Mara nyingi yupo nyuma, mashambulizi yetu mbele yanafika na watu wachache. Pia leo amepoteza mipira mingi tofauti na Kroos(ingawa hata huyu hakuwa na maajabu).
Kama kiungo hiki cha Barca kinatunyong'onyeza hizi huko UEFA sijui itakuwaje.
Tunaenda extra time.,
Ancelotti amefanya hii game kuwa ngumu kwetu, pale kati Casemiro ama Kroos pia anatakiwa kupumzika., Vinicius na yeye amechoka, Benzema baada ya kupata goli na yeye amepotea mazima uwanjani., tunahitaji nguvu mpya uwanjani.
Licha ya kwenda extra time nimependa game ya leo, Barcelona walicheza vizuri, ila si ku zote game kama hizi mbinu ndio huwa zinaamua game., Ancelotti licha ya team yake kucheza mpira mwingi kwenye eneo lao bado alisimama na mbinu yake kutumia mianya kwenye backline ya Barcelona kufanya mashambulizi ya kushtukiza, na ndio aina hiyo ya mpira imeamua matokeo.
Ancelotti hakutaka kupimana ubavu kwenye kiungo, yeye aliingia na idea yake ya kushinda kupitia counter attack, kama alitaka kupimana ubavu angeongeza kiungo mmoja kati ya Valverde ama Camavinga,
Suala la msingi kwangu ilikuwa ni ushindi, makosa yaliyotokea Mwalimu atayafanyia kazi.,