Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,667
- 698,561
Ni tafsiri isiyo rasmi ya mduara/ mzunguko wa milele
Tunaambiwa na kuaminishwa kwamba hakuna kinachodumu milele lakini ni sahihi kabisa... Lakini kuna mwendelezo katika hilo kuna maelezo ya ziada kwamba hakuna kinachodumu milele katika umbo lilelile
Tunaishi katika mzunguko wa mabadiliko wa milele (eternity realm of revolution)
Wewe wa jana si wewe wa leo wala hutakuwa wewe wa kesho nk ulitungwa mimba ukazaliwa ukapitia yote uliyopitia mpaka ukafika muda wa kusoma hii post na niamini ukitoka hapa hutakuwa wewe uliyeingia hapa. Tunaishi katika dunia ya mabadiliko yasiyokoma mpaka kufa na kuingia katika hatua ya ulimwengu mwingine ni nonstop changes to eternity
Tunaambiwa kuwa kifo sio mchakato bali ni mwanzo....death is not a process but a state...! Ni mnyonyoro usio na mwisho na usiokatika
Nawaambiaga watu upya wa kitu ndio mwanzo wa uchakavu wake unanunua gari jipya 0km, linanukia na kupendeza sana lakini unapolitia barabarani ndio mwanzo wa kuwa chuma chakavu, hakuna kitachachorudisha upya wake hakuna
Iitaendelea kuchakaa na kuzeeka mpaka litakapokuwa chuma chakavu kamili ambacho kitarudishwa kiwandani kuchakatwa na kutengenezwa vingine ambavyo navyo vitaingia kwenye mduara uleule wa mabadiliko mpaka navyo vitakaporejea kulekule
Tunamiliki vitu vya thamani na ghali sana tunajaribu kuvitunza na kuvipa ulinzi wa kutosha lakini vinapitia mzunguko uleule hata kufikia mahali vikawa ni vya kutupwa, kugawiwa kuharibiwa, kupotea nk na huko ndio vitakakopita havikai milele vitabadilika nakubadilika mpaka kuwa vitu vingine kabisa
Tunaishi katika ulimwengu wa tamaa ya kumiliki na kuhodhi, vile tunavyovipenda hatutaki vituondoke na huwa tunatumia gharama kubwa kuvilinda na huwa tunakimbia ukweli kuwa kuna siku vitakoma kuwa vyetu
Hivyo basi tufanye kazi tumiliki tuhodhi lakini ubinadamu wetu usitutoke na kufanya mambo mabaya kwakuwa na choyo chuki au roho mbaya kwa vitu ambavyo havikai milele
Wala tusiwe na ile craving iliyopitiliza ili hata siku vikitutoka tujue wazi kuwa hakuna kidumucho milele leo kipo kesho hakipo, penzi leo lipo kesho halipo jumba zuri leo lipo kesho halipo, madaraka leo yapo kesho hayapo
Ni realm of eternity- mzunguko wa milele usiokoma huu pekee ndio utakuwepo milele sio sisi wala vitu tunavyomiliki
Tunaambiwa na kuaminishwa kwamba hakuna kinachodumu milele lakini ni sahihi kabisa... Lakini kuna mwendelezo katika hilo kuna maelezo ya ziada kwamba hakuna kinachodumu milele katika umbo lilelile
Tunaishi katika mzunguko wa mabadiliko wa milele (eternity realm of revolution)
Wewe wa jana si wewe wa leo wala hutakuwa wewe wa kesho nk ulitungwa mimba ukazaliwa ukapitia yote uliyopitia mpaka ukafika muda wa kusoma hii post na niamini ukitoka hapa hutakuwa wewe uliyeingia hapa. Tunaishi katika dunia ya mabadiliko yasiyokoma mpaka kufa na kuingia katika hatua ya ulimwengu mwingine ni nonstop changes to eternity
Tunaambiwa kuwa kifo sio mchakato bali ni mwanzo....death is not a process but a state...! Ni mnyonyoro usio na mwisho na usiokatika
Nawaambiaga watu upya wa kitu ndio mwanzo wa uchakavu wake unanunua gari jipya 0km, linanukia na kupendeza sana lakini unapolitia barabarani ndio mwanzo wa kuwa chuma chakavu, hakuna kitachachorudisha upya wake hakuna
Iitaendelea kuchakaa na kuzeeka mpaka litakapokuwa chuma chakavu kamili ambacho kitarudishwa kiwandani kuchakatwa na kutengenezwa vingine ambavyo navyo vitaingia kwenye mduara uleule wa mabadiliko mpaka navyo vitakaporejea kulekule
Tunamiliki vitu vya thamani na ghali sana tunajaribu kuvitunza na kuvipa ulinzi wa kutosha lakini vinapitia mzunguko uleule hata kufikia mahali vikawa ni vya kutupwa, kugawiwa kuharibiwa, kupotea nk na huko ndio vitakakopita havikai milele vitabadilika nakubadilika mpaka kuwa vitu vingine kabisa
Tunaishi katika ulimwengu wa tamaa ya kumiliki na kuhodhi, vile tunavyovipenda hatutaki vituondoke na huwa tunatumia gharama kubwa kuvilinda na huwa tunakimbia ukweli kuwa kuna siku vitakoma kuwa vyetu
Hivyo basi tufanye kazi tumiliki tuhodhi lakini ubinadamu wetu usitutoke na kufanya mambo mabaya kwakuwa na choyo chuki au roho mbaya kwa vitu ambavyo havikai milele
Wala tusiwe na ile craving iliyopitiliza ili hata siku vikitutoka tujue wazi kuwa hakuna kidumucho milele leo kipo kesho hakipo, penzi leo lipo kesho halipo jumba zuri leo lipo kesho halipo, madaraka leo yapo kesho hayapo
Ni realm of eternity- mzunguko wa milele usiokoma huu pekee ndio utakuwepo milele sio sisi wala vitu tunavyomiliki