Ridhiwani Kikwete ampigia Membe kampeni bungeni

Ridhiwani Kikwete ampigia Membe kampeni bungeni

G Sam

JF-Expert Member
Joined
Apr 20, 2013
Posts
12,431
Reaction score
39,645
Bunge la leo limetawaliwa na vihoja vya hapa na pale wakati wa mjadala.

Wakati Benard Membe akiwasilisha hotuba yake ya bajeti ya wizara ya mambo ya nje alimpongeza Lowassa kama mwenyekiti wa kamati ili kupima upepo na ndipo yakasikika makofi na vigelegele kutoka kwa baadhi ya wabunge.

Hali iliendelea kuwa ya kikampeni zaidi katika mjadala. Huku wabunge wengine akionekana kumwambia Membe 'Mungu akutangulie katika safari yako'

Mbunge wa Chalinze Ridhiwani Kikwete alionyesha dhahiri kuwa anamuunga mkono Membe kwani wakati wa kuchangia bajeti hiyo alimueleza kuwa yupo upande wake na anamuombea Mungu amtangulie katika safari yake.

Vimbwenga vinaendelea na muda huu ni kampeni kwa kwenda mbele huku nje!

Lowassa na team yake hawaonekani hapa!

Kigwangala anagawa vitabu vyake huku akihaha kila kona.

Mwigulu anajichomeka penye kila mkusanyiko wa wabunge na ni kampeni kwa kwenda mbele!
 
lakini wengi tu wametakiwa kila la heri bungeni leo, ridhiwani pekee.
 
Nyie mnahangaika ti!! Rais ajae katulia zake kimyaaaa! Na si mwingine bali ni±--------------Ma ka mbaaaaaaaaaaaaaaa!!!!!!!!!!!
 
Kwa kweli wabunge wanatakiwa kuwa makini sana na kauli zao hasa katika kipindi hiki. Liziwan hakutakiwa kuweka msimamo wake hadharani wakati anatambua kabisa baba yake ni rais. Hii inaleta maana kuwa huo ndio msimamo wa baba yake. Upepo wa kisiasa hubadirika hivyo ni vizuri kuwa na uangalifu wa kila kauli unayotoa. Binafsi membe sioni jipya atakalofanya kwenye nchi hii.
 
Back
Top Bottom