Real Madrid (‎Los Blancos) | Special Thread

sijawahi juta kua fan wa Los blancos
Hasa huyu rais wa Madrid simdai chochote huyu mwamba mpaka anaenda kaburini. Pale Hispania ni mtu anaheshimika sana kutokana na misimamo yake.

Kule uliko uwanja wa REAL MADRID umejengwa pale kwa mawazo yake. Alipingwa sana kupelekwa huko uwanja. Lakini sasa ni mji mmoja maarufu sana
 
Uwanja umepelekwa wapi?
 
Upo sawa mkuu japo hajafikia ile record ya President Santiago Barnabeu ya miaka ile lakini the old man ameifanyia makubwa sana Sana Madrid expecally on his second term as President of Real Madrid.
Kiukweli baada ya Santiago Bernabéu, anyefuata kwa juhudi nyingi kama Rais ni Florentino, jamaa anajali mambo ya club kuliko hata mishe zake., kuna siku jamaa alisema kuwa Florentino akiona kwenye Forbes team imeshuka huwa anawavutia wire mazima kuwauliza, Real Madrid imezidiwa kwenye nini na huyo namba moja., ila yeye akishuka kwenye nafasi za wenye mkwanja wala hajali.
Hopefully bado tutakuwa nae, kwasababu kwa juhudi anazo onyesha plus matengenezo ya uwanja sioni Wajumbe wanaanzia wapi kumnyima kura.
 
Umemuona Gareth Mzee wa Wales, Golf then Madrid 😀😀😀 dah sijui jamaa anaenda timu gani huyu I will remember him kwa lile goal lake against Liverpool 2018.View attachment 2244438
Alikuwepo na alikuwa anashangilia na wenzake., wanadai kuwa anarudi Uingereza.,
Ile ishu yake ya Wales, Golf, Madrid alijiharibia sana, pale ndipo aliwakosea hata waliokuwa wamebakiza imani kidogo juu yake.
 
Niliona Dogo Camavinga alikuwa na mzuka mwingi sana utadhani utadhani ana misimu kadhaa na club kumbe ndio kwanza msimu wa kwanza.,
Tuna bahati sana kupata wachezaji ambao ni mashabiki wa team, hata hupati shida sana kuwaambia wajitume., ndio furaha ya Ancelloti aliyonayo kuifundisha Real Madrid.
 
Hapana, mikataba yao imeisha ndani ya club, so wataungana na Gareth Bale kutafuta nafasi sehemu nyingine, Marcelo haijajulikana ataenda wapi, ila Isco kuna uwezekano akajiunga na Real Betis
Marcelo sioni tatizo akiendelea kubaki Madrid.

Ule upande wa kushoto kuna beki gani wa kupanda na kushuka anamzidi!

Ndio yule Mendy? Aaaah hata simkubali kivile...

Hata Isco mbona anapiga kiungo fresh tu.

Hapo wa kusepa ni Bale tu. Wengine wabaki.
 
Namkubali sana marcelo ila kwa staili ya uchezaji wake na Mendy bora marcelo tumpe heshima aende free. Mendy ni kijana ana nguvu ya kupanda na kushuka. Uwezo wa Mendy naamini unaoneka no DOUBT.
Kwa suala la ISCO ni mzuri akiwa na mpira ngojea timu iwe inashambuliwa asee jamaa hakabi aseee hawezi kucheza defensive. Nae aondolewe free akapate timu anayoona itamfaa. Hata barca wanamtaka ISCO hata leo aende hata huko sawa tuu.
Bale na Harzard nao watupishe aseee. Luka jovic na Mariano wasisahaulike wauze tuu
 
Brother mbona unataka tuuze wachezaje wengi hivo wakati tumesajili mmoja tu so far (Rudiger).

Ama kuna plans za kusajili wengine.

Timu si itabaki finyu sana. Rotation ya wachezaji haitokuepo.

Halafu inaonekana Mendy unamkubali sana... Mbona sijawahi kumuona amepanda mbele kumsaidia Vini Jr mashambulizi upande ule. Yeye muda wote yuko nyuma tu.

Mbona mwenzie wa right back (Carvajal) huwa anapanda na kushuka anawasaidia kina Varverde, Asensio na Rodrygo.
 

MKuu hapo ndipo kwenye hoja kuu, yule haukumgonga bali aliucheza katika harakati za kuokoa. Hiyo ishu mpaka huko ulaya imezungumzwa sana na kumwagiwa povu, imezimika kwa kuwa Real Madrid wameshinda game, bila hivyo ingelileta ni Contravention kubwa sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…