Ripoti ya Richmond Bungeni (FULL TEXT) na yatokanayo

Swali ni moja watu wanalikwepa!Nini kilichofichwa na kamati ya Mwakyembe ili nchi isitikisike?
 
Yaliyopita sindwele tugange yajayo, hata tufanye nini hakuna kinachoweza kubadilika, tunajua vizuri chama chetu.
 
Mara baada ya kuahirishwa kikao cha Bunge jana jioni, Waziri Mkuu aliitisha kikao cha Mawaziri na Manaibu wao akidai ni kikao cha KIKAZI.

Katika kikao hicho aliwaambia kwamba serikali ilikua na nia njema katika suala zima la Richmond na kwamba mawaziri wanaothubutu kushabikia ripoti ya Richmond watajuta na itawagharimu. Akawaambia watumie nafasi zao "Kuwaelimisha" wabunge wote kuhusu nia njema ya serikali katika Richmond ili wasiishambulie. Wanasema aliingia akiwa hana raha na alipotoka wenzake walibaki wameduwaa na wakitafakari kwamba wanaambiwa watetee ripoti ambayo hawajui inasema nini!

Wakasema wanasubiri waione ili wajue ni wapi imekosewa ndipo wajue nini cha kusema, lakini hawawezi kujadili ama kutetea HEWA kwani na wao ni Wabunge ambao wametumwa na wapiga kura wao na hawana UHAKIKA na nafasi za UWAZIRI bali UBUNGE ndio walikotumwa. HATA HIVYO wakaambiwa kwamba SERIKALI HAITAWASILISHA TENA LEO ripoti ya Richmond katika kikao cha wabunge wa CCM bali itawasilishwa kwa wabunge wote na kujadiliwa. LOLOTE linaweza kutokea kati ya LEO (Jumanne) NA KESHO (Jumatano) siku ambayo JK alitoa nafasi ya mwisho kwa wabunge wa CCM KUWATOSA Mawaziri wanaoona kuwa ni MZIGO kwao.

Hapa Dodoma kuna TENSION ya hali ya juu

Na ifuatayo ndiyo ripoti ya kamati ya kina Mwakyembe:

Dah asee tulipigwa sana.

Ukisoma hii taarifa unaweza kulia.So hii Richmond ilikuwa ya Mamvi?
 
Huyu Lowassa sasa kazi imeshamshinda. Yuko busy kuficha madhambi yake. JK amtose haraka sana kabla mambo hayajawa mabaya zaidi.
2015 bado kidogo awe prezidaa.
Ilikuwaje alipata nguvu tena ndabi ya CCM baada ya hii kashfa?
 
Hata katika dunia ya kwanza mashirika nyeti kama ya umeme na maji yanamilikiwa na city councils au serikali. Haiwezekani mashirika nyeti kama TANESCO likaachiwa kuendeshwa na watu binafsi.

Tusifanye mambo ya kubinafsisha kwa pupa, tumeshafanya makosa mengi, lazima tukae chini na kuangalia athari za maamuzi ya kubinafsisha mashirika ya maji na umeme.

Mimi hapa umeme na maji ni bwelele lakini mashirika hayo hayako chini ya watu binafsi bali yako chini ya mji na bei zao ni poa. Pia ukija kwenye supply ya gas nalo linamilikiwa na mji lakini ukilinganisha na bei ya mashirika ya watu binafsi bei yao ni poa sana.

Tuache kufanya mambo kama kichwa cha mwendawzimu lazima tufikiri pia kuhusu athari za maamuzi hayo.
Lakini ukiangalia hapo utaona Uongozi wa Tenesco miaka ile ndio ulikuwa unatetea Tanesco isiingie mikataba hewa ila Waziri Nishati ndio anashinikiza mkataba wa Richmond
 
Mpaka leo shirika linajiendesha kwa hasara kwa kulipa madeni kutokana na huu ufisadi wa Lowassa.

wanatokea watu wachache eti wanajifanya kuumizwa na msiba wake.
 
Mpaka leo shirika linajiendesha kwa hasara kwa kulipa madeni kutokana na huu ufisadi wa Lowassa.

wanatokea watu wachache eti wanajifanya kuumizwa na msiba wake.
Nina swali kwako.
Je ina maana lowassa alikuwa anafanya maamuzi bila kumhusisha Rais?
 
Back
Top Bottom