REINCARNATION maybe is real

REINCARNATION maybe is real

Watu wengi wanaamini ukifa ndio basi tena shughuli imeishia hapo akiwemo Hawking.

Hawking alifananisha maisha ya binadamu na computer, kwamba ikifa ndio basi tena.
Newton yeye aliamini ukifa unaweza fufuliwa tena.

Sasa kwenye point ya Hawking nina swali nataka nijibiwe na wanao muunga mkono, kama computer ikifa ndio basi tena, je haiwezekani ikatengenezwa maana mtengenezaji wa mwanzo alikuwepo?
Mkuu wala usitumie akili kubwa, we angalia tu mazingira yako utagundua kila kitu ni circle na tegemezi ya kitu kingine. Swali ambalo linatuumiza binadamu ni kurudi kwenye ufahamu ulio nao Sasa, mikopo uliyochukua Bank, mwanamke aliyekukataa, kijana au binti uliyemzaa n.k hii ndo linalotusumbua ila swali la sisi kuwa part ya circle ya ulimwengu hilo jibu lake lipo wazi kwenye mazingira tuliyopo. Mwili wako ni part ya mzunguko wa particles za Karne na karne tangu kuwepo kwa ulimwengu na utakapofutika hizo particles zinaenda kuwa sehemu ya kitu kingine humu humu ulimwenguni.
 
"Kujiongeza" na kudadisi ni vizuri mno. Lakini hebu fikiria; Kama ukweli unatokana na kujiongeza na kudadisi, na haupo wazi na thabiti, maana yake si kwamba huo ukweli haujapatikana bado?

Maana yake si kwamba hakuna dini inaweza kujibu kikamilifu tafakuri za maisha...
Kwanini watu hawawezi kuona hilo?

Si bora kukubali tu kuwa hakuna majibu, tuishi tu? Au ndo asili yetu binadamu kuwa wabishi wabishi?
Inshort ni ngumu kuthibitisha kitu ambacho hakina prove, wanaobisha wanasimamia hapo na wanaokubali wanashindwa kuleta prove so mada kama hizi huishia tu hewani na mwisho wa siku Kila mtu anabaki na kile anachokiamini
 

REINCARNATION IS REAL​


Reincarnation wazo kwamba consciousness au utambulisho wa mtu unaweza kuendelea baada ya kifo na kuonekana katika maisha mengine imejadiliwa kwa maelfu ya miaka. Lakini kinachovutia zaidi ni kwamba kuna kesi zilizochunguzwa na watafiti, si hadithi za kawaida tu. Division of Perceptual Studies ya University of Virginia imekusanya zaidi ya kesi 2,500 za watoto wanaodai kukumbuka maisha yaliyopita. Watoto wengi huanza kutoa maelezo wakiwa na miaka 2–5, mara nyingi bila kuambiwa kwamba wanapaswa kuamini reincarnation. Baadhi hutaja majina, maeneo, familia na mazingira ya kifo ambayo baadaye watafiti hujaribu kuyathibitisha.


Case ya James Leininger ni mojawapo ya zinazovutia zaidi. Akiwa mtoto mdogo, James alianza kuwa na nightmares kuhusu ndege ya kivita ikianguka na kutoa taarifa zilizohusishwa na rubani wa Marekani aliyekufa katika Vita vya Pili vya Dunia. Utafiti wa psychiatrist Jim Tucker wa University of Virginia ulipitia documentation ya statements na behaviors za James, ikiwemo taarifa zilizorekodiwa kabla ya rubani aliyedaiwa kuwa “previous personality” kutambuliwa. Tucker alihitimisha kwamba kulikuwa na similarity kubwa kati ya taarifa za mtoto na maisha/kifo cha James M. Huston Jr., ingawa case ina limitations hasa kwa sababu baba wa James ndiye aliyesaidia kumtafuta mtu aliyelingana na taarifa hizo.


Ushahidi mwingine wa kushangaza ni birthmarks na birth defects. Katika utafiti wa Ian Stevenson, baadhi ya watoto waliodai kukumbuka maisha yaliyopita walikuwa na alama au kasoro za kuzaliwa zilizodaiwa kuendana na majeraha ya mtu aliyekufa. Database ya UVA inasema takribani 30% ya cases zao zina birthmark au birth defect. Stevenson pia alichapisha cases ambazo alijaribu kulinganisha alama hizo na medical records, autopsy reports, police reports au ushahidi wa mashahidi. Kuna hata case iliyochapishwa kuhusu birthmarks zenye pattern kama nyuzi za kamba zilizolinganishwa na majeraha ya kamba kwa mtu aliyekufa.


Sasa swali kubwa linabaki: kama reincarnation si kweli, tunazielezaje cases hizi? Inawezekana baadhi zinaelezwa na coincidence, taarifa zilizopatikana bila kujua, influence ya wazazi, memory distortion au confirmation bias. Hiyo ndiyo sababu sayansi bado haijasema “reincarnation imethibitishwa.” Lakini pia si rahisi kuzipuuza zote kama fantasies, kwa sababu baadhi zina documentation na taarifa zinazoweza kuchunguzwa. Kwa hiyo, msimamo wangu si kwamba hizi cases ni proof ya mwisho, bali ni ushahidi unaofanya swali la reincarnation liwe zito zaidi kuliko watu wengi wanavyodhani: Je, consciousness inaweza kuendelea baada ya kifo, na kama ndiyo inawezaje kubeba taarifa kutoka maisha moja kwenda nyingine?

Poker
Every atom in your body was forged through the violent lives and deaths of stars.

The carbon in your cells, the oxygen you breathe, the calcium in your bones, and the iron in your blood were created through nuclear reactions inside stars or during explosive stellar events.

When massive stars reached the end of their lives, they exploded as supernovae, scattering these newly created elements across space.

Over millions and billions of years, that enriched material became part of new stars, planets, and eventually living worlds.

So when you look at the night sky, you're not simply looking at distant stars.

You're looking at the cosmic factories that created much of the material that makes you.

In a very real sense, the universe isn't just around you.

A part of the universe is inside you.

You are made from ancient material forged by stars that existed long before Earth was born.

"NIMEIKUTA SEHEMU"
 
Ni mwendo wa imani kwa wote.
Yeah coz kuna watu wanayaona maisha katika reality yaani kile anachokiona ndicho anachokiamini so chochote kinyume na hapo hana Imani nacho ila kuna watu wanayaona maisha kwenye reality na kwenye dhaania (Hawa ndio watu wa Imani).

Wote wako sahihi coz mchanganyo kama huo ndio uunda maisha kwa ujumla wake.
 
Watu wengi wanaamini ukifa ndio basi tena shughuli imeishia hapo akiwemo Hawking.

Hawking alifananisha maisha ya binadamu na computer, kwamba ikifa ndio basi tena.
Newton yeye aliamini ukifa unaweza fufuliwa tena.

Sasa kwenye point ya Hawking nina swali nataka nijibiwe na wanao muunga mkono, kama computer ikifa ndio basi tena, je haiwezekani ikatengenezwa maana mtengenezaji wa mwanzo alikuwepo?
Hawking alifananisha vipi maisha ya binadamu na computer?

Unaweza kutuwekea maneno yake mwenyewe ili tumuelewe vizuri zaidi na tuhakiki kama wewe pia umemuelewa?
 
Yeah coz kuna watu wanayaona maisha katika reality yaani kile anachokiona ndicho anachokiamini so chochote kinyume na hapo hana Imani nacho ila kuna watu wanayaona maisha kwenye reality na kwenye dhaania (Hawa ndio watu wa Imani).

Wote wako sahihi coz mchanganyo kama huo ndio uunda maisha kwa ujumla wake.
Ni ujuaji tu tunao hamna lolote mkuu.

Kelele zote zinaishaga ukishajifia sababu nature don't care umesoma, una akili au upoje. Fanya mbwembwe za ujuaji wako ila siri ya kifo kama huijui huna tofauti na wengine wanaomini wanaloamini kuhusu maisha na kifo.
 
Ni ujuaji tu tunao hamna lolote mkuu.

Kelele zote zinaishaga ukishajifia sababu nature don't care umesoma, una akili au upoje. Fanya mbwembwe za ujuaji wako ila siri ya kifo kama huijui huna tofauti na wengine wanaomini wanaloamini kuhusu maisha na kifo.
Ni kweli mkuu... Ila wewe uko upande gani?
 
Ni kweli mkuu... Ila wewe uko upande gani?
Nipo kwenye upande wa za kuambiwa "changanya na zako." Penye kutumia akili natumia akili, penye uhitaji wa Imani naipa nafasi Imani.

Kuna mengi sana binadamu hatujui, hatujui hata kama tunayoyaona ndivyo yalivyo. What if mifumo yetu ya ufahamu na utambuzi inatuhadaa?

Huwezi hitimisha jambo usilolielewa. Na uwezekano ni kuwa hatuelewi maisha ni nini, Kifo ni nini, Ulimwengu ni nini. Kama hatuelewi huwezi hitimisha kuwa mwenye Imani A yupo sahihi kiimani na mwenye Imani B anakosea kiimani.

Halafu, kutokuamini ni Imani, ili isiwe Imani inabidi uthibitishe kutokuamini. Mtu akisema haamini it means kinyume cha kutokuamini kwake ndicho anachoamini then tunarudi pale pale kwamba wote ni waamini na tunatumia Imani kusema huyu yupo sahihi na yule hayupo sahihi.
 
Nipo kwenye upande wa za kuambiwa "changanya na zako." Penye kutumia akili natumia akili, penye uhitaji wa Imani naipa nafasi Imani.

Kuna mengi sana binadamu hatujui, hatujui hata kama tunayoyaona ndivyo yalivyo. What if mifumo yetu ya ufahamu na utambuzi inatuhadaa?

Huwezi hitimisha jambo usilolielewa. Na uwezekano ni kuwa hatuelewi maisha ni nini, Kifo ni nini, Ulimwengu ni nini. Kama hatuelewi huwezi hitimisha kuwa mwenye Imani A yupo sahihi kiimani na mwenye Imani B anakosea kiimani.

Halafu, kutokuamini ni Imani, ili isiwe Imani inabidi uthibitishe kutokuamini kwako. Mtu akisema haamini it means kinyume cha kutokuamini kwake ndicho anachoamini then tunarudi pale pale kwamba wote ni waamini na tunatumia Imani kusema huyu yupo sahihi na yule hayupo sahihi.
Jibu lako limenyooka.... Duniani almost kila kitu kinajirudia over and over again ni sawa hii 1 useme moja na 2 useme mbili ila ikiwa 12 utasema kumi na mbili ila ni marudio ya moja na mbili.
 
Hawking alifananisha vipi maisha ya binadamu na computer?

Unaweza kutuwekea maneno yake mwenyewe ili tumuelewe vizuri zaidi na tuhakiki kama wewe pia umemuelewa?
IMG_5878.jpeg

IMG_5879.jpeg
 
Unaelewa kuwa kabla ya hizi computers mashine unazoziita computers leo, kulikuwa na watu wanaokokotoa namba walikuwa wanaitwa computers?

Unaelewa maana halisi ya neno computer, yani maana iliyo kubwa zaidi ya hii mashine inayoitwa computer?

Unaelewa kuwa computer = something that computes?

Na unaelewa kuwa, katika muktadha wa maneno ya Hawking, hiyo computer ya brain haijatengenezwa na mtu wala Mungu, imetokea kwenye mamilioni ya miaka ya evolution, kwa hiyo suala la aliyeitengeneza hiyo computer kuja kuikarabati ifanye kazi upya halipo?
 
Tafuta kitabu chake ukisome kisha utamuelewa zaidi. Na pia alimaanisha computer au kwa kiswahili tarakilishi. Hayo mengine ni yakwako. Kiranga
 
Back
Top Bottom