Mwanajamii
JF-Expert Member
- Mar 5, 2008
- 7,063
- 68
Katika salamu yake kwa waombolezaji,spika wa bunge mama Anne Makinda alitoa hotuba nzito fupi yenye maneno ya busara sana,kwamba Marehemu dada yetu Rejia ametuunganisha kwa utanzania wetu bila kujali tofauti zetu kiitikadi.makinda alimwelezea Rejia kuwa alikuwa mchapakazi hodari,mwenye moyo wa kujituma na kujitolea bila kujali hali yake kiafya kuwa mlemavu.anasema Rejia alikuwa analea yatima,vijana na hata watu wazima aliokuwa anaishi nao nyumbani pamoja na kuwa hakuwa na kipato zaidi ya posho tu ya ubunge.nampongeza makinda kwa kutambua mchango wa rejia na kuuthamini.bravo makunda.tunataka viongozi wa aina yako ambao hawana kinyongo na vijana wao