Mdude_Nyagali
Member
- Dec 11, 2022
- 60
- 1,237
Da! Kifo cha Pande kimeniumiza mno. Alipokuwa ofisi ya DPP kanda ya Mbeya kabla ya kupandishwa cheo mara kadhaa alikuwa anakataa kesi za mchongo dhidi yangu alizopelekewa na polisi. Alishawahi kumkatalia RCO wa Songwe alipotaka niunganishwe kwenye mashtaka ya kuvuruga uchaguzi wa mamlaka ya mji mdogo Mlowo Mbozi na kufanya vujo iliyokuwa inamkabili aliyekuwa mbunge wa eneo hilo Pascal Haonga na wenzake. Baada ya RCO kukataliwa kwa sababu alikuwa na roho mbaya akanifungulia mashtaka mengine ya uchochezi, Pande akamuambia alete ushahidi RCO huyo kachemka kesi ikafutwa mahakamani baada ya ofisi ya DPP kushindwa kuleta mashahidi.
Alifanya hivyo kwa RCO wa Mbeya na askari wengine waliokuwa wananipikia kesi za mchongo. Alipohamishwa 2019 baadaye 2020 nikapewa kesi ya mchongo ya drugs trafficking ambayo ilisukwa na aliyekuwa kuwa RPC wa Mbeya mzee Mtei, RCO anaitwa Katimbo na ASP mmoja anaitwa Siyame, hawa siku yao inakuja lazima waje wajute kwa haya waliyoyanifanya.
Rest In Peace Ngosha Pande.
Alifanya hivyo kwa RCO wa Mbeya na askari wengine waliokuwa wananipikia kesi za mchongo. Alipohamishwa 2019 baadaye 2020 nikapewa kesi ya mchongo ya drugs trafficking ambayo ilisukwa na aliyekuwa kuwa RPC wa Mbeya mzee Mtei, RCO anaitwa Katimbo na ASP mmoja anaitwa Siyame, hawa siku yao inakuja lazima waje wajute kwa haya waliyoyanifanya.
Rest In Peace Ngosha Pande.