Madame S
JF-Expert Member
- Mar 4, 2015
- 17,190
- 34,526
RIWAYA: CODE X 3:
THE REAL ME 1
MTUNZI: Tariq Haji
SEHEMU YA 1
"Niko wapi, niko mbinguni au" aliongea Alex baada kufumbua macho kutoka katka usingizi wa kifo, "tulia kijana, utafikaje mbinguni wakati hujafa" aliongea mzee mmoja wa makamo huku akitabasamu na kumuekea Alex mkono begani "uko mahali salama kabisa" aliendelea kuongea mzee huyo. Alex alijaribu kuzivuta kumbukumbu zake za mara ya mwisho. Na ndipo akakumbuka kuwa alipigwa risasi na Agent Darling, akaanza kuwaza ikiwa risasi ile hajapigwa yeye , je aliepigwa ni nani?. Swali hilo lilizuka ghafla kichwani mwake, "isije ikawa wamemuuwa hawa". "Alex karibu tena duniani" aliingia mwanamke mmoja aliekuwa amevaa kinyago nusu katika uso wake. "unanikumbuka" aliobgea mwanamke na kukaa pembeni kwenye kiti. "hapana sikukumbuki" alijibu Alex huku akijaribu kukaa, "hahaha kweli Alex umenisahau?" aliuliza tena huku akicheka. "subiri hiyo sauti kama naijua" Alex aliongea huku akivuta kumbkumbu zake vizuri ghafla akaruka "Scarlet ni wewe au". "kumbe bado kichwa chako kipo vizuri" alijibu Scarlet, "wema haupotei" aliendelea kuongea mwanamke huyo mwenye tabasamu lenye kumuweka simba kichaa chini. Alionekana kuwa mchangamfu kupita maelezo lakini kwa mtu ambe na uwezo wa kusoma sura vizuri basi angegundua kuwa uchamgamfu wake pamoja na tabsamu vilikuwa ni danganya toto tu. Mtu pekee alielielewa hilo ni General Griffin, ambae ni baba mlezi wa Scarlet. "Hebu nambie nimeokokaje" aliongea Alex, "usijali nitakwambia kila" alijibu Scarlet na kumuangalia Alex.
"Ni hivi, nilisikia kinachoendelea kupitia vyanzo vyangu vya habari na uchunguzi. Taarifa nilizipata wakati natoka Mexico katika kazi maalum niliyopewa na serekali, ndipo nikaskia kuwa kua mtu anaitwa Alex na ni muuaji mkubwa sana. Nikaanza kufatilia na ndipo nikagundua kuwa Alex mwenyewe ni wewe, na pia nilianza kufatilia kwanini ulikuwa unatekeleza mauji hayo. Sasa siku moja nilifika katika ofisi za kitengo maalum cha upelelezi kama mwandishi wa habari. Wakati nashuka gari niliona vikosi vingi sana vya kuimarisha ulinzi wakati nataka kudadisi ghafla nilipitwa na gari ndogo nyeusi ikielekea upande waliopo wanajeshi na ilipofka ikaripuka. Kwa mbali nikauona ukianza kugawa dozi, bila kuchelewa nilipiga simu makao makuu waniletee chopa niondoke. ilichukua muda kufika, wakati naondoka sasa ndipo nikakuona juu ya jengo ukiwa umepiga magoti na mbele alikuwepo mwanamke aliekuwa ameshikilia bastola. Nilichukua sniper na kabla hajakupiga wewe nikamuwahi yeye, sijui hata nilimpiga wapi maana sikulenga kwa makini. Baada hapo nilikuchukua na kukuleta huku" Alimaliza kuongea Scarlet na kumuangalia Alex ambae macho yalikuwa yamemtoka kam mjusi aliebanwa na Mlango.
*******************************
"mkuu, Christina amemka" aliigia mwanamke mmoja aliejiulikana kwa jina la Martina, jeff aliinuka alipokaa na kuelekea chumba alichokuwa amelazwa Christina. "vipi hali yako" Swali a kwanza kuuliza alipofika ndani ya chumba hicho, "Jeff nimefikaje hapa?" aliuliza Christina. "tulia utajua kila kitu lakini kwanza unajiskiaje" Jeff alimtuliza na kumuuliza tena swali la kwanza. "vizuri kiasi na maumivu kwa mbali katika bega la mkono wa kushoto" alijibu Christina huku akijiangalia mkono ambao ulikuwa umefungwa bendeg. "usijali unahitaji siku chache tu, mkono utapona kabisa" alijibu Jeff huku akimshika mkono, "nilikukuta juu ya gorofa ukiwa unavuja damu huku ukiwa umepoteza fahamu,ndipo nikakuchukua na kukuleta huku katika kambi maalum, na wala usijali hakuna mtu anaejua kama uko hai ama umekufa" aliongea Jeff huku akimuangalia kwa makini, kwa vipi atazipokea taarifa hizo. "na kwanini wasijue kama niko hai ama nimekufa" aliuliza kwa mshangao, "nilikuwa nategemea swali hilo kutoka kwako" alijibu Jeff na kuinuka, alisogea mpaka ukutani na kubonyeza pahali. Ukuta ulifunguka na kulikuwa na TV, "naomba usikilize mwenyewe kabla sijakueleza chochote" aliongea Jeff na kuwasha Tv hiyo kubwa kisha akarudi alipokuwa amekaa wali na kukaa.
"mpendwa mwanangu Christina" iliskika sauti ya Allen James, "wakati utakapoupokea ujumbe huu uenda nikawa sipo tena duniani, nakuomba sikiliza kwa makini na uwatabue marafiki zako na maadui zako usije ukatumika kama nilivyotumika mimi" baada hapo sauti ya Allen ilikata na kuanza kusikika sauti nyingine "ndio baada Allen James kukamilisha kazi inabidi na yey afe, si mnaelwa kuwa kazi hii ni siri ya hali ya juu na hatakiwi mtu mwengien asiehusika afahamu, na kama Allen atashidwa kumuua Alex basi itabidi sisi tumuue yeye halafu kesi hii tunambambikizia Alex. Akirudi Christina na kufahamu kuwa babaake ameuwawa na Alex, nina uhakika hatopumzika mpaka atakapohakikisha Aex amekufa na baada ya hapo na yeye pia tunamuua ili kupoteza ushahidi kabisa. Mapinduzi hayawezi kuzuilika, na mtu na mwanae wote watatumika kama mbwa wa kuwindia"baada ya sauti hiyo kukata ilirudi tena sauti ya Allen "natumai utakuwa umefahamu nani mbaya wako na nani rafiki yako, atakae kuletea ujumbe ni Alex na ni mmoja kati ya watu ambao watakuwa msaada mkubwa kwako katika kukamilisha kazi ntakayokupa kama babaako. Nataka uwasambaratishe kama vumbi wale wote wanaotaka kuitndea nchi yetu mabaya, na kunitenda mimi babaako. Ni matumaini yangu kwamba utafanikisha zoezi hili kwa hali na mali, kama ikibidi ufe ili likamilike basi fanya hivo. Nakupenda sana mwanangu...mimi babaako Allen James" hapo ndio ulikuwa mwisho wa rikodi hiyo na katika kioo cha TV hio kutaoke maandishi mekundu yaliosemeka "THE END IS THE BEGINNING".
Christina alijikuta machozi yakimtoka bila mategemeo na kujisemea kwa sauti ya kinyonge "kwanini hukunipa mapema taarifa hii Alex", "Christina punguza jazba" aliongea Jeff. "najaribu ila nshindwa, kwakweli mtu niliokuwa nataka kumuua ndie mtu aliekuwa bega kwa bega na babangu katika mapambano, unafikiri ningemuua ningeenda kuiweka sura yangu siku ambayo ningekutana na babaangu" alianza kujilaumu sasa. "lakini jambo zuri ni kwamba hujamuua" aliongea Jeff akijaribu kumpa moyo. "una uhakika gani, mi sidhani kama atakuwa amepona baada majeraha yale niliompa" alizidi kujilaumu huku moyoni akijiapiza kulipiza kisasi hata kama itabidi damu yake imwagike. Jeff baada kusikia hivo, ikabidi anyamaze kwanza na kisha akainuka na kutoka na kutoka nje huku akimuacha Christina akiendelea kulia. "mbona umemuacha peke yake" aliuliza Talbot, "ndio inavotakiwa, kwa sasa anajaribu kukabiliana na uhalisia kwamba aliekuwa anamuwinda sie aliemuaa baba ake. Na tujiandae kwa mechi ngumu mbele kwasababu lazima atahitaji msaada wetu kukamilisha kazi yake" Jeff alijibu na kuelekea chumbani kwake kwa ajili ya kupumzika.
Christina aliendelea kulia huku akiwa mwekundu kwa hasira ambayo ilianza kukikitesa kichwa chake, mara kadhaa alipiga kelele na kuangusa vitu chini. Lakini hakuna mtu alieingia katika chumba chake, "hahaha....Christina wewe ni mjinga sana tena mjinga wa mwisho, hukuona muda wote kama Alex alikuwa kiajribu kukufikishia ujumbe". "hahaha... lakini amefanya uzembe mwenyewe kwa kutokupa ujumbe mapema", "General David mpumbavu mkubwa wee, utalipa huu unyama kwa damu yako mjinga mkubwa wewe. Ulidhani mimi ni babaangu, umekosea sana kucheza na baba angu kwani umesaini mkataba wa kifo na mimi...hahaha mshenzi wee". Alikuwa akiongea mwenyewe na kujijibu huku akicheka na baadhi ya wakati alikuwa analia, alionekana kama mtu aliechanganyikiwa tena si kidogo maana chumba kizima alikichafua chafua, alikuwa mevunja kila kitu kilichokuwemo katika chumba hicho kuanzia vitu viukubwa mpaka vidogo vidogo. "THE END IS THE BEGINNING....NDIO KWANZA SAFARI IMEANZA" alisema kwa nguvu huku machozi yakimtoka. "furahia siku zako za mwisho na kila anaehusika na wewe,nitauwa kuanzia sisimizi na kila kitu ambacho kimo katika himaya yako na yoyote atakaekaa mbele yangu na yeye pia atakufa...General David" alijisemea na kusimama kwenye kiti alichokuwa amekaa baada ya kushuka kitandani.
CODE X 3: THE REAL ME 2
***************************
"nimekwambia nenda nyumbani ukanyonye. leo ni siku mbya sana" Alex aliikumbuka sentensi aliomwambia Allen Jr kabla ya kumpa kichapo cha fisi mwizi. "natumai kwa sasa utakuwa ushaujua ukweli" alijisemea huku akijisifu kwa kufikisha ujumbe wa mwalimu wake Allen. Siku ile baada ya kumpiga mpaka kumzimisha, alitoa ile recorder alioambiwa kuwa ni kwa ajili ya Christina na kumtilia katika mfuko wa suruali yake kisha yeye akaondoka na kuendelea na pambano lake. "hivi kwanini hukuniacha nife tu maana tayari nilishapanga kwena kukutana na familia yangu mzima" Alex alimuuliza Scarlet aliekuwa pembeni bize akicheza game ya kivita. "unadhani kila mtu ambae anapata mikosi angetaka kufa, unadhani kungekuwa nawatu amabao wangekuwa tayari kupigania haki ya mtu" Scarlet alijibu na kuacha kucheza game, alionekana kukerwa na swali hilo la Alex. " ni bora ushukuru ulikuwa sehemu ambayo ulikuwa na marafiki na walikuwa wakikujali japo mlikuwa kambini" Scarlet aliongea huku akikaa mbele ya Alex na kumuangalia usoni. "mimi nimeishi maisha ya manyanyaso sana tokea nilipozaliwa" Scarlet aliendelea kuongea huku akionekana wazi kuumizwa na anachokiongea. "hebu nielezee maisha yako" Alex aliomba na kukaa mkao wa kula kusuburi binti huo aanze kumporomoshea mkasa wa maisha yake.
********************
Scarlet alianza kuelezea hadithi ya maisha yake "Jina langu halisi sio Scarlet kama wanavolifahamu wengi, ila jina langu ni Ariella Mark. Ni mtoto wa pekee katika familia yangu, na babaangu alinipa jina hilo kwa sababu mama angu alijifungua katika wakati mgumu sana wa maisha yao. Japo hali ilikuwa duni lakini niliweza kukuwa vizuri tu bila kusumbuliwa na magonjwa kama wengi walivyodhani. Ukweli wazazi wangu walinipenda sana, tena sana kupita maelezo. Nilipata kila kitu nilicholikitaka, taratibu maisha yalianza kunyooka na kuwa mazuri huku kubadilika huko kwa maisha kukiwachukiza ndugu wa karibu wa wazazi wangu. Nikiwa na miaka minne tulihama tulipokuwa tunakaa na kuhamia mjini kabisa ambako baba alikuwa amejenga nyumba mpya na ya kisasa kwa wakti huo. Nilianza shule japo nilikuwa nimechelewa lakini wazazi wangu hawakumsikliza mtu, nilianza shule ya awali na baada ya miaka mitatu niliingia darasa la kwanza. Wakati huo nilikuwa na miaka saba lakini kutokana na mwili wangu kuwa mdogo sana hakuna alieamini kuwa nina miaka hiyo. Lakini nashukuru Mungu kwa kunipa wazazi wenye hekima na busara kama wale, lakini kama tunavojua kuwa duniani tunapita hakuna kiumbe kitakachoishi milele. Basi hivyo ndivyo ilivokuwa kwa babaangu ambae nikiwa na kumi alpoteza ajali katika ajali ya ndege nikabaki na mama yangu tu.
THE REAL ME 1
MTUNZI: Tariq Haji
SEHEMU YA 1
"Niko wapi, niko mbinguni au" aliongea Alex baada kufumbua macho kutoka katka usingizi wa kifo, "tulia kijana, utafikaje mbinguni wakati hujafa" aliongea mzee mmoja wa makamo huku akitabasamu na kumuekea Alex mkono begani "uko mahali salama kabisa" aliendelea kuongea mzee huyo. Alex alijaribu kuzivuta kumbukumbu zake za mara ya mwisho. Na ndipo akakumbuka kuwa alipigwa risasi na Agent Darling, akaanza kuwaza ikiwa risasi ile hajapigwa yeye , je aliepigwa ni nani?. Swali hilo lilizuka ghafla kichwani mwake, "isije ikawa wamemuuwa hawa". "Alex karibu tena duniani" aliingia mwanamke mmoja aliekuwa amevaa kinyago nusu katika uso wake. "unanikumbuka" aliobgea mwanamke na kukaa pembeni kwenye kiti. "hapana sikukumbuki" alijibu Alex huku akijaribu kukaa, "hahaha kweli Alex umenisahau?" aliuliza tena huku akicheka. "subiri hiyo sauti kama naijua" Alex aliongea huku akivuta kumbkumbu zake vizuri ghafla akaruka "Scarlet ni wewe au". "kumbe bado kichwa chako kipo vizuri" alijibu Scarlet, "wema haupotei" aliendelea kuongea mwanamke huyo mwenye tabasamu lenye kumuweka simba kichaa chini. Alionekana kuwa mchangamfu kupita maelezo lakini kwa mtu ambe na uwezo wa kusoma sura vizuri basi angegundua kuwa uchamgamfu wake pamoja na tabsamu vilikuwa ni danganya toto tu. Mtu pekee alielielewa hilo ni General Griffin, ambae ni baba mlezi wa Scarlet. "Hebu nambie nimeokokaje" aliongea Alex, "usijali nitakwambia kila" alijibu Scarlet na kumuangalia Alex.
"Ni hivi, nilisikia kinachoendelea kupitia vyanzo vyangu vya habari na uchunguzi. Taarifa nilizipata wakati natoka Mexico katika kazi maalum niliyopewa na serekali, ndipo nikaskia kuwa kua mtu anaitwa Alex na ni muuaji mkubwa sana. Nikaanza kufatilia na ndipo nikagundua kuwa Alex mwenyewe ni wewe, na pia nilianza kufatilia kwanini ulikuwa unatekeleza mauji hayo. Sasa siku moja nilifika katika ofisi za kitengo maalum cha upelelezi kama mwandishi wa habari. Wakati nashuka gari niliona vikosi vingi sana vya kuimarisha ulinzi wakati nataka kudadisi ghafla nilipitwa na gari ndogo nyeusi ikielekea upande waliopo wanajeshi na ilipofka ikaripuka. Kwa mbali nikauona ukianza kugawa dozi, bila kuchelewa nilipiga simu makao makuu waniletee chopa niondoke. ilichukua muda kufika, wakati naondoka sasa ndipo nikakuona juu ya jengo ukiwa umepiga magoti na mbele alikuwepo mwanamke aliekuwa ameshikilia bastola. Nilichukua sniper na kabla hajakupiga wewe nikamuwahi yeye, sijui hata nilimpiga wapi maana sikulenga kwa makini. Baada hapo nilikuchukua na kukuleta huku" Alimaliza kuongea Scarlet na kumuangalia Alex ambae macho yalikuwa yamemtoka kam mjusi aliebanwa na Mlango.
*******************************
"mkuu, Christina amemka" aliigia mwanamke mmoja aliejiulikana kwa jina la Martina, jeff aliinuka alipokaa na kuelekea chumba alichokuwa amelazwa Christina. "vipi hali yako" Swali a kwanza kuuliza alipofika ndani ya chumba hicho, "Jeff nimefikaje hapa?" aliuliza Christina. "tulia utajua kila kitu lakini kwanza unajiskiaje" Jeff alimtuliza na kumuuliza tena swali la kwanza. "vizuri kiasi na maumivu kwa mbali katika bega la mkono wa kushoto" alijibu Christina huku akijiangalia mkono ambao ulikuwa umefungwa bendeg. "usijali unahitaji siku chache tu, mkono utapona kabisa" alijibu Jeff huku akimshika mkono, "nilikukuta juu ya gorofa ukiwa unavuja damu huku ukiwa umepoteza fahamu,ndipo nikakuchukua na kukuleta huku katika kambi maalum, na wala usijali hakuna mtu anaejua kama uko hai ama umekufa" aliongea Jeff huku akimuangalia kwa makini, kwa vipi atazipokea taarifa hizo. "na kwanini wasijue kama niko hai ama nimekufa" aliuliza kwa mshangao, "nilikuwa nategemea swali hilo kutoka kwako" alijibu Jeff na kuinuka, alisogea mpaka ukutani na kubonyeza pahali. Ukuta ulifunguka na kulikuwa na TV, "naomba usikilize mwenyewe kabla sijakueleza chochote" aliongea Jeff na kuwasha Tv hiyo kubwa kisha akarudi alipokuwa amekaa wali na kukaa.
"mpendwa mwanangu Christina" iliskika sauti ya Allen James, "wakati utakapoupokea ujumbe huu uenda nikawa sipo tena duniani, nakuomba sikiliza kwa makini na uwatabue marafiki zako na maadui zako usije ukatumika kama nilivyotumika mimi" baada hapo sauti ya Allen ilikata na kuanza kusikika sauti nyingine "ndio baada Allen James kukamilisha kazi inabidi na yey afe, si mnaelwa kuwa kazi hii ni siri ya hali ya juu na hatakiwi mtu mwengien asiehusika afahamu, na kama Allen atashidwa kumuua Alex basi itabidi sisi tumuue yeye halafu kesi hii tunambambikizia Alex. Akirudi Christina na kufahamu kuwa babaake ameuwawa na Alex, nina uhakika hatopumzika mpaka atakapohakikisha Aex amekufa na baada ya hapo na yeye pia tunamuua ili kupoteza ushahidi kabisa. Mapinduzi hayawezi kuzuilika, na mtu na mwanae wote watatumika kama mbwa wa kuwindia"baada ya sauti hiyo kukata ilirudi tena sauti ya Allen "natumai utakuwa umefahamu nani mbaya wako na nani rafiki yako, atakae kuletea ujumbe ni Alex na ni mmoja kati ya watu ambao watakuwa msaada mkubwa kwako katika kukamilisha kazi ntakayokupa kama babaako. Nataka uwasambaratishe kama vumbi wale wote wanaotaka kuitndea nchi yetu mabaya, na kunitenda mimi babaako. Ni matumaini yangu kwamba utafanikisha zoezi hili kwa hali na mali, kama ikibidi ufe ili likamilike basi fanya hivo. Nakupenda sana mwanangu...mimi babaako Allen James" hapo ndio ulikuwa mwisho wa rikodi hiyo na katika kioo cha TV hio kutaoke maandishi mekundu yaliosemeka "THE END IS THE BEGINNING".
Christina alijikuta machozi yakimtoka bila mategemeo na kujisemea kwa sauti ya kinyonge "kwanini hukunipa mapema taarifa hii Alex", "Christina punguza jazba" aliongea Jeff. "najaribu ila nshindwa, kwakweli mtu niliokuwa nataka kumuua ndie mtu aliekuwa bega kwa bega na babangu katika mapambano, unafikiri ningemuua ningeenda kuiweka sura yangu siku ambayo ningekutana na babaangu" alianza kujilaumu sasa. "lakini jambo zuri ni kwamba hujamuua" aliongea Jeff akijaribu kumpa moyo. "una uhakika gani, mi sidhani kama atakuwa amepona baada majeraha yale niliompa" alizidi kujilaumu huku moyoni akijiapiza kulipiza kisasi hata kama itabidi damu yake imwagike. Jeff baada kusikia hivo, ikabidi anyamaze kwanza na kisha akainuka na kutoka na kutoka nje huku akimuacha Christina akiendelea kulia. "mbona umemuacha peke yake" aliuliza Talbot, "ndio inavotakiwa, kwa sasa anajaribu kukabiliana na uhalisia kwamba aliekuwa anamuwinda sie aliemuaa baba ake. Na tujiandae kwa mechi ngumu mbele kwasababu lazima atahitaji msaada wetu kukamilisha kazi yake" Jeff alijibu na kuelekea chumbani kwake kwa ajili ya kupumzika.
Christina aliendelea kulia huku akiwa mwekundu kwa hasira ambayo ilianza kukikitesa kichwa chake, mara kadhaa alipiga kelele na kuangusa vitu chini. Lakini hakuna mtu alieingia katika chumba chake, "hahaha....Christina wewe ni mjinga sana tena mjinga wa mwisho, hukuona muda wote kama Alex alikuwa kiajribu kukufikishia ujumbe". "hahaha... lakini amefanya uzembe mwenyewe kwa kutokupa ujumbe mapema", "General David mpumbavu mkubwa wee, utalipa huu unyama kwa damu yako mjinga mkubwa wewe. Ulidhani mimi ni babaangu, umekosea sana kucheza na baba angu kwani umesaini mkataba wa kifo na mimi...hahaha mshenzi wee". Alikuwa akiongea mwenyewe na kujijibu huku akicheka na baadhi ya wakati alikuwa analia, alionekana kama mtu aliechanganyikiwa tena si kidogo maana chumba kizima alikichafua chafua, alikuwa mevunja kila kitu kilichokuwemo katika chumba hicho kuanzia vitu viukubwa mpaka vidogo vidogo. "THE END IS THE BEGINNING....NDIO KWANZA SAFARI IMEANZA" alisema kwa nguvu huku machozi yakimtoka. "furahia siku zako za mwisho na kila anaehusika na wewe,nitauwa kuanzia sisimizi na kila kitu ambacho kimo katika himaya yako na yoyote atakaekaa mbele yangu na yeye pia atakufa...General David" alijisemea na kusimama kwenye kiti alichokuwa amekaa baada ya kushuka kitandani.
CODE X 3: THE REAL ME 2
***************************
"nimekwambia nenda nyumbani ukanyonye. leo ni siku mbya sana" Alex aliikumbuka sentensi aliomwambia Allen Jr kabla ya kumpa kichapo cha fisi mwizi. "natumai kwa sasa utakuwa ushaujua ukweli" alijisemea huku akijisifu kwa kufikisha ujumbe wa mwalimu wake Allen. Siku ile baada ya kumpiga mpaka kumzimisha, alitoa ile recorder alioambiwa kuwa ni kwa ajili ya Christina na kumtilia katika mfuko wa suruali yake kisha yeye akaondoka na kuendelea na pambano lake. "hivi kwanini hukuniacha nife tu maana tayari nilishapanga kwena kukutana na familia yangu mzima" Alex alimuuliza Scarlet aliekuwa pembeni bize akicheza game ya kivita. "unadhani kila mtu ambae anapata mikosi angetaka kufa, unadhani kungekuwa nawatu amabao wangekuwa tayari kupigania haki ya mtu" Scarlet alijibu na kuacha kucheza game, alionekana kukerwa na swali hilo la Alex. " ni bora ushukuru ulikuwa sehemu ambayo ulikuwa na marafiki na walikuwa wakikujali japo mlikuwa kambini" Scarlet aliongea huku akikaa mbele ya Alex na kumuangalia usoni. "mimi nimeishi maisha ya manyanyaso sana tokea nilipozaliwa" Scarlet aliendelea kuongea huku akionekana wazi kuumizwa na anachokiongea. "hebu nielezee maisha yako" Alex aliomba na kukaa mkao wa kula kusuburi binti huo aanze kumporomoshea mkasa wa maisha yake.
********************
Scarlet alianza kuelezea hadithi ya maisha yake "Jina langu halisi sio Scarlet kama wanavolifahamu wengi, ila jina langu ni Ariella Mark. Ni mtoto wa pekee katika familia yangu, na babaangu alinipa jina hilo kwa sababu mama angu alijifungua katika wakati mgumu sana wa maisha yao. Japo hali ilikuwa duni lakini niliweza kukuwa vizuri tu bila kusumbuliwa na magonjwa kama wengi walivyodhani. Ukweli wazazi wangu walinipenda sana, tena sana kupita maelezo. Nilipata kila kitu nilicholikitaka, taratibu maisha yalianza kunyooka na kuwa mazuri huku kubadilika huko kwa maisha kukiwachukiza ndugu wa karibu wa wazazi wangu. Nikiwa na miaka minne tulihama tulipokuwa tunakaa na kuhamia mjini kabisa ambako baba alikuwa amejenga nyumba mpya na ya kisasa kwa wakti huo. Nilianza shule japo nilikuwa nimechelewa lakini wazazi wangu hawakumsikliza mtu, nilianza shule ya awali na baada ya miaka mitatu niliingia darasa la kwanza. Wakati huo nilikuwa na miaka saba lakini kutokana na mwili wangu kuwa mdogo sana hakuna alieamini kuwa nina miaka hiyo. Lakini nashukuru Mungu kwa kunipa wazazi wenye hekima na busara kama wale, lakini kama tunavojua kuwa duniani tunapita hakuna kiumbe kitakachoishi milele. Basi hivyo ndivyo ilivokuwa kwa babaangu ambae nikiwa na kumi alpoteza ajali katika ajali ya ndege nikabaki na mama yangu tu.