RITA yapiga marufuku uvaaji wa mavazi yasiyofaa

Ukiondoa hiyo namba moja mengine yote ni kweli yanatekelezwa ktk ofisi za umma. Kama huamini wewe vaa kaptula halafu nenda kwa ofisi ya wizara yoyote ndo utajua!
 
Mie nilishajivumbulia utamaduni wetu waswahili wa kuthamini wageni zaidi. Nikiingia mahali nikahisi watanimind mavazi yangu, najidai sijui kiswahili. Nawatania kidhungu nalegeza ulimi slang kama Nyani Ngabu, wananipa priority huyooo naishia zangu! Cha kufia! Hamna ufanisi, hamtimizi ahadi kwa wateja mnataka wavai wardrobe zenu! Eboo!

Heheheheee una visa wewe!
 
Huyu yupo amemlenga na akatoa ahadi kwamba atamkomesha! Haingii akilini mtu mwenye mamlaka kutoa ****** kama huo ingawa hakuna kisichowezekana TZ.
 
Hiyo namba 1 sio sahihi kabisa. Ku-list nikab kama mavazi yasiyofaa ni uonevu.
Sasa hata wateja wanakuwa monitored, kama natoka kukaanga samaki ferry napitia vyeti vyangu inabidi nibebe suti kwenye kirambo? Badala ya kukazania ufanisi wanaangalia mavazi, bongo bwana!


ofisi yoyote ya kiserikali hawaruhusiwi kuvaa kininja hiyo inaeleweka, vaa hijabu hakuna atakaye kuuliza hiyo inaeleweka kuwa ni vazi la kina mama wa kiisalm,
 
Jamani acheni jazba zisizo na mpango. Kila ofisi lazima iweke taratibu za kimaadili kulingana na hadhi ya ofisi hiyo ua sababu za kiusalama. Nendeni basi Ikulu au ofisi ya waziri mkuu muone kama mtaruhusiwa kuingia Ninja style.

Ofisi ya waziri mkuu kuna tangazo kama hilo na ukienda na kimini au singlet yako haupiti hata kama unapeleka magazeti.

Naomba kuwauliza swali mnaosema watu wanaoenda na Nikab waruhusiwe kuingia RITA. Wakifika mbele ya Ofisa mtoa cheti na mtu kaja anataka kupewa cheti cha kuzaliwa, unathibitishaje kuwa huyu ndo mhusika kwa kutazama picha yake na sura yake halisi? Imagine ndiyo wewe umesimamiwa na mtu mbele yako hauoni kitu zaidi ya macho, je unamwambia jifunue au?

Kila ofisi ina taratibu zake kama unajisikia sana hamu ya kuvaa mlegezo au singlet Dar ni joto sana nenda kavae wanakoruhusu. Ofisi zote za umma zinafanya kazi kwa niaba ya Mkuu wa Nchi hata kama ni ofisi ya kata. Kama mtu anadhani anaweza kwenda mbele ya Mkuu wa Nchi akiwa maziwa yako nje au na singlet au Nikab basi atetee hoja hii.

Tuvae jeans na tops huku ambako wanaruhusu kujirusha maofisini tuwaachie wengine na ofisi na masharti yao.
 
Mavazi yasiyo na heshima??????? Hii inatia shaka kama nikabu ni vazi lisilo na heshima. Unategemea vazi gani liwe la heshima kuliko nikabu???? Shaka ni pale unapokataza nikabu na kuruhusu kimini (hakuna katika orodha) hivyo kimini ni vazi la heshima.
Unatakiwa kutoa vigezo vya kujumuisha nikabu kwenye vazi lisilo la heshima vinginevyo utaeleweka tofauti -kuwa unapinga utamaduni wa dini ya kiislamu kwa msimamo hasi. POLE hapa siyo ufaransa kwa makafiri waliokubuhu eh. Jihadhali ndugu
 
nakubaliana na wewe @ Chupaku-kuhusu kumtambua mtu. iwapo lengo ni kutaka kuwatambua watu kwa sura zao hilo ni sahihi, lakini kama ni mavazi yasiyo ya heshima kama inavyosomeka hapo kwenye tangazo basi kuna kasoro. Nikab na hijabu ni nguo za heshima. Ofisi kuwa na utaratibu huo ni sahihi kabisa lakini mbona kimini kimeachwa -je ni nguo ya heshima hiyo kuliko nikabu? Wambie RITA warekebishe tangazo lao. Ikiwa lengo pia ni kumtambua -bado ofisa husika anayo haki ya kumwambia naomba utoe nikab yako-kila mwenue kuvaa nikab anajua hilo atatekeleza iwapo ni kwa ajili ya kulinganisha picha ya kitambulisho na mhusika.
 
Hiyo namba 1 sio sahihi kabisa. Ku-list nikab kama mavazi yasiyofaa ni uonevu.
Sasa hata wateja wanakuwa monitored, kama natoka kukaanga samaki ferry napitia vyeti vyangu inabidi nibebe suti kwenye kirambo? Badala ya kukazania ufanisi wanaangalia mavazi, bongo bwana!

Saa nyingine tuwe tunatumia akili zetu hata kama ni gharama. Hivi ukivaa nguo ukaacha macho tu, tunawezaje kukutambua wewe ni nani?
 
Yaani huyo muandishi kwanza hajui kuandika Kiswahili fasaha, hajui kanuni za uandishi, hana mantiki ya kuweza kujua namna ya kutenganisha mavazi ya kiimani na mavazi yasiyofungamana na imani, hana mantiki ya kuelewa kuwa pale ni ofisi ya serikali na haiwezi kunyima watu huduma kwa sababu tu ya "maadili" ambayo hayajaainishwa popote kwenye waraka wa serikali

Hajafika hata la saba huyu, mie nakataa kuwa kafika

NIkukumbushe kuwa, katiba yetu vile vile haina sehemu inayokataza mtu kuvaa kimini. KAtiba yetu haimkatazi mtu kuweka miguu juu ya meza anapoingia kwenye ofisi ya mtu. Sasa tumia akili yako kujua kuwa kuna mazingira ambayo lzm yakae kwa mkao wa shughuli za mahali u\husika.
 
Wakuu wangu ni lazima tutambue kwamba ofisi za serikali na taasisi zake siyo sehemu za starehe,nyumbani kwako ama vijiwe ambako unaweza ukajivalia unavyotaka wewe. Kuhusu nikab mimi nasema ni sahihi kabisa. Haiwezekani uende ktk taasisi muhimu kama RITA umeziba uso. Ikiendekezwa tabia ya kuacha mambo eti tusihudhi dini ama dhehebu fulani kuna siku wengine watajitokeza watadai dini yao ama dhehebu lao hawavai nguo.
 
Muongozo wa mavazi ya staha kwa wafanyakazi na wateja/ wahudumiwa ni muhimu kuwepo hususan kwenye ofisi za umma. Hakuna ubaya wowote katika hilo.

Ubaya unajitokeza pale ambapo busara inakosekana katika huo muongozo.
 
Nimeshaelewa nia yenu nyie Wasomali mnaokazania kufunika nyuso. Mnataka janja ya kuwachukulia ndugu zenu vyeti kimtindo. Basi poleni, serikali imeshtuka. Ukitaka cheti, weka uso wazi ujulikane wewe ni nani
 
Hiyo namba 1 sio sahihi kabisa. Ku-list nikab kama mavazi yasiyofaa ni uonevu.
Sasa hata wateja wanakuwa monitored, kama natoka kukaanga samaki ferry napitia vyeti vyangu inabidi nibebe suti kwenye kirambo? Badala ya kukazania ufanisi wanaangalia mavazi, bongo bwana!

sio uonevu
 
Kwenye ofisi za RITA kuna hili tangazo.

TANGAZO

Ndugu wapendwa wateja wetu, mnakumbushwa kwamba hii ni taasisi ya Serikali ambayo inaendeshwa kimaadili hivyo basi hatutapendelea baadhi ya mavazi yasiyofaa na yasiyo na heshima kuvaliwa ofisi kama yafuatayo:-
  1. Mavazi yanayofunika uso wote - Kininja "Nikab".
  2. Singet (fulana zisizo na mikono)
  3. Kaptula
  4. Suruali zinazolegea "Mlegezo"
  5. Kofia kubwa "Parma"
  6. Vitop vya kike vinavyoonyesha vitovu
Wateja wetu mnakumbushwa kwamba atakayekiuka maagizo hayo hapo juu hataruhusiwa kuingia ndani kupata huduma zinazotolewa na Wakala.

UTAWALA
08 Februari 2011


rita.jpg

Pale makao makuu RITA joto kali, maana ni nje na watu wamebanana kwenye foleni ndefu - hivyo kutokwa jasho ni lazima. Ofisi za RITA Kinondoni utakutana na vilio vya watoto tokana na jasho - sasa ukivaa kaptula na fulana ingefaa sana ama la sivyo ofisi za RITA zifungwe air conditioners hapo ndio waje na hayo mawazo finyu. Waboreshe Maofisi yao kabla ya kuja na hayo mawazo. Itafika siku watatuambia asiyepiga mswaki hatapewa huduma. Lakini haya mambo wayafanye kwa mtu anayeomba kazi, anayeomba huduma apewe tu hata angefaa chupi. Kavaa chupi ni aibu yake si ya RITA.
 
Wakuu wangu ni lazima tutambue kwamba ofisi za serikali na taasisi zake siyo sehemu za starehe,nyumbani kwako ama vijiwe ambako unaweza ukajivalia unavyotaka wewe. Kuhusu nikab mimi nasema ni sahihi kabisa. Haiwezekani uende ktk taasisi muhimu kama RITA umeziba uso. Ikiendekezwa tabia ya kuacha mambo eti tusihudhi dini ama dhehebu fulani kuna siku wengine watajitokeza watadai dini yao ama dhehebu lao hawavai nguo.

oK RITA wamesema hilo, utaenda ofisi nyingine utaona vazi linaloziba uso lhalijazuiwa. Cha muhimu ni kua serikali ya CCM kila KIONGOZI anajiamulia tu anachopenda ama anachoamini - hamna miongozo, team work wala vipa umbele. Wajifunze mawasiliano kati yao ili wapeane mawazo mazuri - kukurupuka tu kwa kua unaamini una nia nzuri si vizuri.

Huu ni muda mzuri RITA wapanue maofisi ili wateja wasiwe nje ama kwenye makorido, pia ofisi ziwe na viyoyozi - DAR ni joto sana.
 
Jamani acheni jazba zisizo na mpango. Kila ofisi lazima iweke taratibu za kimaadili kulingana na hadhi ya ofisi hiyo ua sababu za kiusalama. Nendeni basi Ikulu au ofisi ya waziri mkuu muone kama mtaruhusiwa kuingia Ninja style.

Ofisi ya waziri mkuu kuna tangazo kama hilo na ukienda na kimini au singlet yako haupiti hata kama unapeleka magazeti.

Naomba kuwauliza swali mnaosema watu wanaoenda na Nikab waruhusiwe kuingia RITA. Wakifika mbele ya Ofisa mtoa cheti na mtu kaja anataka kupewa cheti cha kuzaliwa, unathibitishaje kuwa huyu ndo mhusika kwa kutazama picha yake na sura yake halisi? Imagine ndiyo wewe umesimamiwa na mtu mbele yako hauoni kitu zaidi ya macho, je unamwambia jifunue au?

Kila ofisi ina taratibu zake kama unajisikia sana hamu ya kuvaa mlegezo au singlet Dar ni joto sana nenda kavae wanakoruhusu. Ofisi zote za umma zinafanya kazi kwa niaba ya Mkuu wa Nchi hata kama ni ofisi ya kata. Kama mtu anadhani anaweza kwenda mbele ya Mkuu wa Nchi akiwa maziwa yako nje au na singlet au Nikab basi atetee hoja hii.

Tuvae jeans na tops huku ambako wanaruhusu kujirusha maofisini tuwaachie wengine na ofisi na masharti yao.

Mkuu soma tena tangazo. Sidhani kama umelielea. Nikab imeelezwa kwenye tangazo kama moja ya vazi lisilo na heshima. Unakubaliana na hilo? Kwamba Nikab sio vazi la heshima Tanzania? Kama dhumuni la tangazo lilikuwa uliyoandika hapo kwenye red, then si wangesema kwenye tangazo husika?
 
Nimeshaelewa nia yenu nyie Wasomali mnaokazania kufunika nyuso. Mnataka janja ya kuwachukulia ndugu zenu vyeti kimtindo. Basi poleni, serikali imeshtuka. Ukitaka cheti, weka uso wazi ujulikane wewe ni nani

Kwa kumbukumbu zangu hizi nikab zilianza valiwa na akina mama/dada wa Kisomali katikati ya miaka ya 80. Wakati huo wengi wakiishi maeneo ya Ilala NHC Flats na baadhi ya maeneo ya Kariakoo. Siku hizi dada na mama zetu wanavaa nikab. Ni haki yao kuvaa wanavyotaka lakini wakija ktk Ofisi za Serikali watambue kwamba wanapaswa kuonekana sura zao.
 
Back
Top Bottom