Matanga
JF-Expert Member
- Nov 13, 2019
- 2,281
- 3,973
.
Mishale ya saa tatu usiku Avenida Diagonal ilipo hoteli ya Gran Melia, siku moja kabla ya fainali wakati Sir Alex Ferguson na Steve McLaren (Kocha Msaidizi) wakiwa wanakuna vichwa nani aanze kikosini, hawana Paul Scholes wala Roy Keane
.
Baada ya kupokea ripoti ya msoma mbinu wao walielekea kwenye chumba cha mkutano, waliitwa wachezaji wote kwa ajili ya maamuzi ya kikosi cha fainali, Fergie alimpanga David Beckham na Nick Butt kama viungo wa kati, watu walistaajabu ila Fergie alimtaka Becks kwa kazi maalum
.
Giggs aliwekwa winga kulia na Jesper Blomqvist kushoto, United bila Henning Berg hapo ila Babu Fergie anacheza karata za hatari mno, Ronny Johnsen aliyetarajiwa acheze Kiungo akapelekwa beki ya kati na Jaap Stam, golini alikaa Schmeichel na kitambaa chake kwenye mechi yake ya mwisho
.
Wakati Babu kashafanya uchaguzi wa kikosi, alicheza na akili ya adui yake Ottmar Hitzfeld alitegemea White ila Babu kaja na Black, inaitwa Tactical Wizard and Prophetic ile pete ya Babu ilikua na Uchawi pamoja na Unabii, Babu kamaliza kazi anasubiri maajabu
.
Alasiri ile ya Mei 26, Mashetani Wekundu wanaagwa hotelini kuelekea Nou Camp ni mwendo wa dakika kadhaa tu, nalikumbuka bus aina ya 'Hyundai Faire' linashika njia, huku bendera za United njiani zinapepea, wanakwambia "The Red Devils and the Famous United" watu washalewa sana hapo
.
Ngoma inaanza kwa presha kubwa mno, United wanafanya makosa Johnsen anamchezea rafu Jancker kilichotokea ni faulo ya Mario Basler wanaingia kambani, United wanapigwa msako mkubwa sana Fergie hajui wapi atazame, Beckham kapotezwa mno eneo la Kiungo
.
Dakika zile tatu za Maajabu baada ya Supersub OGS na Sherringham, namwona Becks kwenye kibendera, dakika ya 90:36 analiachia gozi la mnyama hewani, Teddiee watu kati bado United wanapiga msako wa kufa mtu, United wamecharuka mno
.
Becks nywele zimetimka, Ole Gunnar anakuja pembeni, Nick Butt anawaambia pandeni nitabaki nyuma na Jaap Stam, dakika ya 92:15 ni Becks tena kona, analiachia gozi la Mnyama NIKE Nik Geo 800, Ole Gunnaar kambani 2-1
.
Thats the end of the 1999 Treble, GGMU
Sent using Jamii Forums mobile app
Mishale ya saa tatu usiku Avenida Diagonal ilipo hoteli ya Gran Melia, siku moja kabla ya fainali wakati Sir Alex Ferguson na Steve McLaren (Kocha Msaidizi) wakiwa wanakuna vichwa nani aanze kikosini, hawana Paul Scholes wala Roy Keane
.
Baada ya kupokea ripoti ya msoma mbinu wao walielekea kwenye chumba cha mkutano, waliitwa wachezaji wote kwa ajili ya maamuzi ya kikosi cha fainali, Fergie alimpanga David Beckham na Nick Butt kama viungo wa kati, watu walistaajabu ila Fergie alimtaka Becks kwa kazi maalum
.
Giggs aliwekwa winga kulia na Jesper Blomqvist kushoto, United bila Henning Berg hapo ila Babu Fergie anacheza karata za hatari mno, Ronny Johnsen aliyetarajiwa acheze Kiungo akapelekwa beki ya kati na Jaap Stam, golini alikaa Schmeichel na kitambaa chake kwenye mechi yake ya mwisho
.
Wakati Babu kashafanya uchaguzi wa kikosi, alicheza na akili ya adui yake Ottmar Hitzfeld alitegemea White ila Babu kaja na Black, inaitwa Tactical Wizard and Prophetic ile pete ya Babu ilikua na Uchawi pamoja na Unabii, Babu kamaliza kazi anasubiri maajabu
.
Alasiri ile ya Mei 26, Mashetani Wekundu wanaagwa hotelini kuelekea Nou Camp ni mwendo wa dakika kadhaa tu, nalikumbuka bus aina ya 'Hyundai Faire' linashika njia, huku bendera za United njiani zinapepea, wanakwambia "The Red Devils and the Famous United" watu washalewa sana hapo
.
Ngoma inaanza kwa presha kubwa mno, United wanafanya makosa Johnsen anamchezea rafu Jancker kilichotokea ni faulo ya Mario Basler wanaingia kambani, United wanapigwa msako mkubwa sana Fergie hajui wapi atazame, Beckham kapotezwa mno eneo la Kiungo
.
Dakika zile tatu za Maajabu baada ya Supersub OGS na Sherringham, namwona Becks kwenye kibendera, dakika ya 90:36 analiachia gozi la mnyama hewani, Teddiee watu kati bado United wanapiga msako wa kufa mtu, United wamecharuka mno
.
Becks nywele zimetimka, Ole Gunnar anakuja pembeni, Nick Butt anawaambia pandeni nitabaki nyuma na Jaap Stam, dakika ya 92:15 ni Becks tena kona, analiachia gozi la Mnyama NIKE Nik Geo 800, Ole Gunnaar kambani 2-1
.
Thats the end of the 1999 Treble, GGMU
Sent using Jamii Forums mobile app