwake haikuwa hivyo, tuli, alitulia. Alihakikisha ananyamazisha kelele zote ubongoni mwake ili achambue kimoja baada ya kingine.
Mwanamama huyu alikuwa mbobevu sana katika maswala ya kijasusi, daima alijua anachofanya. Uongozi wake katika kitengo cha siri cha serikali ulitambulika vyema na Mkuu wan chi, aliheshimika kwa siri vilevile. Kazi yake ilionesha matunda. Vijana wake hawakumwangusha. Mpaka siku hii alipojilaza kitandani, uzee ulikuwa unapiga hodi. Mvi zilikijaza kichwa chake na kumfanya awe mrembo maradufu. Hakuwahi kuolewa. Ijapokuwa alikuwa na mabwana wa hapa na pale ili kukata kiu yake ya kike, bado hakuwahi kupata mtoto. Si kwamba alikuwa tasa, la, ila majukumua na kazi yake vilimfanya aepuke kushika mimba. Haya yote yalimpa mawazo mengi kadiri umri ulivyokuwa ukienda. Watoto pekee aliyewaona ni wake ni vijana wa TSA na si wengine. Aliwaita wanangu, nao wakamwita mama.
Akili ya Madam S ilizimika na kuacha giza nene katika ubongo wake. Hii alijifunza huko Mongolia katika pitapita zake za mafunzo ya Kiintelijensia. Akarudisha kumbukumbu moja moja za nyuma. Kumbukumbu zake zikamrudisha alipokuwa na umri wa wastani. Siku alipopokea barua ya kutakiwa kuripoti Ikulu katika kitengo cha usalama.
Alipokelewa na watu wawili wacheshi ambao aneweza kumwita mmoja baba na mwingine baba mdogo. James Msambamagoya na Chameleone, walimpokea, wakampa ofisi na kumsimamia kwa ukaribu sana katika kazi waliyompa. Selina akafanya vizuri, aliweza kuratibu vyema safari za ndani za Rais, kupanga makabrasha na mambo mengine ya kiitifaki. Alimheshimu sana Chameleone kwa jinsi alivyokuwa akipanga mambo yake. Akajitahidi kujifunza na kuiba mambo kadhaa. Akafanikiwa. ‘Binti Chameleone’ wakampa jina. Kwa sababu mwishowe alikuwa na tabia kama za mzee huyo. Hakuwa na ukaribu sana na James Msambamagoya, kwa kuwa alimtaka kimapenzi mara kadhaa.
“Sikiliza binti… nakupa kazi ya siri, na uifanye kwa umakini”. Sauti ya Chameleone ilimrudia kwenye kumbukumbu zake.
“Nahitaji umfuatilie au umchunguze James… ila uwe makini sana asijue hili. Nataka unambie, akimaliza kazi hupendelea kwenda wapi, na nani ikiwezekana nipe hata orodha ya marafiki zake anaokutana nao mara kwa mara.” Agizo.
Madam S aliikumbuka siku hii, jinsi alivyoweza kumfuatilia mwanausalama huyo. Aligundua kuwa, baa aipendayo ni Banana. Aliwatambua marafiki zake, aliokuwa anakunywa nao. Wanajeshi. Sura zao aliziona mara kadhaa walipokuwa wakija Ikulu kwa kazi maalumu. Alivuta sura ya mmoja mmoja, alikumbuka wapo waliofungwa kwa kesi ya uhaini, wengine walitoroka. Kati ya waliotoroka alikumbuka Mwanachia aliyejulikana kwa jina la Chatu, alikwishauawa. Alimkumbuka Mwakibinga naye alikwishauawa kwa mkono wa TSA. Bado wawili.
Yuko wapi aliyekuwa waziri wa mambo ya nje wakati ule? Ambaye iligundulika kuwa ndiye mpanga mipango, anayeitaka nchi, aitwe rais. Uchu wa madaraka.
Madam S alikuwa bado kitandani, chali. Akili yake ilikuwa imepaa mbingu ya saba, nje ya upeo wake wa kawaida. Iliitaji utulivu mkubwa kuweza kuwasha sakiti mpya ya umeme katika ubongo, kucukua tafutishi kutoka kwenye memori za muda za wakati huo. Kutafuta wapi zilitupa kumbukumbu hizo na kuzirudisha kwenye mfumo wa LTM yaani Long Time Memory. Ni zoezi gumu ambalo majasusi ujifunza. Katika zoezi hili mfumo wa kumbukumbu wa Madam S ulirudi kwa Chameleone.
“Nina ofisi yangu ya siri ambayo taarifa nyingi zinapatikana…” sauti ya Chameleone ilimrudia kichwani.
Hospitali ya Ocean Road! Akajikuta akiwaza.
Ding! Dong! Sauti ya kengele ilimgutua. Akafumbua macho na kushusha pumzi kwa nguvu.
Ding! Dong! Ikajirudia tena. Haraka haraka, akachukua kitabu chake cha kumbukumbu. Akafyatua kalamu na kuandika mambo machache muhimu. Akakiacha kitanda na kuliendea kabati la nguo. Akachojoa na kuchukua koti refu na kujitupia mwilini. Akafunga zipu yake mpaka chini. Akaenda sebuleni na kuwasha taa. Alielewa ni nani anayegonga mlangoni kutokana na jinsi alivyoibonya kengele hiyo.
Kabla hajafungua geti akatazama saa yake. Saa sita kasoro robo usiku. Akafungua geti.
Kamanda Amata akajitoma ndani na Madam S akafunga geti lile. Hatua chache wakafika sebuleni, pombe kali ikawekwa kati. Wote wawili, kila mmoja, akajitupa kitini.
“Yes Kamanda!” Madam S akamsabahi kwa namna hiyo mara baada ya kushusha bilauri yenye kinywaji.
“Madam, akili yangu haijatulia kabisa…” akasema na kupiga tena funda moja la kinywaji kile.
“Nini unafikiri?” Madam akamrudishia swali.
“Madam nimetoka kuachana na mtoto wa Mtokambali, nililoambiwa sijalitegemea,”
“Nambie mwanangu…”
“Kibwana Mtokambali alikwishafariki na amezikwa huko Kiev,”
“Nani amekwambia?”
“Mtoto wake wa kwanza, Bwana Onesmo anaishi Mwananyamala,”
“Umeonana naye?”
“Ndiyo, nilimtafuta nikampata nyumbani kwake, nikazungumza naye mengi sana. Anailaumu serikali kwa kutomjali baba yake. Anauliza, ukiachana na kosa alilohukumiwa kama mhaini mbona mmeusahau utumishi wake kwa miaka yote?” Amata akaeleza. Kutoka mfukoni mwake akachomoa rekoda ndogo, akawasha. Wote wawili wakaanza kusikiliza mazungumzo yale kutoka Alfa hadi Omega.
* * *
KIEV 1980
Katika Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Boryspil Kyiv, Kibwana Mtokambali alipokelewa na swahiba wake Colonel Ivan Chernyakhovsky. Colonel huyu alimfahamu vyema Kibwana Mtokambali kwa kuwa walikutana kwenye mafunzo ya kijeshi mwaka 1968 huko katika Akademia ya Kijeshi ya Kiev. Ivan alijua fika nini dhamira ya swahiba wake. Tangu wakiwa katika academia hiyo, Mtokambali hakuweza kuficha hisia yake.
“Utakuwa mwanaume kamili ukifanikiwa hilo, hata ukishindwa, utakuwa umejaribu pakubwa…” Ivan alimwambia mara kadhaa wakiwa katika mafunzo yao. Tofauti na Kibwana, Ivan yeye akili yake yote ilikuwa ni kuanzisha chuo cha maswala ya usalama katika Kiev. Ndoto yake haikufa mpaka alipofanikiwa kwa asilimia kubwa na serikali kumsaidia.
Siku hii, ndani ya uwanja wa ndege alimpokea shujaa wake huyu.
“Tovarishch, ya ne smog…” Kibwana akamwambia Ivan kwa Kirusia kuwa ameshindwa jaribio lake.
“Ne volnuysya, moy pokazhu tebe drugoy put,” brat. YA Ivan akamtoa wasiwasi na kumwahidi kumwonesha njia nyingine ya kufanikisha lengo hilo. Wakakumbatiana kwa sekunde kadhaa kisha wakaelekea garini ambako mizigo yote ilikuwa tayari imekwisha pakiwa.
“Karibu tena Kiev komredi…”Ivan akamwambia Mtokambali.
“Nimekaribia, asante sana…”
Wote wawili wakaondoka uwanjani hapo kwa gari maalum la kijeshi. Baada ya mwendo wa takribani dakika arobaini na tano, waliwasili katika kitongoji kimoja mashambani. Lile Fiat likaingizwa ndani ya wigo mkubwa uliuzungukwa na kila aina ya ulinzi. Jumba la kifahari lilikuwa katikati ya wigo huo. Mara tu alipokanyaga ardhi, Kibwana akapokelewa na mwaDanada mrefu wa wastani, mwenye nywele nyeupe zilizomwagika mgongoni mwake. Suruali yake ya kijeshi ilimkaa vyema na kumpendezesha haswa.
“Kutana na Barbier Saratov,” Ivan akamwambia mgeni wake.
 “Nafurahi kukutana nawe Barbier…”wakasalimiana na kuzungumza machache kisha wakaelekea ndani ya jumba hilo. Moja kwa moja walifikia katika meza kubwa ya chakula, iliyopambwa na pombe kali kali. Kijindoo kidogo chenye barafu kilikuwa kikifuka mvuke. Kibwana Mtokambali aliitazama ile meza na kukumbuka miaka ya nyuma alipokuwa katika nchi hiyo kwa mafunzo ya kijeshi. Katika meza hiyo kulikuwa na watu watatu tu, Ivan, Barbier na Mtokamba. Akukuwa na mtu mwingine na wala hakukuonesha dalili ya kuwa na mtu wa ziada katika jumba hilo, ukiachana na walinzi wa nje.
Baada ya glasi mbili tatu kumiminiwa tumboni, ukimya ulivunjwa.
“Kwa katiba ya nchi yetu, nitahukumiwa kifo,” Kibwana alimweleza Ivan.
“Kamanda haogopi kufa, kwa kuwa ni sehemu ya maisha yake hasa anapopigania taifa lake,” Ivan akajibu.
“Najua comrade!”
“Sasa wasiwasi wako ni nini?” Ivan akamuuliza swahiba wake.
“Sina wasiwasi,”
“Hayo ndiyo maneno. By the way, utakuwa na Barbier kwa takriban wiki tatu au mwezi hivi. Yeye atakupitisha katika michakato tofauti ya kukubadili na kukurudisha tena kwenye uwanja wa vita,” Ivana akamwambia Mtokambali.
“Kunibadili?” akauliza.
“Naam, wewe utahukumiwa kufa, na utakufa, sasa sisi tunakuua mapema na kukurejesha vitani,” akamweleza, “Barbier!” akaita.
“Yes Sir!”
“Mweleze kinachoendelea kwa ajili yake,” Ivan akamwambia yule mwanamke. Barbier akavuta droo kubwa chini ya meza hiyo, akatoa kabrasha moja na kuliweka mezani. Alipoifunga ile droo, akalifungua lile kabrasha. Ndani yake kulikuwa na karatasi kama kumi hivi zote zikiwa na sura za watu, wazungu na majina yao. Zaidi ya hapo kuliokuwa na tarakimu nyingi sana.
“Nani unampenda kati ya hawa?” Barbier akamuuliza Mtokambali huku akimsogezea lile kabrasha. Mgeni huyo akachukua lile kabrasha na kuanza kulipekuapekua. Picha namba kumi na moja, akaipenda. Akamrudishia Barbier lila kabrasha kama alivyopewa, yaani kwa kulisukuma.
“Ok!” Barbier akatamka. Akaitatua ile karatasi na kuondoka pale mezani akiwaacha Mtokambali na Ivan, marafiki wawili.
“Don’t worry Kibwana. Hakuna linaloshindikana chini ya jua, utaona tu. Mimi na watu wangu tutakupa kila kitu ili ufanikishe lengo. Mafanikio yako ndiyo yetu kama tulivyopanga,” Ivan akamtoa wasiwasi.
Dakika kumi baadae, Barbier alirudi na kuketi katika kiti kilekile.
“Kila kitu sawa?” Ivan akamuuliza.
“Ndiyo! Kinachofuata ni kujiandaa kwa safari wiki moja ijayo. Dakta Punchkunel yuko tayari na atakuwa kwa ajili yetu siku hiyo,” Babier akatoa maelezo. Wakati yuote haya yakionelewa, Kibwana alikuwa kimya akigugumia vodka yake. Hakuna alichokielewa zaidi ya kusikia tu.
ITAENDELEA