ChoiceVariable
JF-Expert Member
- May 23, 2017
- 43,045
- 49,728
Kwa mujibu wa Utafiti wa Repoa Watanzania Katika ngazi zote Wana Imani na Rais Samia na Serikali yake.
DAR: Utafiti uliofanywa na Taasisi inayojishughulisha na Utafiti, masuala ya Uchumi, Umaskini na Maendeleo ya Nchi ( Repoa), umeonesha Watanzania wana imani na Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan.
Mkurugenzi wa Utafiti Repoa, Dk Lucas Katera amesema hayo alipokuwa akiwasilisha repoti ya Mpango wa Tisa wa Afro Barometer.
Amesema katika masuala ya uchumi, Watanzania wanahofia kuhusu kupanda kwa bei za vitu na ajira kwa vijana, lakini wana matumaini na muelekeo kama nchi kutokana na utendaji kazi wa serikali na kwenye baadhi ya mambo.
Amesema katika eneo la utawala na sheria, utafiti unaonesha kuwa asilimia 82 wa Watanzania wametoa maoni yao kuwa Rais anaheshimu Mahakama na Sheria, huku asilimia 81 maoni yaliyokusanywa yanaonesha Rais anaheshimu Mahakama.
Kwa upande wa imani katika taasisi za umma, Dk Katera amesema utafiti umebaini kuwa asilimia 82 raia wana imani na Rais, huku asilimia 78 wakionyesha imani yao kwa Bunge lakini pia asilimia 79 wana imani na Tume ya Taifa ya Uchaguzi.
Habari Leo
DAR: Utafiti uliofanywa na Taasisi inayojishughulisha na Utafiti, masuala ya Uchumi, Umaskini na Maendeleo ya Nchi ( Repoa), umeonesha Watanzania wana imani na Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan.
Mkurugenzi wa Utafiti Repoa, Dk Lucas Katera amesema hayo alipokuwa akiwasilisha repoti ya Mpango wa Tisa wa Afro Barometer.
Amesema katika masuala ya uchumi, Watanzania wanahofia kuhusu kupanda kwa bei za vitu na ajira kwa vijana, lakini wana matumaini na muelekeo kama nchi kutokana na utendaji kazi wa serikali na kwenye baadhi ya mambo.
Amesema katika eneo la utawala na sheria, utafiti unaonesha kuwa asilimia 82 wa Watanzania wametoa maoni yao kuwa Rais anaheshimu Mahakama na Sheria, huku asilimia 81 maoni yaliyokusanywa yanaonesha Rais anaheshimu Mahakama.
Kwa upande wa imani katika taasisi za umma, Dk Katera amesema utafiti umebaini kuwa asilimia 82 raia wana imani na Rais, huku asilimia 78 wakionyesha imani yao kwa Bunge lakini pia asilimia 79 wana imani na Tume ya Taifa ya Uchaguzi.
Habari Leo
REPOA: 88% ya Watanzania hawawezi kuandamana dhidi ya Serikali
Utafiti wa Taasisi ya Utafiti REPOA unaonesha Watanzania wana hofu ya kukosa huduma muhimu za kijamii endapo watamchagua kiongozi yeyote kutoka vyama vya upinzani. Utafiti huo umeonesha kuwa asilimia 88 ya wananchi waliohojiwa walisema hawapo tayari kuandamana kuishinikiza Serikali kuwapatia...
www.jamiiforums.com