Record za utendaji wa Edward Lowassa zinashangaza sana

Record za utendaji wa Edward Lowassa zinashangaza sana

Jamani CCM kuna watu wa maana wenye akili utendaji mzuri, wasio mafisadi, wasio na laana ya Nyerere na wenye afya njema kama kina Warioba, hamuwaoni? achaneni na haya mafisadi?
 
Lowasa nimeshatamka hawezi kuwa raisi wa nchi hii. Mbona unajiuma uma hutaki kuongelea uchafu wake? Is better ukaishi kwa utu wako kulikok hiyo fedheha!.

Weewe jibu hoja, umsafishe tumuelewe. Sasa hivihata mfanye nini hamtatulazimishia jitu kama hili, mtahama nchi ninyi na lowasa wenu kwa taarifa. au mkakae msituni! Siyo hapa Tanzania!.

Usije ukahama nchi kama wenzio wanavyosema lowassa ni moto mwingine umpende au umchukie
 
LOWASSA njoo uzime moto huku, siasa hazitusaidii na wala hazitukwamui na maisha magumu uliyotuachia baada ya wewe na mafisadi wenzako kuifilisi nchi.
14421_316927498494810_6215977630423186609_n.jpg

Edward Lowassa ndio waziri mkuu aliewai kukaa katika kiti cha uwaziri mkuu kwa muda mfupi zaidi kuliko waziri mkuu yeyote yule; sasa angalia hii record yake ya kushangaza!!!!

One,
Ndani ya muda mfupi sana alionyesha nia ya dhati kukabiliana na foleni ya jiji la dsm; ambalo kimsingi ni kama jinamizi kwa sasa!!!!

Two,
Ndani ya muda mfupi sana alionyesha kukabiliana na tatizo la ajira kwa vijana. Pale Bandarini kulikuwa na watu waliokuwa vibarua kwa muda wa zaidi ya miaka 15 lakini alipoingia uwaziri mkuu, ile hali kaisimamia jamaa wale wakapa mkataba wa kudumu.

Three,
Ndani ya muda mfupi alionyesha kujali elimu kwa wananchi. Hizi shule za kata ambazo ndizo zinazosaidia wananchi kuamka kwa sasa ni matunda ya Lowassa.

Four,
Tatizo la mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu. Akiwa bungeni mara nyingi amekuwa akiongelea suala hili la mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu kiasi kwamba ilibaki kidogo tu ingekuwa malalamiko ya mikopo kwa wanafunzi ingekuwa historia.

Five,
Wakati akiwa waziri mkuu, kwa muda mfupi sana ilionekana kuwa uchumi sasa utapaa; na tayari kulikuwa na indicators za kutosha kuashiria hilo

Six,
Kwa muda mfupi sana utendaji serikalini ulikuwa unaenda kwa kasi ya ajabu. Kuanzia mdogo hadi mkubwa.

Seven,
Kwa muda aliokaa hajawahi hata mara moja kutoa kauli tata za kuashiria ubabe kwa wale wanaopingana naye. Kauli zake siku zote zimekuwa very straight kuwakabili watumishi wazembe na watendaji wanaotenda kazi katika mfumo wa business as usual.

Eight,
Ndio kiongozi pekee serikalini ambae ana record ya kutoa individual support kwa mwananchi mmoja mmoja pale atakapobaini kuwa panahitajika support kwa ajili ya huyo mwananchi. Hata bbc swahili walishawahi kuripoti kuhusu hili.

Nine,
Akiwa waziri mkuu alimbeba sana Kikwete kwenye utendaji wa kiserikali! Hadi sasa Kikwete amekata tamaa kabisa na mambo ya serikali. Anatamani siku anarudi toka maryland akute tayari 2015 imefika maana hana hamu kabisa na mwenendo wa mambo ndani ta taifa hili.

Ten,
Kikwete hatakaa amsahau kwa kumpoteza katika utendaji wa serikali yake. Na ndo maana uchaguzi wa 2010 Kikwete alipata shida sana! Na hadi leo anamlilia sana, ila mfumo wa chama chake unamgandamuiza sana.

etc,


HAYA SASA
Kuna waliokaa kwa muda waliokaa waliishia kuwaambia wafanyabiashara ukitaka mambo yako yawe mazuri jiunge na ccm!!!

Kuna waliokaa kwa kipindi walichokaa lakini kwa muda mfupi sana walionekana mara kidume kinalia bungeni, mara katoa kauli tata za kuwatisha wapinzani; eti wapigwe tu. Uwapige wapinzani ili iweje?

Hii nchi ya kwako peke yako?

Ahsanteni wakuu
 
team LOWASSA vs team SLAA kazi kwenu. Wote wa Kaskazini.

Aaah...mwanzo nilidhani una hoja wakati unahitaji kupima hoja zenyewe "should be measurable"....hapo ulikua unawabana vzr....lkn hapa umeharibu tena....Kumbe huna tofauti na mleta mada....siasa tu.

Ww unataka wa kutoka kanda gani? Tuanzie hapo....
 
Ukienda Misri ukawauliza kuhusu Tanzania watakuambia iko Afrika Mashariki...ukiwauliza wanafahamu nini ndani ya Tanzania watakutajia Mlima kilimanjaro, ziwa victoria, Simba SportvClub
 
Twelve : Ndii kiongozi pekee East Africa anaeabudiwa na viongozi wa Kenya, kwa kuwa ndie Mfalme wa Wamasai wote Duniani, basi ukitaka uwaone mawazi wa Kenya wakija kuhiji kwake na kupokea maelekezo na muongozo, karibu ni Munduli.

Thirteen,

Lowasa ndio kiongozi pekee mwenye familia ya mke mmoja na watoto wa ndoa basi,wengine wote ndani ya CCM na nje ni michepuko kwa kwenda mbele,nyumba ndogo na kutawanya mbegu hovyo hovyo.
Kwa kweli hii ni rekodi ya kipekee,ni wazi atatuunganisha tena watanzania tukiwa katika dira.
 
Mnaboa sasa. Kama ni mzuri si mmuache atajiuza mwenyewe!!!!!!!!!! Debe jingi kwa vile mnajua ni mtupu! Anyway, kama watoto wenu wanapata choo sio mbaya!
 
Lowasa ni jembe kama wasemavyo vijana wa mjini na hata ukawa wanajua hilo kwa maslahi ya taifa hili tumuunge mkono
 
Kama ni lazima kabisa kuwa lazima mmojawapo kutoka chama cha wezi awe Rais basi aheri Lowasa kuliko mwingine yeyote toka CCM.

Lakini wazalendo tumedhamiria kumpata Rais safi asiye na kashfa za wizi, ufisadi wala kushirikiana na wevi, toka UKAWA. Lazima tumpate Rais ambaye hana najisi ya CCM. Kwa sasa CCM ni uchafu amabao ukikugusa ni lazima utoe harufu/unuke.
 
Haujatuambia kwanini alikaa kwenye kiti cha uwaziri mkubwa muda mfupi kuliko yeyote tz.nini kilipelekea iwe hivyo!!
 
Ndugu wana JF,
Nimefikiria kwa umakini sana na kugundua hapa tulipo tunahitaji watu wenye sifa zifuatazo kututoa hapa tulipo na kwenda hatua nyingine
  • Visionary- tunahitaji mtu mwenye vision na mwenye uwezo wa kusimamia maamuzi na maelekezo aliyoyatoa mfano mrahisi ni shule za kata Tanzania alitoa agizo la hilo limefanyika
  • Maamuzi magumu- hapa sina cha kuongezea sana kwani wote mnalifahamu hili though wengi watasema ni shinikizo,but mkikumbuka bunge lililomalizika juzi spika wa bunge aliongea kitu,na kwa akili ya kawaida mtaelewa kwamba alikuwa na uwezo wa kukataa kuachia ngazi,but kwa ajili ya mapenzi yake na nchi aliona kwamba nchi ya tanzania ni kubwa zaidi kuliko yeye akaamua kuachia ngazi
  • Personality-Hili pia nadhani liko wazi rais wa nchi anatakiwa awe ni mtu ambaye ni presentable hata akiwa katikati wa wakuu wengine ukimuangalia unafurahi kwamba hapa tuna rais
  • muajibikaji-hili halina ubishi huyu muheshimiwa tangu alipokuwa mkuu wa kituo cha kimataifa AICC Arusha alianza kuonesha kwamba ni mtu mchapakazi asiyependa ulege lege,kituo kilikuwa katika hali nzuri sana na naamini hadi leo wanamkumbuka sana,pia ukiangalia wizara zote alizowahi kuziongoza kuanzia maji,mifugo,tamisemi zote zilionesha matunda sasa je kwanini tusijisifie kuwa na kiongozi kama huyu
Sasa kwa maelezo ya hapo juu,though kuna wanaoipinga kila kitu naombeni kauli zenu
 
Lana ya Baba wataifa inamutafuna hataakiwa raisi atachinjwa na wananchi kwa muda wa miaka miwili.
 
.... Watanzania Mbona Wepesi Wa Kusahau.? Yaani Mnataka Mtu JAMBAZI, MWIZI NA FISADI Aliyetukuka Na Anayenunua Uongozi Awe Rais Wenu? Mtoa Mada Sikubaliani Na Wewe Hata Kidogo.
 
Back
Top Bottom