Ripoti ya "ajabu" ya NAPE huko Houston...!

Bahati mbaya..,ndio nasema ni bahati mbaya sana kwa mahali kama JF, sehemu pekee katika social media ambapo watu wengi tunaoamini wanauelewa na ufahamu wa kutathmini na kufikiri kwa upana na umaridadi.,wanapokuwepo watu ambao akili zao na uwezo wao wa kufikiri hauzidi hata ule wa kidole cha "majivuno wa kusadikika"
 
Nyumbani ccm imegawika makundi makundi, magamba yamekwamia kiunoni, wewe unaenda kutatua migogoro Houston! Hayo si matumizi mabaya ya fedha? Au mnatuzuga umetumwa na mzee wa kuhemea ukatembeze bakuli? Angalia huko wanakuita duani! Safari ijayo sijuwi utatuambia unafuata nini make mgogoro alioushindwa jk wewe umeumaliza.
 
Nachelea kusema hao aliokutana nao sio watz ama ni watu wasiona uzalendo kwa nchi yao kwa waliowatz na wanaishi ughaibuni wanafahamu hali halisi ya ndugu, jamaa na marafiki zao wa huku tz sidhani wanaweza kupumbazwa na maneno ya Nape.
 

Hii imenoga zaidi,yaani kama tunatafuta post
ya kufungia mjadala hii ndiyo mwake! Brouha!ha!ha!
 
Mbona habari yako ni ya kiujumla kama kawaida ya habari zisizo na kichwa? Unasema alikwenda kutatua matatizo ya wana CCM Houston; Mbona hakuna picha kudhihirisha upatanishi? na Ijumaa Houston alikutana na viongozi wa upinzani wa CCM -- Jumamosi alikutana na jumuia ya Watanzania wapi alipata muda huo wa kuutatua mgogoro? Sasa kama umetatuliwa Viongozi ni kina nani sasa?

Upo USA jaribu kutupa in and out and the outcome --- hakuna cha kuficha...



 

Ndugu yangu nani kakwambia wanaweza kuja nchini, hao wengi wabeba maboksi wasiokuwa hata na makaratasi, hawawezi kurudi nyumbani, wakirudi ndio kimoja. Na kukaa marekani sio kigezo pekee cha kuwa na uelewa mpana, kama huna juhudi za kujielimisha unaweza ukawa marekani na uelewa wako ukawa kama mtu wa kutoka Sigimbi huko Newala. Sishangai kuwa Nape kawateka kiakili hawa jamaa, wengi upeo wao umemalizwa na kubeba maboksi.
 
Haya matatizo ya kutanguliza mbele hisia na kuweka nyuma ubongo sijui yataisha lini, yaani unajitengenezea karipoti kako kutokana na hisia zako halafu unategemea nini, machale kuncheza nkastuka!
 
kaka napata shida kidogo katika kuelewa na kupima uwezo wako wa kujadili nje ya hisia zako..,nani kakwambia picha ni kielelezo cha suluhu ya mjadala.,unaulizia muda ama wakati..??? na mwisho je unaamini kuwa ili sehemu yenye mgogoro itulie ni lazima viongozi wabadilishwe..,sio kosa lako ni MWALIMU wako....!
 
Not so fast ndugu yangu. Kujulikana kuwa mgogoro umeisha itachukua muda kidogo... Umeshawahi kuisikia ile methali inasema kupaka mafuta kwa mgongo wa chupa? kama kweli kulikuwa na mgogoro mkubwa kiasi hicho, si rahisi ukauisha kwa kasi hii unayoisimulia. Subira yavuta heri
 
Aisee! Naona mtu anaamua kujifagilia mwenyewe hapa! Kuwakutanisha watu wa familia mbili ndio uzoefu wa diplomasia za kimataifa? Hapa la ajabu liko wapi? Kwa siasa hizi za kitapeli na propaganda za kitaahira, Tanzania bado tuna safari ndefu!
 
Hii ripoti ni upuuzi tu na upiga debe usio na maana! Maisha nyumbani ni magumu sana sukari 3000 leo, dolla ndo hiyo inaelekea 2000. ninyi wazee wa Texas mnasumbuliwa na njaa tu hamna lolote! pigeni box acheni upuuzi wenu. Kwanza sina hakika kama hata wewe unayeandika umehwahi kutembela nyumbani hivi karibuni! Njia ina miiba ukitoka hurudi hahahahahahahahahaa
 

Naona baadhi ya watu wa Missouri kumbe wako Houston sasa.

Na huyo mmoja hapo katikati, si nilisikia alikuwa na kesi za mambo kama ya Mponjoli au mambo ya unga-unga? Au taarifa mbovu kama kawaida ya bongo?

Anyway, tukirudi kwa Nape wakati yeye anatalii huko wenzake wanakutana hapa na suala la uhai wake kama Mwenezi wa chama litagusiwa bila ajizi. Kuna watu wanakuja na agenda moja ya Nape na Chiligati waondoke. Watamsikiliza Mukama, ila nao watataka Mukama awasikilize. Mukama ana kazi.
 
Unamzungumzia nape yupi? huyu aliyekuwa anaongea matusi ya nguoni pale mwanza? au mwingine ? harafu si busara kumkejeri mwenyekiti unaposema nape kaonesha uwezo mkubwa kumshinda mwenyekiti, binafsi nahisi kizungu zungu kwa sababu huyo nape namfahamu kwa jinsi alivyo na akiri mbovu. sasa unaposifia kwamba hizo akiri ambazo mimi najua ni mbovu kwamba zimekuwa bora kuliko za mwenyekiti wake kwa hiyo kama nape anawezo mkubwa kuliko kikwete basi ikulu hakuna kitu , tunaenda kwa neema ya mungu
 
Inasikitisha!
Kama Watanzania hao waliridhika na majibu ya Nape, huku wakijua waziwazi hali halisi ya Mtanzania wa kawaida, BASI nashawishika kuzua shaka juu ya uzalendo wao, na huenda walifika Tanzania zamani mno!

Sina shaka kwamba hao waliomsikilkiza na kuridhika na majibu yake ni wale wasio na makaratasi, wanaishi huko kwa kuunga unga.

Mtu makini kabisa hawezi kuridhika na taarabu za nape hata siku moja, labda kama walimtangulizia maswali akaandaliwa majibu.
 
Kama ni muhimu kuweka Utanzania kwanza, mambo ya kuanzisha Matawi ya Vyama vya siasa nje yanasaidia nini ??? Kuna matawi mangapi ya CDM, CUF, TLP, NCCR MAGEUZI, PPT-Maendeleo n.k.
 

MAELEZO HAYA YOTE NI UONGO WA KUTUNGA.. MTU MZIMA MWONGO.. MAREKANI UNAYOONGELEA NI IPI.. TANDALE?.. UONGO MKUBWA HUU.. Halafu we Nape Unapata wapi Ujasiri wa Kutunga Uongo na kuumwaga JF this way..Kesho tunaamka na wewe Utuelezee nani kaandika Upupu Huu.. kwanini watanzania wa Migodini uwaaibishe.. that much you are.. nakwambia Kesho jamaa wanakusaka uingie mji wa watu, watu wanabondeka na maisha, kisha unawanyea kwa kutaka sifa zako..Ugomvi gani uliokuwepo na Umeutatua nini.. na hapanakukana thread hii.. Yaani kwmba wewe ni mbabe kuliko mzee?, Kitoga Yupi.. Kitoga huyu anaejifanya protokali ya viongozi.. si huyu tapeli ambaye anaishi kwa kumangamanga. si huyu kila pull ya greenvisa yumo na anatupwa nje. sasa habari za Kiherehere mmoja anauzia jina?.
 
Nape ni NURU na TAA ya matumaini yaliopotea CCM kwa siku nyingi.Anawanyima usingizi wapinzani wake na anazidi kuwatimulia vumbi, ushahidi ni Igunga.viva nape viva ccm viva kikwete.

Umesema vyema... Nape ni nuru na taa ya matumaini yaliyopotea CCM, sio Tanzania.... ni CCM!!!

at least ume-qualify statement yako....

As far as I am concerned, Nape is significant to CCM, and not Tanzania

Am I right?
 
Hapa jf unatakiwa uandike habari za mbowe,slaa,lema,ndesa kina lisu na kina halima mdee.ukiandika za kina nape unachefua watu kaka..learn the behaviours of jf b4 hujaingia kichwakichwa.
 
Wote waliopo huko hawajui maisha halisi ya mtanzania wa kawaida huku vijijini. Nape anapoteza tu muda huko wakati chama huku kina mgogoro mkubwa sana!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…