RITA NA KULIPIA VYETI MARA MBILI!

RITA NA KULIPIA VYETI MARA MBILI!

Mwene chungu

JF-Expert Member
Joined
Nov 12, 2016
Posts
915
Reaction score
752
Habari wanajamvi!

Nimebahatika kutembelea ofisi za RITA pale posta Mara kadhaa kufuatilia VYETI vya kuzaliwa vya vijana wangu.

Mara ya kwanza nilifuatilia Cha kijana wangu mkubwa nikafanya malipo ya 10,000 wakanipangia tarehe ya kukifuata lakini nilipoenda wakadai stakabadhi haisomeki kwenye mfumo (invalid receipt) yaani malipo si halali hivyo niamue moja ama kulipa tena au nisubiri hadi zitakapofanyiwa kazi.

Na kwa mjibu wa maelezo ya aliyekuwa ananihudumia hakusita kusema inaweza kuchukua miezi kadhaa..akanishauri nilipie tena ili kupata cheti haraka! Nilifanya hivyo mara ya hivyo,awamu hii nikakipata!.

Mapema mwa mwezi wa tatu mwaka huu nilienda kuandaa kingine,nikalipia 3500/= kwani mtoto bado mdogo.Kama kawaida nilipokifuata nikaambiwa invalid receipt na hivyo Kama nakihitaji haraka nilipie tena au kiwekwe foleni hadi receipt itakapohakikiwa kuwa ni halali!!


Kwa shingo upande nililipia tena huku nikagundua siko pekee yangu wenye tatizo Hilo,mathalani kwa wakati ule tuliolipia tena hatukuwa chini ya 20.


Nikakumbuka mwezi mmoja nyuma tulilipia tena karibu watu 7 au nane hivi kwa muda niliokaa pale Ofisini..nikajiuliza siku zingine wangapi wanalipia tena?.

Nikajiuliza hizi hela za Mara ya pili zinaenda wapi? ..Je viongozi tuliowapa dhamana ya kutatua matatizo hili hawajaliona? Kwanini waache litutese?

SIKUONA BOX LA MAONI PALE OFISINI

LAKINI NAAMINI KUPITIA MTANDAO HUU RITA MTALIFANYIA KAZI TATIZO HILI..

SIKU NYINGINE SITAANDIKA KWA LUGHA LAINI KAMA LEO.SITAKI KUTOA MAONI MAANA NYIE MNALIJUA ZAIDI HILI NI TATIZO KWA KIWANGO GANI.
IMG_20190512_155353.jpeg
 
Mnataka tukale wapi kwani huelewi iweje risiti ya mara ya pili haisumbui? Na Tunazipiga kweli Magu akishtuka mjengo umeisha.
 
Wamebuni njia ya kula kwa urefu wa kamba
 
Habari wanajamvi!

Nimebahatika kutembelea ofisi za RITA pale posta Mara kadhaa kufuatilia VYETI vya kuzaliwa vya vijana wangu.

Mara ya kwanza nilifuatilia Cha kijana wangu mkubwa nikafanya malipo ya 10,000 wakanipangia tarehe ya kukifuata lakini nilipoenda wakadai stakabadhi haisomeki kwenye mfumo (invalid receipt) yaani malipo si halali hivyo niamue moja ama kulipa tena au nisubiri hadi zitakapofanyiwa kazi.

Na kwa mjibu wa maelezo ya aliyekuwa ananihudumia hakusita kusema inaweza kuchukua miezi kadhaa..akanishauri nilipie tena ili kupata cheti haraka! Nilifanya hivyo mara ya hivyo,awamu hii nikakipata!.

Mapema mwa mwezi wa tatu mwaka huu nilienda kuandaa kingine,nikalipia 3500/= kwani mtoto bado mdogo.Kama kawaida nilipokifuata nikaambiwa invalid receipt na hivyo Kama nakihitaji haraka nilipie tena au kiwekwe foleni hadi receipt itakapohakikiwa kuwa ni halali!!


Kwa shingo upande nililipia tena huku nikagundua siko pekee yangu wenye tatizo Hilo,mathalani kwa wakati ule tuliolipia tena hatukuwa chini ya 20.


Nikakumbuka mwezi mmoja nyuma tulilipia tena karibu watu 7 au nane hivi kwa muda niliokaa pale Ofisini..nikajiuliza siku zingine wangapi wanalipia tena?.

Nikajiuliza hizi hela za Mara ya pili zinaenda wapi? ..Je viongozi tuliowapa dhamana ya kutatua matatizo hili hawajaliona? Kwanini waache litutese?

SIKUONA BOX LA MAONI PALE OFISINI

LAKINI NAAMINI KUPITIA MTANDAO HUU RITA MTALIFANYIA KAZI TATIZO HILI..

SIKU NYINGINE SITAANDIKA KWA LUGHA LAINI KAMA LEO.SITAKI KUTOA MAONI MAANA NYIE MNALIJUA ZAIDI HILI NI TATIZO KWA KIWANGO GANI.View attachment 1095229
Na hata cheti wakikosea jina wao ili kukilekebisha lazima ulipe tena 3500!!
 
Hapo Naona RITA Wamebuni Mbinu Mbaya Sana Control Number Wanatoa Wao Baadaye Wanaleta Ujanjaujanja. RITA Haina Viongozi Kweli Ama Watu Wamechoka Wanachota
 
Back
Top Bottom